JamiiForums
52.8K subscribers
34.4K photos
2.44K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Wizara ya Afya Nchini #Kenya imelegeza masharti ya kupambana na #COVID19 ikiwemo kuondoa ulazima wa kuvaa Barakoa kwenye maeneo ya umma

Pia, Wagonjwa wasio na dalili hawatatengwa na hakutakuwa na ulazima wa kukaa Karantini kwa wenye virusi

Soma - https://jamii.app/COVID19Mask
#UVIKO3
JE, WAJUA? - KUTUMIA UGONJWA KUOMBA FEDHA BILA KIBALI NI KOSA KISHERIA

Wakili wa Kujitegemea, Justine Kaleb anasema Mgonjwa akitaka kuombaomba Mtaani lazima apate kibali maalum cha Serikali au Taasisi zinazotambua Ugonjwa wake

Kufanya tofauti na hivyo adhabu yake ni kifungo cha miaka mitatu jela au faini ya Tsh. milioni tano au vyote kwa pamoja

Soma - https://jamii.app/Ombaomba
#JFLeo
TANZIA: RAIS RUPIAH BANDA AFARIKI DUNIA

> Aliyewahi kuwa Rais wa #Zambia, Rupiah Banda amefariki dunia akiwa na miaka 85. Aligundulika kuwa na saratani ya utumbo

> Banda ni Rais wa 4 wa Zambia aliyechaguliwa kidemokrasia na aliongoza kuanzia mwaka 2008 hadi 2011

Soma https://jamii.app/RupiaBanda

#RIPBanda
SERIKALI YAPENDEKEZA BAJETI YA TSH. TRILIONI 41 MWAKA 2022/23

Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Tsh. Trilioni 28, sawa na 70% ya Mapato itatokana na makusanyo ya ndani

Bajeti itagusa Maendeleo ya Jamii hususani Sekta ya Kilimo

Soma - https://jamii.app/MapendekezoBajeti

#JFLeo
UNHCR: WATU MILIONI 12.5 WAMEATHIRIKA NA MZOZO WA #URUSI NA #UKRAINE

Shirika la Umoja wa Mataifa Linalohudumia Wakimbizi (UNHCR) limeripoti watu zaidi ya milioni 4.4 wamelazimika kuhama makazi yao

> Walioathirika zaidi ni Wazee, Watoto na Wanawake

Soma https://jamii.app/AthariMzozo
CCM: MWENENDO WA JESHI LA POLISI UCHUNGUZWE

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM imeagiza Serikali ilichunguze Jeshi la Polisi baada ya Wananchi kupoteza imani nalo

> Imedaiwa, Polisi hutenda majukumu bila kufuata Mwongozo wa Kisheria (PGO)

Soma https://jamii.app/PolisiCCM
RAIS SAMIA AAGIZA KANUNI ZA MIKUTANO YA SIASA KUANDALIWA

Rais Samia Suluhu Hassan ameagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge kwa kushirikiana na TLS pamoja na ZLS kuandaa Kanuni zitakazoelekeza namna ya kufanya mikutano ya hadhara ya Vyama vya Siasa

Soma - https://jamii.app/AgizoMikutanoSiasa

#JFLeo
MAKONDA: KUNA BAADHI YA MAAFISA WA POLISI WANALIPAKA TOPE JESHI LA POLISI

Aliyekuwa RC wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema baadhi ya Polisi hulinda Wafanyabiashara wakubwa wanaodhulumu mali za watu

> Ameunga mkono mienendo ya Polisi kuchunguzwa

Soma https://jamii.app/MakondaPolisi
MAKONDA: GHALIB USINILAZIMISHE KUSEMA UOZO WENU. WALIO NYUMA YENU NAWAJUA

Kauli hiyo ya Paul Makonda ni baada ya Wakili wa Ghalib Said Mohamed (GSM) kuweka vielelezo vinavyoonesha Ghalib ndiye Mmiliki wa kiwanja kilichopo Regent Estate Kinondoni

Soma - https://jamii.app/JFSiasa
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: KIWANDA CHA GSM CHAWAKA MOTO

> Kiwanda cha kutengeneza magodoro kinachomilikiwa na Kampuni ya GSM kilichopo Mikocheni jijini Dar es Salaam kimeungua moto

Chanzo cha moto huo bado hakijajulikana kwa sasa

Soma - https://jamii.app/MotoGSM

#JamiiForums #JFLeo
UINGEREZA: SERIKALI KUWALIPA WATAKAOWAPA MAKAZI RAIA WA UKRAINE

Raia watakaoruhusu wanaokimbia mapigano Ukraine kukaa nyumbani kwao/ kuwapa eneo kwa kipindi kisichopungua miezi 6 watalipwa Paundi 350 (Takriban Tsh. 1,065,143.415) kwa mwezi

Soma - https://jamii.app/UKRaiaMalipo

#JFLeo
MADAI SUMU MTO MARA, SERIKALI YAZUIA MATUMIZI YA MAJI, UVUVI, ULAJI SAMAKI

Baada ya kuwepo kwa taarifa za sumu katika maji ya Mto Mara, tamko la Serikali ya Mkoa wa Mara limezuia matumizi ya maji kwa Vijiji kando ya mto huo

Soma - https://jamii.app/MtoMara

#JamiiForums #MtoMara
UKRAINE: Urusi imeishambulia Kambi ya Kijeshi ya #Ukraine, Yavoriv ambayo ilikuwa inatumika na NATO kuwapa mafunzo Wanajeshi wa Nchi hiyo

> Watu 35 wameuawa katika shambulio hilo, 134 wamejeruhiwa na makombora 30 yameharibiwa

Soma - https://jamii.app/UkraineNATO

#RussiaUkraineWar
VITA YA #URUSI NA #UKRAINE: Shirika la Afya Duniani limesema kiwango kidogo cha utoaji chanjo nchini Ukraine kitaongeza madhara ya COVID-19 kipindi hiki cha vita

> Vifo 8,012 vya Corona vimerekodiwa nchini humo kuanzia Machi 6 hadi 9, 2022

Soma https://jamii.app/CoronaVita
SONGWE: Basi la #Kilimanjaro Express limepata ajali kwa kupinduka asubuhi ya leo Machi 14, 2022 likitokea Tunduma kuelekea Dar es Salaam

> Taarifa za awali zinasema watu kadhaa wamejeruhiwa huku chanzo cha ajali hiyo kikiwa bado hakijafahamika

Soma > https://jamii.app/SongweAjali
#UKRAINE: Brent Renaud (50), Mwandishi wa Habari wa #Marekani aliyekuwa akifanyakazi nchini humo ameuawa kwa kupigwa risasi na Wanajeshi wa #Urusi Mjini Irpin

> Pia, Waandishi wa Hahari wengine wawili wamejeruhiwa akiwemo mmoja toka Italia

Soma https://jamii.app/BrentRenaud
#JFLeo
MDAU: KUMPA MTOTO UHURU WA KUJIELEZA KWENYE FAMILIA SIO UZUNGU

Ushiriki wa Mtoto kwenye masuala yanayomuhusu unapatikana pale anapopewa nafasi ya kutoa mawazo kuhusu maamuzi ya Maendeleo yake

Familia zinazowapa Watoto uhuru wa kujieleza na kutoa maoni yao kuanzia kwenye umri mdogo humuandaa Mtoto katika kutafuta Haki zake za Msingi mbele ya Jamii kubwa zaidi

Soma - https://jamii.app/FreeSpeecChild
#FreeSpeech
UPDATE: Watu wanne wamefariki dunia huku wengine 35 wakijeruhiwa katika ajali ya basi la Kilimanjaro Express lililopindukia korongoni eneo la Senjele Wilayani Mbozi Mkoa wa Songwe

Ajali hiyo imetokea baada ya Dereva kuwa kwenye mwendokasi

Soma - https://jamii.app/SongweAjali

#JFLeo
Ripoti ya Uwajibikaji Serikali Kuu na Mashirika ya Umma 2019-2020 imeonesha Miradi iliyosajiliwa na TIC (Kituo cha Uwekezaji) kwa Mwaka 2015/16 ni 420, wakati kwa Mwaka 2019/20 ilisajiliwa Miradi 219. Idadi hiyo imeshuka kwa asilimia 48

#JamiiForums #JFUwajibikaji #Accountability #WAJIBU