This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Akizungumza Agosti 21, 2025, Naibu Katibu Mkuu wa CHAUMMA, Benson Kigaila amesema Chama kimefanikiwa kuteua wagombea wa Udiwani 3,182 kati ya Kata 3,962 Tanzania Bara, na wagombea hao wanaruhusiwa kuchukua fomu katika Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (#INEC) huku akibainisha kuwa mchakato kwa Kata zilizobaki unaendelea.
Zaidi soma https://jamii.app/WagombeaChaummaUdiwani
#JamiiForums #JamiiAfrica #Siasa #UchaguziMkuu2025 #Governance #UtawalaBora
Zaidi soma https://jamii.app/WagombeaChaummaUdiwani
#JamiiForums #JamiiAfrica #Siasa #UchaguziMkuu2025 #Governance #UtawalaBora
👎1
SOMALIA: Marais watatu wastaafu Sharif Sheikh Ahmed, Abdiqasim Salad Hassan na Mohamed Abdullahi Farmaajo wameungana kutoa tamko dhidi ya Serikali ya Rais Hassan Sheikh Mohamud, wakiilaani kwa uporaji na uuzaji holela wa ardhi ya umma bila kuzingatia taratibu za Kisheria na usimamizi unaostahili.
Viongozi hao wamesema Serikali imekuwa ikihamisha umiliki wa ardhi bila kuhusisha Mamlaka ya Mikataba ya Taifa, na kutoingiza mapato kwenye Hazina ya Taifa. Hali inayosababisha Wananchi maskini wa Mogadishu kufukuzwa na kuondolewa katika makazi yao.
Wametaka Wananchi na Wafanyabiashara kuepuka kununua au kushiriki katika mali zilizopatikana kwa njia zisizo halali, wakisema ni mikataba hatarishi na isiyo na uhalali, hatua ambayo imepongezwa na makundi ya uharakati.
Soma zaidi https://jamii.app/Somalia
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Governance
Viongozi hao wamesema Serikali imekuwa ikihamisha umiliki wa ardhi bila kuhusisha Mamlaka ya Mikataba ya Taifa, na kutoingiza mapato kwenye Hazina ya Taifa. Hali inayosababisha Wananchi maskini wa Mogadishu kufukuzwa na kuondolewa katika makazi yao.
Wametaka Wananchi na Wafanyabiashara kuepuka kununua au kushiriki katika mali zilizopatikana kwa njia zisizo halali, wakisema ni mikataba hatarishi na isiyo na uhalali, hatua ambayo imepongezwa na makundi ya uharakati.
Soma zaidi https://jamii.app/Somalia
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Governance
❤1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mwenyekiti wa Asasi ya Wanafunzi Siasa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Antony Severine amesema mustakabali wa Vijana katika #Siasa unaathiriwa na ilani za vyama, kwani wengi hufuata fursa ili watoboe. Ameeleza nafasi nyingi zinazotolewa nchini haziangalii uwezo wa Vijana bali zinawapendelea wale waliopo ndani ya vyama.
Alisema hayo Agosti 21, 2025 katika mahojiano ya Kipindi cha Malumbano na Hoja cha ITV.
Soma zaidi https://jamii.app/VijanaSiasa
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #UchaguziMkuu2025 #Democracy
Alisema hayo Agosti 21, 2025 katika mahojiano ya Kipindi cha Malumbano na Hoja cha ITV.
Soma zaidi https://jamii.app/VijanaSiasa
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #UchaguziMkuu2025 #Democracy
👍3❤2
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Akizungumza kwa njia ya Mtandao, Susan Lyimo ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (#BAZECHA), amesema Uchaguzi Mkuu wa 2025, ukifanyika kwa Sheria na Kanuni zilizopo, utakosa mvuto wa Kitaifa na Kimataifa kutokana na madhila kwa Vyama vya Upinzani, hususan CHADEMA.
Amesema hayo leo Agosti 22, 2025, ambapo ameongeza kuwa, "BAZECHA tunawataka watawala kusikiliza matakwa ya Watanzania na kufanya mabadiliko ya Kikanuni na Kisheria ili Taifa liingie kwenye Uchaguzi Huru na wa haki."
Soma zaidi https://jamii.app/SuzanUhalali
#JamiiForums #JamiiAfrica #Demokrasia #Siasa #UchaguziMkuu2025
Amesema hayo leo Agosti 22, 2025, ambapo ameongeza kuwa, "BAZECHA tunawataka watawala kusikiliza matakwa ya Watanzania na kufanya mabadiliko ya Kikanuni na Kisheria ili Taifa liingie kwenye Uchaguzi Huru na wa haki."
Soma zaidi https://jamii.app/SuzanUhalali
#JamiiForums #JamiiAfrica #Demokrasia #Siasa #UchaguziMkuu2025
❤1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mkuu wa Mkoa, Albert Chalamila ametoa kiasi cha Tsh. 20 Milioni na Viwanja viwili Kigamboni kwa Wachezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania (#TaifaStars) ikiwa ni sehemu ya motisha kuelekea mchezo wa Robo Fainali dhidi ya Morocco katika Michuano ya CHAN, unaotarajiwa kuchezwa leo Agosti 22, 2025, kuanzia Saa 2:00 Usiku kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa.
RC Chalamila amesema fedha hizo zitakabidhiwa kwa wachezaji bila kujali matokeo ya mchezo huo.
Zaidi soma https://jamii.app/ChalamilaAmwagaPesa
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFSports
RC Chalamila amesema fedha hizo zitakabidhiwa kwa wachezaji bila kujali matokeo ya mchezo huo.
Zaidi soma https://jamii.app/ChalamilaAmwagaPesa
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFSports
❤1
Mwanamitindo na Mtangazaji, Ney Paul ameshauri Vijana kufikiria kabla ya 'kuposti' kauli za Chuki Mtandaoni kwa kujiuliza kama wanajenga au wanabomoa wangejisikiaje iwapo Mtu mwingine angetumia kauli hiyo kwao.
Amesema “Epuka jazba, Usijibu kwa hasira Chukua muda kupumua na kufikiri kabla ya kujibu maoni au jumbe zinazokukasirisha”.
Aidha, amesema Mitandao imebeba fursa nyingi na fedha nyingi, hivyo ni vizuri kama Vijana wataamua kuitumia vizuri.
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #KauliZaChuki #StopHateSpeech #DigitalPeace #NoToHateSpeech #ResponsiblePosting #JamiiYenyeUelewa
Amesema “Epuka jazba, Usijibu kwa hasira Chukua muda kupumua na kufikiri kabla ya kujibu maoni au jumbe zinazokukasirisha”.
Aidha, amesema Mitandao imebeba fursa nyingi na fedha nyingi, hivyo ni vizuri kama Vijana wataamua kuitumia vizuri.
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #KauliZaChuki #StopHateSpeech #DigitalPeace #NoToHateSpeech #ResponsiblePosting #JamiiYenyeUelewa
KENYA: Safari ya Timu ya Taifa ya #Kenya imekwama kuingia Nusu Fainali ya Michuano ya Afrika kwa Wachezaji wa Ligi ya Ndani (#CHAN) baada ya kufungwa na Madagascar kwa penati 4-3, muda mfupi baada ya matokeo ya sare ya Goli 1-1 katika dakika 120.
Mchezo huo umepigwa kwenye Uwanja wa Moi International Sports Centre Jijini Nairobi leo Agosti 22, 2025.
Michezo ya Robo Fainali ya Agosti 23, 2025 itakuwa ni Uganda dhidi ya Senegal (Uwanja wa Mandela National, Kampala), Sudan wakikipiga na Algeria (Uwanja wa Amaan, Zanzibar)
https://jamii.app/CHANRobo
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFSports #CHAN2024
Mchezo huo umepigwa kwenye Uwanja wa Moi International Sports Centre Jijini Nairobi leo Agosti 22, 2025.
Michezo ya Robo Fainali ya Agosti 23, 2025 itakuwa ni Uganda dhidi ya Senegal (Uwanja wa Mandela National, Kampala), Sudan wakikipiga na Algeria (Uwanja wa Amaan, Zanzibar)
https://jamii.app/CHANRobo
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFSports #CHAN2024
❤2
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (#JAB), Wakili Patrick Kipangula ametoa angalizo kwa Waandishi wa Habari wasiokuwa na ithibati, kuwa hawataruhusiwa kuripoti Uchaguzi Mkuu 2025.
Amefafanua kuwa Mwandishi kufanya kazi bila kitambulisho cha Bodi ya Ithibati ni kosa linaloweza kusababisha faini ya hadi Tsh. Milioni 5 au kifungo cha miaka mitatu hadi mitano. Ameeleza hayo wakati wa Mkutano wa Wadau wa Habari na Utangazaji Kanda ya Mashariki, Agosti 21, 2025.
Zaidi soma https://jamii.app/JABWaandishiUchaguzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFUwajibikaji #Accountability #JFSiasa
Amefafanua kuwa Mwandishi kufanya kazi bila kitambulisho cha Bodi ya Ithibati ni kosa linaloweza kusababisha faini ya hadi Tsh. Milioni 5 au kifungo cha miaka mitatu hadi mitano. Ameeleza hayo wakati wa Mkutano wa Wadau wa Habari na Utangazaji Kanda ya Mashariki, Agosti 21, 2025.
Zaidi soma https://jamii.app/JABWaandishiUchaguzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFUwajibikaji #Accountability #JFSiasa
DAR: Chama cha Demokrasia na Maendeleo (#CHADEMA) kimetoa wito kwa Watanzania kushiriki kikamilifu katika maombi ya Novena Takatifu yanayoratibiwa na Kanisa Katoliki kufikia kilele cha maombi hayo Agosti 23, 2025, kwa ajili ya kuliombea taifa amani, haki na mshikamano wa kitaifa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na chama hicho , John Heche amesisitiza umuhimu wa maombi hayo akisema: “Ninawasihi tuliombee taifa letu liwekwe mikononi mwa Mungu, tukimwomba atujalie hekima, ujasiri wa kudai haki, na mabadiliko ya msingi kwa mustakabali wa taifa letu. Pia tuliombee amani ya kweli itakayojengwa juu ya haki na umoja wa wananchi bila kujali dini au itikadi.”
Ikumbukwe, Juni 19, 2025, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (#TEC) lilitangaza maombi ya kitaifa na mfungo kuombea haki na amani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025.
Zaidi soma https://jamii.app/KatolikiChademaMaombi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFMatukio #UchaguziMkuu2025
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na chama hicho , John Heche amesisitiza umuhimu wa maombi hayo akisema: “Ninawasihi tuliombee taifa letu liwekwe mikononi mwa Mungu, tukimwomba atujalie hekima, ujasiri wa kudai haki, na mabadiliko ya msingi kwa mustakabali wa taifa letu. Pia tuliombee amani ya kweli itakayojengwa juu ya haki na umoja wa wananchi bila kujali dini au itikadi.”
Ikumbukwe, Juni 19, 2025, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (#TEC) lilitangaza maombi ya kitaifa na mfungo kuombea haki na amani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025.
Zaidi soma https://jamii.app/KatolikiChademaMaombi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFMatukio #UchaguziMkuu2025
❤1
DAR: Timu ya Taifa ya Tanzania (#TaifaStars) imeondolewa katika Michuano ya Afrika kwa Wachezaji wa Ligi ya Ndani (#CHAN2024) kwa kufungwa Goli 1-0 dhidi ya Morocco kwenye Uwanja wa Mkapa, mfungaji akiwa ni Oussama Lamlioui.
Hivyo, Morocco inatarajiwa kucheza na timu itakayoshinda kati ya Uganda dhidi ya Senegal. Wakati huohuo Madagascar ambayo imeiondoa Kenya, yenyewe itacheza na mshindi wa mchezo wa Sudan dhidi ya Algeria.
Michezo mingine ya Robo Fainali inatarajiwa kuchezwa Agosti 23, 2025, itakuwa ni Uganda Vs Senegal (Uwanja wa Mandela National, Kampala), Sudan Vs Algeria (Uwanja wa Amaan, Zanzibar)
Zaidi soma https://jamii.app/CHANRobo
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFSports #CHAN2024
Hivyo, Morocco inatarajiwa kucheza na timu itakayoshinda kati ya Uganda dhidi ya Senegal. Wakati huohuo Madagascar ambayo imeiondoa Kenya, yenyewe itacheza na mshindi wa mchezo wa Sudan dhidi ya Algeria.
Michezo mingine ya Robo Fainali inatarajiwa kuchezwa Agosti 23, 2025, itakuwa ni Uganda Vs Senegal (Uwanja wa Mandela National, Kampala), Sudan Vs Algeria (Uwanja wa Amaan, Zanzibar)
Zaidi soma https://jamii.app/CHANRobo
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFSports #CHAN2024
❤1👍1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
JF KUMBUKIZI: Akizungumza siku ya Mei Mosi, 1995, katika hotuba yake Mwl. Julius Kambarage #Nyerere alisema kuwa mwenye akili akikupa mawazo ya kipumbavu, ukayakubali, anakudharau.
"Na wewe una akili, anajua unajua kwamba ni ya kipumbavu, ukayakubali, anakudharau."
Zaidi Soma https://jamii.app/MawazoKipumbavu
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Siasa #JFKumbukizi #AmkaNaJamiiAfrica #GoodMorning
"Na wewe una akili, anajua unajua kwamba ni ya kipumbavu, ukayakubali, anakudharau."
Zaidi Soma https://jamii.app/MawazoKipumbavu
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Siasa #JFKumbukizi #AmkaNaJamiiAfrica #GoodMorning
❤5
Serikali ya Uganda imethibitisha kuwa imeingia makubaliano na Marekani yatakayohusisha Wahamiaji kutoka Marekani kupokelewa nchini humo, ikiwa ni sehemu ya mpango wa #DonaldTrump unaolenga kuwarudisha maelfu ya Wahamiaji walioko katika hifadhi za Marekani.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Uganda imesema wapo tayari kupokea Wahamiaji hao na kudokeza kuwa itawapa kipaumbele zaidi wale ambao wana asili ya Kiafrika na ambao hawana rekodi yoyote ya Uhalifu.
Kando na Uganda nchi nyingine kutoka Afrika ambazo zimekubali kupokea wahamiaji kutokea Marekani ni Eswatini, Rwanda pamoja na Sudan ya Kusini.
Zaidi Soma: https://jamii.app/WahamiajiUganda
#JamiiAfrica #JamiiForums #HakiZaBinadamu #Utawala
Wizara ya Mambo ya Nje ya Uganda imesema wapo tayari kupokea Wahamiaji hao na kudokeza kuwa itawapa kipaumbele zaidi wale ambao wana asili ya Kiafrika na ambao hawana rekodi yoyote ya Uhalifu.
Kando na Uganda nchi nyingine kutoka Afrika ambazo zimekubali kupokea wahamiaji kutokea Marekani ni Eswatini, Rwanda pamoja na Sudan ya Kusini.
Zaidi Soma: https://jamii.app/WahamiajiUganda
#JamiiAfrica #JamiiForums #HakiZaBinadamu #Utawala
❤1
KIGOMA: Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa imewahukumu kifungo cha Miaka 22 jela aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji, Athuman Msabila pamoja na Watumishi wenzake watatu baada ya kupatikana na hatia ya makosa ya kughushi nyaraka na utakatishaji fedha.
Msabila na Salum Juma wamehukumiwa Miaka 20 kwa utakatishaji fedha na Miaka miwili kwa kughushi nyaraka, huku Ferdinand Filimbi na Frank Nguvumali wakihukumiwa miaka miwili kwa kosa la kughushi nyaraka.
Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi wa Mkoa, Misana Majula katika kesi ya Jinai Namba 5546 ya Mwaka 2024 iliyowakabili Watumishi 11 wa Serikali.
Zaidi Soma https://jamii.app/KigomaJela
#JamiiAfrica #JamiiForums #HakiZaBinadamu #Sheria #Uwajibikaji
Msabila na Salum Juma wamehukumiwa Miaka 20 kwa utakatishaji fedha na Miaka miwili kwa kughushi nyaraka, huku Ferdinand Filimbi na Frank Nguvumali wakihukumiwa miaka miwili kwa kosa la kughushi nyaraka.
Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi wa Mkoa, Misana Majula katika kesi ya Jinai Namba 5546 ya Mwaka 2024 iliyowakabili Watumishi 11 wa Serikali.
Zaidi Soma https://jamii.app/KigomaJela
#JamiiAfrica #JamiiForums #HakiZaBinadamu #Sheria #Uwajibikaji
ZIMBABWE: Mfungwa anayefahamika kwa jina la Emmanuel Mugede, ambaye tayari alikuwa akitumikia kifungo cha miaka 14 kwa ubakaji wa mtoto, amehukumiwa miaka 20 zaidi gerezani kwa kumlawiti mfungwa mwenzake mwenye umri wa miaka 24 Julai 23, 2025 katika gereza kuu la Harare.
Tukio hilo lilishuhudiwa na wafungwa wengine, Tinashe Muyambo na Antony Chambarambanda, ambao walidai kumwona Mugede akiingia bafuni na kushuhudia kumfanyia mfungwa mwenzao kitendo hicho, Hatimaye, taarifa iliripotiwa kwa afisa wa gereza na polisi.
Aidha, Hakimu Letwin Rwodzia amemuongezea hukumu Emmanuel, huku akisisitiza kuwa mashambulizi ya kijinsia yenye ukatili hayakubaliki hata ikiwa ni gerezani.
Zaidi https://jamii.app/KubakaGerezani
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #CivilRights
Tukio hilo lilishuhudiwa na wafungwa wengine, Tinashe Muyambo na Antony Chambarambanda, ambao walidai kumwona Mugede akiingia bafuni na kushuhudia kumfanyia mfungwa mwenzao kitendo hicho, Hatimaye, taarifa iliripotiwa kwa afisa wa gereza na polisi.
Aidha, Hakimu Letwin Rwodzia amemuongezea hukumu Emmanuel, huku akisisitiza kuwa mashambulizi ya kijinsia yenye ukatili hayakubaliki hata ikiwa ni gerezani.
Zaidi https://jamii.app/KubakaGerezani
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #CivilRights
Mdau wa JamiiForums.com kupitia Jukwaa la JF Chit-Chats and Jokes anauliza umewahi kusahau kitu nyumbani kikakulazimisha kurudi haraka, kwa sababu bila hicho huwezi kuendelea na kazi zako ofisini au katika shughuli zako nyingine?
Ni kitu gani hicho bila kuwa nacho huwezi kufanya kazi zako kwa amani?
Zaidi https://jamii.app/NyumbaniKitu
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFChitChats #JFUtani
Ni kitu gani hicho bila kuwa nacho huwezi kufanya kazi zako kwa amani?
Zaidi https://jamii.app/NyumbaniKitu
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFChitChats #JFUtani
Serikali ya Nigeria imewafukuza raia wa kigeni wakiwemo Wachina 50 baada ya msako mkali uliofanyika Jijini Lagos, ambapo jumla ya raia wa kigeni 192 walikamatwa huku 148 wakiwa ni raia wa China wakihusishwa na makosa ya udanganyifu na uwizi Mtandaoni.
Kwa mujibu wa Taarifa ya Taasisi ya Kupambana na Ufisadi nchini humo (EFCC) imeeleza tangu operesheni hiyo ilipoanza Agosti 15, 2025 jumla ya Wageni 102 wameshafukuzwa ikiwa ni sehemu ya mpango wa Serikali ya Nigeria wa kukomesha uhalifu wa kimtandao.
Kulingana na takwimu za Mwaka 2024 za Chuo cha Oxford, Nigeria iko kwenye orodha ya nchi 5 zinazoongoza kwa uhalifu Mtandaoni, ikizidiwa na Urusi, Ukraine, Marekani na China.
Zaidi https://jamii.app/WachinaNigeria
#JamiiForums #JamiiAfrica #CyberCrimes #DigitalFrauds
Kwa mujibu wa Taarifa ya Taasisi ya Kupambana na Ufisadi nchini humo (EFCC) imeeleza tangu operesheni hiyo ilipoanza Agosti 15, 2025 jumla ya Wageni 102 wameshafukuzwa ikiwa ni sehemu ya mpango wa Serikali ya Nigeria wa kukomesha uhalifu wa kimtandao.
Kulingana na takwimu za Mwaka 2024 za Chuo cha Oxford, Nigeria iko kwenye orodha ya nchi 5 zinazoongoza kwa uhalifu Mtandaoni, ikizidiwa na Urusi, Ukraine, Marekani na China.
Zaidi https://jamii.app/WachinaNigeria
#JamiiForums #JamiiAfrica #CyberCrimes #DigitalFrauds