JamiiForums
52.6K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
USAJILI WA JESUS KUTUA ARSENAL MAMBO SAFI

Taarifa ni kuwa Arsenal imekamilisha usajili wa Gabriel Jesus kwa ada ya Paundi Milioni 45 (takriban Tsh. Bilioni 128) kutoka Man. City

> Wameafikiana mahitaji binafsi ya mchezaji, imebaki kutangazwa tu

Soma https://jamii.app/JesusArsenal
👍13👏1
TSH. MILIONI 700 UKIMPATA MTUHUMIWA

Familia ya Fu Nannan raia wa China aliyeuawa Juni 11, 2022 kwa kupigwa risasi Jijini Dar es Salaam imeahidi kutoa Tsh. Milioni 700 kwa atakayefanikisha kupatikana kwa mtuhumiwa, Zheng Lingyao

Soma: https://jamii.app/MchinaAliyeuawa

#JamiiForums
👍13🤔2
SUDAN: Jeshi limeishutumu Ethiopia kwa kuwanyonga Wanajeshi wake 7 na raia 1 waliokuwa mateka Nchini humo na kuonesha miili yao hadharani

> Hadi sasa, hakuna majibu yoyote kutoka Mamlaka za Ethiopia kuhusiana na tuhuma hizo

Soma: https://jamii.app/EthiopiaYashutumiwa
#JamiiForums
🤔11👍2
Rais wa Urusi, Vladimir Putin anatarajiwa kufanya ziara ya kwanza nje ya Urusi tangu kuibuka kwa vita ya Urusi dhidi ya Ukraine, Februari 24, 2022

> Anatarajiwa kutembelea Mataifa ya Tajikistan na Turkmenistan

Soma https://jamii.app/PutinZiara

#JamiiForums #RussiaUkraineWar
👍18
JAPAN: Serikali imewataka wakazi wa Tokyo na maeneo jirani kupunguza matumizi ya umeme kwa kuzima taa zisizo za lazima huku ikisisitiza matumizi ya viyoyozi ili kukabiliana na ongezeko la joto

> Aidha, Watu 46 wamelazwa kutokana na joto hilo

Soma: https://jamii.app/WimbiLaJotoJapan
👍19🔥1
BUNGENI: Halima Mdee ameshauri Serikali kupunguza kodi ktk ndege zinazotumika kwa utalii Nchini akisema kufanya hivyo kutafanya Watalii waongezeke

> Amesema ripoti imeonesha Ndege za Kukodi zimepungua toka 200 hadi 105 na hii si nzuri kwa Utalii

Soma https://jamii.app/HalimaMdee
👍18🥰1
AFRIKA KUSINI: Mwanafunzi mwenye miaka 17 (aliyenusurika kifo) amesema kwamba alihudhuria sherehe katika Klabu ya East London kwa sababu aliarifiwa iliandaliwa na Waigizaji Mashuhuri

Anasema idadi ya Watu ilizidi katika Klabu hiyo na baadhi ya washiriki walitakiwa kuondoka na hawakutii ndipo Walinzi walifunga mlango na kuanza kupulizia 'Gesi' kwenye umati

> Tulikosa hewa kwa muda mrefu na tulikuwa tukisukumana lakini hakukuwa na manufaa

Soma - https://jamii.app/VifoKlabuAfrikaKusini
🤔12😢9👍21🎉1
USHAURI: ILI KUPUNGUZA MATUKIO YA KUUANA, WENZA WAACHE KUTUNZA CHUKI

Mwanasaikolojia anasema Matatizo ni kama kidonda, usipotibu kinaendelea kukua. Wenza watengeneze tabia ya kutafuta suluhusho la matatizo yao kwani migogoro inazaa chuki

Soma https://jamii.app/MatukioYaKuuana
#JamiiForums
👍5🔥1🥰1🤔1
MAHAKAMA YAZUIA UBUNGE WA KINA MDEE KUGUSWA

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, leo Jumatatu Juni 27, 2022 imetoa zuio la muda kuhusu kutofanyika chochote kwenye Ubunge wa Halima Mdee na wenzake 18 mpaka pale Mahakama hiyo itakaposikiliza maombi ya Rufaa yao

#JamiiForums
👍19👎5🤮5👏1🤯1🎉1
MAMBO YANAYOKUWEKA HATARINI KUPATA MAGONJWA YA INI

Kushiriki ngono na mwenye virusi vya Homa ya Ini, kuchangia vifaa vyenye ncha kali, kuongezewa damu yenye virusi, vyakula au bidhaa zenye kemikali

> Pia, matumizi makubwa ya vilevi & sigara

Soma https://jamii.app/MagonjwaYaIni
#JamiiForums
👍5👏5
UKRAINE: Kombora la Urusi limelipua sehemu yenye mkusanyiko wa maduka makubwa katika Mji wa Kremenchuk na kusababisha vifo vya Watu 16 na kujeruhi wengine 59

> Viongozi wa Umoja wa G7 wamelaani tukio hilo wakisema lililenga Wananchi wa kawaida

Soma - https://jamii.app/KomboraLaua
😢7👏6👍3
MAREKANI: Takriban Watu 46 wanaoaminika kuwa Wahamiaji wamepatikana wamekufa, huku 16 wakiokolewa wakiwa na hali mbaya kwenye lori lililotelekezwa pembezoni mwa Jiji la San Antonio, Texas

> Watu 3 wanashikiliwa kuhusiana na tukio hilo

Soma: https://jamii.app/WahamiajiMarekani

#JamiiForums
👍7😢3👎2
JORDAN: Tanki la tani 25 za gesi ya Klorini lililokuwa likisafirishwa kwenda Djibouti limepasuka na kusababisha vifo 10 na kujeruhi 251

> Wakazi wanaoishi maeneo ya karibu na Bandari wameamrishwa kufunga milango na madirisha ili kuzuia madhara zaidi

Soma: https://jamii.app/VifoJordan
👍7😢3👎1
MDAU: WAZAZI WANAAMINISHWA KIINGEREZA NI KILA KITU

Anasema Mfumo wa Shule za English Medium haufundishi elimu ya kupanua uelewa, badala yake wanakomalia Somo la Lugha hivyo Watoto wakihitimu wanakosa upeo wa kuchanganua mambo

Soma https://jamii.app/ShuleZaKingereza
#JamiiForums
👍20
MAREKANI: Mzunguko wa usambazaji na mauzo ya magazeti umeshuka kwa 12% ndani ya mwaka mmoja uliopita katika takwimu zilizoishia Machi 2022

> Sababu ya kushuka inatajwa kuwa ni uchumi kuyumba kutokana na COVID-19 pamoja na Matumizi ya Digitali

Soma https://jamii.app/MagazetiYashuka
#JamiiForums
👍7🤔3
UHALIFU MTANDAONI: Watu 25 wanashikiliwa kwa tuhuma za kufanya uhalifu kwa njia ya mtandao Jijini Dar es Salaam na Mkoani Morogoro

> Baadhi yao waliigiza kuwa Waganga, Wahudumu wa Makampuni ya Simu, Wakuu wa Shule na Mawakala wa Freemason

Soma https://jamii.app/WiziMtandaoni

#JamiiForums
🤩14👍5😁3👏1
TANZANIA NA KENYA KUSHIRIKIANA KUPAMBANA NA ULANGUZI WA WALEMAVU

Inadaiwa Waathirika huchukuliwa toka kwa Wazazi wao kwa ahadi ya maisha bora lakini wanapofika Nairobi hulazimishwa kuomba barabarani huku mapato yakienda kwa waliowachukua

Soma: https://jamii.app/HumanTraffickingInTz
#JamiiForums
👍7
UGANDA: Wanafunzi wa kiume ktk Shule ya Sekondari Nyakasura huvaa sketi ambayo ni sare ya shule hiyo iliyoanzishwa kipindi cha Ukoloni

> Mkuu wa Shule hiyo amesema hizo sio sketi bali ni "Mavazi ya Heshima" yanayovaliwa na Wanaume huko Scotland

Soma - https://jamii.app/WanafunziSketi

#JamiiForums
😁21👎12👍10👏1🤔1🤯1
KAZI ZA SANAA ZILIZOCHUKULIWA ENZI ZA UKOLONI KUTOKA TANZANIA KURUDISHWA

Rais wa Taasisi ya Prussian Cultural Heritage ya Mjini Berlin inayosimamia sehemu za makumbusho ameidhinisha kutia saini makubaliano ya kurejeshwa kwa vitu hivyo

Soma - https://jamii.app/UjerumaniUkoloni
👍9🤮5
TUNISIA: WAZIRI MKUU WA ZAMANI AACHIWA HURU

Hamadi Jebali anayetuhumiwa kwa utakatishaji fedha ameachiwa huru baada ya kushikiliwa kwa siku ya nne

Aligoma kula wakati alipokuwa kizuizini na kusisitiza alikamatwa kwa sababu za kisiasa

Soma > https://jamii.app/TunisiaPolitics
👍12