JamiiForums
52.5K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Fuatilia Kongamano la Miaka 30 ya Mfumo wa Demokrasia ya Vyama Vingi

Mjadala unahusu mafanikio na changamoto za Kidemokrasia, Utawala wa Kisheria na Ushiriki wa Umma

Link > https://youtu.be/GE2-ZKvPjSU

#Democracy30
👍7
GEOPHREY PINDA (NAIBU WAZIRI KATIBA NA SHERIA): Tanzania hakuna Sheria mbovu, bali tuna Sheria zilizopitwa na wakati, zinazohitaji kufanyiwa marekebisho ili kuendana na wakati tuliopo

Fuatilia > https://jamii.app/KongamanoTLS

#Democracy30 #30YrsOfMultipartism
👍14
JOHN MNYIKA (CHADEMA): Ukosefu wa Katiba Mpya ni Mzizi wa Matatizo. Vyama vya Siasa havina ruhusa ya kufanya Mikutano ya Hadhara pamoja na kuwa na Sheria zinaruhusu hili. Pamoja na mabadiliko ya kiutawala bado katazo hili linaendelea

> Kuingia kwenye Mfumo wa Vyama vingi kulipaswa kutanguliwe na mfumo unaoruhusu uwepo wa vyama vingi. Sasa ni miaka 30 ya Vyama vingi lakini bado hakuna Katiba inayoruhusu Mfumo wa Vyama vingi Nchini

Fuatilia - https://jamii.app/KongamanoTLS

#Democracy30 #30YrsOfMultipartism
👍14
JENERALI ULIMWENGU: Magufuli aliamua Wabunge watakaoingia Bungeni yeye mwenyewe. Takwimu zilikuwa ni haramu kama hazikutolewa na Serikali

> Azaki zilishindwa kufanya kazi na katika awamu yake wajinga waliibuka kwa wingi na kujiona bora

> Rais Samia ameonesha nia ya kuleta maridhiano. Nasi tuunge Mkono juhudi hizo lakini tunapaswa kufanya hivyo kwa umakini ili tusirudi tulipotoka

Soma zaidi - https://jamii.app/KongamanoTLS

#Democracy30 #30YrsOfMultipartism
👍20👎4🤩3
KAIZA BUBERWA: Miaka ya zamani Vyama vya Siasa vilipoteza dira baada ya kuweka nguvu nyingi kwenye kutaka kuiondoa CCM madarakani

> Wakati huo huo wanufaika wa CCM wakizuia kwa nguvu kutoondolewa Madarakani

#Democracy30
HAMAD RASHID MOHAMED (ADC): Wanasiasa wa Upinzani kukosa ushirikiano wenyewe kwa wenyewe ni chanzo kikuu cha kukosekana kwa Upinzani imara nchini. Udhaifu wetu mkubwa ni kukosa umoja

> Katiba sio mwarobaini bali utashi ndio unatakiwa. Nilimwambia Mnyika 'Hamuwezi kuandamana kama tulivyokuwa tunafanya sisi'

> Nilikuwa tayari kukaa ndani kutetea wenzangu lakini wao wakisikia kuna kukamatwa watakimbia watajificha uvunguni

Soma - https://jamii.app/KongamanoTLS

#Democracy30 #30YrsOfMultipartism
👍13
SIKU YA KIMATAIFA YA KUPINGA USAFIRISHAJI HARAMU WA BINADAMU

Usafirishaji Haramu unatajwa kuwa janga linaloendelea kukua na Wanawake na Watoto ndio wahanga wakubwa

Maadhimisho ya Mwaka 2022 yanaangazia nafasi ya Teknolojia katika kuwezesha na kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu

Fahamu zaidi https://jamii.app/HumanTRF2022

#EndHumanTrafficking
👍4😢1
USAFIRISHAJI HARAMU WA BINADAMU MITANDAONI

Usafirishaji Haramu wa Binadamu kupitia Mitandao unashika kasi kutokana na kuongezeka kwa matumizi ya Teknolojia

Majukwaa ya Kidigitali yamekuwa fursa kwa Watuhumiwa wa Biashara hii Haramu

Wanayatumia kuwatambua na kuwapata Wahanga, miongoni mwao wakiwemo Watoto

Soma zaidi - https://jamii.app/HumanTRF2022

#EndHumanTrafficking
👍6😢1
Teknolojia inaweza kuwa na nafasi muhimu katika Mapambano dhidi ya Usafirishaji Haramu wa Binadamu endapo itatumika ipasavyo

Utoaji Elimu zaidi juu ya Matumizi Salama ya Intaneti na Mitandao ya Kijamii unaweza kusaidia kupunguza hatari ya Watu kuwa Wahanga

Soma > https://jamii.app/HumanTRF2022

#EndHumanTrafficking
👍3
FATMA KARUME: Uchaguzi wa 2020 ulikuwa wa ovyo kuliko chaguzi zote zilizopita. Hakujawahi kutokea chaguzi yoyote tangu Mfumo wa Vyama Vingi uanzishwe kusiwe na kesi Mahakamani isipokuwa wa 2020, na hii ni kwa sababu Watu hawana Imani na Mahakama

> Tumetengeneza Mhimili wa Mahakama usioweza kufanya kazi yake. Rais kuwa na Uwezo wa Kumteua na Kumuondoa Jaji Mkuu kunaondoa Uhuru wa Mahakama

> Pia, Mahakama kutegemea Bajeti ya Serikali kufanya shughuli zake hudunisha uhuru wa Mahakama

Soma - https://jamii.app/KongamanoTLS

#Democracy30 #30YrsOfMultipartism
👍14
MAKARAMBA (JAJI MSTAAFU): Kuna tatizo kubwa Watanzania kuchanganya mambo. Sheria mbovu huwa inatamkwa na Mahakama siyo Mwanasiasa

> Ila wanasiasa ndio ambao tunaamini wanaweza kutunga Sheria mbovu na ndio mwanzo wa kuingiliana Mamlaka katika vile vyombo vitatu

> Wale ambao hawapaswi kutunga Sheria ndio wanatunga Sheria, ambao hawapaswi kutafsiri ndio wanatafsiri Sheria. Ndio maana mnasikia mtu anasema 'Nitakuweka ndani' yaani anakuwa Sheria, Mahakama na Polisi kitu ambacho tulipiga marufuku

#30YrsOfMultipartism
#Democracy30
👍12
FRANCIS STOLLA (RAIS MSTAAFU WA TLS): Mahakama ni Mhimili unaojitegemea ukiachana na Teuzi

> Nchi yetu inapaswa ijengwe na Mifumo. Inabidi Tawala na Idara mbalimbali nchini zifanye kazi kimfumo

Soma - https://jamii.app/KongamanoTLS

#Democracy30 #30YrsOfMultipartism
👍5
ADO SHAIBU (ACT WAZALENDO): Vyama vya Siasa viwajibike kutengeneza mazingira bora ya Ushiriki wa Wanawake ktk Siasa

> Demokrasia isipoimairishwa, Siasa zikiendelea kuwa za piga ua, za baruti, za mabomu, za kukimbizana itawafanya Wanawake washindwe kushiriki Kisiasa

#Democracy30
👍2
USAFIRISHAJI HARAMU WA BINADAMU: UNAWEZAJE KUJILINDA MTANDAONI?

- Kuwa Makini na Urafiki wa Mitandaoni: Wahalifu hutumia Mitandao kujenga uaminifu

- Usiamini kila tangazo kirahisi: Wanaofanya Biashara Haramu ya Usafirishaji Binadamu hutoa ahadi nono ambazo ni rahisi kumshawishi yeyote

Fahamu zaidi > https://jamii.app/HumanTRF2022

#EndHumanTrafficking
👍6
ALPHONCE SIMBU ASHINDA MEDALI YA FEDHA

Mwanariadha Mtanzania, Alphonce Felix Simbu ametwaa Medali ya Fedha baada ya kuibuka mshindi wa pili wa Mbio za Riadha katika Michezo ya Jumuiya ya Madola Jijini Birmingham, Uingereza

Simbu ametumia muda wa 2:12:29 huku Mshindi wa Kwanza, Victor Kiplagat ambaye ni Raia wa Uganda akitumia 2:10:55

#JFSports
👏19👍7
SENZO KUONDOKA YANGA, WAKILI SIMON PATRICK AKABIDHIWA MIKOBA

Klabu ya Yanga imetangaza kutomuongezea Mkataba Afisa Mtendaji Mkuu, Senzo Mazingiza anayemaliza mkataba wake kesho Julai 31, 2022

Yanga imesema Senzo ndiye ameomba kutoongezewa mkataba kutokana na sababu za kifamilia. Wakili Simon Patrick ameteuliwa kukaimu nafasi

Soma - https://jamii.app/SenzoYangaApart

#JFSports
BONDIA MANDONGA APIGWA KWA KO

Bondia Karim Mandonga amepoteza dhidi ya Shabani Kaoneka, Raundi ya 4 kwenye Uwanja wa Majimaji, Songea

Baada ya pambano Mandonga amesema: "Ni ajali kazini lakini nipo tayari kurudiana na mpinzani wangu."

Soma > https://jamii.app/MandongaApoteza

#JFSports
😁32👍6🔥3
KIDUNDA AMPIGA KATOMPA KWA POINTI

Bondia Mtanzania Selemani Kidunda ameshinda Mkanda wa WBF Inter Continental kwa pointi dhidi ya Eric Katompa wa DRC

Pambano lilikuwa la Super Middleweight Raundi 10 kwenye Uwanja wa Majimaji, Songea

Soma > https://jamii.app/NdondiSongea

#JFSports
👍17👏5👎1
UKRAINE: Rais Volodymyr Zelensky ameamuru Raia waliopo katika Mji wa Donetsk kuondoka haraka kutokana na kuendelea kwa mapigano dhidi ya Vikosi vya Urusi

> Rais huyo amesema Serikali itawasaidia kwa Fedha wote wanaohamishwa

Soma https://jamii.app/KuhamaDonetsk

#RussiaUkraineWar
👍5😁2
MISRI: Wafungwa 7 wakiwemo Mwandishi wa Habari, Hisham Fouad pamoja na Mtafiti wa Masuala ya Binadamu (Anthropology), Ahmed Samir ambao walishtakiwa kwa Makosa ya Ugaidi wameachiwa huru

> Wameachiwa kwa msamaha wa Rais

Soma https://jamii.app/WafungwaWaachiwa

#JamiiForums
👍7