JamiiForums
βœ”
52.9K subscribers
34.3K photos
2.43K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Jamii Forums kwa kushirikiana na Muhimbili University of Health and Applied Science (MUHAS), Muhimbili National Hospital (MNH), Tumaini la Maisha (TLM) na Wadau wengine wameandaa Mjadala utakaofanyika kupitia Clubhouse ya JamiiForums ili kuongeza uelewa juu ya Saratani kwa Watoto Nchini #Tanzania

Mjadala huu unatarajiwa kufanyika Jumanne, Februari 15, 2022

Link > https://jamii.app/MjadalaSarataniWatoto

#JamiiForums #CancerDay2022 #JFAfya
Marekani imetangaza dau la takriban Tsh. Bilioni 11.5 kwa atakayetoa taarifa zitakazofanikishwa kukamatwa kwa Kiongozi wa Waasi Nchini #Uganda, Joseph Kony

Joseph Kony ni kiongozi wa Kundi la Waasi la LRA na amesababisha mauaji zaidi ya 100,000

Soma - https://jamii.app/JosephKony

#JFMatukio
MAREKANI YAAHIRISHA UTOAJI WA CHANJO YA #COVID19 KWA WATOTO

Utoaji wa Chanjo kwa Watoto wenye miezi 6 hadi miaka 4 umeahirishwa baada ya idara ya Chakula na Dawa (FDA) kuhitaji Data zaidi

Chanjo hiyo ingeanza kutolewa Februari 21, 2022

Soma - https://jamii.app/COVID19Variants

#UVIKO3 #JFAfya
AFYA: Kwa mujibu wa Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (CDC) mtu anaweza kupata madhara kiafya ikiwa kukosa usingizi wa kutosha ni sehemu ya maisha yake ya kila siku

Ili kupata usingizi mzuri, inashauriwa kuweka pembeni vifaa vya kielektroniki wakati wa kulala. Pia, kufanya mazoezi ya mwili kunaweza kukusaidia kulala kirahisi

Soma - https://jamii.app/AfyaUsingizi

#JFAfya
UJERUMANI: RAIS FRANK-WALTER STEIMEIER ACHAGULIWA KUONGOZA MUHULA WA PILI

Ameungwa Mkono na Vyama vyote 3 vinavyounda Serikali ya Mseto, pamoja na Chama cha Upinzani cha Wahafidhina cha CDU

Wadhifa wa Rais Nchini Ujerumani ni wa Heshima

Soma - https://jamii.app/RaisUjerumani

#Governance
SPIKA TULIA: HALIMA MDEE NA WENZAKE WAPO BUNGENI KIHALALI

Amesema, "Nchi yetu inaendeshwa Kisheria. Jambo moja tu linalosubiriwa ni watu kumaliza michakato yao inayohusika"

Ameeleza, Mtu anakosa Uhalali wa kuwepo Bungeni akifukuzwa Uanachama

Soma - https://jamii.app/UhalaliWabunge19

#Democracy #JFSiasa
MDAU: VIJANA TUSIISHI KWA NADHARIA, MAZOEA NA KUKARIRI

Anasema kati ya vitu vinavyofelisha sana Vijana ni kuogopa kuthubutu, akieleza wamekuwa waoga na wenye aibu kupindukia

Asema masuala ya "watanionaje au watanichukuliaje" yamefanya wazidi kuwa masikini

Msome - https://jamii.app/MafanikioSOC

#StoriesOfChange #JFMdau
WAZIRI MKUU: HUWEZI KUZUNGUMZIA UTALII BILA KUWATAJA WAMAASAI

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema hauwezi kuzungumzia Utalii wa #Tanzania bila kutaja Wamaasai na suala la wao kuishi na Wanyamapori Hifadhi ya Ngorongoro linavutia

Soma - https://jamii.app/WamaasaiNgorongoro

#Utalii #JFLeo #Governance
SARATANI KWA WATOTO: Kila mwaka, inakadiriwa takriban Watoto/Vijana 400,000 wa umri kuanzia 0 - 19 hupata Saratani

Katika Nchi zilizoendelea zaidi ya 80% ya Watoto hupona. Kwa Nchi zenye kipato cha Chini na Kati, Watoto chini ya 30% ndiyo hutibiwa

Soma - https://jamii.app/ChildCancers

#JFAfya
Shirika la UN linaloshughulika na Idadi ya Watu (UNFPA) linasema Wasichana milioni 12 Duniani huolewa kabla ya kufikisha miaka 18

Kwa siku ya wapendanao, UNFPA wanasema β€˜Mtaje Valentine wako, lakini tafadhali asiwe Mtoto’

Soma - https://jamii.app/ChildMarriage

#EndChildMarriage #HakiMtoto
PARIS, UFARANSA: Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amekutana na kuzungumza na Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron katika Ikulu ya ElysΓ©e leo Februari 14, 2022

Rais Samia yupo Nchini Ufaransa kwa ziara ya kikazi

Soma - https://jamii.app/RaisSamiaParis

#JamiiForums #Governance
MBOWE: TUMEKOSA HAKI YA CHAKULA MCHANA KWA MIEZI MITANO

Amesema, "Mwanzo tuliambiwa kuwa kama Chakula tuchukue kutoka Jela, tutoke nacho Jela tuje nacho Mahakamani. Tukitoka hapa tunakuta Magereza wameshakula tunakwenda kulala na njaa siku zote"

Soma - https://jamii.app/MboweHakiChakula

#JFSiasa
MARA: KIZIMBANI KWA TUHUMA ZA KUMUUA MJUKUU WAKE

Nkwandu Kayenze (76) Mkazi wa Natta, Wilayani Serengeti amefikishwa Mahakamani kwa kosa la kumpiga na kumsababishia kifo Matoja Deus (11) aliyetumia Tsh. 2,000 bila ruhusa

Soma https://jamii.app/MaraBibi

#JFMatukio
KENYA: Kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Agosti, Serikali imewahakikishia Washirika wake wa Maendeleo utayari wao kuhakikisha Makabidhiano ya Madaraka yanafanyika kwa Amani

Usalama kuimarishwa ili kutoa usaidizi kwa Tume

Soma https://jamii.app/KEGovTransition

#KenyaElections #Democracy
SUDAN: Waandamanaji wawili wameuawa na Vikosi vya Usalama ktk harakati za kuwatawanya wanaopinga Utawala wa Kijeshi na kuachwa huru waliokamatwa baada ya mapinduzi Oktoba 2021

> Idadi ya waliouawa tangu kuanza kwa maandamano hayo imefikia 80.

Soma https://jamii.app/SudanProtestors

#Democracy #HumanRights
Jamii Forums kwa kushirikiana na Muhimbili University of Health and Allied Science (MUHAS), Muhimbili National Hospital (MNH), Tumaini la Maisha (TLM) na Wadau wengine wameandaa Mjadala utakaofanyika kupitia Clubhouse ya JamiiForums ili kuongeza uelewa juu ya Saratani kwa Watoto Nchini #Tanzania

Mjadala huu unatarajiwa kufanyika leo Februari 15, 2022

Link > https://jamii.app/MjadalaSarataniWatoto

#JamiiForums #CancerDay2022 #JFAfya
WAWILI WADAIWA KUFARIKI KUTOKANA NA KIPIGO CHA POLISI

Gazeti la Mwananchi limeripoti kufariki kwa Koba Ndalu(23) wa Morogoro na Jacob Elias wa Tabora

Walikamatwa kwa makosa ya Wizi ambapo Koba alifariki Februari 7 na Jacob alifariki Februari 12, 2022

Soma - https://jamii.app/TaboraMorogoro

#JFMatukio
MALI: Kwa mujibu wa Maafisa wa Fedha Afrika Magharibi, Nchi hiyo imeshindwa kulipa Madeni yanayofikia Euro Milioni 81 katika Soko la Fedha la Ukanda huo

Siku kadhaa zilizopita, Serikali ya Kijeshi ilitoa rai ya kuondolewa vikwazo vilivyowekwa ikionya vitaleta madhara makubwa kiuchumi na kijamii

Soma - https://jamii.app/MadeniMali

#JFUchumi #Governance