JamiiForums
52.5K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
NGAO YA JAMII: YANGA 2-1 SIMBA

Yanga imeshinda magoli 2-1 dhidi ya Simba na kubeba Ngao ya Jamii kwenye Uwanja wa Mkapa, leo Agosti 13, 2022

Fiston Mayele amefunga magoli yote ya #Yanga, mfungaji wa #Simba ni Pape Sakho

Soma > https://jamii.app/Yanga2Simba1

#JFSports
🔥11👎6😁61👏1🤩1
BRENTFORD YAITANDIKA MAN UNITED 4-0

Manchester United imepoteza mchezo wa pili wa #EPL baada ya kufungwa goli 4-0 na Brentford leo Agosti 13, 2022

Hadi dakika ya 35, kikosi hicho cha Kocha Erik ten Hag kilikuwa nyuma kwa goli 4-0

Soma https://jamii.app/Brentford4ManU0

#JFSports #BREMUN
😁27👍11🤯4👎3
#JFMaisha: Kila Mmoja ana safari tofauti ya Mafanikio. Sio rahisi kufikia Mafanikio kwani inahitaji juhudi nyingi na juu ya yote uwe unapiga hatua katika mwelekeo ulio sahihi

- Je, ulishawahi kutengwa na rafiki yako wa karibu baada ya yeye kufanikiwa?

Mjadala - https://jamii.app/KutengwaRafiki
👍13
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Wewe ni rafiki wa aina gani?

Ukiona mambo hayaendi unapambana kuyajenga au unakubali hali halisi na kusonga mbele?

#JamiiForums
👍9
#SUDAN: MAFURIKO YAUA WATU ZAIDI YA 50. NYUMBA 8,170 ZASOMBWA

Takriban ekari 540 za Ardhi ya Kilimo, Ofisi 16 za Serikali na Maduka 40 yameharibiwa

UN inasema takriban Watu 38,000 wameathiriwa na Mvua hizo zilizoanza Mei 2022

Soma - https://jamii.app/SudanFlood

#JamiiForums #Flood
👍2😢2
MALI: Ujumbe wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa (MINUSMA) utaanza tena shughuli zake kuanzia Agosti 15 kwa taratibu mpya zilizoidhinishwa

#MINUSMA ilisitisha shughuli zake Julai baada ya #Mali kuwakamata Wanajeshi 49 wa Ivory Coast

Zaidi - https://jamii.app/MINUSMAMali

#Diplomacy
👍4
RUVUMA: Jeshi la Polisi linawashikilia Watu 13 kwa tuhuma za kumzika akiwa hai, Mzee Frolence Komba (78)

Chanzo cha tukio ni tuhuma za kumuhusisha Mzee huyo na kumuua Mtoto wake, Severine Komba (34) kwa imani za kishirikina

Soma - https://jamii.app/KombaAzikwa

#HumanRights
👍6
KENYA: UBALOZI WA MAREKANI WAKANUSHA RAIS BIDEN KUMPONGEZA ODINGA

Ubalozi umewataka Wakenya na wadau wengine wa Uchaguzi kuipuuza taarifa hiyo kwasababu Rais Joe Biden hajafanya mazungumzo na Mgombea yeyote

Soma - https://jamii.app/BidenOdinga

#KenyaDecides2022 #JamiiForums
👍7
WAZIRI MKUU WA MALI ALAZIMISHWA KUPUMZIKA

Waziri Mkuu wa #Mali, Choguel Maiga amelazwa kwa mapumziko aliyolazimishwa na Daktari kwa kile kilichodaiwa amefanya kazi kwa muda wa Miezi 14 bila kupumzika

- Alichaguliwa Agosti 2020

Soma > https://jamii.app/MaliPM

#Governance
👍7
UCHAGUZI KENYA: WAIHIGA AKUBALI KUSHINDWA

Mgombea Urais kupitia Chama cha Agano, David Mwaure Waihiga amekubali kushindwa na kukiri kura alizopata hadi sasa wakati mchakato unaendelea ni ndogo

Amesema anamuunga mkono William Ruto

Soma - https://jamii.app/KenyaElect2022

#KenyaDecides2022
👍2😁2
MAREKANI: ADHABU YA KUKUTWA NA HATI ZA SIRI NI JELA

Rais wa zamani wa Marekani, Donald Trump yupo kwenye wakati mgumu baada ya kupekuliwa na Maofisa wa FBI katika Nyumba yake ya Florida na kudaiwa kukutwa na nyaraka 11 za siri za Serikali

Soma > https://jamii.app/SecretDocuments
👍4
TANGA: Watu watatu wamefariki dunia kwenye ajali iliyohusisha Lori lililobeba Wafanyabiashara waliokuwa safarini kwenda Handeni kwa ajili ya Mnada

> Ajali imetokea eneo la Kwamagome baada ya Lori hilo kushindwa kukata kona

Soma - https://jamii.app/AjaliTA

#JFMatukio
😢5👍3
MISRI: Watu 41 wanadaiwa kufariki dunia na wengine 55 kujeruhiwa baada ya moto uliosababishwa na hitilafu ya umeme kuzuka katika Kanisa la Abu Sifin Coptic katika Mji wa Giza, Cairo

> Waumini takriban 5,000 walikuwa katika Ibada moto huo ulipozuka

Soma https://jamii.app/EgyptChurchFire

#JFMatukio
😢3
WACHEZAJI MAN UNITED WAFUTIWA MAPUMZIKO

Kocha Erik ten Hag amefuta mapumziko kwa Wachezaji wa Manchester United baada ya kufungwa 4-0 dhidi Brentford

Wamekutana mazoezini kutathmini kilichotokea, Mechi ijayo ni dhidi ya #Liverpool

Soma > https://jamii.app/ManUtdUpdates

#JFSports
👍5😁2
CHELSEA, SPURS HAKUNA MBABE

Timu ya Chelsea imelazimishwa sare ya magoli 2-2 ikiwa nyumbani dhidi ya Tottenham katika Premier League, leo Agosti 14, 2022

Timu hizo zimefikisha pointi 4 kila moja katika michezo miwili ya #EPL

Soma > https://jamii.app/Chelsea2Spurs2

#JFSports
👍14🎉1
WATOTO 80 WAFARIKI KWA SURUA ZIMBABWE

Mlipuko wa Surua unaosambaa #Zimbabwe tangu Aprili 2022 unaongezeka huku mikusanyiko ya Watu ikitajwa kuwa chanzo cha kusambaa kwa maambukizi

Kati ya walioambukizwa, 6.9% wamefariki Dunia

Soma > https://jamii.app/MlipukoWaSurua

#JamiiForums #Afya
👍4😢3👎1🤔1
KENYA: PROFESA WAJACKOYAH ANAAMINI YEYE NDIYE RAIS MPYA

Mgombea Urais wa Chama cha Roots, Profesa George Wajackoyah amesema ana imani ya kushinda Urais

Anachosubiri ni matokeo rasmi ya Tume na hajali kuhusu matokeo ya awali

Soma > https://jamii.app/KenyaElect2022

#KenyaDecides2022
😁24👍1
MALI: Wanajeshi 49 wa Ivory Coast waliokuwa wamezuiliwa kwa zaidi ya mwezi mmoja nchini humo wamefunguliwa mashtaka ya kujaribu kuharibu Usalama wa Taifa

> Ivory Coast imekanusha shutuma za Wanajeshi hao kuwa Mamluki

Soma https://jamii.app/DetainedSoldiers

#Diplomacy
👍7
Unyonyeshaji Watoto Maziwa ya Mama ukifanyika ipasavyo Familia, Jamii na Taifa kwa ujumla watapata faida zifuatazo:

1. Watoto wachanga watakuwa na hali nzuri ya Lishe itakayoboresha ukuaji na Maendeleo yao Kimwili na Kiakili

2. Kasi ya Watoto kupata Magonjwa hatari ya kuambukizwa au kuugua mara kwa mara itapungua na hivyo kupunguza Vifo vya Watoto Nchini

3. Hali ya Lishe na Afya ya Wanawake itaboreka kwa kupunguza uwezekano wa kupata Saratani ya Matiti na via vya Uzazi

#JamiiForums #BreastFeeding #WBW2022
👍6👏1
UCHAGUZI KENYA: Tume ya Uchaguzi (IEBC) inatarajiwa kumtangaza atakayeshika nafasi ya Urais baada ya zoezi la kuhesabu Kura kukamilika

Hadi leo alfajiri, matokeo ya Tume yanaonesha Azimio ina Wabunge 162 na UDA ina 159

Soma -https://jamii.app/IEBCKenya
#KenyaDecides2022
👍9