JamiiForums
52.4K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
HAITI: Marekani imetenga Tsh. Bilioni 11.6 kusaidia hali mbaya ya Chakula inayosababishwa na ghasia za Magenge ya Waasi

20% ya Watoto chini ya Miaka 5 wanasumbuliwa na #Utapiamlo huku Watu Milioni 4.4 wakikosa Chakula

Soma - https://jamii.app/HaitiAID

#JamiiForums #HumanRights
👍2
PAKISTAN: WAZIRI MKUU WA ZAMANI ASHTAKIWA CHINI YA SHERIA YA UGAIDI

Polisi wamemfungulia mashtaka #ImranKhan kwa madai ya kutoa vitisho dhidi ya Maafisa wa Serikali

Mashtaka hayo ni Siku moja baada ya kuwashutumu Polisi kumtesa #ShahbazGill

Soma - https://jamii.app/WaziriAshtakiwa
👍7🤔2
WAZIRI WA ZAMANI GUINEA, LOUNCENY CAMARA AFARIKI AKIWA GEREZANI

Familia yake ilikata rufaa Mahakamani ili Camara aruhusiwe kusafiri nje ya Nchi kupata Matibabu lakini hawakufanikiwa

Tangu 2021, Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Amnesty International limekuwa likikosoa kukosekana kwa Haki za Binadamu katika Magereza ya Guinea.

Soma > https://jamii.app/WaziriGuineaAfariki

#HumanRights
👍4
Mafuriko yameua zaidi ya Watu 50 ktk Jimbo la Logar Nchini #Afghanistan na sehemu ya #Pakistan huku baadhi wakiwa hawajulikani walipo

Pia, Nyumba zaidi ya 1,000 zimeharibiwa, Mazao kuharibika, Wanyama kupotea na wengine kufariki

Soma > https://jamii.app/MafurikoAfghan
#FloodSituation
👍2😢1
KWANINI KILA MTU ANAPASWA KUSHIRIKI KUPAMBANA NA RUSHWA

1) Rushwa ni kikwazo kwa Huduma za Msingi za Umma

2) Inapelekea Ukosefu wa Usawa na #Haki katika Jamii

3) Inaongeza Umasikini kwa Wananchi

4) Inarudisha nyuma #Demokrasia na Maendeleo ya Nchi

#KemeaRushwa
👍4
#PAKISTAN: Mamlaka ya Udhibiti wa Vyombo vya Habari vya Utangazaji (PEMRA) imepiga marufuku Vituo vya Runinga kurusha matangazo ya moja kwa moja ya mkutano wa Waziri Mkuu wa zamani, #ImranKhan unaotarajiwa kufanyika leo, Agosti 22

Soma - https://jamii.app/KhanMediaBan
#PressFreedom
👍7🤔1🎉1
UFILIPINO: WANAFUNZI WAREJEA SHULENI BAADA YA ZUIO LA MIAKA 2

Wanafunzi wote watalazimika kuendelea kuvaa Barakoa, kukaa kwa idadi ndogo na kutumia vipukusi (Sanitizer) ili kujikinga na maambukizi

Pia, watahudhuria Masomo kwa Siku tatu za Wiki

Soma - https://jamii.app/ShulePHP

#COVID19
👍6
Kwa mujibu wa Katiba ya #Kenya, baada tu ya Uchaguzi Mkuu wa Agosti 9, 2022 Rais anayemaliza muda wake anapoteza;

Mamlaka ya kuteua Majaji wa Mahakama Kuu, kuteua Afisa yeyote wa Umma, kuteua au kumfukuza kazi Katibu wa Baraza la Mawaziri, Katibu Mkuu na Maafisa wengine wa Serikali

Zaidi, soma - https://jamii.app/KatibaKE

#JFGovernance
👍11
UMUHIMU WA BODI ZA WAKURUGENZI: Uwepo wa Bodi za Wakurugenzi ni muhimu katika kuhakikisha kunakuwa na usimamizi mzuri na kuwa na Taasisi imara

Wakati wa Ukaguzi Mwaka 2020/21, CAG alibaini Mashirika ya Umma 31 hayakuwa na Bodi za Wakurugenzi. Mwaka 2019/20, Taasisi ambazo hazikuwa na Bodi zilikuwa 30

Kutokuwa na Bodi za Wakurugenzi kunapelekea kukosekana kwa #UtawalaBora kwenye uendeshaji wa Mashirika/Taasisi za Umma. Pia, hukwamisha juhudi za utekelezaji wa lengo Namba 16.6 la Malengo Endelevu (SDGs)

#WAJIBU #JFUwajibikaji
👍7
PICHA: Aliyekuwa Mgombea Urais wa Kenya, Raila Odinga akiwasilisha rasmi Pingamizi la Matokeo ya Urais wa Nchi hiyo Mahakamani

Siku chache zilizopita, Odinga alikataa Matokeo ya Urais kwa madai kuwa ni batili

#KenyaDecides2022 #Democracy
😁12🤔4👍3
BAADA YA RAILA ODINGA KUWASILISHA OMBI LA PINGAMIZI

Ndani ya saa 24, Mahakama itatoa uamuzi. Upande wa Rais Mteule utakuwa na siku 4 za kutoa majibu juu ya ombi hilo. Majaji 7 wakiongozwa na Jaji Mkuu wataamua kesi hiyo ndani ya siku 14

Iwapo Majaji watatoa uamuzi wa kuhesabiwa upya kwa Kura za Urais, Mahakama Kuu itasimamia zoezi hilo na itamtangaza mshindi na kutoa cheti

> Rais Mteule kisha ataapishwa Novemba 12, 2022 na kuwa Rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya

Soma - https://jamii.app/KenyaPetition

#KenyaDecides2022
👍16😁6🥰1
KENYA: Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) imetangaza Agosti 29, 2022 kuwa tarehe ya uchaguzi ulioahirishwa katika maeneo mbalimbali

> Wagombea wameruhusiwa kufanya Kampeni kwa hadi saa 48 kabla ya uchaguzi

Soma https://jamii.app/MarudioUchaguzi

#Democracy #KenyaDecides2022
👍3
MBEYA: TAKUKURU inawachunguza Hawa Kajula na Baita Sanga kwa tuhuma za kupokea rushwa kutoka kwa Watahiniwa wa Usaili wa kazi ya Sensa ya Watu na Makazi ili wapitishe majina yao

> Wanadaiwa kupokea kiasi cha Tsh. 200,000 kila mmoja

Soma https://jamii.app/RushwaMakarani

#KemeaRushwa
👍12
UTAFITI: VIFO VINGI VYA SARATANI VINASABABISHWA NA MTINDO WA MAISHA

Utafiti huu wa jarida la #Lancet umeongeza kuwa 44.4% ya vifo vilivyotokana na Saratani Duniani Mwaka 2019 vilichangiwa na tabia za Watu

Watafiti wamegundua tabia hatarishi 34 ambapo Uvutaji wa Sigara, Unywaji wa Pombe na uzito mkubwa zinaongoza miongoni mwa tabia hizo.

Soma - https://jamii.app/MaishaSaratani
#CancerResearch
👍11
FINLAND: Vipimo vimeonesha Waziri Mkuu, Sanna Marin hakutumia dawa zozote za kulevya baada video kuvuja iliyomuonesha akicheza, kuimba na kunywa katika sherehe ya hivi karibuni

Miongoni mwa dawa zilizopimwa ni 'Cocaine' na bangi

Soma https://jamii.app/FinlandWaziri

#Governance
👍6😁2
KURA YA MAONI MAREKANI: 57% WAUNGA MKONO FBI KUMPEKUA TRUMP

Asilimia kubwa ya Raia wamesema upekuzi uendelee na hakuna kibaya kuhusu hilo

FBI walifanya upekuzi Nyumbani kwa #DonaldTrump, #Florida akidaiwa kumiliki nyaraka za siri za Serikali

Soma > https://jamii.app/USPolitics
👍81😁1
UINGEREZA: Chama cha Soka Nchini humo kimemshtaki Kocha Thomas Tuchel kwa utovu wa nidhamu

Anadaiwa kutoa maoni yaliyotafsiriwa kama kuhoji uadilifu wa Mwamuzi Anthony Taylor baada ya sare ya #Chelsea dhidi ya #Tottenham Agosti 14, 2022

Zaidi https://jamii.app/TuchelAshtakiwa

#JFSports
👍4👎3😁1
UGANDA: Watu 14 wamefariki Dunia ktk Mji wa #Arua baada ya kudaiwa kunywa Pombe aina ya City 5 inayodhaniwa kuwa na sumu

Watu 4 wanashikiliwa kufuatia vifo hivyo, huku Kiwanda kinachotengeneza Pombe kikifungwa hadi uchunguzi utakapokamilika

Soma - https://jamii.app/14PeopleDie
#JFLeo
👍4
#KENYA: TUME YADAI WATU WENYE SILAHA WALITAKA KUSHAMBULIA MAAFISA WAO

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) imedai Wafanyakazi wake walitaka kushambuliwa Usiku wa Agosti 22, 2022 walipokuwa wakiandaa majibu ya malalamiko ya Uchaguzi Jijini #Nairobi

Soma https://jamii.app/MadaiYaTume
🤯2👍1
MAREKANI: TRUMP AIOMBA MAHAKAMA KUZUIA FBI KUKAGUA NYARAKA ALIZOKUTWA NAZO

Kwa mujibu wa ombi lake, #DonaldTrump anataka ateuliwa Mtu mwingine kukagua ili kuwepo usiri kwa madai ipo kanuni inayoruhusu Marais kuzuia taarifa zao kuwekwa wazi kwa umma

Soma https://jamii.app/TrumpFBI
👍12🤬1