JamiiForums
52.7K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
MALI: Ubalozi wa Marekani umetoa tahadhari ya Shambulio la Kigaidi ambalo linalenga Vituo muhimu vya Serikali na maeneo ya Umma Mjini Bamako

> Hii ni siku chache baada ya raia 22 kuuawa Nchini humo na Watu wanaohisiwa kuwa Wanamgambo

Soma - https://jamii.app/ShambulioMali
👍3😁1
MAN. CITY INASHUGHULIKIA USAJILI WA CUCURELLA NA PHILLIPS

Manchester City inashughulikia kumsajili Beki Marc Cucurella kutoka Brighton na ofa rasmi itawasilishwa hivi karibuni

Aidha, Klabu hiyo inaangalia uwezekano wa kumsajili Kiungo Kalvin Phillips kutoka Leeds

#JFSports
👏7👍4😢2
Uingereza imeidhinisha Julian Assange kupelekwa Nchini Marekani ambapo anatafutwa kuhusiana na nyaraka zilizofichuliwa na mtandao wa #WikiLeaks mwaka 2010 na 2011

> Nyaraka hizo zilionesha Wanajeshi wa Marekani wakiua Raia Nchini Afghanistan

Soma - https://jamii.app/AssangeExtradition
👎14👍2🔥2💩1
Kamisheni ya Ulaya imetoa mapendekezo ya kutaka Ukraine iruhusiwe kuwa Mwanachama wa Umoja wa Ulaya (EU), kauli iliyotolewa wakati Urusi ikishinikiza Nchi hiyo kutoruhusiwa kujiunga

> Kamisheni hiyo imekutana leo Juni 17, 2022 Jijini Brussels

Soma - https://jamii.app/UmojaWaUlaya
👍4
Mawakili wa "Mfalme Zumaridi" wamewasilisha maombi kwa Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mwanza, Monica Ndyekobora kutaka Mteja wao kuhamishwa Gereza la Butimba kwa kuhofia usalama wake kutokana na uwepo taarifa za njama za kutaka kuawa

Soma - https://jamii.app/ZumaridiKuhamishwaGereza

#JamiiForums
👍6😱6😁4👎1
MDAU: MIAKA 25 NI MINGI SANA KUTOKUWA NA MAISHA YANAYOELEWEKA?

Anasema ameshahangaika ila bado hajafanikiwa kuwa na Biashara ya kueleweka au kazi nzuri

Anajikuta kwenye dimbwi la mawazo kwani anaona amekuwa mkubwa sana, na ni ngumu kupata maisha mazuri

Unaweza kumpa ushauri gani?

Mjadala zaidi - https://jamii.app/UmriMaisha
👍7🤯3
MWAKINYO ASHUKA VIWANGO VYA NDONDI DUNIANI

Bondia Hassan Mwakinyo ambaye yupo Marekani anashika nafasi ya 35 katika ubora wa Viwango vya Ubora wa Ndondi Uzani wa Super Welter

Wiki moja nyuma alikuwa akishika nafasi ya 17

Soma > https://jamii.app/BondiaMwakinyo

#JamiiForums #JFSports
😁17😢12👍4👎3🤮1
MALORI ZAIDI YA 40 YAKWAMA MPAKANI NAMANGA

Wafanyabiashara wa mazao wanadaiwa kuwa katika wakati mgumu mpakani mwa Tanzania na Kenya baada ya kuambiwa vibali vya kuvusha bidhaa hiyo kuelekea nchi jirani kumalizika muda wake

Soma - https://jamii.app/MagariYakwama

#JamiiForums
😁5😢4👎1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Watendee watu jinsi unavyotaka kutendewa, heshimu wengine nao watakuheshimu

Tunawatakia Weekend njema!

#JamiiForums
👍26👏3
MLIPUKO WA UGONJWA WA TUMBO WAIBUKA KOREA KASKAZINI

Inaripotiwa Ugonjwa huo unatokana na chakula na maji, pia unaweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine

Kiongozi wa Taifa hilo, Kim Jong Un ameelekeza Wataalamu wa Afya kufuatilia

Soma - https://jamii.app/UgonjwaKorea
😢5👍3🤯2🤬1
FUNDI JOKOFU ATUHUMIWA KUMKATA KICHWA MKEWE

Godbless Sawe (47) Mkazi wa Kimara Suka, Dar anadaiwa kumuua Mkewe, Ester Gadau kwa kumkata kichwani na kitu chenye ncha kali Juni 14, 2022

Alitoroka baada ya tukio hilo na hajulikani alipo

Soma - https://jamii.app/TuhumaZMauaji

#JamiiForums
😢12👍8
RUVUMA: Aleyanda Mdendemi (54) Mkazi wa Kijiji cha Luhagala Wilayani Mbinga amefikishwa Mahakamani kwa tuhuma za kufanya mapenzi na Watoto wake wawili, na kuzaa na mmoja wao

Pia anatuhumiwa kumuachisha masomo Binti yake wa Shule ya Sekondari

Soma - https://jamii.app/UnyanyasajiWatoto
👍11👏3👎2😁1
SOMALIA: Wanamgambo 67 wa Al-Shabaab wameuawa kwenye mapigano katika Mji wa Galgaduud

> Pia, katika mapigano hayo raia waliungana na Jeshi dhidi ya Kikundi cha Al-Shabaab na jumla ya Wanajeshi na raia waliopoteza maisha ni 6

Soma - https://jamii.app/SomaliaChaos

#JamiiForums
👍4👏4😁2
MDAU: MAISHA NI VITA, USIKARIRI KUTUMIA SILAHA MOJA

Anasema ikiwa unafikiri Elimu ni silaha pekee uliyonayo ni rahisi kushindwa kwani zipo silaha mbalimbali katika maisha zikiwemo Nguvu, Akili, Rasilimali, Muda na Imani

Anashauri ikiwa Mazingira hayaruhusu Nguvu, basi tumia akili. Yasiporuhusu akili, tumia nguvu na pale ambapo hayaruhusu akili na nguvu, tumia imani. Usikubali kushindwa!

Mjadala - https://jamii.app/MaishaMdau
👍35👏4💩2
PUTIN: VIKWAZO WANAVYOTUWEKEA VITAWAUMIZA WAO WENYEWE

Rais wa Urusi amesema vikwazo hivyo ni vya ovyo na havina malengo, pia haviwezi kuwarudisha nyuma

> Pia, amesema Umoja wa Ulaya unaweza kupoteza Dola Bilioni 400 kutokana na vikwazo hivyo

Soma - https://jamii.app/PutinVikwazo
👍27😁6👎1
Uhitaji wa damu salama Nchini kwa mwaka ni chupa 550,000 hadi 600,000 wakati kwa mwaka 2021 takwimu zilionesha akiba ilikuwa ni chupa 375,000

> Je, unadhani jamii ina uelewa mzuri kuhusu umuhimu wa uchangiaji damu?

Soma - https://jamii.app/DamuSalama

#JamiiForums
👍41
Jumapili ya tatu ya Mwezi Juni kila mwaka, Siku ya Baba inaadhimishwa duniani kote. Ni Siku Maalum ya kuwaenzi, na kuthamini mchango mkubwa wa Baba katika Maisha yetu

Nafasi ya Baba katika Malezi na Familia ni ya kipekee; Baba ni Mshauri, Mwalimu na Mlezi. Tunawatakia wote Heri ya Siku ya Baba Duniani

#FathersDay #JamiiForums
👍2110🔥2
NEYMAR KUSTAAFU KUICHEZEA BRAZIL

Inadaiwa amewajulisha marafiki zake juu ya mpango huo, ambapo jezi namba 10 ataikabidhi kwa Rodrygo

Kombe la Dunia 2022 Nchini Qatar inaweza kuwa mara ya mwisho kwake kuichezea Brazil

Soma > https://jamii.app/NeymarBrazil

#JamiiForums #JFSports
🤔12👍4
UKRAINE: Katibu Mkuu wa NATO, Jens Stoltenberg ameonya kuwa Vita kati ya Urusi na Ukraine inaweza kuendelea kwa miaka kadhaa

Inaripotiwa, hivi sasa Vikosi vya Urusi vinazidisha mashambulizi dhidi ya #Ukraine eneo la Mashariki mwa Nchi hiyo

Soma - https://jamii.app/NATOVita
😁9👍6😢3👎1