JamiiForums
55.5K subscribers
33.3K photos
2K videos
30.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
JOHN KITIME: HII NI MARA YA 3 KUZUIA MAONESHO YA MUZIKI NCHINI

> Amesema, kwa mara ya kwanza mwaka 1984 alipofariki Sokoine maonesho ya Muziki yalizuiliwa kwa mwezi 1 na alipofariki Mwl. Julius Nyerere yalizuiliwa kwa miezi 3

> Kwa sasa yamezuiliwa kutokana na #CoronaVirus

Soma https://jamii.app/HistoriaZuio
#JFBurudani
BODI YA MIKOPO YAPELEKA TSH. BILIONI 122.8 VYUONI

> Imesema wanaostahili kupata mikopo kwa mwaka wa masomo 2019/2020 ni Wanafunzi 132,119

> Pesa hiyo ni kwa ajili ya ada, Malazi na posho kwa siku 60 kuanzia Juni 1 mpaka Julai 30

Soma https://jamii.app/HESLBVyuo
#JFLeo
KENYA: MAAMBUKIZI YA #COVID19 YAFIKA 1,745

> Maambukizi mapya 127 yamethibitishwa baada ya sampuli 3,831 kupimwa ndani ya saa 24 zilizopita

> Watu 4 zaidi wamefariki na kufanya idadi ya vifo kufikia 62. Waliopona wafikia 438

Soma https://jamii.app/COVID19KE1745
#JFCOVID19_Updates
SERIKALI: TUKO VIZURI KIUCHUMI, MISHAHARA YA WATUMISHI HAIJAPUNGUZWA

> Msemaji Mkuu wa Serikali amesema wagonjwa wa #COVID19 walioko Tanzania hawafiki 60

> Amesema hatua zilizochukuliwa na Tanzania zimeiweka nchi katika nafasi nzuri ya kulinda Uchumi wake

Soma https://jamii.app/UchumiUkoVizuri
#JFCOVID19_Updates
MAXENCE: ULINZI WA DATA UTAPUNGUZA WATU KUTUMIWA TAARIFA NA MATANGAZO BILA HIARI ZAO
-
Akiongea kupitia Kituo cha East Africa Radio, Mkurugenzi Mtendaji wa Jamii Forums, Maxence Melo amesema Sheria ya #UlinziWaData ni muhimu nchini
-
Asisitiza bila sheria madhubuti ya ulinzi wa data, Kampuni za simu, taasisi zinazochakata taarifa za Watanzania hazibanwi vilivyo kuhakikisha usalama wa taarifa za wateja wao
-
Aidha, amekumbushia kuwa kumekuwepo Muswada wa Sheria tangu mwaka 2014 hivyo wadau washirikishwe ili iwepo Sheria rasmi ya kuwahakikishia Watanzania usalama wa data zao
YAJUE MAJUKUMU YA AFISA MTENDAJI WA KATA

> Afisa Mtendaji Kata ni Mtumishi wa Serikali ambaye huwa ni Mtendaji Mkuu wa Kata na humsaidia Mkurugenzi Kuratibu na kusimamia shughuli za Uchaguzi katika Kata

Soma https://jamii.app/MKitiMajukumu
#Uongozi #Jamiiforums
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
ZANZIBAR: ALIYELALAMIKIA ZOEZI LA VITAMBULISHO AKAMATWA NA POLISI

- Abdalla Khamis Mohammed (Tuba) anashikiliwa kwa madai ya kufanya uchochezi baada ya kudai kitambulisho cha Mzanzibar Mkazi

- Alisema wananchi wengi katika eneo lao hawajapatiwa kitambulisho kitakachowawezesha kuhakikiwa kwenye daftari la Wapiga kura

Soma https://jamii.app/MbaroniMalalamikoVitambulisho
#JFLeo
RAIS TRUMP: MAREKANI INAVUNJA RASMI MAHUSIANO NA WHO

- Asema ni kwa uzembe wa Shirika hilo kushindwa kudhibiti mapema kusambaa kwa #COVID19

- Adai China ilijilinda dhidi ya maambukizi zaidi ya #coronavirus lakini ikaacha mataifa mengine yataabike kwa gharama kubwa

Soma > https://jamii.app/USvWHO
#CORONAVIRUS-MAREKANI: JIMBO LA WASHINGTON KUENDELEA NA SHUGHULI KESHO

> Ni kati ya majimbo ya awali kushambuliwa zaidi na #COVID19 ila Gavana wao amesema sasa wanaendelea vizuri

> Ila ametahadharisha kuwa hiyo haimaanishi kuwa wanarejea kuishi kama ilivyokuwa awali

Soma https://jamii.app/CurfewEnds
#JFCOVID19_Updates
ZOOM YAONGEZA USALAMA WA MAWASILIANO KWA WANAOLIPIA HUDUMA

> Zoom ni mtandao unaotumika zaidi kufanya mikutano kwa njia ya video na umekuwa udukuliwa mara kwa mara

> Ulinzi utakaoongezwa utapunguza hatari ya kudukuliwa kwa watakaolipia kupata huduma hiyo

Soma https://jamii.app/ZoomEncryption
#JFLeo #Jamiiforums
MAREKANI: ASKARI ALIYEMUUA 'MTU MWEUSI' ASHTAKIWA. MKEWE ATAKA TALAKA

- Derek Chauvin ameshtakiwa kwa mauaji daraja la 3 na mauaji ya bila kukusudia daraja la 2

- Mkewe Kellie Chauvin ameeleza kufungua jalada akitaka kuachana naye

Soma https://jamii.app/MauajiFloyd
#BlackLivesMatter
CHAMWINO: UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI UJENZI WA IKULU

- Rais Magufuli ameshiriki uwekwaji wa jiwe la msingi katika Ikulu ya Chamwino , Dodoma

- Marais Wastaafu; Mwinyi, Mkapa, Kikwete na Mama Maria Nyerere pia wamehudhuria

Fuatilia https://jamii.app/UzinduziIkuluChamwino
RAIS MAGUFULI: SIKUWA NA UHAKIKA KAMA NDANI YA MIAKA MITANO TUTAKUWA TUMEHAMIA DODOMA

- Amesema wakati anapokea Uenyekiti wa CCM, Julai 2016 aliahidi kwa kipindi cha miaka mitano angehakikisha Serikali yote inahamia Dodoma

- Amesema hakuwa na uhakika kama kwa muda huo angefanikiwa na ila anafaraja sana kwani ametekeleza ahadi hiyo

Soma https://jamii.app/UzinduziIkuluChamwino
RAIS MAGUFULI: WAKULIMA UZENI MAZAO YENU KWA BEI YA JUU. WATWANGENI SANA

- Amewatahadharisha Wakulima kuuza mazao yao kwa bei ya kutupa kwa Walanguzi kwani mwaka huu au ujao mambo yanaweza yasiwe mazuri sana

- Amesisitiza hakuna chakula cha bure hivyo Wakulima wasubiri muda muafaka wa kuuza au kama wanauza basi wauze bei ya juu

Soma https://jamii.app/UzinduziIkuluChamwino
UTAFITI: MWAMKO WA WANAWAKE KUJIFUNZA ‘CODING’ NI MDOGO SANA

> Utafiti uliofanywa na Free Code Camp kwa Watu 65,000 ulibaini Wanawake (7.7%) walikuwa wanajifunza 'coding'

> Pia, umeonesha Watanzania wachache hujifunza kuhusu Mtandao

Soma https://jamii.app/CodeLearning
LWAKATARE ARUDI CUF, KUTUMIKA KUIANGAMIZA CHADEMA

> Mbunge wa Bukoba Mjini, Wilfred Lwakatare amesema ametengua kauli yake ya kustaafu siasa baada ya CUF kumuomba arudi

> CUF imesema itamtumia Mbunge huyo kuviangamiza vyama vya upinzani hususan CHADEMA katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020

Soma https://jamii.app/LwakatareArudiCUF
#JFSiasa
SERIKALI: MCHAKATO MAHABUSU KUFANYA KAZI KAMA WAFUNGWA WAANDALIWA

- Waziri Simbachawene amesema lengo sio kuwafanyisha kazi za sulubu au kazi zinazotweza utu wao

- Amesisitiza kuwa wanataka kuwatumia kwa nia njema tu ya kuongeza uzalishaji

Soma https://jamii.app/MahabusuKaziGerezani
#JFLeo
KENYA: VISA VIPYA 143 VYA #COVID19 VYAREKODIWA AKIWEMO MTOTO WA MWEZI 1

- Ni baada ya sampuli 2,959 kupimwa ndani ya saa 24 zilizopita. Visa vyafikia 1,888

- Katika visa vipya; Wanaume 110 na Wanawake 33 na umri ni kati ya mwezi 1 na miaka 88

Soma https://jamii.app/COVID19KE-1888
#JFCOVID19_Updates
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
MSAMVU, MOROGORO: VIBANDA 8 VYA BIASHARA VYATEKETEA KWA MOTO

- Vibanda hivyo katika eneo la stendi ya Msamvu vimeteketea kwa Moto ambao haujafahamika chanzo chake, usiku wa kuamkia leo

- Kamanda wa Zimamoto mkoani humo, Godluck Zerote amesema hakuna mtu aliyedhurika bali mali pekee

Soma https://jamii.app/MotoMsamvuMoro
#CORONAVIRUS: BRAZIL IMERIPOTI VISA VIPYA 33,274 NDANI YA SAA 24

- Jumla ya visa imefikia 499,966 ikiwa ni nchi ya pili kwa visa vingi nyuma ya Marekani (2,036,110)

- Pia, imerekodi vifo vipya 956 na kuwa na jumla ya vifo 28,849

Soma https://jamii.app/COVID19Updates
#JFCOVID19_Updates