JamiiForums
52.7K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
UHISPANIA: WALIOBAKA WAACHIWA HURU KWA KUWA HAWAKUTUMIA NGUVU KUBAKA

- Mahakama imewaachia huru Wanaume 5 waliohukumiwa kifungo kwa kumbaka msichana wa miaka 14

- Nchini humo shtaka linaweza kuwa ubakaji iwapo nguvu ama vitisho vitatumika

Zaidi, soma https://jamii.app/WabakajiHuruUhispania
KATAVI: AFUNGWA MAISHA KWA KUMPA UJAUZITO MTOTO WAKE

- Lazaro Charles(35) amehukumiwa baada ya kupatikana na hatia ya kumpa ujauzito mtoto wake (14)

- Mshtakiwa alikuwa akimbaka kwa nguvu wakiwa nyumbani wakati mama yake alipokuwa amesafiri

Zaidi, soma https://jamii.app/KifungoMimbaMwanaye
IGP SIRRO AMTAKA ALIYEMTISHIA MWENZAKE BASTOLA KUFIKA POLISI

- Amemtaka kijana aitwaye Shaban anayeonekana kwenye video iliyosambaa mtandaoni akimtishia bastola mwenzake kuripoti Kituo cha Polisi mara moja na kusalimisha silaha yake

Zaidi, soma https://jamii.app/AliyetishiaBastola-Polisi
ACT WAZALENDO: UCHUKUAJI WA FOMU KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA UMEJAA HUJUMA

- Kimesema wanachama wake wanaochukua fomu wanakumbana na vikwazo mbalimbali ikiwemo kunyimwa fomu, ofisi kufungwa, kutishwa na kupewa fomu zisizo kamili

Zaidi, soma https://jamii.app/ACT-HujumaUchaguziS-Mitaa
ALIYEKUWA 'MISS GAMBIA' AMTUHUMU ALIYEKUWA RAIS WA NCHI HIYO YAHYA JAMMEH KWA KUMBAKA

> Akiwa mbele ya Kamisheni ya Maridhiano baada ya utawala wa Jammeh kuanguka amesema pia alilazimishwa kumkataa mchumba wake na ahadi ya kuolewa

Zaidi, soma => https://jamii.app/FatouVsJammeh
BILIONI 40 KUTUMIKA KULIPA MADENI YA WAKULIMA WA KOROSHO

- Rais Magufuli ameiagiza Wizara ya Fedha na Mipango kutoa Tsh. Bilioni 40 ili kumalizia madeni yote ya Wakulima wa Korosho yaliyobaki baada ya Serikali kununua korosho msimu ulioisha

Zaidi, soma https://jamii.app/Bilioni40MadeniKorosho
MKURUGENZI ALIYETAKA MWEKEZAJI ALIPIE VIKAO KUCHUKULIWA HATUA

- Waziri Mkuu ameagiza Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mtwara, Maisha Mtipa achukuliwe hatua

- Alimtaka Mwekezaji alipe Tsh. Milioni 31.6 ya vikao ili kumpatia eneo

Zaidi, soma https://jamii.app/MkurugenziMwekezajiVikao-MTR
LEO NI SIKU YA KIMATAIFA YA KUPINGA UKATILI DHIDI YA WANAHABARI DUNIANI

- Ripoti ya Kamati ya Kuwalinda Wanahabari Ulimwenguni(CPJ) imeeleza kuwa Mataifa 13 yamekumbwa na visa vya mauaji ya kikatili dhidi ya Wanahabari

- Mauaji haya yanatekelezwa na vikundi vya uhalifu, viongozi wa kisiasa, na Wafanyabiashara kwa lengo la kuficha uovu wao

Zaidi, soma https://jamii.app/CPJVsImpunity
MAKONDA APIGA MARUFUKU KAMPUNI YA NYANZA KUPEWA MRADI DAR

- RC Makonda aipiga marufuku TANROADS kuipa mradi Kampuni hiyo ya Ujenzi ndani ya mkoa wa Dar

- Ni baada ya Kampuni hiyo kutumia miezi 12 kujenga Barabara ya Km 3.2 ya Kitunda-Kivule

Zaidi, soma https://jamii.app/NyanzaMradiDar
MALI: WANAJESHI 35 WAFARIKI BAADA YA KAMBI YA JESHI KUSHAMBULIWA

- Wameuawa katika shambulio lililotokea jana kwenye Kambi ya Jeshi huko Indelimane

- Al-Qaeda na makundi yanayoshirikiana na kundi la Dola la Kiislamu yanahusishwa na shambulio

Zaidi, soma https://jamii.app/Wanajeshi35Wauawa-Mali
MAONI YA WANANCHI SIKU YA KIMATAIFA YA KUPINGA UKATILI KWA WANAHABARI

- Watanzania wanasema wenye madaraka huwashawishi Polisi wawanyamazishe Wanahabari

- Raia wa Afrika Mashariki wanaunga mkono Uhuru wa Habari kuliko Udhibiti wa Serikali

Soma > https://jamii.app/UhuruHabari

#JFLeo
MAONI YA WANANCHI: Raia wa Tanzania na Kenya wanasema Uhuru wa Vyombo vya Habari ni nyenzo nzuri ya Demokrasia

- Watanzania na Waganda, wanaamini wana haki ya kuwakosoa viongozi wao lakini mara zote wameshindwa kutumia haki hii

Zaidi, soma > https://jamii.app/UhuruHabari
#EndImpunity
AFRIKA KUSINI MABINGWA WA MICHUANO YA DUNIA YA RUGBY

- South Africa imefanikiwa kunyakua taji la Dunia la Rugby kwa kuifunga England katika mchezo wa fainali kwa alama 32-12

- Ni mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 12, Nchi hiyo kuchukua taji hilo
BAKWATA: MAADHIMISHO YA MAULID KUFANYIKA NOVEMBA 09

- BAKWATA imetangaza kuwa Novemba 09, 2019 yatafanyika maadhimisho ya Kitaifa ya Maulid jijini Mwanza

- Baraza la Maulid litafanyika Novemba 10, katika Ukumbi wa Benki Kuu (BOT) Capripoint

Zaidi, soma https://jamii.app/Maulid2019
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: JENGO MOJA LATEKETEA KWA MOTO

- Ghorofa moja lililopo Kariakoo, Mtaa Livingstone na Mkunguni linawaka moto huku chanzo kikiwa hakijajulikana bado

- Kikosi cha Zima Moto na Uokoaji kimeshawasili na juhudi za kuuzima moto zinaendelea

Zaidi, soma https://jamii.app/MotoGhorofaKKoo
MICHEZO: Klabu ya Manchester United ikiwa ugenini katika uwanja wa Vitality imefungwa goli 1-0 na Klabu ya Bournemouth katika mchezo wa Ligi Kuu England, Mzunguko wa 11

- Kwa matokeo hayo, Bournemouth ipo nafasi ya 6 katika msimamo wa Ligi ikiwa na alama 16 huku Manchester United ikiwa nafasi ya 8 na alama 13
WANAHABARI WATANZANIA WALIOFARIKI NA KUPATA MISUKOSUKO WAKIWA KAZINI

- Stanley Katabalo, alikuwa Mwandishi wa Gazeti la Mfanyakazi, aliibua kashfa ya Pori Tengefu la Loliondo

- Yadaiwa, habari hizi zilimgharimu maisha yake

Soma > https://jamii.app/KumbukumbuWanahabari

#EndImpunity
- Daudi Mwangosi, alikuwa Mwandishi wa "Channel Ten', alifariki kwa kulipuliwa na Bomu la Machozi

> Alikuwa Nyololo, Iringa akiripoti kuhusu Mkutano wa CHADEMA

#EndImpunity #JFLeo
- Adam Mwaibabile maarufu 'Mwana' huyu aliwahi kuwekwa rumande na aliyewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Nicodemus Banduka kwa kukutwa na nyaraka za Serikali zenye Muhuri wa 'SIRI'

#EndImpunity #JFLeo