JamiiForums
52.8K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
RIPOTI: Takriban Watoto Milioni 25 duniani walishindwa kupatiwa kwa wakati Chanjo muhimu zinazowalinda dhidi ya Magonjwa mbalimbali mwaka 2021

Ripoti ya Shirika la Afya Duniani (WHO) na Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Watoto (UNICEF) inasema hali hiyo ilitokana na utoaji wa huduma za Afya kuathiriwa na COVID-19

Soma - https://jamii.app/WatotoChanjo

#JFAfya
👍4🤔2
JULAI 15: SIKU YA UJUZI KWA VIJANA DUNIANI

Inakadiriwa kuwa, nafasi za kazi Milioni 600 zitahitajika kuundwa katika kipindi cha miaka 15 ijayo ili kukidhi mahitaji ya Ajira kwa Vijana

Idadi ya Vijana inatarajiwa kuongezeka kwa zaidi ya Milioni 78 kati ya 2021 - 2030, ikielezwa takriban nusu ya ongezeko hilo itakuwa katika Nchi masikini

Soma - https://jamii.app/UjuziVijana

#WYSD2022
👍6
Kwa mujibu wa Shirika la UNICEF, Vijana watatu kati ya wanne hawana Ujuzi unaohitajika kwenye Ajira

Waliopo Nchi masikini wana uwezekano mdogo zaidi wa kuwa na Ujuzi muhimu kwa fursa za Ajira/Ujasiriamali

Mifumo ya Elimu inatajwa kukwamisha Vijana na Watoto wengi, ikiwaacha bila Maarifa, Ujuzi na hamasa yoyote

Soma - https://jamii.app/UjuziVijana

#WYSD2022
👍5😁3😢1
LUGHA: NINI KINASABABISHA WATU KUCHANGANYA MATUMIZI YA "R" NA "L"?

Mdau wa Jukwaa la Lugha anahoji ni nini kinapelekea makosa kwenye matumizi ya herufi "R" na "L" kuanzia kuyaandika mpaka kutamka?

Anatolea mfano maneno "Rakini" badala ya "Lakini", "Kalili" badala ya "Kariri"

Je, unapata changamoto kwenye matumizi ya herufi hizo?

Mjadala - https://jamii.app/MdauLughaRL

#JFLugha
👍11
MAHAKAMA: ZUIO LA TWITTER NIGERIA LILIKIUKA SHERIA

Mahakama ya Haki ya ECOWAS imesema zuio hilo la mwaka 2021 lilikiuka Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na kunyima Wananchi Haki ya #UhuruWaKujieleza na kupata taarifa

Nigeria imetakiwa kuhakikisha marufuku kama hiyo haijirudii

Soma - https://jamii.app/TwitterBanNGR

#DigitalRights #FreedomOfExpression
👍6
Taasisi ya WAJIBU imezindua Ripoti za Uwajibikaji, Mapato na matumizi ya Fedha za Umma 2020/21 iliyotokana na ripoti za Ukaguzi za Mamlaka ya Serikali za Mitaa, Miradi ya Maendeleo, Mashirika ya Umma na Serikali Kuu zilizotolewa na CAG

Dhumuni ni kuwapatia Wananchi taarifa ya namna Serikali ilivyotekeleza Bajeti ya Taifa katika ukusanyaji wa Mapato na Matumizi ya fedha za Umma kwa mwaka

#JFUwajibikaji
👍8
10% PUNGUFU KWENYE MAKUSANYO: Mwaka 2020/21 Serikali ilipanga kukusanya Tsh. trilioni 34.8, hata hivyo ilikusanya Tsh. trilioni 31.3 (90% ya makadirio)

> Hili ni ongezeko la 5% ikilinganishwa na 2019/20 ambapo Serikali ilishindwa kukusanya Mapato iliyokadirikia kwa 5%

#JFUwajibikaji
👍6🤔2🔥1
UPUNGUFU WA MAJENGO YA MAHABUSU NA WAFUNGWA

Gereza la Keko lilikuwa na msongamano mkubwa zaidi ambapo lilikuwa na Wafungwa 1,075 zaidi ya uwezo wake sawa na 194%

Magereza 8 kati ya 15 yaliyokaguliwa hayakuwa na huduma ya Maji Safi na Salama kutokana na kutolipia Huduma ya Maji kwa Mamlaka husika

#JFUwajibikaji
😢7🤔3👍2
KUCHELEWA KWA RIPOTI ZA CAG

Mwenyekiti wa Kamati ya PAC, Japhet Hasunga amesema CAG anatumia mifumo kuandaa ripoti yake hivyo ripoti hizo zitoke mapema ili Bunge pia liweze kuzijadili mapema

Hasunga amesema hiyo itatoa fursa ya Uwajibikaji kabla fedha nyingine hazijaombwa Bungeni

#JFUwajibikaji
👍14🤔2
SOMALIA: WAANDISHI WAHIMIZA SHERIA ZA VYOMBO VYA HABARI KUREKEBISHWA

Wamesema Kanuni za Adhabu na Sheria ya Vyombo vya Habari zimekuwa tishio kwa usalama wao

Wameeleza kuwa Sheria mpya hailindi usiri wa Vyanzo vya Habari, na inaruhusu Waandishi kuhukumiwa bila kupewa nafasi ya kukata rufaa

Soma - https://jamii.app/SomaliaJounalists

#PressFreedom
👍7
RAIS WA MPITO AAPISHWA SRI LANKA

Ranil Wickremesinghe aliyekuwa Waziri Mkuu ameapishwa kuwa Rais wa Mpito, akimrithi Gotabaya Rajapaksa aliyejiuzulu kufuatia maandamano

Atahudumu kwa muda uliosalia katika Muhula wa Rajapaksa unaokamilika 2024

Soma - https://jamii.app/RaisMpyaSriLanka

#Governance
👍11🔥1
GEITA: Mkuu wa Wilaya ya Geita, Wilson Shimo amethibitisha vifo vya Wachimbaji 3 wa dhahabu na majeruhi wawili baada ya kuangukiwa na kifusi katika machimbo ya Nyamatagata

> Shughuli kwenye machimbo hayo zimesimamishwa kwa muda

Soma - https://jamii.app/VifoGeita

#JFMatukio
👍8😢3👎2
MANCHESTER UNITED YAMSAJILI ERIKSEN

Christian Eriksen (30) amesaini mkataba wa miaka mitatu kufuatia kufanyiwa uchunguzi mkali wa afya

Mchezaji huyo anaimarisha safu ya kiungo ya Erik ten Hag baada ya kuchagua kutosalia Brentford, alikokuwa msimu uliopita kwa mkopo

#JFSports
👍16👏1
JOTO KALI: UINGEREZA YATANGAZA HALI YA DHARURA

Mamlaka imetangaza hali ya dharura ya Kitaifa na kutoa onyo la joto kali katika baadhi ya maeneo

Wataalamu wamesema joto linaweza kufikia viwango vya juu vinavyoweza kuathiri watu na miundombinu

Soma - https://jamii.app/UKHeatRise
👍8🤔4👎21🔥1😁1
UGANDA: Zaidi ya watu 500,000 katika Mkoa wa Karamoja wanakabiliwa na njaa iliyosababishwa na ukame uliodumu kwa muda mrefu

Aidha, watu kadhaa wameripotiwa kufariki dunia maeneo ya Kaskazini Mashariki ya Nchi hiyo kutokana na njaa

Soma - https://jamii.app/UgandaNjaa
😢11👍4😱1
MISRI KUONDOA VIKOSI VYAKE VYA KULINDA AMANI NCHINI MALI

UN imesema Misri itaondoa Wanajeshi wake ifikapo Agosti 15. Kujitoa kwao ni pigo jingine baada ya doria za Wanajeshi wa Umoja wa Mataifa nchini Mali kusitishwa kwa muda

Wanajeshi 7 wa Misri wameuawa mwaka 2022

Soma https://jamii.app/VikosiMali

#Diplomacy
👍11👏1
AFRIKA KUSINI: Mamia waandamana kushinikiza kuondolewa kwa Rais Ramaphosa kutokana na kupanda kwa gharama za maisha na kukatika kwa umeme mara kwa mara

> Sababu nyingine ni kukithiri kwa rushwa ktk Taasisi za Umma na ukosefu wa ajira

Soma https://jamii.app/MaandamanoAfrikaKusini

#Democracy
👍14🔥4😁2
BARCELONA YAKUBALIWA KUMSAJILI LEWANDOWSKI

Mshambuliaji wa Bayern Munich, Robert #Lewandowski atasajiliwa kwa takriban Tsh. Bilioni 117

> Anasafiri leo kwenda Hispania kukamilisha usajili huo, anatarajiwa kusaini miaka mitatu

Soma https://jamii.app/LewandowskiBarca

#JFSports
👍21
TMA: NJOMBE KUNA SAKITU SIYO THELUJI

Mamlaka Hali ya Hewa (TMA) imefafanua kuwa kinachotokea Njombe hivi karibuni ni Sakitu inayosababishwa na umande kuganda na siyo Theluji

> Pia, Upepo wa Kusi unasababisha baridi kali maeneo mengine Nchini

Soma https://jamii.app/BaridiLaNjombe
👍11😁2🎉1
UTAFITI: KANDA YA ZIWA YAONGOZA UKATILI WA WENZA

Wataalamu wa Afya wamesema Mikoa inayoongoza ni Mara, Mwanza, Shinyanga, Simiyu na Geita

> Mikoa ambayo ina kiwango cha chini cha ukatili kwa wenza ni Pemba, Ukanda wa Pwani na Tanga

Soma https://jamii.app/UkatiliRipoti

#JFSaikolojia
👍14🤔1