JamiiForums
52.7K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
RAIS SAMIA: LUKUVI HATOKUWA SPIKA WA BUNGE

Akanusha uvumi William Lukuvi ameandaliwa kuwa Spika wa Bunge baada ya kutoteuliwa katika Baraza la Mawaziri

Pia, amekanusha kuwa Lukuvi ni kati ya watu waliokuwa wanataka kugombea Urais 2025

Soma - https://jamii.app/UapishoIkuluDodoma

#Governance
RAIS SAMIA: NILIWAACHA LUKUVI NA PROF. KABUDI ILI WAJE KWANGU KUWASIMAMIA MAWAZIRI

Amesema amewaacha Wiliam Lukuvi na Prof. Palamagamba Kabudi kwasababu ya umri, hivyo atafanya nao kazi kwa ukaribu ili kuweza kuwasisimamia mawaziri

Soma - https://jamii.app/UapishoIkuluDodoma

#Governance
UTAFITI: GONGO HUSABABISHA SARATANI YA TUMBO

Shirika la Kimataifa la Utafiti wa Saratani, IARC limebaini gongo, Chang'aa na Kachasu zinasababisha Saratani ya Tumbo hasa kwa wanaume

Saratani hii imeshamiri zaidi Kusini na Mashariki mwa Afrika

Soma https://jamii.app/GongoSaratani

#JFAfya
SOMALIA: Viongozi wa kisiasa wamefikia makubaliano ya kukamilisha Uchaguzi wa Bunge la chini kati ya Januari 15 na Februari 25, 2022

Waziri Mkuu na Rais wamekuwa wakijibizana kuhusu zoezi hilo, hali iliyozua wasiwasi wa ghasia Nchini humo

Soma https://jamii.app/UchaguziSomalia
#Democracy
Aliyewahi kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais, Bunge la Afrika(PAP), Stephen Masele na Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Dkt. Tulia Ackson wamechukua fomu kuomba kuteuliwa kugombea Uspika wa Bunge

Wengine waliojitokeza ni Patrick Nkamah na Godwin Kunambi

Soma https://jamii.app/SpikaWaBunge

#Governance #Democracy
MDAU: MAONESHO YA VYAKULA VYA ASILI NI FURSA NZURI YA KUKUZA UTALII

Anasema Tanzania bado hatujanufaika na Utalii wa matukio na maonesho (Event Tourism) kwa namna ya kuridhisha. Hatujaweza kuandaa maonesho makubwa ya kitamaduni ambayo yangeweza kuvutia Watu

Mfano #Brazil huvutia maelfu ya Watu katika ngoma yao ya Samba. #Tanzania tunaweza kuanzisha maonesho ya vyakula vya asili na kuandaa msimu wa maonesho hayo ambayo ungepambwa na matukio mbalimbali

Soma - https://jamii.app/VyakulaUtalii

#StoriesOfChange #JFMdau
UTAFITI: COVID-19 YABAINIKA KUSHUSHA UZALISHAJI WA MBEGU ZA KIUME

Utafiti uliofanywa kwa Wanaume 120 waliougua na kupona #COVID19 nchini Ubelgiji umebaini ujazo wa mbegu za kiume hupungua kwa wanaume baada ya kupata Ugonjwa huo

Soma - https://jamii.app/MbeguZaKiume

#JFAfya
#AFCON2021: GUINEA, MOROCCO ZAPATA USHINDI

Mchezo wa 2 wa Kundi B kwa siku ya leo, umemalizika kwa #TeamGuinea kupata ushindi wa 1-0 dhidi ya #TeamMalawi

Pia, mchezo wa kwanza wa Kundi C kwa leo, umemalizika kwa #TeamMorocco kupata ushindi wa goli 1-0 dhidi ya #TeamGhana

#JFSports
KAZAKHSTAN: Rais Kassym-Jomart Tokayev amesema Nchi imerejea katika utulivu, na maandamano yaliyotokea yalikuwa ni jaribio la mapinduzi

Wananchi waliandamana kupinga ongezeko la bei za mafuta. Watu zaidi ya 150 waliuawa kwenye machafuko hayo

Soma https://jamii.app/KazakhstanMapinduzii

#Governance
MYANMAR: KIONGOZI WA KIRAIA AONGEZEWA MIAKA 4 JELA

Mahakama Nchini #Myanmar imemhukumu tena Aung San Suu Kyi miaka mingine 4 kwa kumiliki na kuingiza vifaa vya mawasiliano kinyume cha #Sheria na kuvunja masharti ya kupambana na #COVID19

Soma - https://jamii.app/Suu4yrsJail
#Democracy
UGANDA: SHULE ZAFUNGULIWA BAADA YA MIAKA TAKRIBAN MIWILI

Ili kudhibiti usambaaji wa maambukizi ya #COVID19, Uganda ilifunga Shule tangu Machi 2020

> Mtaala utawekwa sawa ili kuwasaidia Wanafunzi ambao hawakutumia Teknolojia kuendelea kujifunza

Soma https://jamii.app/ShuleUganda

#Governance #JFElimu
AJALI SIMIYU: Takriban Watu 14 wamefariki Dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya magari waliyokuwa wakisafiria kugongana

Kati ya waliopoteza maisha ni Waandishi wa Habari 5 waliokuwa katika msafara wa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza

Soma - https://jamii.app/Ajali14Simiyu

#JFMatukio
JE, WAJUA KUWA SPIKA SIO LAZIMA AWE MBUNGE?

Kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, Ibara ya 84(9) iwapo mtu asiye Mbunge akichaguliwa kuwa Spika wa Bunge atatakiwa kuapa kiapo cha Uaminifu

Soma - https://jamii.app/SpikaBunge

#JamiiForums #JFMaarifa
MBINU UNAZOWEZA KUTUMIA KULINDA AFYA YA MACHO YAKO

1. Unashauriwa kuvaa Miwani ya kuzuia Mionzi ya Jua ili kuzuia Mionzi ya UV na hakikisha unatumia Miwani yenye uwezo wa kuzuia Mionzi kwa 99%-100%

2. Kula Mlo wenye Virutubisho Kamili: Virutubisho muhimu kwa utunzaji wa Macho ni Vitamini A, Vitamini E, Vitamini C, Asidi ya Mafuta ya Omega-3, Zinki, Lutein na Zeaxanthin zinazopatikana kwenye Karoti, Mchicha, Samaki na Mayai.

Soma - https://jamii.app/RoutineEyeCare

#JFAfya #EyeCare
#ZIMBABWE: Rais Emmerson Mnangagwa amemfuta kazi Waziri wa Usalama wa Nchi hiyo, Owen Ncube kwa kufanya vitendo visivyofaa kama Kiongozi wa Serikali

Owen anadaiwa kuwatisha baadhi ya Wanachama wa ZANU-PF ktk Uchaguzi wa ndani hivi karibuni

Soma - https://jamii.app/OwenOutZimb

#Accountability
UTAFITI: MAFUA YANAWEZA KUZUIA KUPATA #COVID19

Watafiti wa Imperial College of London wamebaini 'T-Cells' husaidia kuzuia maambukizi. Mafua yamebainika kuzalisha 'T-Cells' nyingi

Chanjo imetajwa kuwa njia thabiti kukabiliana na Corona

Soma - https://jamii.app/CommonCold

#UVIKO3 #JFAfya
RAIS SAMIA: AJIRA NDIYO NGUZO YAKO YA MAISHA, SIO 'BY THE WAY'

Rais Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kubadilika wakiajiriwa sekta binafsi hata Serikalini huku akiongeza "sekta binafsi ukizubaa nafasi yako inachukuliwa"

Amefafanua "Nilishawahi kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara Zanzibar, wakati ule kesi nyingi nilizokuwa nikipokea ni uzembe, kutokuwa na nidhamu sehemu za kazi, umefiwa na shangazi wa shangazi yako unakwenda kuzika bila kutoa taarifa"

Soma - https://jamii.app/SamiaAjira

#Governance
MDAU: MAMBO YANAYOWEZA KUKUSABABISHIA LAANA KWENYE MAISHA

1. Kumdhulumu Mtu: Jasho la Mtu huzaa mikosi. Machozi na manung'uniko anayoyatoa Mtu aliyeumizwa kwa kudhulumiwa, hugeuka laana

2. Kuua au kutoa kafara: Damu ya Mtu ni laana, Damu ya Mtu ni mkosi, Damu ya Mtu ni nuksi. Ukisikia kuwa kuna vitu havina midomo lakini vinaongea, basi ni Damu ya Mtu

3. Kumkana au kumtukana Mzazi: Vitabu vya Mungu vinaeleza, "Waheshimu Baba na Mama upate kheri na miaka mingi Duniani"

Soma - https://jamii.app/TabiaLaana

#StoriesOfChange #JFMdau
KENYA YAZUIA NDEGE ZA UAE

Mamlaka ya Usafiri wa Anga (KCAA) yapiga marufuku ndege za Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kujibu marufuku iliyowekwa kwa ndege za Kenya

UAE iliweka marufuku baada ya kubaini udanganyifu katika vipimo vya #COVID19

Soma - https://jamii.app/KenyaVsUAE

#Governance
#UGANDA: MWANDISHI ASHTAKIWA KWA KUTUMA TAARIFA ZA KASHFA DHIDI YA RAIS NA MWANAE

Kakwenza Rukirabashaija anayetuhumiwa kutuma taarifa za kashfa kuhusu Rais na Mtoto wake kwenye #Twitter amefunguliwa mashtaka 2 ya Mawasiliano ya kukera

Soma - https://jamii.app/RukirabashaijaCourt

#FreeSpeech