JamiiForums
52.5K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
GUINEA: Serikali ya kijeshi nchini imesitisha kwa miezi mitatu shughuli za vyama vitatu vikubwa vya Siasa, ikiwemo chama cha Rais wa zamani Alpha Condé (RPG), Union of Democratic Forces kinachoongozwa na Waziri Mkuu wa zamani Cellou Dalein Diallo na chama cha Renewal and Progress. Hatua hii imechukuliwa wakati Taifa hilo linajiandaa kwa Kura ya Maoni ya Katiba Septemba 21, 2025.

Wapinzani na Asasi za Kiraia pamoja wametangaza maandamano makubwa kuanzia Septemba 5, 2025 kupinga kile wanachokiita jaribio la kunyakua madaraka. Tangu Doumbouya achukue madaraka Mwaka 2021 kupitia mapinduzi, maandamano yamepigwa marufuku na viongozi wa upinzani wengi wamewekwa kizuizini au kulazimishwa uhamishoni.

Mashirika ya kimataifa ya kutetea Haki za Binadamu yameilaani Guinea kwa hatua hizi, yakionya #Demokrasia changa ya Taifa hilo ipo hatarini.

Zaidi soma https://jamii.app/Guinea

#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Democracy #Governance #JFAfricanPolitics
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MOROGORO: Akizungumza katika Misa Takatifu ya kuombea haki na amani nchini Tanzania, iliyofanyika Agosti 23, 2025 katika Parokia Teule ya Mt. Agnes Nanenane, Jimbo Katoliki Morogoro, Padre Emilius Kobelo amesema Watu wanaodai kura zinaibiwa siyo wendawazimu, kwani huwezi kuzungumzia jambo ambalo halipo.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuwepo haki, amani, utulivu na utengamano nchini ili kuendeleza maendeleo.

Soma zaidi https://jamii.app/PadreKobelo

#JamiiAfrica #JamiiForums #Demokrasia
👍1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MOROGORO: Padre Emilius Kobelo amesisitiza umuhimu wa Kuliombea Taifa na kutambua wajibu katika kulinda haki na amani, akisisitiza anayeharibu amani ya nchi ni Mtanzania na anayevunja haki ya Mtanzania ni Mtanzania.

Ameyasema hayo Agosti 23, 2025 katika Misa Takatifu ya kuombea haki na amani nchini Tanzania, iliyofanyika katika Parokia Teule ya Mt. Agnes Nanenane, Jimbo Katoliki Morogoro.

Zaidi soma https://jamii.app/HakiMtanzania

#JamiiAfrica #JamiiForums #Uwajibikaji #JFMatukio
1👍1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
RUVUMA: Mhashamu Damian Denis Dallu, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Songea ametoa wito kwa Viongozi mbalimbali wanapostaafu waiache Serikali mpya kufanya kazi kwa uhuru kwani inakuwa tayari ina mipango yao.

Ameyasema hayo katika maadhimisho la Misa Takatifu ya Jubile Kuu ya Ukristo ya Waseminari wa Jimbo Kuu Katoliki Songea, iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Kiaskofu la Mtakatifu Matias Mulumba Kalemba Jimbo Kuu Katoliki Songea, Agosti 23, 2025.

Soma https://jamii.app/AskofuDalluWastaafu

#JamiiAfrica #JamiiForums #Governance #JFUtawalaBora
3👍1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa imempitisha aliyekuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Uchaguzi Tanzania (NEC), Dkt. Wilson Mahera Charles kuwa Mgombea Ubunge Jimbo la Butiama katika Uchaguzi Mkuu 2025.

Ikumbukwe, Dkt. Mahera aliteuliwa Oktoba 1, 2019 na Hayati Rais John Pombe Magufuli kuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, baadaye Februari 26, 2023 aliteuliwa na Rais Samia Suluhu kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Soma zaidi https://jamii.app/DktMahera

#JamiiAfrica #JamiiForums  #UchaguziMkuu2025 #Siasa
1
NIGERIA: Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Mamlaka, Agosti 23, 2025, Jeshi la Anga limewaokoa Watu 76 waliokuwa wametekwa nyara, wakiwemo Wanawake na Watoto, baada ya kufanya shambulio la angani kwa usahihi kwenye ngome ya majambazi katika Jimbo la Katsina Kaskazini Magharibi.

Operesheni hiyo ililenga eneo la Pauwa Hill katika Halmashauri ya Kankara kama sehemu ya msako dhidi ya kiongozi wa genge kwa jina la Babaro, anayetuhumiwa kuhusika na shambulio la msikiti Mjini Malumfashi. Wakati wa uokoaji, Mtoto mmoja alipoteza maisha, ingawa haijabainika kama kulikuwa na vifo vingine vya mateka au wanachama wa genge.

Shambulio hilo linaweza kuashiria hatua muhimu katika jitihada za kuvunja mitandao ya uhalifu kaskazini magharibi mwa #Nigeria, ambako makundi yenye silaha yamekuwa yakiwatisha wakazi wa vijijini kwa miaka mingi.

Soma zaidi https://jamii.app/JeshiNigeria

#JamiiAfrica #JamiiForums #Uwajibikaji #HumanRights
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Sheikh Iddi Abdallah Chaurembo amewaombea wale wote wanaopanga kuleta chuki, kutumia mitandao kudhuru au kuhujumu kura, wapate upofu ili wasifanikiwe katika mipango yao.

Ameyasema hayo leo, Agosti 24, 2025, wakati akishiriki Kongamano la Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025, lililoandaliwa na Umoja wa Maimamu Tanzania (#UMATA) na kufanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, kongamano hilo pia limehudhuriwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Zaidi soma https://jamii.app/SheikhChauremboUpofu

#JamiiAfrica #JamiiForums #UchaguziMkuu2025 #Demokrasia
2
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
LINDI: Baadhi ya Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (#CCM) Jimbo la Nachingwea wamerudisha vifaa mbalimbali na kadi za chama huku wakionekana kutoridhishwa na jambo fulani wakati wa kikao kilichohusisha Wananchi mbalimbali.

Akielezea tukio linaloonekana katika video inayosambaa Mtandaoni ikidaiwa limetokea jana Agosti 23, 2025, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Nachingwea, Longinus Nambole amesema “Eneo hilo kuna mgogoro wa muda mrefu wa Wakulima na Wafugaji, hivyo inawezekana Wananchi wametumia nafasi hiyo kufikisha ujumbe kuwa hawaridhishwi na maamuzi ya Viongozi.”

Ameongeza “Unajua CCM ndio chama Tawala hivyo kama chenyewe hakifanyi maamuzi sahihi basi Wananchi wanaonesha hisia zao kwa kwa kukiadhibu Chama, lakini nitafuatilia zaidi kujua kilichotokea.”

Soma zaidi https://jamii.app/Nachingwea

#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #UchaguziMkuu2025 #Demokrasia
2
Wakati Wazazi wao wakiwa ni maarufu kwa makubwa waliyoyafanya kwenye mchezo wa soka, wao wameshindwa kufikia angalau nusu ya mafanikio ya kile ambacho baba zao walikifanya walipokuwa wakicheza.

Enzo Zidane mtoto wa #ZinedineZidane ‘Zizzou’, Romeo Beckham mtoto wa #DavidBeckham na Cristian Totti kijana wa #FrancescoTotti.

Enzo alistaafu kwa sababu aliona hawezi kufika mbali kwenye soka, Romeo sababu Brentford FC haikumpa mkataba mpya kwa kutoridhishwa na kiwango chake wakati Cristian amestaafu kutokana na sababu za kuonekana haoneshi dalili za kufikia mafanikio ya baba yake.

Zaidi soma https://jamii.app/EarlyRetirement

#JFSports #JamiiAfrica #JamiiForums
2
MICHEZO: Wikiendi inaelekea kumalizika, haya ni baadhi ya matokeo katika Ligi na Michuano mbalimbali Duniani.

Ngazi ya klabu, timu kutoka Jiji la Manchester hazijapata ushindi, moja imepigwa nyingine imepata sare, #Arsenal, #Chelsea, #BayernMunich zote zimepata ushindi mnono.

Tembelea JamiiForums.com kushiriki kwenye mijadala mbalimbali inayohusu Soka.

#JFSports #JamiiForums #JFEPL2025 #JamiiAfrica #CHAN2024 #JFBundesliga2025
Mdau wa JamiiForums.com kutoka Jukwaa la Mahusiano, Mapenzi na Urafiki anaomba ushauri kuhusu changamoto ya mahusiano anayopitia, ameeleza kuwa awali aliwahi kuwa kwenye uhusiano wa mapenzi ya dhati, baadaye alisalitiwa hadi mpenzi wake akapata ujauzito wa mwanaume mwingine.

Anasema kwa sasa ana mwenza mpya na uhusiano wao upo vizuri, lakini bado anapata ugumu kuamini masuala ya ndoa, kwani kila akikumbuka yaliyompata huko nyuma moyo wake unakuwa mgumu.

Kushiriki mjadala soma https://jamii.app/KupendaTena

#JamiiForums #JamiiAfrica #JFMahusiano
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Akizungumza leo Agosti 24, 2025 kwa njia ya Mtandao, Mwanasiasa na Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amesema, “Mungu akituvusha, nashauri Sheria irekebishwe ili Viongozi (Rais) wawajibishwe kwa kushtakiwa kwa makosa waliyoyafanya wakiwa madarakani.”

Soma https://jamii.app/PolepoleTumeuzwa

#JamiiAfrica #JamiiForums #Uwajibikaji #Siasa
4👍1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Akizungumza kwa njia ya Mtandao, Agosti 24, 2025, Mwanasiasa na Kada wa CCM, Humphrey Polepole amesema Mfanyabiashara Rostam Aziz ameuziwa Asilimia 70 ya Mgodi wa Makaa ambao ni Mkubwa Afrika Mashariki na Kati kwa kiwango cha Tsh. Bilioni 5 na kwamba ameshalipa Tsh. Bilioni 2.5.

Zaidi soma https://jamii.app/PolepoleMakaa

#JamiiAfrica #JamiiForums #Uwajibikaji #Siasa
3👎2
Kusoma kwa undani habari hizi na mengine yaliyojiri juma lililopita bofya https://jamii.app/YaliyojiriJumaLililopita

#JamiiAfrica #JamiiForums #YaliyojiriJumaLililopita #JFToons
👏2
ARUSHA: Jeshi la Polisi limetoa taarifa kuwa linafanya uchunguzi kuhusiana na tukio la Mtu mmoja aitwaye Bakari Halifa Daud (18) Mkazi wa Sombetini kujeruhiwa kwa kupigwa risasi mguuni na Abdulaziz Abubakari (Dogo Janja).

Kamanda wa Polisi Mkoa, SACP Justine Masejo amesema uchunguzi wa awali umebaini tukio hilo lilitokea Agosti 23, 2025 Saa 5:30 Usiku maeneo ya Sombetini na kwamba Jeshi linawashikilia Watu wawili kuhusiana na tukio hilo huku uchunguzi ukiendelea.

SACP Masejo ameongeza kuwa wakati Abdulaziz Abubakari (30), Mkazi wa Levolosi akiwa anashuka kwenye gari alidai kutaka kuvamiwa na Bakari akiwa na mwenzake kwa kutumia silaha ya jadi hali iliyosababisha kutumia silaha aliyokuwa nayo.

Zaidi https://jamii.app/DogoJanjaKumpigaRisasi

#JamiiAfrica #JamiiForums #HumanRights #Accountability #Uwajibikaji
Mdau ikiwa mwenza uliyeachana nae ameshinda kiasi kikubwa cha fedha unaweza kuamua kurudiana nae au utakaza uendelee na Maisha yako?

Shiriki mjadala huu https://jamii.app/TalakaNaEx

#JamiiForums #JamiiAfrica #JukwaaLaMahusiano #Maisha #JFChitChats
🔥1
Kupitia Jukwaa la Entertainment ndani ya JamiiForums.com Waadau wanajadili kuhusu nyimbo za Kitanzania ambazo zilifanya vizuri ngazi ya Kimataifa kiasi cha kuweza kuutangaza muziki wa Bongo Fleva kwa kiwango kikubwa.

Unadhani ngoma gani kati ya hizi au kama nyingine ilitoboa zaidi Kimataifa?

Shiriki mjadala huu https://jamii.app/HitKimataifa

#JamiiForums #JamiiAfrica #JFBurudani #JFEntertainment #JFBongoFleva
Mwanasaikolojia Nadia Ahmed amesema kuwa kauli za Chuki Mtandaoni huleta madhara mbalimbali ya Kisaikolojia kwa Mtu anayekumbana nazo Mtandaoni na husababisha kuathiri matendo na maamuzi ya muhusika.

Tembelea Jukwaa la JamiiForums.com

#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #KauliZaChuki #StopHateSpeech #DigitalPeace #NoToHateSpeech #ResponsiblePosting #JamiiYenyeUelewa
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR ES SALAAM: Jaji Mkuu wa Tanzania, George Mcheche Masaju akifungua Mkutano wa Tisa wa Kamati ya Utatu kwenye Ukumbi wa PSSSF TOWER - Mawasiliano, leo Agosti 25, 2025 amesema angependelea utaratibu wa Kikokotoo kwa Watumishi wa Serikali Kuu kurudi kama ilivyokuwa zamani.

Jaji Masaju alisema “Haiwezekani mimi nastaafu kisha ndiyo mnaanza kusema sijui nilete hiki, nilete hiki. Taarifa hizi mlikuwa nazo kuanzia mwanzo, kabla ya kustaafu niliwapa taarifa miezi sita kabla. Sisi tungependa Kikokotoo kirudi kwa Watumishi wa Serikali Kuu kama ilivyokuwa.”

Zaidi Soma https://jamii.app/JajiMkuuKikotoo

#JamiiForums #JamiiAfrica #Uwajibikaji #Kikotoo
Mdau wa JamiiForums.com kutoka Jukwaa la Siasa anasema katika kipindi hiki cha Uchaguzi na uteuzi wa Wagombea, Wananchi wameonekana kuwakataa wale Wagombea walioteuliwa na chama husika.

Shiriki Mjadala https://jamii.app/MtuBinafsi

#JamiiForums #Accountability #Misinformation #Disinformation #ElectionInformation2025 #MisDis2025 #TaarifaZaUchaguzi2025