JamiiForums
52.4K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Akizungumzia uamuzi wa baadhi ya kesi kufanyika kwa njia ya Mtandao, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa ametolea mfano Viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (#CHADEMA) walitoa tamko linaloashiria uvunjifu wa Amani na Usalama, hali iliyosababisha baadhi ya Wafungwa na Mahabusu kusikiliza mashauri yao kwa njia ya Mtandao

Amesema "Watanzania waelewe kuwa Jeshi linapokuwa na taarifa za Kiusalama linashirikiana na Mahakama kutoa Haki ile ile lakini kwa kutumia Teknologia ya Mahakama Mtandao ili kuzuia fujo Mtaani, naomba Watanzania watuelewe.”

Soma https://jamii.app/BashungwaAprili29

#JamiiForums #Accountability #Governance #HumanRights #CivilRights
1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa, ameliagiza Jeshi la Magereza kusimamia Sheria na taratibu kwa wanaotaka kuwaona Wafungwa na Mahabusu, akieleza taratibu hizo lazima ziheshimiwe bila upendeleo na hakuna wanaotakiwa kupewa Huduma Maalum (V.I.P)

Soma https://jamii.app/BashungwaAprili29

#JamiiForums #Accountability #Governance #HumanRights #CivilRights
JamiiAfrica inawatakia Wafanyakazi wote Maadhimisho mema ya Siku ya Wafanyakazi Duniani

Tukumbuke, nyuma ya kila Huduma bora, Bidhaa nzuri na Maendeleo ya Taifa kuna jasho, Maarifa na Bidii ya Mfanyakazi

Tuendelee kusimamia Haki, Mazingira salama ya Kazi na Maslahi bora kwa Wafanyakazi wote. Bila Mfanyakazi, hakuna Mafanikio

#JamiiAfrica #JamiiForums #MeiMosi2025 #WorkersDay
2
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amesema Jeshi la Magereza kwa kushirikiana na Mahakama ya Tanzania litaendelea kuwawezesha Wafungwa na Mahabusu kusikiliza mashauri yao wakiwa Magerezani kupitia Mahakama Mtandao, hasa kunapokuwepo na viashiria vya matishio ya kiusalama

Ameyasema hayo Aprili 30, 2025 alipoambatana na Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), kukagua Makasha ya kisasa ya Mahakama Mtandao yanayowezesha usikilizaji wa mashauri kwa njia ya Kiteknolojia katika Gereza la Isanga -Dodoma

Soma https://jamii.app/BashungwaAprili29

#JamiiForums #Accountability #Governance #HumanRights #CivilRights
👍1
DAR: Akizungumzia tukio la Katibu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), Padri Charles Kitima kujeruhiwa, Rais wa TEC, Askofu Wolfgang Pisa amesema eneo alikoshambuliwa hulitumia kufanyia kazi zake baada ya shughuli za pamoja na hakuwa anapata kinywaji, wala si sehemu kunakopatikana kinywaji chochote

Askofu Pisa amesema Padri Kitima alikuwa na Mapadri wenzake katika kikao, walipomaliza wenziwe waliondoka, akabaki eneo la mgahawa anakofanyia shughuli zake siku zote na kuwa hakuna baa wala vinywaji na kama kuna anayehitaji kupata vinywaji kwa kawaida angeenda nje ya eneo hilo

Ameongeza “Maana ukisema Mtu alikuwa anakunywa kwa saa zote hizo maana yake alikuwa anakunywa pombe, si hivyo. Wakati anatoka kurejea ndani kuna uchochoro wenye giza, hapo ndipo akavamiwa na kujeruhiwa na kitu kizito kichwani na kidevuni”

Soma https://jamii.app/TECPadriKitima

#JFMatukio #JamiiForums
👍3🔥1
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimesema kimepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa za kushambuliwa kwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padre Dkt. Charles Kitima, tukio lililotokea usiku wa Aprili 30, 2025, katika eneo la Kurasini, Dar es Salaam

Padre Kitima alivamiwa na watu Wawili wasiojulikana na kushambuliwa kichwani na mwilini na kusababishiwa majeraha mbalimbali

CCM imesema inalaani vikali kitendo hicho cha kikatili na kisicho na utu dhidi ya kiongozi wa dini, ambaye kimesema amejitolea maisha yake kuhudumia jamii kwa upendo na uadilifu

CCM imetoa wito kwa vyombo vya usalama kufanya uchunguzi wa kina na wa haraka ili kuwabaini na kuwachukulia hatua kali wahusika wa tukio hilo

Soma https://jamii.app/CCMKitima

#JamiiForums #Governance #Accountability #HumanRights
Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) limelaani vikali tukio la kushambuliwa kwa Padre Charles Kitima, Katibu Mkuu wa baraza hilo lililotokea usiku wa Aprili 30, 2025 katika Makao Makuu ya TEC, Kurasini, Dar es Salaam

Kwa mujibu wa taarufa ya Baraza hilo, Padre Kitima kwa sasa anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Aga Khan

Aidha, TEC imetoa wito kwa Jeshi la Polisi na Vyombo vya Usalama kuhakikisha wahusika wanakamatwa na kufikishwa mbele ya sheria. Vilevile uchunguzi wa tukio hili ufanyike kwa haraka, kwa uwazi na bila upotoshaji ili kurejesha imani ya wananchi

Soma https://jamii.app/TamkoTECMei1

#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #SocialJustice
Hatua ndogo ni hatua bado. Usijione mdogo kwa sababu hujafika kule unapotamani kufika

Acha kujilaumu kwa kile ambacho hujafanya jana, leo ni nafasi nyingine ya kujaribu tena, kujifunza tena na kusonga mbele

#Goodmorning #JamiiAfrica #JamiiForums #AmkaNaJF
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Kada wa CHADEMA, Mdude Nyagali anadaiwa kukamatwa usiku wa kuamkia leo Mei 2, 2025 akiwa katika makazi yake Mbeya na Watu wanaodaiwa kujitambulisha kuwa ni Polisi

Taarifa iliyochapishwa na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Wakili Boniface Mwabukusi imeeleza kuwa inadaiwa Watu hao walibomoa mlango wa nyumbani kwa Mdude na kisha kuingia ndani wakiwa na silaha za moto, ambapo walimpiga na kuondoka naye

JamiiForums inaendelea na jitihada za kutafuta taarifa ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kuhusu taarifa hizo zilizotolewa na Mwabukusi

Zaidi soma https://jamii.app/MdudePolisi

#HakiZaBinadamu #Demokrasia #HumanRights #SocialJustice
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mwanasiasa James Mbatia amezungumzia tukio la kujeruhiwa kwa Katibu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), Padri Charles Charles Kitima akidai waliofanya tukio hilo wanaonekana ni Watu wenye mafunzo ya juu na kwamba walilenga kumdhulumu uhai wa Kiongozi huyo wa Dini

Ikumbukwe tukio hilo lilitokea Aprili 30, 2025, baadaye Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salam, Jumanne Muliro akasema wanamshikilia Rauli Mahabi “Haraja” na uchunguzi unaendelea kuhusu tukio hilo

Soma https://jamii.app/MbatiaOnKitima

#JamiiForums #HumanRights #JFMatukio
👍2
Mdau kupitia Jukwaa la Habari na Hoja Mchanganyiko ndani ya JamiiForums.com ameanzisha mjadala kuhusu maslahi ya Watumishi wa Sekta Binafsi, baada ya Serikali kuongeza Mishahara kwa asilimia 35.1 kwa Wafanyakazi wa Umma wanaolipwa kima cha chini, huku kukiwa bado na hali ya sintofahamu kwa upande wa Wafanyakazi wa Sekta Binafsi

Wafanyakazi wa Sekta binafsi wamekuwa wakilalamikia Mazingira duni ya Kazi, Mishahara midogo isiyoendana na gharama za Maisha, kutokuwepo kwa Mikataba ya Ajira iliyo wazi na ya Haki, nk

Kwa mtazamo wako, nini kinakwamisha upatikanaji wa maslahi bora kwa Wafanyakazi wa Sekta Binafsi?

Mjadala https://jamii.app/MishaharaSektaBinafsi

#JamiiForums #JamiiAfrica
👍1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Wakili Boniface Mwabukusi amekosoa utaratibu uliotokea Mahakama ya Kisutu kuhusu uamuzi wa shauri linalomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu kusikilizwa kwa njia ya Mtandao badala ya kufikishwa Mahakamani, akidai uamuzi huo ulikuwa wa Hakimu na siyo Mahakama

Soma https://jamii.app/MwabukusiMay2

#Accountability #CivilRights #JamiiForums #Kuelekea2025
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Wakili Boniface Mwabukusi ametoa wito kwa Waziri wa Mambo ya Ndani kutoa maelekezo na kama hatatimiza hilo awajibike kuhusu tukio la Raia kukamatwa, kuzungushwa kwenye Magari na baadaye baadhi yao kutupwa kwenye Msitu

Amesema hayo akikumbushia matukio kadhaa yaliyotokea Aprili 24, 2025 wakati wa mchakato wa kufuatilia shauri linalomhusu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu katika Mahakama ya Kisutu

Soma https://jamii.app/MwabukusiMay2

#Accountability #CivilRights #JamiiForums #Kuelekea2025
2👍1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Wakili Boniface Mwabukusi akizungumza na Wanahabari, leo Mei 2, 2025 ametoa wito kuwa kuna umuhimu wa uwepo wa chombo kinachoweza kusimamia utendaji wa Mamlaka mbalimbali za Serikali ikimemo Jeshi la Polisi ili kuongeza Uwajibikaji

Soma https://jamii.app/MwabukusiMay2

#Accountability #CivilRights #JamiiForums #Kuelekea2025
👍1
KAGERA: Meneja wa Wakala wa Barabara (#TANROADS) Mkoa, Mhandisi Ntuli Mwaikokesya amesema ujenzi wa Barabara njia Nne Bukoba kutoka Rwamishenye - Makutano ya Barabara ya Stendi ya Mabasi unaendelea baada ya kusuasua kwa muda, akieleza unatarajiwa kukamilika Novemba 2025

Kutokamilika kwa Barabara hiyo kumelazimisha Wananchi kutumia njia mbadala kwa kuzunguka kupitia Nyakanyasi, ambapo Mhandisi Ntuli amesema “Wananchi wamekuwa na maswali, hatujalala, kazi inaendelea, tunaendelea na ukarabati wa Daraja la Kanoni.”

Ikumbukwe Desemba 6, 2024, Mdau wa JamiiForums.com alihoji kuhusu mchakato huo kwa kuandika “Ujenzi wa Njia Nne Bukoba unasuasua, Mamlaka hazifahamu Barabara hiyo ndio mlango wa Uchumi wa Mji?”

Soma https://jamii.app/BarabaraKagera

#JamiiForums #Uwajibikaji #Accountability
👍1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mkuu wa Mkoa, Albert Chalamila amesema madai ya Waandishi wa Habari kudaiwa kupigwa na Jeshi la Polisi wanatakiwa kwenda Mahakamani ili kupata Haki. Pia, ametoa wito kuwa raia hawatakiwi kujifanya ‘Wadwanzi’ bila kuangalia hatari zinazoweza kutokea mbele, hawatakiwi kulaumu Jeshi la Polisi

Soma https://jamii.app/ChalamilaOnKitima

#JamiiForums #Governance #JFMatukio
1