JamiiForums
52.7K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
UTEUZI MAKATIBU TAWALA: Kamishna Dkt. Mussa Ali Mussa ameteuliwa kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro. Prof. Godius Kahyarara Mkoa wa Geita na Mhandisi Leonard Robert anakuwa Katibu Tawala Mkoa wa Iringa

Wengine ni Toba Nguvila (Kagera), Elikana Mayuganya Balandya (Mwanza), Prof. Siza Donald Tumbo (Shinyanga) na Dkt. John Rogath Mboya (Tabora)

Mbali na Uteuzi, amewahamisha Vituo vya Kazi Makatibu Tawala wa Mikoa 10 na wengine 9 wamesalia kwenye Vituo vyao vya Kazi

Soma - https://jamii.app/KatibuTawala2022

#Governance
👍7
JULAI 28: SIKU YA HOMA YA INI DUNIANI

Homa ya Ini (#Hepatitis) ni Ugonjwa unaosababishwa na Virusi vya aina mbalimbali

Virusi vinavyosababisha Homa ya Ini vipo katika makundi matano: A, B, C, D na E

Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) takriban 90% ya watu waishio na Homa ya Ini hawafahamu kuwa wanaugua Ugonjwa huo

Fahamu zaidi > https://jamii.app/HomaIni2022

#WorldHepatitisDay2022 #JFAfya
👍9
DALILI ZA HOMA YA INI

Baadhi ya dalili ni Homa, Kukosa Hamu ya Kula, Kuharisha, Kichefuchefu, Maumivu ya Tumbo, Macho kuwa ya Njano, Kutapika, Maumivu ya Misuli, Uchovu na Mwili kukosa nguvu

Soma zaidi - https://jamii.app/HomaIni2022

#WorldHepatitisDay2022 #PublicHealth #JFAfya
👍9
MAAMBUKIZI YA HOMA YA INI (HEPATITIS)

Mtu anaweza kupata maambukizi ya Homa ya Ini (hutofautiana kulingana na aina ya Kirusi) kupitia Chakula/Maji yaliyochafuliwa na kinyesi cha mtu mwenye maambukizi, kujamiiana bila Kinga na mtu mwenye Ugonjwa na kuchangia matumizi ya vitu vyenye ncha kali

Pia, maambukizi yanaweza kutoka kwa Mama kwenda kwa Mtoto wakati wa kujifungua

Zaidi, soma - https://jamii.app/HomaIni2022

#WorldHepatitisDay2022 #JFAfya
👍9
MAJERAHA KUMUWEKA POGBA NJE HADI 2023

Paul Pogba wa Juventus anatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa goti, hivyo anaweza kukosa Michuano ya Kombe la Dunia 2022

> Aliumia goti akiwa mazoezini siku chache tangu asajiliwe akitokea Man. United

Soma https://jamii.app/PogbaAumia

#JFSports
😁5👍2🤯2😢2
#JFAFYA: Takwimu za UNAIDS zinaonesha kuongezeka kwa Maambukizi ya VVU huku ikikadiriwa kuwa kila dakika 2 kwa mwaka 2021, msichana mmoja aliambukizwa VVU

> Pia, kila dakika 1 kwa mwaka huo mtu mmoja alifariki kutokana na magonjwa yanayohusiana na UKIMWI

Soma https://jamii.app/VVUAfrika
👍9😱5😢5😁2
NIGERIA: Raia wamedai kuwa Serikali imetelekeza Vyuo Vikuu vya Umma kwa kuwa Watoto wao wanasoma Vyuo vya Nje ya Nchi hivyo itungwe Sheria itakayodhibiti Maafisa wa Serikali kusomesha Watoto wao nje ya Nchi

> Wahadhiri wa Vyuo Vikuu wapo kwenye mgomo

Soma https://jamii.app/VyuoNigeria

#Governance
👍22😁21
#TUNISIA: MABADILIKO YA KATIBA YAMUONGEZEA RAIS MAMLAKA

Tunisia imepitisha #Katiba mpya baada ya kura ya maoni ya 30% ya wapigakura

Inampa Rais udhibiti wa Serikali, Amri juu ya Jeshi na uwezo wa kuteua Serikali bila idhini ya #Bunge

Soma - https://jamii.app/KatibaMpyaTuns

#Democracy
👎16😁5
KUCHELEWESHA MALIPO HUSABABISHA MIRADI KUKAMILIKA CHINI YA KIWANGO

Kumekuwepo na ukiukwaji wa Matakwa ya Mikataba katika Miradi ya Maendeleo. Kwa mujibu wa Ripoti ya CAG 2020/21 hii imesababisha hasara kubwa kwa Serikali, hali iliyopelekea kutozwa Riba ya Tsh. Bilioni 6,311.83

Kucheleweshwa kwa malipo ya Wakandarasi kuna athari mbalimbali ikiwemo Miradi kukamilika chini ya kiwango, Kukosekana thamani ya fedha na Wakandarasi kukosa Imani na Serikali kutokana na kuvunjwa kwa vipengele vya Mikataba yao

#JFUwajibikaji
👍12🤬1
UNAWEZAJE KUJIKINGA NA HOMA YA INI?

1) Usichangie matumizi ya vitu vyenye ncha kali vikiwemo viwembe

2) Kunywa Maji na kula Chakula kilichoandaliwa katika mazingira safi na salama

3) Jua Afya yako kwa kufanya vipimo vya Homa ya Ini

4) Tumia Kinga kwa usahihi wakati wa kujamiiana

Fahamu zaidi > https://jamii.app/HomaIni2022

#WorldHepatitisDay2022 #JFAfya
👍5
LOLIONDO: Washtakiwa 3 kati ya 27 waliokuwa wanakabiliwa na makosa mawili likiwamo la mauaji ya Askari katika eneo la Loliondo, wamefutiwa kesi na kuachiwa huru na Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha

> Wameachiwa baada ya DPP kukosa nia ya kuwashtaki

Soma https://jamii.app/KesiLoliondo
👍12😁3🥰1
#JFSHAIRI: Ukatili ni kitendo anachofanyiwa Mtu yeyote kwa lengo la kumdhuru au kumuumiza Kisaikolojia, Kimwili, Kiafya, Kingono na Kiuchumi

Jifunze kupitia Shairi hili kutoka kwa Mdau wa JamiiForums.com likizungumzia Ukatili unaofanyika kwenye Jamii

#JamiiForums #Violence #GBV
👍10
KENYA: Serikali imetaifisha takriban Tsh. Bilioni 3.9 za Rigathi Gachagua (Mgombea Mwenza wa Urais kupitia Kenya Kwanza) kwa kushindwa kueleza jinsi alivyozipata kutoka kwa Mashirika ya Serikali

> Anashukiwa kuhusika na Utakatishaji Fedha

Soma https://jamii.app/UtaifishajiKenya

#Kenya2022
👍13😁2
#GUINEA: Maandamano dhidi ya Serikali ya Kijeshi na usimamizi wake wa mipango ya kurejesha Demokrasia yameripotiwa Jijini #Conakry

Inadaiwa, Utawala wa Kijeshi haupo tayari kufanya mazungumzo yatakayofafanua Kanuni za Kipindi cha Mpito

Soma https://jamii.app/GuineaProtests1

#Democracy
👍10
NIGERIA: Serikali imesema itaweka vikwazo kwa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) na Trust TV kwa kutukuza Ugaidi baada ya vituo hivyo na kuonesha Filamu kuhusu Magenge ya Uhalifu ya Kaskazini Magharibi mwa Nchi hiyo

Soma https://jamii.app/NigeriaNaBBC
👍8
MSUMBIJI: Aliyekuwa Waziri wa Kazi, Maria Helena Taipo amehukumiwa kifungo cha Miaka 16 jela kwa Makosa ya Rushwa yanayohusisha kujipatia takriban Tsh. Bilioni 3.96 kutoka katika Fedha za Umma kati ya mwaka 2014-2015

Soma - https://jamii.app/WaziriUfisadi

#KemeaRushwa
👏7👍4
RUKWA: Mwalimu wa Shule ya Sekondari Tanga, Emmanuel Jerome anadaiwa kumuua Mkewe, Lucy Nshoma kwa kumnyonga kisha na yeye kujiua kwa kujinyonga siku moja baadaye

> Emmanuel alimtuhumu mkewe kuwa na uhusiano na Wanaume wengine

Soma https://jamii.app/WanandoaWafariki

#JFMatukio
👍6🤔4👎1🎉1
UTOLEWAJI FEDHA PUNGUFU HUATHIRI UTOAJI HUDUMA KWA WANANCHI

Serikali Kuu ilipanga kutoa Tsh. Bilioni 928.05 ya utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo katika Mamlaka za Serikali za Mitaa. Hata hivyo, kiasi kilichotolewa ni Tsh. Bilioni 662.68, sawa na 71% ya Bajeti iliyopangwa

Kutolewa Fedha pungufu kwenye baadhi ya Halmashauri husababisha Halmashauri hizo zishindwe kutoa Huduma zilizopangwa kwa Wananchi

#JFUwajibikaji
👍3