JamiiForums
52.8K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
KOCHA WA BARCELONA AZUIWA MAREKANI

Kocha Xavi Hernandez amezuiwa kwenda Marekani kutokana na rekodi ya kuingia Nchini Iran zaidi ya mara tatu

Ili kuingia Marekani, yeyote mwenye rekodi kama hiyo anatakiwa kupata kibali maalum

Soma > https://jamii.app/XaviMarekani

#JFSports
😱12👍7😁7💩7🤔5🎉1
KENYA: MTENGENEZA MAUDHUI YA 'TIKTOK' ALAZWA BAADA YA KULA BUIBUI

Inadaiwa Aq9ine alianza kuumwa kifua huku joto la mwili likifika 48℃ baada ya kula buibui

Baada ya kushambuliwa Mitandaoni amesema akipona, atapika na kula chura na nyoka

Soma - https://jamii.app/TiktokerHospitalized
😁10🤔6👍1
MEXICO: Helikopta iliyokuwa ikitumika kusaka wahalifu wakiwemo wa dawa za kulevya imeanguka na kuua watu 14, huku mmoja akijeruhiwa vibaya

Chanzo cha ajali ya ndege hiyo hakijawekwa wazi

Soma - https://jamii.app/HelikoptaMexico
👍8😁4🤔4👎2🤮1
Huduma ya Intaneti imetoa usaidizi mkubwa katika kutafuta kazi, lakini bado ina safari ndefu kuwa namna ya kutegemewa katika kutafuta kazi kwenye jamii masikini kwani ufikiaji wake ni changamoto

Kwa mujibu wa Takwimu za Benki ya Dunia, ongezeko la 10% la upenyaji wa Intaneti Afrika linaweza kuongeza Pato la mtu mmoja mmoja kwa karibu 2.5%

Soma - https://jamii.app/HudumaIntaneti

#JFData #DigitalRights
👍7
WAMAREKANI 61 MARUFUKU KUINGIA IRAN

Iran imetoa orodha ya majina 61 ya Wamarekani ambao hawaruhusiwi kuingi Iran. Sababu kubwa ni kuunga mkono kikundi cha MEK ambacho wanakishutumu kwa ugaidi

Wengi wao ni Maofisa wa Serikali

Soma - https://jamii.app/IranUSA

#JFDiplomasia
👍14👎1
MDAU: JINSI YA KUTIBU/KUZUIA KISUKARI KWA KUTUMIA LISHE

Saga Karoti, Tango, Kitunguu Maji, Hoho, Nyanya na Limau likiwa na maganda na mbegu zake

> Kunywa mchanganyiko huo kila asubuhi dakika 45 au 60 kabla ya kula kitu kingine

Je, unafahamu lishe gani nyingine?

Soma https://jamii.app/TibaYaKisukari

#PublicHealth #JFAfya
👍293🤮3😁2
MANCHESTER UNITED KUMSAJILI LISANDRO

Imefikia makubaliano na Ajax kumsajili Lisandro Martinez (24) kwa £55.3m (Tsh. 151,522,000,000)

Atakuwa beki wa 2 ghali zaidi ktk klabu hiyo baada ya Harry Maguire

Atasaini mkataba wa miaka 5 na kulipwa £120,000 (Tsh. 328,800,000) kwa wiki

#JFSports
👍23😁9🔥3💩2
#UKRAINE: Rais Volodymyr Zelensky amewafuta kazi Mkuu wa Idara ya Usalama, Ivan Bakanov na Mwendesha Mashtaka Mkuu, Iryna Venediktova

Amesema hatua hiyo ni kufuatia tuhuma za maafisa wao kushirikiana na #Russia

Soma https://jamii.app/MaafisaUkaine
👍11😢1
CHELSEA YATAKA KUWASAJILI KIMPEMBE NA KOUNDE

Chelsea imetoa ofa ya Paundi Milioni 40 (Tsh. 109,600,000,000) ili kumnasa Beki wa PSG, Presnel Kimpembe (26)

Aidha, imerejea kwenye mazungumzo ya kumsajili Beki wa Sevilla, Jules Kounde (23) anayewaniwa pia na Barcelona

#JFSports
👍8🥰1
ARSENAL MBIONI KUMSAJILI ZINCHENKO

Arsenal ina tumaini la kumsajili Beki wa Manchester City, Oleksandr Zinchenko (25) wiki hii, baada ya kutoa ofa ya Paundi Milioni 35 (Tsh. 95,900,000,000)

Kocha wa Arsenal, Mikel Arteta anathamini sana uwezo wa Beki huyo wa Kushoto

#JFSports
👍9🔥1
Kila Julai 18, Siku ya Mandela au Siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela inasherehekewa duniani kote kuenzi mafanikio ya Kiongozi huyo

Kwa mwaka 2022, Maadhimisho haya yanaangazia Usalama wa Chakula na Mabadiliko ya TabiaNchi

Mandela alizaliwa Julai 18, 1918 na kufariki dunia Desemba 5, 2013. Alikuwa Rais wa Afrika Kusini kati ya 1994 - 1999

Soma zaidi - https://jamii.app/Mandela2022

#MandelaDay
👍9👏1
GHANA: Visa viwili vya Virusi vya #Marburg vimethibitishwa huku Wagonjwa wote wawili wakiripotiwa kufariki kwa Virusi hivyo vilivyo kundi moja na Virusi vya #Ebola

> Hadi sasa Watu 98 wapo karantini kwa kushukiwa kuugua Ugonjwa huo

Soma https://jamii.app/MarburgGhana

#JFAfya #PublicHealth
👍6😢3🤔1
SUDAN: Idadi ya Watu waliofariki kutokana na ghasia za Kikabila katika Jimbo la Blue Nile imefikia 65 na wengine 150 wamejeruhiwa tangu yalipozuka machafuko

> Chanzo ni mgogoro wa ardhi kati ya Watu wa Kabila la Berti na Haswa

Soma - https://jamii.app/ChaosSudan2022
👍5😢4
#MANDELADAY: Maadhimisho ya kumuenzi Nelson Mandela yalipitishwa na Umoja wa Mataifa (UN) mnamo Novemba 2009, na Siku ya Mandela imekuwa ikiadhimishwa kila mwaka tangu 2010

Hatua hiyo ni ishara ya kutambua mchango wake katika nyanja mbalimbali zikiwemo Demokrasia, Amani, Usawa wa Kijinsia, Haki za Binadamu, Haki za Watoto na vita dhidi ya Umasikini

Zaidi, soma > https://jamii.app/Mandela2022
👍13
DE LIGT AKUBALI KUJIUNGA NA BAYERN MUNICH

Juventus imekubali kumuuza Beki wake wa Kati, Matthijs de Ligt (22) kwenda Bayern Munich kwa Paundi Milioni 68 (Tsh. 186,320,000,000)

Atasaini mkataba wa miaka 5 baada ya kukamilisha vipimo vya afya anavyotarajia kufanya leo

#JFSports
👍2👎1🎉1
WAZIRI UMMY: UGONJWA WA MKOANI LINDI NI HOMA YA MGUNDA

Amesema Vipimo vilivyofanyika vimeonesha Ugonjwa ulioripotiwa siku chache zilizopita Mkoani Lindi ni Homa ya Mgunda (Leptospirosis)

Imeelezwa kuwa, Ugonjwa huo huambukizwa kutoka kwa Wanyama mbalimbali wakiwemo Panya na Swala. Mtu anaweza kuupata kwa kugusa Mkojo, Maji, Udongo au Chakula kilichochafuliwa na mkojo wa Wanyama wenye Maambukizi

Soma - https://jamii.app/HomaMgunda

#JFAfya
👍19
SUDAN YAFUNGUA MPAKA WAKE NA ETHIOPIA

Mpaka wa Gallabat ulifungwa Juni 27, 2022 baada ya Sudan kuishutumu Ethiopia kwa kuwanyonga Wanajeshi wake 7

> Hatua hiyo ni baada ya Viongozi wa nchi hizo kukubaliana kutatua mzozo maeneo ya mpakani

Soma https://jamii.app/MpakaSudanEthiopia

#JFDiplomasia
👍6
DAR: Serikali imekata rufaa kupinga Mahakama ya Kisutu kumfutia Kesi ya Uhujumu Uchumi Jitesh Jayantilal Ladwa (wa Hoteli za Golden Tulip) ikidai Mahakama hiyo haina Mamlaka ya kutoa uamuzi huo

> Alikuwa anakabiliwa mashtaka 24 yakiwemo ya kujihamishia Hisa za Wanahisa wenzake

Soma https://jamii.app/SerikaliRufaa
👍3
Siku ya Mandela inalenga kuhamasisha watu wote kuchukua hatua na kuleta mabadiliko katika Jamii kwani kila mmoja ana uwezo kufanya hivyo

#MandelaDay
👍10🎉2😁1
TETESI: RONALDO ANATAKA KUICHEZEA ATLETICO

Inadaiwa Cristiano Ronaldo anamshawishi Kocha Diego Simeone ili amsajili kwa ajili ya kuichezea Atletico Madrid msimu ujao

> Anataka kuondoka Man. United ili apate nafasi ya kucheza UEFA Champions League

Soma https://jamii.app/UsajiliWaCR7

#JFSports
👍8