This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (#JAB), Wakili Patrick Kipangula ametoa angalizo kwa Waandishi wa Habari wasiokuwa na ithibati, kuwa hawataruhusiwa kuripoti Uchaguzi Mkuu 2025.
Amefafanua kuwa Mwandishi kufanya kazi bila kitambulisho cha Bodi ya Ithibati ni kosa linaloweza kusababisha faini ya hadi Tsh. Milioni 5 au kifungo cha miaka mitatu hadi mitano. Ameeleza hayo wakati wa Mkutano wa Wadau wa Habari na Utangazaji Kanda ya Mashariki, Agosti 21, 2025.
Zaidi soma https://jamii.app/JABWaandishiUchaguzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFUwajibikaji #Accountability #JFSiasa
Amefafanua kuwa Mwandishi kufanya kazi bila kitambulisho cha Bodi ya Ithibati ni kosa linaloweza kusababisha faini ya hadi Tsh. Milioni 5 au kifungo cha miaka mitatu hadi mitano. Ameeleza hayo wakati wa Mkutano wa Wadau wa Habari na Utangazaji Kanda ya Mashariki, Agosti 21, 2025.
Zaidi soma https://jamii.app/JABWaandishiUchaguzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFUwajibikaji #Accountability #JFSiasa
DAR: Chama cha Demokrasia na Maendeleo (#CHADEMA) kimetoa wito kwa Watanzania kushiriki kikamilifu katika maombi ya Novena Takatifu yanayoratibiwa na Kanisa Katoliki kufikia kilele cha maombi hayo Agosti 23, 2025, kwa ajili ya kuliombea taifa amani, haki na mshikamano wa kitaifa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na chama hicho , John Heche amesisitiza umuhimu wa maombi hayo akisema: “Ninawasihi tuliombee taifa letu liwekwe mikononi mwa Mungu, tukimwomba atujalie hekima, ujasiri wa kudai haki, na mabadiliko ya msingi kwa mustakabali wa taifa letu. Pia tuliombee amani ya kweli itakayojengwa juu ya haki na umoja wa wananchi bila kujali dini au itikadi.”
Ikumbukwe, Juni 19, 2025, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (#TEC) lilitangaza maombi ya kitaifa na mfungo kuombea haki na amani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025.
Zaidi soma https://jamii.app/KatolikiChademaMaombi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFMatukio #UchaguziMkuu2025
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na chama hicho , John Heche amesisitiza umuhimu wa maombi hayo akisema: “Ninawasihi tuliombee taifa letu liwekwe mikononi mwa Mungu, tukimwomba atujalie hekima, ujasiri wa kudai haki, na mabadiliko ya msingi kwa mustakabali wa taifa letu. Pia tuliombee amani ya kweli itakayojengwa juu ya haki na umoja wa wananchi bila kujali dini au itikadi.”
Ikumbukwe, Juni 19, 2025, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (#TEC) lilitangaza maombi ya kitaifa na mfungo kuombea haki na amani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025.
Zaidi soma https://jamii.app/KatolikiChademaMaombi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFMatukio #UchaguziMkuu2025
❤1
DAR: Timu ya Taifa ya Tanzania (#TaifaStars) imeondolewa katika Michuano ya Afrika kwa Wachezaji wa Ligi ya Ndani (#CHAN2024) kwa kufungwa Goli 1-0 dhidi ya Morocco kwenye Uwanja wa Mkapa, mfungaji akiwa ni Oussama Lamlioui.
Hivyo, Morocco inatarajiwa kucheza na timu itakayoshinda kati ya Uganda dhidi ya Senegal. Wakati huohuo Madagascar ambayo imeiondoa Kenya, yenyewe itacheza na mshindi wa mchezo wa Sudan dhidi ya Algeria.
Michezo mingine ya Robo Fainali inatarajiwa kuchezwa Agosti 23, 2025, itakuwa ni Uganda Vs Senegal (Uwanja wa Mandela National, Kampala), Sudan Vs Algeria (Uwanja wa Amaan, Zanzibar)
Zaidi soma https://jamii.app/CHANRobo
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFSports #CHAN2024
Hivyo, Morocco inatarajiwa kucheza na timu itakayoshinda kati ya Uganda dhidi ya Senegal. Wakati huohuo Madagascar ambayo imeiondoa Kenya, yenyewe itacheza na mshindi wa mchezo wa Sudan dhidi ya Algeria.
Michezo mingine ya Robo Fainali inatarajiwa kuchezwa Agosti 23, 2025, itakuwa ni Uganda Vs Senegal (Uwanja wa Mandela National, Kampala), Sudan Vs Algeria (Uwanja wa Amaan, Zanzibar)
Zaidi soma https://jamii.app/CHANRobo
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFSports #CHAN2024
❤1👍1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
JF KUMBUKIZI: Akizungumza siku ya Mei Mosi, 1995, katika hotuba yake Mwl. Julius Kambarage #Nyerere alisema kuwa mwenye akili akikupa mawazo ya kipumbavu, ukayakubali, anakudharau.
"Na wewe una akili, anajua unajua kwamba ni ya kipumbavu, ukayakubali, anakudharau."
Zaidi Soma https://jamii.app/MawazoKipumbavu
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Siasa #JFKumbukizi #AmkaNaJamiiAfrica #GoodMorning
"Na wewe una akili, anajua unajua kwamba ni ya kipumbavu, ukayakubali, anakudharau."
Zaidi Soma https://jamii.app/MawazoKipumbavu
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Siasa #JFKumbukizi #AmkaNaJamiiAfrica #GoodMorning
❤5
Serikali ya Uganda imethibitisha kuwa imeingia makubaliano na Marekani yatakayohusisha Wahamiaji kutoka Marekani kupokelewa nchini humo, ikiwa ni sehemu ya mpango wa #DonaldTrump unaolenga kuwarudisha maelfu ya Wahamiaji walioko katika hifadhi za Marekani.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Uganda imesema wapo tayari kupokea Wahamiaji hao na kudokeza kuwa itawapa kipaumbele zaidi wale ambao wana asili ya Kiafrika na ambao hawana rekodi yoyote ya Uhalifu.
Kando na Uganda nchi nyingine kutoka Afrika ambazo zimekubali kupokea wahamiaji kutokea Marekani ni Eswatini, Rwanda pamoja na Sudan ya Kusini.
Zaidi Soma: https://jamii.app/WahamiajiUganda
#JamiiAfrica #JamiiForums #HakiZaBinadamu #Utawala
Wizara ya Mambo ya Nje ya Uganda imesema wapo tayari kupokea Wahamiaji hao na kudokeza kuwa itawapa kipaumbele zaidi wale ambao wana asili ya Kiafrika na ambao hawana rekodi yoyote ya Uhalifu.
Kando na Uganda nchi nyingine kutoka Afrika ambazo zimekubali kupokea wahamiaji kutokea Marekani ni Eswatini, Rwanda pamoja na Sudan ya Kusini.
Zaidi Soma: https://jamii.app/WahamiajiUganda
#JamiiAfrica #JamiiForums #HakiZaBinadamu #Utawala
❤2
KIGOMA: Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa imewahukumu kifungo cha Miaka 22 jela aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji, Athuman Msabila pamoja na Watumishi wenzake watatu baada ya kupatikana na hatia ya makosa ya kughushi nyaraka na utakatishaji fedha.
Msabila na Salum Juma wamehukumiwa Miaka 20 kwa utakatishaji fedha na Miaka miwili kwa kughushi nyaraka, huku Ferdinand Filimbi na Frank Nguvumali wakihukumiwa miaka miwili kwa kosa la kughushi nyaraka.
Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi wa Mkoa, Misana Majula katika kesi ya Jinai Namba 5546 ya Mwaka 2024 iliyowakabili Watumishi 11 wa Serikali.
Zaidi Soma https://jamii.app/KigomaJela
#JamiiAfrica #JamiiForums #HakiZaBinadamu #Sheria #Uwajibikaji
Msabila na Salum Juma wamehukumiwa Miaka 20 kwa utakatishaji fedha na Miaka miwili kwa kughushi nyaraka, huku Ferdinand Filimbi na Frank Nguvumali wakihukumiwa miaka miwili kwa kosa la kughushi nyaraka.
Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi wa Mkoa, Misana Majula katika kesi ya Jinai Namba 5546 ya Mwaka 2024 iliyowakabili Watumishi 11 wa Serikali.
Zaidi Soma https://jamii.app/KigomaJela
#JamiiAfrica #JamiiForums #HakiZaBinadamu #Sheria #Uwajibikaji
ZIMBABWE: Mfungwa anayefahamika kwa jina la Emmanuel Mugede, ambaye tayari alikuwa akitumikia kifungo cha miaka 14 kwa ubakaji wa mtoto, amehukumiwa miaka 20 zaidi gerezani kwa kumlawiti mfungwa mwenzake mwenye umri wa miaka 24 Julai 23, 2025 katika gereza kuu la Harare.
Tukio hilo lilishuhudiwa na wafungwa wengine, Tinashe Muyambo na Antony Chambarambanda, ambao walidai kumwona Mugede akiingia bafuni na kushuhudia kumfanyia mfungwa mwenzao kitendo hicho, Hatimaye, taarifa iliripotiwa kwa afisa wa gereza na polisi.
Aidha, Hakimu Letwin Rwodzia amemuongezea hukumu Emmanuel, huku akisisitiza kuwa mashambulizi ya kijinsia yenye ukatili hayakubaliki hata ikiwa ni gerezani.
Zaidi https://jamii.app/KubakaGerezani
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #CivilRights
Tukio hilo lilishuhudiwa na wafungwa wengine, Tinashe Muyambo na Antony Chambarambanda, ambao walidai kumwona Mugede akiingia bafuni na kushuhudia kumfanyia mfungwa mwenzao kitendo hicho, Hatimaye, taarifa iliripotiwa kwa afisa wa gereza na polisi.
Aidha, Hakimu Letwin Rwodzia amemuongezea hukumu Emmanuel, huku akisisitiza kuwa mashambulizi ya kijinsia yenye ukatili hayakubaliki hata ikiwa ni gerezani.
Zaidi https://jamii.app/KubakaGerezani
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #CivilRights
Mdau wa JamiiForums.com kupitia Jukwaa la JF Chit-Chats and Jokes anauliza umewahi kusahau kitu nyumbani kikakulazimisha kurudi haraka, kwa sababu bila hicho huwezi kuendelea na kazi zako ofisini au katika shughuli zako nyingine?
Ni kitu gani hicho bila kuwa nacho huwezi kufanya kazi zako kwa amani?
Zaidi https://jamii.app/NyumbaniKitu
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFChitChats #JFUtani
Ni kitu gani hicho bila kuwa nacho huwezi kufanya kazi zako kwa amani?
Zaidi https://jamii.app/NyumbaniKitu
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFChitChats #JFUtani
Serikali ya Nigeria imewafukuza raia wa kigeni wakiwemo Wachina 50 baada ya msako mkali uliofanyika Jijini Lagos, ambapo jumla ya raia wa kigeni 192 walikamatwa huku 148 wakiwa ni raia wa China wakihusishwa na makosa ya udanganyifu na uwizi Mtandaoni.
Kwa mujibu wa Taarifa ya Taasisi ya Kupambana na Ufisadi nchini humo (EFCC) imeeleza tangu operesheni hiyo ilipoanza Agosti 15, 2025 jumla ya Wageni 102 wameshafukuzwa ikiwa ni sehemu ya mpango wa Serikali ya Nigeria wa kukomesha uhalifu wa kimtandao.
Kulingana na takwimu za Mwaka 2024 za Chuo cha Oxford, Nigeria iko kwenye orodha ya nchi 5 zinazoongoza kwa uhalifu Mtandaoni, ikizidiwa na Urusi, Ukraine, Marekani na China.
Zaidi https://jamii.app/WachinaNigeria
#JamiiForums #JamiiAfrica #CyberCrimes #DigitalFrauds
Kwa mujibu wa Taarifa ya Taasisi ya Kupambana na Ufisadi nchini humo (EFCC) imeeleza tangu operesheni hiyo ilipoanza Agosti 15, 2025 jumla ya Wageni 102 wameshafukuzwa ikiwa ni sehemu ya mpango wa Serikali ya Nigeria wa kukomesha uhalifu wa kimtandao.
Kulingana na takwimu za Mwaka 2024 za Chuo cha Oxford, Nigeria iko kwenye orodha ya nchi 5 zinazoongoza kwa uhalifu Mtandaoni, ikizidiwa na Urusi, Ukraine, Marekani na China.
Zaidi https://jamii.app/WachinaNigeria
#JamiiForums #JamiiAfrica #CyberCrimes #DigitalFrauds
❤3
Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (#CCM) Taifa imetangaza mabadiliko katika safu yake ya Uongozi, ambapo imemteua Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Kenani Kihongosi kuwa Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, nafasi iliyokuwa ikishikiliwa na Amos Makalla ambaye ameteuliwa na Rais Samia kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
Aidha, Dkt. Asha-Rose Migiro ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM akichukua nafasi ya Dkt. Emmanuel John Nchimbi ambaye chama kimempitisha kuwa Mgombea Mwenza wa Dkt. Samia Suluhu katika Uchaguzi Mkuu wa 2025.
Soma Zaidi: https://jamii.app/MigiroKatibuCCM
#JamiiForums #JamiiAfrica #Uteuzi #Siasa
Aidha, Dkt. Asha-Rose Migiro ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM akichukua nafasi ya Dkt. Emmanuel John Nchimbi ambaye chama kimempitisha kuwa Mgombea Mwenza wa Dkt. Samia Suluhu katika Uchaguzi Mkuu wa 2025.
Soma Zaidi: https://jamii.app/MigiroKatibuCCM
#JamiiForums #JamiiAfrica #Uteuzi #Siasa
❤1👍1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (#CCM) Taifa, imemteua Tauhida Gallos kuwa Mbunge wa Viti Maalum katika Mkoa wa Mjini Magharibi.
Tauhida aliingia bungeni akiwa Ubunge wa Viti Maalum Mwaka 2020 akiwakilisha Mkoa wa Mjini Magharibi Visiwani Zanzibar.
Zaidi Soma https://jamii.app/MigiroKatibuCCM
#JamiiForums #JamiiAfrica #Uteuzi #Siasa
Tauhida aliingia bungeni akiwa Ubunge wa Viti Maalum Mwaka 2020 akiwakilisha Mkoa wa Mjini Magharibi Visiwani Zanzibar.
Zaidi Soma https://jamii.app/MigiroKatibuCCM
#JamiiForums #JamiiAfrica #Uteuzi #Siasa
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
JFKUMBUKIZI: Nape Nnauye alipokuwa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wakati akizungumza na Wananchi Julai, 2024 katika Soko la Kashai Mjini Bukoba alisema aliyekuwa Mbunge Stephen Byabato atashinda uchaguzi ujao, akibainisha matokeo ya kura si lazima yatokane na yaliyomo kwenye maboksi ya kura bali yanategemea anayehesabu na kutangaza.
Nape kwa sasa ni Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mtama ambapo atawania nafasi hiyo kupitia CCM katika Uchaguzi Mkuu wa 2025
Soma https://jamii.app/NapeUchaguzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFKumbukizi #Democracy #JFDemocracy #Demokrasia
Nape kwa sasa ni Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mtama ambapo atawania nafasi hiyo kupitia CCM katika Uchaguzi Mkuu wa 2025
Soma https://jamii.app/NapeUchaguzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFKumbukizi #Democracy #JFDemocracy #Demokrasia
Mdau, umepata funzo gani kupitia picha hii?
Tembelea JamiiForums.com kushiriki kwenye mijadala mbalimbali yenye tija.
#JamiiForums #JamiiAfrica #AmkaNaJamiiAfrica #GoodMorning
Tembelea JamiiForums.com kushiriki kwenye mijadala mbalimbali yenye tija.
#JamiiForums #JamiiAfrica #AmkaNaJamiiAfrica #GoodMorning
❤1
GUINEA: Serikali ya kijeshi nchini imesitisha kwa miezi mitatu shughuli za vyama vitatu vikubwa vya Siasa, ikiwemo chama cha Rais wa zamani Alpha Condé (RPG), Union of Democratic Forces kinachoongozwa na Waziri Mkuu wa zamani Cellou Dalein Diallo na chama cha Renewal and Progress. Hatua hii imechukuliwa wakati Taifa hilo linajiandaa kwa Kura ya Maoni ya Katiba Septemba 21, 2025.
Wapinzani na Asasi za Kiraia pamoja wametangaza maandamano makubwa kuanzia Septemba 5, 2025 kupinga kile wanachokiita jaribio la kunyakua madaraka. Tangu Doumbouya achukue madaraka Mwaka 2021 kupitia mapinduzi, maandamano yamepigwa marufuku na viongozi wa upinzani wengi wamewekwa kizuizini au kulazimishwa uhamishoni.
Mashirika ya kimataifa ya kutetea Haki za Binadamu yameilaani Guinea kwa hatua hizi, yakionya #Demokrasia changa ya Taifa hilo ipo hatarini.
Zaidi soma https://jamii.app/Guinea
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Democracy #Governance #JFAfricanPolitics
Wapinzani na Asasi za Kiraia pamoja wametangaza maandamano makubwa kuanzia Septemba 5, 2025 kupinga kile wanachokiita jaribio la kunyakua madaraka. Tangu Doumbouya achukue madaraka Mwaka 2021 kupitia mapinduzi, maandamano yamepigwa marufuku na viongozi wa upinzani wengi wamewekwa kizuizini au kulazimishwa uhamishoni.
Mashirika ya kimataifa ya kutetea Haki za Binadamu yameilaani Guinea kwa hatua hizi, yakionya #Demokrasia changa ya Taifa hilo ipo hatarini.
Zaidi soma https://jamii.app/Guinea
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Democracy #Governance #JFAfricanPolitics
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MOROGORO: Akizungumza katika Misa Takatifu ya kuombea haki na amani nchini Tanzania, iliyofanyika Agosti 23, 2025 katika Parokia Teule ya Mt. Agnes Nanenane, Jimbo Katoliki Morogoro, Padre Emilius Kobelo amesema Watu wanaodai kura zinaibiwa siyo wendawazimu, kwani huwezi kuzungumzia jambo ambalo halipo.
Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuwepo haki, amani, utulivu na utengamano nchini ili kuendeleza maendeleo.
Soma zaidi https://jamii.app/PadreKobelo
#JamiiAfrica #JamiiForums #Demokrasia
Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuwepo haki, amani, utulivu na utengamano nchini ili kuendeleza maendeleo.
Soma zaidi https://jamii.app/PadreKobelo
#JamiiAfrica #JamiiForums #Demokrasia
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MOROGORO: Padre Emilius Kobelo amesisitiza umuhimu wa Kuliombea Taifa na kutambua wajibu katika kulinda haki na amani, akisisitiza anayeharibu amani ya nchi ni Mtanzania na anayevunja haki ya Mtanzania ni Mtanzania.
Ameyasema hayo Agosti 23, 2025 katika Misa Takatifu ya kuombea haki na amani nchini Tanzania, iliyofanyika katika Parokia Teule ya Mt. Agnes Nanenane, Jimbo Katoliki Morogoro.
Zaidi soma https://jamii.app/HakiMtanzania
#JamiiAfrica #JamiiForums #Uwajibikaji #JFMatukio
Ameyasema hayo Agosti 23, 2025 katika Misa Takatifu ya kuombea haki na amani nchini Tanzania, iliyofanyika katika Parokia Teule ya Mt. Agnes Nanenane, Jimbo Katoliki Morogoro.
Zaidi soma https://jamii.app/HakiMtanzania
#JamiiAfrica #JamiiForums #Uwajibikaji #JFMatukio
❤1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
RUVUMA: Mhashamu Damian Denis Dallu, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Songea ametoa wito kwa Viongozi mbalimbali wanapostaafu waiache Serikali mpya kufanya kazi kwa uhuru kwani inakuwa tayari ina mipango yao.
Ameyasema hayo katika maadhimisho la Misa Takatifu ya Jubile Kuu ya Ukristo ya Waseminari wa Jimbo Kuu Katoliki Songea, iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Kiaskofu la Mtakatifu Matias Mulumba Kalemba Jimbo Kuu Katoliki Songea, Agosti 23, 2025.
Soma https://jamii.app/AskofuDalluWastaafu
#JamiiAfrica #JamiiForums #Governance #JFUtawalaBora
Ameyasema hayo katika maadhimisho la Misa Takatifu ya Jubile Kuu ya Ukristo ya Waseminari wa Jimbo Kuu Katoliki Songea, iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Kiaskofu la Mtakatifu Matias Mulumba Kalemba Jimbo Kuu Katoliki Songea, Agosti 23, 2025.
Soma https://jamii.app/AskofuDalluWastaafu
#JamiiAfrica #JamiiForums #Governance #JFUtawalaBora
❤1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa imempitisha aliyekuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Uchaguzi Tanzania (NEC), Dkt. Wilson Mahera Charles kuwa Mgombea Ubunge Jimbo la Butiama katika Uchaguzi Mkuu 2025.
Ikumbukwe, Dkt. Mahera aliteuliwa Oktoba 1, 2019 na Hayati Rais John Pombe Magufuli kuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, baadaye Februari 26, 2023 aliteuliwa na Rais Samia Suluhu kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).
Soma zaidi https://jamii.app/DktMahera
#JamiiAfrica #JamiiForums #UchaguziMkuu2025 #Siasa
Ikumbukwe, Dkt. Mahera aliteuliwa Oktoba 1, 2019 na Hayati Rais John Pombe Magufuli kuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, baadaye Februari 26, 2023 aliteuliwa na Rais Samia Suluhu kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).
Soma zaidi https://jamii.app/DktMahera
#JamiiAfrica #JamiiForums #UchaguziMkuu2025 #Siasa
NIGERIA: Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Mamlaka, Agosti 23, 2025, Jeshi la Anga limewaokoa Watu 76 waliokuwa wametekwa nyara, wakiwemo Wanawake na Watoto, baada ya kufanya shambulio la angani kwa usahihi kwenye ngome ya majambazi katika Jimbo la Katsina Kaskazini Magharibi.
Operesheni hiyo ililenga eneo la Pauwa Hill katika Halmashauri ya Kankara kama sehemu ya msako dhidi ya kiongozi wa genge kwa jina la Babaro, anayetuhumiwa kuhusika na shambulio la msikiti Mjini Malumfashi. Wakati wa uokoaji, Mtoto mmoja alipoteza maisha, ingawa haijabainika kama kulikuwa na vifo vingine vya mateka au wanachama wa genge.
Shambulio hilo linaweza kuashiria hatua muhimu katika jitihada za kuvunja mitandao ya uhalifu kaskazini magharibi mwa #Nigeria, ambako makundi yenye silaha yamekuwa yakiwatisha wakazi wa vijijini kwa miaka mingi.
Soma zaidi https://jamii.app/JeshiNigeria
#JamiiAfrica #JamiiForums #Uwajibikaji #HumanRights
Operesheni hiyo ililenga eneo la Pauwa Hill katika Halmashauri ya Kankara kama sehemu ya msako dhidi ya kiongozi wa genge kwa jina la Babaro, anayetuhumiwa kuhusika na shambulio la msikiti Mjini Malumfashi. Wakati wa uokoaji, Mtoto mmoja alipoteza maisha, ingawa haijabainika kama kulikuwa na vifo vingine vya mateka au wanachama wa genge.
Shambulio hilo linaweza kuashiria hatua muhimu katika jitihada za kuvunja mitandao ya uhalifu kaskazini magharibi mwa #Nigeria, ambako makundi yenye silaha yamekuwa yakiwatisha wakazi wa vijijini kwa miaka mingi.
Soma zaidi https://jamii.app/JeshiNigeria
#JamiiAfrica #JamiiForums #Uwajibikaji #HumanRights
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Sheikh Iddi Abdallah Chaurembo amewaombea wale wote wanaopanga kuleta chuki, kutumia mitandao kudhuru au kuhujumu kura, wapate upofu ili wasifanikiwe katika mipango yao.
Ameyasema hayo leo, Agosti 24, 2025, wakati akishiriki Kongamano la Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025, lililoandaliwa na Umoja wa Maimamu Tanzania (#UMATA) na kufanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, kongamano hilo pia limehudhuriwa na Rais Samia Suluhu Hassan.
Zaidi soma https://jamii.app/SheikhChauremboUpofu
#JamiiAfrica #JamiiForums #UchaguziMkuu2025 #Demokrasia
Ameyasema hayo leo, Agosti 24, 2025, wakati akishiriki Kongamano la Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025, lililoandaliwa na Umoja wa Maimamu Tanzania (#UMATA) na kufanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, kongamano hilo pia limehudhuriwa na Rais Samia Suluhu Hassan.
Zaidi soma https://jamii.app/SheikhChauremboUpofu
#JamiiAfrica #JamiiForums #UchaguziMkuu2025 #Demokrasia