JamiiForums
54.1K subscribers
34K photos
2.25K videos
30.9K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
'THE AFRICAN RENAISSANCE': SANAMU REFU ZAIDI BARANI AFRIKA

Sanamu inapatikana Nchini #Senegal na ina urefu wa Mita 49. Ilizinduliwa Aprili 2010 na aliyekuwa Rais kwa wakati huo, Abdoulaye Wade

Sanamu hii ilikusudiwa kuashiria ushindi wa ukombozi wa Afrika na kushindana na Statue of Liberty na Eiffel Tower kama kivutio cha Watalii

Soma - https://jamii.app/AfricanRenaissance

#JFMaarifa #JFHistoria
#AUSTRIA: KUANZIA FEBRUARI WASIOCHANJWA KUTOZWA FAINI HADI TSH. 9,414,826

Kuanzia Februari Chanjo kwa Watu wazima itakuwa ni lazima na wote ambao watagoma kuchanjwa watatozwa faini

Sheria hiyo imepangwa kutumika hadi Januari 31, 2024

Soma - https://jamii.app/MustVaccineAustria

#UVIKO3 #JFAfya
AFGHANISTAN: Mullah Hasan Akhund anayekaimu nafasi ya Waziri Mkuu wa Nchi hiyo amesema Utawala wa #Taliban umekidhi vigezo vyote hivyo utambuliwe na Serikali za Kimataifa

Serikali zimekuwa zikisita kuitambua Taliban tangu ichukue Madaraka Agosti 2021

Soma - https://jamii.app/UongoziTaliban

#Governance
MDAU: BAADHI YA WANAUME HUTUMIA POSA KUWALAGHAI WANAWAKE

Anasema kutokana na Wanawake wenye msimamo kutokukubali kufanya baadhi ya mambo bila utambulisho wowote kwa Wazazi, hupelekea Wanaume kutafuta washenga uchwara na baadaye kuingia Mitini bila Kuoa

Anafafanua, Posa zisizokamilika kuwa Ndoa husababisha Msongo wa Mawazo na Mfadhaiko wa Akili kwa Mwanamke na huleta hali ya kukata tamaa ya maisha

Soma - https://jamii.app/PosaFeki

#StoriesOfChange #JFMdau
UINGEREZA: WABUNGE WAWASILISHA BARUA ZA KUTOKUWA NA IMANI NA BORIS

Wabunge 11 wa Chama cha Kihafidhina cha Waziri Mkuu, Boris Johnson wamewasilisha barua za kutokuwa na imani na Kiongozi huyo

Kisheria barua 54 zinahitajika ili kutekeleza kura hiyo

Soma https://jamii.app/KuraImaniBoris

#Accountability
UJERUMANI YAREKODI MAAMBUKIZI MAPYA 112,323

Imetajwa kuwa idadi kubwa zaidi tangu kuanza Mlipuko wa #COVID19. Maambukizi yamefikia 8,186,850

Waziri wa Afya anaamini idadi ya Visa ambavyo havijaripotiwa ni mara mbili ya takwimu za sasa

Soma - https://jamii.app/VisaUjerumani

#UVIKO3 #JFAfya
MDAU: FAIDA ITAKAYOPATIKANA TAIFA LIKIWEKEZA KWA VIJANA

Kupunguza utegemezi wa Wataalamu kutoka Nje: Taifa likiwekeza vya kutosha na kwa ubora, uhakika wa kupata wataalamu mbalimbali utakuwepo

Kukuza Biashara, Uchumi wa Nchi na Maendeleo: Taifa likiwekeza kwa Vijana, litajihakikishia kukuza Uchumi na kurahisisha kukua kwa Maendeleo

Soma - https://jamii.app/VijanaSOC

#StoriesOfChange #JFMdau
AFYA: SEHEMU ZA SIKIO AMBAZO HUWEZA KUATHIRIWA KIAFYA

1. Sikio la nje: Huwa na Ngozi laini ambayo inaweza kuumizwa kwa vidonda au kujikuna kwa kidole kichafu au kwa kutumia vijiti

2. Sikio la kati: Inaweza kupata matatizo kama kiwambo cha Sikio kuumizwa kwa kuingiza kitu ndani ya sikio, mlio mkubwa au Bakteria

3. Sikio la ndani: Huumia kama kelele zimezidi au kupokea mlio mkubwa wa mlipuko wa karibu unaoweza kuharibu Neva ndogo

Soma - https://jamii.app/AfyaSikio

#JFAfya
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema Serikali itatekeleza uwekaji wa mfumo wa anwani za makazi kwa Miezi 5 badala ya Miaka 5

Lengo ni kuboresha Mawasiliano katika sehemu mbalimbali ikiwemo makazi, sehemu za biashara na huduma za kijamii

Soma - https://jamii.app/MfumoAnwani

#Governance
UINGEREZA YALEGEZA KANUNI ZA #COVID19

Barakoa hazitokuwa lazima maeneo ya Umma na Shule. Raia hawataendelea kusisitizwa kufanya kazi Nyumbani

Wanasayansi wanaamini Wimbi la maambukizi yaliyotokana na Kirusi cha #Omicron limefikia kilele

Soma - https://jamii.app/KanuniCoronaUK

#UVIKO3 #Governance #JFAfya
AFGHANISTAN: RAIA ZAIDI YA LAKI 5 WAPOTEZA AJIRA SABABU YA TALIBAN

Shirika la Kazi Duniani (ILO) limesema idadi ya ajira zilizopotea huenda zikafikia Laki tisa ifikiapo katikati ya 2022

Makundi athirika ni Wanajeshi, Majaji na Wanawake

Soma - https://jamii.app/ILOAjiraAfghan

#HumanRights
KAZAKHSTAN: WAZIRI WA ULINZI ATIMULIWA KUTOKANA NA GHASIA

Rais Kassym-Jomart Tokayev amemtuhumu Murat Bektanov kutosimama ktk nafasi yake Nchi ilipopata ghasia

Rais alilazimika kuomba Wanajeshi wa Sovieti wakiongozwa na Urusi ili kutuliza ghasia

Soma - https://jamii.app/BektanovRemoved

#Governance
MAREKANI: Mahakama yakataa ombi la Donald Trump la kuzuia kutolewa rekodi za White House kwa jopo linalochunguza vurugu zilizotokea eneo la Bunge

Wafuasi wake walikusanyika kujaribu kusimamisha uidhinishaji wa matokeo ya Uchaguzi wa Urais 2020

Soma - https://jamii.app/TrumpMahakama

#Accountability
ALGERIA: SHULE ZAFUNGWA KUDHIBITI MAAMBUKIZI YA CORONA

Serikali imezifunga Shule kwa muda wa siku 10 na kuimarisha upimaji katika Viwanja vya Ndege kufuatia ongezeko la maambukizi

Wananchi wahimizwa kupata Chanjo ili kupambana na #COVID19

Soma https://jamii.app/COVIDAlgeria

#UVIKO3 #Governance #JFElimu
UMUHIMU WA KUWA NA SHERIA YA ULINZI WA DATA

Maendeleo ya Teknolojia yanaweza kuathiri Ulinzi wa Data Binafsi za Watu, hivyo uwepo wa Sheria hii utawalinda dhidi ya athari zinazoweza kujitokeza

Itahakikisha Haki ya Faragha inasimamiwa na kutekelezwa kwa vitendo kama ilivyoandikwa kwenye Katiba ya Tanzania

Soma - https://jamii.app/UlinziDataTZ

#DataProtection #DigitalRights
MDAU: KIONGOZI NI KIUNGO. ANAPASWA KUWA NA HEKIMA NA ULIMI WENYE STAHA

Kiongozi bora ni kuwa na Ubongo wenye Hekima, unaowaza, kuainisha, kuchambua, na kuweza kufanya tathmini. Awe na kinywa chenye maneno ya uhakika, weledi na nasaha bora

Aghalabu Vitu hivyo vikichagizwa na Kifua kilicho na Moyo wa Wema, Utu na Busara, pasipo na shaka Haki, Umoja, Upendo, Amani vitatamalaki katika Taifa

Soma zaidi - https://jamii.app/StahaKiongozi

#StoriesOfChange #Governance
'SERVER' ZA MSALABA MWEKUNDU ZADUKULIWA. TAARIFA ZA MAELFU ZAATHIRIWA

Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu (ICRC) imesema Taarifa Binafsi za Watu zaidi ya 500,000 zimeathiriwa ktk shambulio hilo, na waliohusika hawajajulikana

Soma - https://jamii.app/ICRCHacked

#DataProtection #DigitalRights
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum imetoa siku 30 hadi Februari 18, 2022 kwa Makao ya watoto yasiyo na leseni kuwasilisha maombi ya usajili

Hadi kufikia Januari 2022, Makao ya Watoto 244 kati ya 473 ndiyo yaliyokidhi vigezo na kupata leseni huku Makao 229 yakiendeshwa kinyume cha taratibu

Soma - https://jamii.app/UsajiliMakaoWtt

#ChildSafety #HakiMtoto
NAFASI YA VYOMBO HURU VYA HABARI KATIKA MAENDELEO YA JAMII

Mdau wa JamiiForums anasema Vyombo vya Habari vinapokuwa Huru vitaweza kuandaa Mijadala ya wazi ya Kimaendeleo bila kuogopa kuchokoza upande wowote kihoja

Wanahabari wataweza kuandaa mijadala ya kisiasa, kuhoji na kutoa mtazamo bila hofu, na hivyo kupatikana suluhisho ya matatizo ya Wananchi

Msome - https://jamii.app/HabariUhuruSOC

#StoriesOfChange #PressFreedom
DKT. TULIA APITISHWA KUWA MGOMBEA WA USPIKA

Dkt. Tulia Ackson ambaye amekuwa akihudumu kama Naibu Spika wa Bunge amepitishwa na Kamati Kuu ya CCM kuwa Mgombea wa nafasi ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Soma - https://jamii.app/DktTuliaUspika

#Democracy #Governance