JamiiForums
βœ”
52.7K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
SERIKALI YAANDAA MUSWADA WA TARATIBU ZA UVUNAJI NA UPANDIKIZAJI VIUNGO VYA BINADAMU

- Naibu Waziri wa Afya ameeleza hayo akimjibu Mbunge aliyehoji mkakati wa kuanzisha utaratibu wa kuvuna viungo

- Asema kwa sasa Nchi inatumia miongozo ya Kimataifa

Soma https://jamii.app/MuswadaViungo
WANAOISHI KARIBU NA HIFADHI WASHAURIWA KULIMA PILIPILI KUEPUKA UVAMIZI WA TEMBO

> Naibu Waziri wa Maliasili amesema maboga na matikiti huvutia Tembo kuvamia mashamba

> Njia nyingine ni kumwaga Oil chafu iliyochanganywa na Pilipili na majivu

Soma https://jamii.app/MbinuMbadala
SITI BINTI SAAD: MWANAMUZIKI WA KWANZA KUTOKA ZANZIBAR KWENDA KUREKODI NCHINI INDIA.

- Siti binti Saad alizaliwa mwaka 1880 na alifariki 1950.

- Alikuwa Mwanamke wa kwanza Afrika Mashariki kurekodi muziki wake katika mfumo wa albamu.

Soma > https://jamii.app/WasifuSiti
HASUNGA: USHIRIKA UNALAZIMISHA WASIO WANACHAMA KUUZA MAZAO KUPITIA VYAMA

- Amehoji Serikali haioni ulazima wa kuruhusu Wafanyabiashara kununua kwa Wakulima bila Ushirika

- Serikali yasema inaamini Mfumo wa Ushirika ni njia itakayomsaidia Mkulima

Soma > https://jamii.app/MazaoUshirika
ZINGATIA YAFUATAYO UNAPOOMBA USHAURI

- Kuwa makini unapochagua mtu wa kumuomba ushauri. Zingatia uzoefu wa huyo mtu kwenye jambo husika na ukaribu mlionao

- Kuwa wazi juu ya unachotaka kushauriwa, elezea vizuri chanzo cha tatizo lako

- Ikiwezekana jaribu kutatua tatizo mwenyewe kwanza, kisha umweleze mtu unayemuomba ushauri mahali ulipokwama ili akusaidie kutokea hapo

#JamiiForums #JamiiTalks
KILIMANJARO: WAGONJWA WA AKILI WAONGEZEKA

> Mwaka 2019, Wagonjwa walikuwa 8,691 na mwaka 2020 idadi ilipanda hadi 12,152

> Kushindwa kukabiliana na changamoto za maisha kumetajwa kuwa moja ya sababu za ongezeko

Soma https://jamii.app/WagojwaWaAkil
PROF. KABUDI: SHERIA ZITAKUWA ZIMETAFSIRIWA IFIKAPO DESEMBA

- Akiwa Bungeni, Waziri amesema Wizara nyingine na Taasisi zinaendelea na zoezi la kutafsiri #Sheria zinazosimamia ili ifikapo Desemba Sheria zote ziwe zimetafsiriwa kwa Kiswahili

Soma > https://jamii.app/TafsiriSheria
MBUNGE: KUNA MRUNDIKANO MAGEREZANI KWASABABU YA KESI ZA KUBAMBIKIWA

- Agnesta Kaiza amesema "Kila leo unasikia fulani ana kesi ya Uhujumu Uchumi"

- Asema uwepo wa masharti magumu ya dhamana ni sababu nyingine ya mrundikano ktk Magereza na Mahabusu

Soma - https://jamii.app/MbungeMagereza
AUSTRALIA: JELA MIEZI 10 KWA KUWAPIGA PICHA POLISI WALIOKUWA WANAKATA ROHO

- Richard Pusey (42) amekutwa na hatia kwa kuwadhihaki na kuwapiga picha Maafisa wa Polisi waliofariki ajalini

- Familia za Marehemu hazijaridhishwa na kifungo kilichotolewa

Soma https://jamii.app/PolisiWakikataRoho
MORRIS NYUNYUSA MLEMAVU WA MACHO ALIYEKUWA NA KIPAJI CHA KUPIGA NGOMA

- Yeye ndiye aliyepiga ngoma zinazosikika kupitia TBC Taifa kama kiashiria cha kuanza kwa taarifa ya habari

- Inaelezwa kuwa Mzee Nyunyusa hakunufaika na kazi zake hata nyumba yake iliponea chupuchupu kuuzwa kwa deni la mkopo wa benki

- Ingawa Morris Nyunyusa ameshafariki lakini kazi zake ni tunu ya Taifa kwenye sanaa

Soma https://jamii.app/HistoriaNyunyusa

#JamiiForums #JamiiTalks #Historia
UGANDA YASITISHA MATUMIZI YA VITAMIN C KATIKA KUTIBU COVID19

- Vidonge vya Vitamin C vinapatikana kirahisi hivyo Watu hutumia kiholela na kuleta madhara ikiwemo Figo kutofanya kazi

- Vitamin C husaidia chembe hai nyeupe kupambana na virusi

Soma - https://jamii.app/UgandaVitaminC
DRC: UMOJA WA MATAIFA WACHUKUA DOZI MILIONI 1.3 ZA COVID19 ILI ZISIISHE MUDA WA MATUMIZI

> Chanjo ya #Astrazeneca iliyopokelewa DRC itaisha muda wa matumizi Juni 24

> UNICEF imechukua dozi hiyo ili kuzipeleka #Senegal, Comoros, #Ghana na Angola

Soma - https://jamii.app/DRCChanjoUN
MOROGORO: MBARONI KWA KUUZA MISHKAKI YA NYAMA YA MBWA

> Hamza Rajabu (20), Omary Mohamed (12) na Mussa Juma (30) wanashikiliwa na Polisi kwa kuuza mishkaki ya Mbwa maeneo ya Msamvu

> Walikutwa wakimchuna ngozi Mbwa Darajani ktk barabara ya Iringa

Soma - https://jamii.app/MbwaMoro
WALIOSTAAFU 1996 OFISI YA MAKAMU WA RAIS HAWATALIPWA PENSHENI

> Wizara ya Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira imesema waliostaafishwa walishalipwa stahiki zao

> Hawatalipwa pensheni kwani waliajiriwa kwa β€œOperational Services”

Soma - https://jamii.app/SerikaliPensheni
MBUNGE ASEMA SHERIA YA BIMA INA MATATIZO NA WANANCHI HAWATENDEWI HAKI

- Dkt. Oscar Kikoyo amesema mhanga wa ajali za barabarani anapokwenda kudai fidia, Sheria ya Bima ipo kimya

- Ameeleza, kiasi anachoenda kulipwa ni maamuzi ya Kampuni ya Bima

Soma > https://jamii.app/BungeSheriaBima
#COVID19: KENYA YAZUIA NDEGE KUTOKA INDIA

- Zuio hilo la siku 14 ni kufuatia ongezeko la maambukizi Nchini India

- Wataowasili #Kenya kutoka India katika saa 72 zijazo watafanyiwa vipimo na watakaokutwa na maambukizi watalazimika kujitenga siku 14

Soma https://jamii.app/KenyaNdegeIndia
KENYA: KITUO CHA RUNINGA CHAFUNGIWA KWA KUONESHA VIBONZO VYA NGONO

> Mt. Kenya TV kimefungiwa kwa wiki nne na kutakiwa kulipa faini ya takriban Tsh. Milioni 11.5

> Mamlaka ya Mawasiliano zimesema kituo hicho kilirusha picha zisizofaa mchana

Soma https://jamii.app/KituoChaRuninga