JamiiForums
55.9K subscribers
33K photos
1.91K videos
30.1K links
Official JamiiForums Telegram Channel | Be Informed, Engaged & Entertained
Download Telegram
NDUGAI: NAMUOMBA RADHI RAIS NA WANANCHI WOTE

Spika wa Bunge, Job Ndugai amemuomba radhi Rais Samia Suluhu na Wananchi wote kwa sintofahamu iliyotokana na kauli yake

> Amesema wana CCM lengo lao ni moja na hawawezi kutofautiana

Soma https://jamii.app/SpikaNdugai

#Accountability
NDUGAI: NIMEUMIA KUOENEKANA NAPINGA MKOPO WA SERIKALI WA TSH. TRILIONI 1.3

Spika Job Ndugai amesema kauli aliyoitoa Desemba 26, 2021 imenukuliwa vibaya, video iliyosambazwa haikuwa na ujumbe aliokusudia

> Amesema Serikali inafanya vizuri

Soma https://jamii.app/SpikaNdugai

#Accountability #JFUwajibikaji
HONG KONG: UHURU WA HABARI WAENDELEA KUZOROTA. TOVUTI NYINGINE YAFUNGWA

Citizen News itafungwa kuanzia Januari 04 kutokana na mazingira ya Vyombo vya Habari kuzorota

Sheria mpya zilizowekwa na China zataka kuzuia #UhuruWaKujieleza

Soma - https://jamii.app/CitizenNewsHK

#PressFreedom #UhuruWaHabari
ZANZIBAR: Rais Hussein Mwinyi ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji (ZBC), Dkt. Saleh Yussuf Mnemo leo Januari 03, 2022

Dkt. Mnemo aliteuliwa kuhudumu nafasi hiyo Mwezi Mei 2021

Soma - https://jamii.app/UtenguziZBC

#Governance
LAMU, KENYA: Watu sita wameuawa na nyumba kuchomwa moto na Wanamgambo wanaoshukiwa kuwa ni Al Shabaab

Wapiganaji wa Al Shabaab wamefanya mashambulizi kadhaa Nchini humo baada ya Wanajeshi kupelekwa Somalia mwaka 2011

Soma - https://jamii.app/6DeadLamu
MDAU: MAMBO YA KUZINGATIA UNAPOTAKA KUJENGA NIDHAMU BINAFSI ILI KUFIKIA MALENGO

Muda: Jifunze kusema 'Hapana' kwenye matukio yanayopoteza muda wako na wekeza muda mwingi kwenye masuala yanayokuongezea ujuzi

Fedha: Nidhamu bora ya fedha huchochea kutengeneza uwezekano wa ndoto zako. Wekeza katika maeneo yanayoendana na ndoto zako

Soma Makala - https://jamii.app/NidhamuSOC

#StoriesOfChange #JFMdau
TANZIA: MZEE KAMBAULAYA AFARIKI DUNIA

Msanii maarufu na Mwanahabari mkongwe, Barnabas Maro maarufu kama Mzee Kambaulaya au Baba Bishanga amefariki dunia Januari 4, 2022 Hospitali ya Taifa ya Muhimbili akipatiwa matibabu

Soma https://jamii.app/Kambaulaya
IRAN YATAKA TRUMP AWAJIBISHWE KWA MAUAJI YA SOLEIMANI

Rais Ebrahim Raisi ataka kuundwe Mahakama ambayo Donald Trump, Mike Pompeo na wengine watashtakiwa kwa mauaji ya Jenerali Qassem Soleimani yaliyotokea miaka 2 iliyopita, au Iran italipiza kisasi

Soma https://jamii.app/TrumpSoleimani

#JFUwajibikaji #Accountability
ISRAEL YAWA NCHI YA KWANZA KUTOA CHANJO YA NNE YA #COVID19

Ongezeko la maambukizi ya #Omicron limefanya watu wenye umri wa zaidi ya miaka 60 wapewe 'booster' ya pili

Wengine wanaopewa kipaumbele ni wenye Magonjwa Sugu na Wahudumu wa Afya

Soma https://jamii.app/SecondBoosterDose

#UVIKO3 #JFAfya
KENYA: Kiongozi wa ODM, Raila Odinga amehoji chanzo cha Mamilioni ya Fedha ambayo amesema Naibu Rais, William Ruto anamwaga kwenye Kampeni zake

Awataka Wakenya kutomchagua Ruto kuongoza Taifa hilo akisema Uongozi wake utatawaliwa na Ufisadi

Soma https://jamii.app/RailaRutoKE

#Accountability
MDAU: NAMNA SERIKALI INAVYOWEZA KUWASAIDIA WAHITIMU KATIKA UTAFUTAJI

1. Serikali na Sekta Binafsi zinapaswa kuwaamini Vijana na kuondoa kigezo cha uzoefu

2. Serikali itengeneze mahusiano mazuri na mataifa mengine, kwani hii itasaidia kupanua soko la nje

3. Kuwepo uwazi katika masuala ya Ajira kuanzia Serikali mpaka Mashirika Binafsi. Ukabila, Rushwa na Udini viepukwe

Soma - https://jamii.app/WahitimuSerikaliSOC

#StoriesOfChange #JFMdau
UTEUZI: Rais Samia amteua Dkt. Baghayo Saqware kuwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima (TIRA)

Charles Itembe ateuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Eneo Maalum la Mauzo ya Nje (EPZA), na Ernest Mchanga Katibu wa Tume ya Pamoja ya Fedha

Soma - https://jamii.app/Uteuzi3Rais

#Governance
MSUMBIJI: Rais Filipe Nyusi na mkewe Isaura Nyusi wamekutwa na #COVID19 na wamelazimika kujitenga

> Nchi hiyo imethibitisha kuwa na watu 193,000 wanaougua COVID-19, na vifo 2,031

Soma https://jamii.app/FilipeNyusi

#UVIKO3 #JFAfya
SUDAN: WANAHARAKATI WAITISHA MAANDAMANO ZAIDI

Wanaoongoza Kampeni dhidi ya Utawala wa Kijeshi wamesema Waandamanaji watakuwa wakielekea Ikulu hadi ushindi utakapopatikana

Idadi ya waliopoteza maisha tangu Mapinduzi kufanyika imefikia 56

Soma - https://jamii.app/ProtestsSdn

#Democracy
UTAJIRI WA KAMPUNI YA APPLE WAZIDI GDP YA AFRIKA

Kampuni ya Apple imefikisha thamani ya Dola trilioni 3 (takriban Tsh. Trilioni 6,920.88) katika Soko la Hisa

Pato la Ndani la Afrika (GDP) ni Dola Trilioni 2.6 sawa na Tsh. Trilioni 5,998.1

Soma - https://jamii.app/AppleUtajiri

#JFTech
MWIGULU: DENI NI HIMILIVU, TUTAENDELEA KUKOPA

Asema Mkopo sio Msaada na hutolewa kwa mwenye chanzo cha kulipa

Pia, amesema sio uungwana kusema Rais anakopa akisisitiza Marais hawakopi bali ni Serikali akisema "Hilo si jambo la Familia, ni la Nchi"

Soma https://jamii.app/MwiguluDeni

#Governance
RAIS SAMIA: TANZANIA IMEKUWA IKIKOPA TANGU UHURU

Amesema inashangaza Mtu anayetegemewa kushirikiana na Serikali kwenye safari ya maendeleo 'kuargue' kuhusu Tozo na Mkopo wa Trilioni 1.3 akisema, "Ni homa (fever) ya 2025, wasameheni"

Asema "Toka tunapata Uhuru ni Mikopo kwenda mbele. Na katika Mikopo yote huu ni mkopo mzuri zaidi"

Soma - https://jamii.app/RaisTozoMikopo

#Governance
RAIS SAMIA: TAIFA HALIWEZI KUENDESHWA NA TOZO PEKEE

Rais Samia asema kumekuwepo watu wanaohoji kwanini Nchi imekopa japokuwa kuna fedha za tozo, akifafanua kuwa Taifa haliwezi kwenda na fedha za tozo pekee

Amesema kuleta ustawi wa Nchi sio miujiza na ni lazima kutumia mbinu zote zilizopo

Soma - https://jamii.app/SSHTozo

#Governance
RAIS SAMIA KUFANYA MABADILIKO YA BARAZA LA MAWAZIRI HIVI KARIBUNI

Amesema ataenda na wale wote anaohisi wanaweza kwenda naye kuleta maendeleo kwa Watanzania na kwamba wale ambao anahisi ndoto zao ni "kule" atawapa nafasi waende kujiandaa

Asema, "Wakajitayarishe vizuri huko nje kwasababu nikiwatuma ndani nitawasumbua"

Soma - https://jamii.app/RaisBarazaMawaziri

#Governance
RAIS SAMIA: UMEME HAUWEZI KUUNGANISHWA KWA ELFU 27

Rais Samia Suluhu amesema ni ngumu kwa TANESCO kuwaunganishia umeme Watanzania kwa Tsh. 27,000

> Amesema Wananchi wamelipa lakini wanashindwa kuunganishiwa umeme kwa kuwa TANESCO hawana nguzo

Soma - https://jamii.app/Tsh27kTANESCO

#ServiceDelivery