JamiiForums
52.5K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Charles Kichere (CAG): Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ambayo inahusika na Kusimamia, Kudhibiti na Kushtaki Kesi za Jinai Nchini ina upungufu mkubwa wa Watumishi kwa 89%, hiyo inachangia ucheleweshaji wa utoaji wa haki

Soma - https://jamii.app/CAGReport2022

#RipotiCAG #CAGReport2022
CAG: Tathmini ya ufanisi ya Miradi iliyokamilika imeonesha ktk Halmashauri 30, miradi yenye thamani ya Tsh. Bilioni 7.68 ilikuwa imekamilika lakini haitumiki

> Hii imehusishwa na sababu kadhaa ikiwemo ukosefu wa Umeme na Wataalamu

Soma https://jamii.app/CAGReport2022

#CAGReport2022
#CAGReport2022: Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali alibaini jumla ya Tsh. bilioni 19.72 zilikusanywa na Halmashauri 36 lakini hazikupelekwa benki

> Tsh. Bilioni 10.13 kati ya hizo ni kutoka iliyokuwa Halmashauri ya Wilaya ya Ilala

Soma - https://jamii.app/CAGReport2022
Charles Kichere (CAG): Mamlaka 46 za Serikali za Mitaa zilikuwa na dawa zilizoisha muda wake wa matumizi

> Dawa hizo zilizopitiliza Muda wa Matumizi kuanzia miezi mitatu hadi miaka 20 zilikuwa na thamani ya Tsh. bilioni 3.49 na hazikuteketezwa

Soma: https://jamii.app/CAGReport2022
KILIMANJARO: TAKUKURU imethibitisha kuchunguza sakata la aliyekuwa Meya wa Manispaa ya Moshi, Juma Raibu

> Tuhuma zinazomkabili ni pamoja na Matumizi Mabaya ya Ofini, Rushwa na kushiriki Sherehe ya wanaojihusisha na Mapenzi ya Jinsia Moja

Soma - https://jamii.app/MoshiTakukuru
SIMBACHAWENE: MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA YAMEKUWA 'FASHION'

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Bunge, Sera na Uratibu, George Simbachawene asema kwa sasa, si ajabu kukuta pengine matumizi ya Dawa hizo yanafanywa hata na watu wenye nafasi kubwa

Soma - https://jamii.app/DawaMatumiziTZ
CAG: MTU MMOJA APIMWA DAMU MARA 30 KWA SIKU

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere amesema alipokagua taarifa za Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwa mwaka 2020/21 alibaini kuna mtu mmoja imeonekana katika Nyaraka zake za Hospitali kuwa amefanyiwa vipimo vya damu (Full Blood Picture) mara 30 kwa siku moja

#CAGReport2022
CAG: MASHIRIKA 16 YANA MADENI ZAIDI YA MTAJI

Miongoni mwa Mashirika hayo ni Benki ya Maendeleo, Kampuni ya Magazeti ya Serikali, Shirika la Umeme Tanzania, Mamlaka ya Bandari, Shirika la Madini la Taifa na Bohari Kuu ya Dawa

Soma - https://jamii.app/CAGReport2022

#RipotiCAG
CAG: MALIPO YA BILIONI 2.44 HAYAKUIDHINISHWA

Ukaguzi umebaini Taasisi 9 zilifanya Malipo hayo bila kuidhinishwa na Maafisa husika

Ikiwa hakuna Mifumo Imara ya uidhinishaji malipo, kuna hatari ya Watumishi wasio waaminifu kutumia vibaya Fedha za Umma

Soma - https://jamii.app/DawaMatumiziTZ

#RipotiCAG
SUDAN KUSINI: RAIS AUNDA JESHI LINALOJUMUISHA PANDE HASIMU

Hatua hiyo ni kipengele muhimu cha Makubaliano ya Amani

Taifa hilo lilipata changamoto ya kumaliza vita ya wenyewe kwa wenyewe kati ya Majeshi ya Rais Kiir na Makamu Rais, Riek Machar

Soma - https://jamii.app/SudanKusini
WAZIRI MKUU WA IVORY COAST AJIUZULU

Patrick Achi amewasilisha barua ya kujiuzulu kwake na kwa Serikali yake. Alikuwa Waziri Mkuu wa Tatu katika kipindi cha miaka mitatu

Rais Alassane Outtara amekubali ombi hilo

Soma - https://jamii.app/WaziriAjiuzulu

#JFLeo
CAG: HALI YA MAGEREZA NI MBAYA, WAFUNGWA WANALALA VYUMBA VYA MABATI

Pia, Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali imesema nyumba za Watumishi wa magereza hazina Maji safi na ya kutosha, na mifumo ya majitaka ni chakavu

Soma - https://jamii.app/MagerezaTZ

#CAGReport2022
Je, wewe ungeongeza Sheria gani?

Mjadala zaidi > https://jamii.app/SheriaSokaMdau

#JamiiForums #Michezo
UBER YASITISHA HUDUMA ZAKE NCHINI TANZANIA

Kampuni ya #Uber imetangaza kusitisha huduma za UberX, UberXL na UberX Saver, ikizitaja nauli elekezi za LATRA kama sababu

Katika ujumbe wao kwa wateja, wameahidi kurejesha huduma pindi kanuni zikibadilishwa

Soma https://jamii.app/UberSitishaHuduma

#JamiiForums #UberTZ
TANZIA: MSANII MAUNDA ZORRO AFARIKI DUNIA

Mwanamuziki wa Bongo Fleva, #Maunda Zorro, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo (Alhamisi ya Aprili 14, 2022) kufuatia ajali ya gari Kigamboni, Dar

Mwili wa marehemu upo Hospitali ya #Kigamboni

Soma https://jamii.app/MaundaZorroAfariki

#JamiiForums
AFRIKA KUSINI: MAFURIKO YAUA TAKRIBAN WATU 306

Mvua zimesababisha maporomoko ya udongo na kusomba makazi ya watu

Idadi ya waliofariki inatarajiwa kuongezeka wakati zoezi la utafutaji na uokoaji likiendelea katika Jimbo la KwaZulu-Natal

Soma - https://jamii.app/MafurikoSauzi

#JFLeo
CAG: Mamlaka 22 za Serikali za Mitaa hazikuwa na programu iliyohuishwa ya kuzuia Virusi katika Kompyuta kwa ajili ya kulinda Taarifa zake

Mamlaka 23 hazikuwa na mpango wa mafunzo ya kuwajengea uwezo Watumishi katika Usalama wa Taarifa

Soma - https://jamii.app/CAGReport2022

#RipotiCAG
CAG: Malimbikizo ya mishahara na madeni ya Watumishi wa Mashirika na Taasisi za Umma ni Tsh. Bilioni 2.72 na hii ni kuanzia mwaka 1 hadi miaka 7

> Mashirika hayo ni kama Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere na Chuo Kikuu Mzumbe

Soma - https://jamii.app/CAGReport2022
👍2
CAG: Tathmini imeonesha Mamlaka 10 za Serikali za Mitaa zilitekeleza Miradi ya Ujenzi yenye viwango duni vya ubora iliyo na thamani ya Tsh. Bilioni 6.06

Baadhi ya mapungufu ni nyufa kwenye Majengo, huku mengine yakiwa na Misingi iliyotitia

Soma - https://jamii.app/CAGReport2022

#RipotiCAG
SERIKALI YATENGA TSH. BILIONI 10 UJENZI SOKO LA KARIAKOO

Waziri Innocent Bashungwa asema Fedha hizo ni kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa soko jipya na kukarabati Soko kuu lililoungua

Pia, Wizara hiyo imeomba kuidhinishiwa Trilioni 8.76 na Bunge

Soma - https://jamii.app/UjenziKariakoo