JamiiForums
52.7K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Dkt. Ahmed Yousef wa Hospitali ya Chuo Kikuu cha Aga Khan amesema 15% hadi 20% ya wenye matatizo ya Nguvu za Kiume huteseka kimyakimya

Dalili ni kushindwa kushiriki Tendo kwa Dakika 15 mfululizo, kushindwa kusimamisha na kuwahi kumaliza

Soma - https://jamii.app/UpandikizajiUume

#JFAfya
Wadau wa Jukwaa la Elimu ndani ya JamiiForums.com wametaja mbinu kadhaa zilizokuwa zinatumika kukariri Sayari ikiwemo, "Mama Veronica Endeleza Mapishi Jikoni Sitaki Ugali Nataka Pilau"

Ulitumia njia gani kufahamu Formula na Mipangilio ukiwa Shuleni?

Mjadala zaidi > https://jamii.app/FormulaShule

#JFMdau
TETEMEKO LATOKEA MPANDA, KATAVI

Tetemeko la Ardhi la kipimo cha Richa 4.6 limeripotiwa kutokea Mpanda, Katavi usiku huu

> Hakuna taarifa ya kifo madhara yoyote yalioripotiwa hadi sasa. JamiiForums inaendelea kufuatilia kwa karibu tukio hilo

Soma https://jamii.app/TetemekoKatavi

#JFMatukio
TANZANIA YAPATA MSAADA WA TSH. TRILIONI 1.15 KUTOKA ULAYA

Fedha hizo zitatumika ktk Miradi mbalimbali ya Maendeleo

Serikali imeainisha kutumia Tsh. Bilioni 480 (Euro Milioni 180) kwenye miradi mitatu ikiwemo kuimarisha Mifumo ya Kidijitali

Soma - https://jamii.app/TZFedhaUlaya

#Governance
MDAU ASHAURI VYA KUFANYA KUEPUKA AJALI ZA MOTO

Mshiriki wa #StoriesOfChange ashauri kuelimisha Jamii. Pia kuwa na Sheria ya kudhibiti mafundi holela

> Kufunga vifaa vya kutaarifu kuhusu moto. Vifaa vya kuzima moto vipatikane kwa bei nafuu

Soma https://jamii.app/MotoAjali

#JFMdau
RADI YAJERUHI WAWILI NGORONGORO

Jeshi la Polisi limesema Uchunguzi umebaini chanzo ni matumizi ya simu wakati mvua kubwa ikinyesha huku ikiambatana na radi kali

Waliojeruhiwa wamepata majeraha sehemu mbalimbali, na wanapatiwa matibabu Zahanati

Soma > https://jamii.app/2MvuaSimu

#JFMatukio
UGAWAJI WA MIRABAHA WAKOSOLEWA

Mtandao wa Sekta ya Ubunifu Tanzania(CINT) umesema mirabaha inapaswa kulipwa kwa kazi zote za ubunifu sio wanamuziki pekee

> COSOTA imekosolewa kukosa uwazi wa kanuni iliyotumika kugawa mirabaha

Soma https://jamii.app/MirabahaCOSOTA

#JFBurudani
NAPE: SHERIA INALENGA KUADHIBU MWANAHABARI SIO CHOMBO

Waziri wa Habari, Nape Nnauye amesema Sheria ya Habari ya 2016 inalenga kutoa leseni kwa wanahabari ili likitokea kosa aadhibiwe mtu sio Chombo cha Habari

> Nia ni kufanya tasnia ya habari kuwa taaluma

Soma https://jamii.app/KufungiaMtu

#PressFreedom
RUKWA: AMCHAPA MKEWE VIBOKO MPAKA KIFO

Kamanda wa Polisi Rukwa, ACP William Mwampaghale amesema Mwanaume huyo alianza kumshambulia Mkewe kwa fimbo maeneo mbalimbali ya Mwili na kusababisha kuvuja Damu nyingi kwa ndani na baadaye kusababisha mauti

Soma - https://jamii.app/KifoViboko

#JFMatukio #UkatiliKijinsia
SIKU YA KIMATAIFA YA HAKI ZA KIJAMII

Siku hii huangazia hitaji la kukuza Haki za Kijamii ambazo zinahusisha jitihada za kushughulikia masuala mbalimbali kama Umasikini, Ukosefu wa Usawa wa Kijinsia, Ajira na #HakiZaBinadamu

Soma - https://jamii.app/SJD2022

#SocialJusticeDay #SocialJustice
KAMATI YA KUCHUNGUZA MAUAJI YA MTWARA NA TANGA YAONGEZEWA SIKU 7

Kamati hiyo iliyoanza kazi Februari 4, 2022 ilipaswa kukamilisha ripoti yake Februari 17, 2022 ila imeomba muda zaidi kutokana na ukubwa wa kazi na kujiridhisha na baadhi ya masuala

Soma - https://jamii.app/KamatiMauaji7

#Accountability
NINI MAANA YA DHANA YA HAKI ZA KIJAMII?

Humaanisha uwepo wa Haki sawa kwa watu wote na uwezekano wa kila mtu, bila ubaguzi, kufaidika na Maendeleo ya Kiuchumi na Kijamii

Baadhi ya Haki za Kijamii ni pamoja na Usawa mbele ya #Sheria na Haki ya kupata Huduma za Afya

Soma - https://jamii.app/SJD2022

#SocialJusticeDay #SocialJustice
NIGER: Watoto saba (7) wameuawa na wengine watano (5) kujeruhiwa vibaya nchini humo baada ya shambulizi la anga la Jeshi la #Nigeria lililolenga wapiganaji walioko mpakani

> Mamlaka zinaendelea kufuatilia tukio hilo

Soma https://jamii.app/NigeriaNiger

#JFMatukio
HISTORIA: Chips za Viazi (Crisps) zilianza kutengenezwa Mwaka 1853 baada ya Mmarekani mweusi, George Speck (Mpishi) kupokea malalamiko ya Mteja akimlaumu kuwekewa Viazi vyenye mapande makubwa sana

Inadaiwa ili kuwakomoa Wateja, Speck alianza kukata vipande vidogovidogo mfano wa Karatasi lakini Wateja wakatokea kuvipenda sana.

Soma zaidi - https://jamii.app/SaratogaChips

#JFHistoria
40% YA WATU HAWATUMII LUGHA MAMA KWENYE ELIMU

Shirika la UN linalohusika na Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limesema Jamii hizo zimelazimika kufahamu Lugha zaidi ya moja

Februari 21 ni Siku ya Kimataifa ya Lugha Mama

Soma - https://jamii.app/LughaMama

#MotherLanguageDay #JFLugha
MALEZI: TUNZA AFYA YA MTOTO KWA KUMFUNDISHA USAFI

Usafi wa Kinywa: Mpigishe Mtoto Mswaki kila siku Asubuhi na ikiwezekana kila baada ya kula. Mfundishe namna ya kuswaki vizuri ili kuzuia kuoza kwa Meno na Magonjwa ya Fizi

Usafi wa Mikono: Wafundishe Watoto kunawa Mikono kwa Maji safi na sabuni kila wanapotoka Kucheza, kabla ya Kula, baada ya Kula na baada ya kutoka Maliwato

Soma - https://jamii.app/UsafiWatotoAfya

#JFMalezi #Parenthood
Uwajibikaji unapima kiwango ambacho Serikali inatekeleza majukumu yake katika kueleza na kuhalalisha Maamuzi yake kwa Umma

Ufanisi mkubwa wa #Uwajibikaji unaainishwa kwa namna ambavyo Wadai Haki/Wananchi wanaelezea mahitaji yao, lakini pia unahusiana na Nafasi, Uwezo na Utayari wa Watendaji kuwajibika kwa Matendo

Soma - https://jamii.app/UwajibikajiUfanisi
#Accountability #Democracy
MAGU: WAVUNJA MAKABURI NA KUIBA MISALABA, NONDO

Wananchi wamedai baadhi ya Makaburi yameharibiwa na kuachwa wazi au na mianya mikubwa huku vitu vikiibwa

Mkuu wa Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza, Salum Kalli ameagiza wahusika wasakwe na kutiwa nguvuni

Soma - https://jamii.app/MakaburiMagu

#JFUwajibikaji
LINDI: Wanachama Wanne wa CHADEMA wamehukumiwa kifungo cha miaka 8 kwa kosa la kuharibu mali na kujeruhi watu wakiwemo Askari Polisi siku ya Uchaguzi Mkuu (Oktoba 28, 2020)

Katika utetezi walisema wahurumiwe kwa madai wana Familia zinazowategemea

Soma - https://jamii.app/LindiChadema

#JFSiasa