JamiiForums
βœ”
52.5K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
#COVID19: Shirika la Watoto la Umoja wa Mataifa (UNICEF) limesema Nchi tajiri zinagawia Nchi masikini chanjo zinazokaribia kuisha muda wake wa matumizi

Mataifa masikini yatajwa kuwa na changamoto ya ukosefu wa vifaa vya uhifadhi wa chanjo

Soma - https://jamii.app/ChanjoUNICEF

#UVIKO3
ARUSHA: Mahakama ya Hakimu Mkazi imemkuta na kesi ya kujibu aliyekuwa DC wa Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wanaokabiliwa na kesi ya Uhujumu Uchumi

Washtakiwa wataanza kujitetea Januari 17 wakiwa na mashahidi wasiozidi 10 na vielelezo kadhaa

Soma - https://jamii.app/SabayaKesiUhujumu

#Accountability
IKULU, CHAMWINO: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amepokea Hati za Mabalozi wa Nchi 4

Mabalozi waliowasilisha Hati zao Ikulu Mkoani Dodoma leo Januari 14, 2022 ni wa Saudi Arabia, Jamhuri ya Korea, Indonesia na Morocco

Soma https://jamii.app/Mabalozi

#Governance
DODOMA: JELA MIAKA MIWILI KWA KUJIFANYA AFISA WA TRA

Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma imemhukumu Mkazi wa Dar es Salaam, Kitareti Mahuti kwa kosa la kutumia kitambulisho bandia cha TRA kuwatapeli watu kwa kuwatishia kuwapa makosa mbalimbali

Soma - https://jamii.app/TapeliJela

#JFMatukio
MOROGORO: WATAKAOSHINDWA KUPELEKA WATOTO SHULE KUKAMATWA

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Alhaji Majdi Mwanga ameandaa mikataba kati ya Wazazi kuhusu kudhibiti tabia za baadhi yao kuwa chanzo cha Wanafunzi kukatisha Masomo na kukosa Haki ya kupata Elimu

Soma - https://jamii.app/WazaziWalezi

#JFElimu
AL-SHABAAB YATISHIA KUSHAMBULIA KENYA

Wapiganaji hao wametuma ujumbe wa kuishambulia #Kenya kama kisasi cha uwepo wa Majeshi yake Nchini Somalia

Watu 13 wameuawa tangu kuanza mwaka 2022. Vifo vimehusishwa na wapiganaji wa Al-Shabaab

Soma - https://jamii.app/KenyaAlShabaab
UGANDA KUHARIBU DOZI ZAIDI 400,000 ZILIZOISHA MUDA

Kasi ndogo ya utoaji Chanjo dhidi ya #COVID19 imesababisha Chanjo za Moderna na #AstraZeneca kuisha muda wa matumizi

Dozi 12,220,106 zimetolewa hadi sasa. Uganda imerekodi Vifo 3,378

Soma - https://jamii.app/DoziLakiNne

#UVIKO3 #JFAfya
AUSTRALIA YAFUTA VISA YA NOVAK DJOKOVIC KWA KUTOCHOMA CHANJO YA #COVID19

Waziri wa masuala ya Uhamiaji amesema wamechukua uamuzi huo kwa kuzingatia Sheria ya Afya

Djokovic bado anaweza kufungua kesi nyingine kupinga kufukuzwa Nchini humo

Soma https://jamii.app/DjokovicVisaBan
#UVIKO3
MALEZI: NAMNA YA KUMSAIDIA MTOTO KUWA MTU BORA KWENYE JAMII

1. Mfundishe kufanya kazi kwa Ushirikiano (Teamwork). Mfano unaweza kutenga muda kusaidiana naye kwenye 'Homework' au majukumu ya Nyumbani

2. Shiriki au Mfundishe kupanga malengo pamoja na maono mliyonayo. Washirikishe Watoto kwenye uwekaji wa Sheria/Miongozo itakayowasaidia kitabia

Soma - https://jamii.app/MtotoBora
#Malezi
UGANDA: WANAFUNZI MILIONI 4.5 HAWATARUDI SHULE

Ripoti ya Mamlaka ya Mipango ya Taifa imeonesha Wanafunzi hao hawataweza kurudi Shule kwa sababu mbalimbali ikiwemo Ujauzito

Uganda imefungua Shule hivi karibuni baada ya kuzifunga kwa takriban miaka 2

Soma https://jamii.app/MilioniWanafunzi

#JFElimu
WHO YAPENDEKEZA DAWA MBILI KUTUMIKA KUTIBU #COVID19

Baricitinib imependekezwa kutumika kutibu wagonjwa mahututi wa #COVID19 na Sotrovimab kutumika kwa Corona isiyo kali

Dawa zimependekezwa baada ya majaribio saba yaliyohusisha watu 4,000

Soma - https://jamii.app/DawaCorona

#UVIKO3 #JFAfya
WATOA HUDUMA ZA 'MASSAGE' WATAKIWA KUJISAJILI KABLA YA MACHI 31, 2022

Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala limesema huduma ya 'Massage' ni tiba asili hivyo watoa huduma wanatakiwa kupata Mafunzo Maalum na Leseni ya kutoa huduma hiyo

Soma https://jamii.app/MassageService
#JFAfya
12.7% YA WALIOMALIZA KIDATO CHA NNE 2021 WAPATA SIFURI

NECTA imetangaza matokeo ya Kidato cha Nne. Wanafunzi 652,611 walifanya mitihani na 422,388 wamefaulu kwa kupata Daraja la Kwanza hadi Daraja la Nne sawa na 87.3%

> 19.24% wamefaulu Hisabati

Soma https://jamii.app/CSEE2021

#JFElimu
MATOKEO KIDATO CHA 4: WANAFUNZI WAONESHA UMWAMBA KWENYE KISWAHILI NA KEMIA

Katika wanafunzi waliofaulu mtihani wa kidato cha nne 2021, waliofaulu Kiswahili ni 95.58% na Kemia 92.02%

> Hisabati imeendelea kuwaburuza, waliofaulu Hisabati ni 19.24%

Soma https://jamii.app/CSEE2021

#JFElimu
WASICHANA WANG’ARA KUMI BORA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2021

Nafasi ya Kwanza hadi ya Saba zimeshilikiliwa na Wasichana, ya Nane na Tisa zimeshikiliwa na Wavulana

Nafasi ya Kumi pia imefungwa na Msichana

Soma - https://jamii.app/CSEE2021

#JFElimu
UN: WATU TAKRIBAN 108 WAMEUAWA TANGU JANUARI MOSI 2022 NCHINI #ETHIOPIA

Raia hao wameuawa ktk mashambulizi ya anga kwenye Jimbo la #Tigray

Mashambulizi yalifanyika dhidi ya Basi dogo, Uwanja wa Ndege na kambi ya Watu wasio na makazi

Soma - https://jamii.app/DeathTigrayJAN

#HumanRights
SHULE MOJA YA SERIKALI YAINGIA KUMI BORA

Mzumbe Sekondari iliyopo Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro imekuwa Shule pekee ya Serikali iliyoingia kumi bora

Imeshika nafasi ya kumi huku nafasi tisa za awali zikishikwa na Shule binafsi

Soma - https://jamii.app/CSEE2021

#JFElimu
UTAFITI: 2021 UMESHIKA NAFASI YA 6 KWA MIAKA YENYE JOTO ZAIDI

Ni kwa Takwimu za Shirika la Utafiti wa Anga za Mbali (NASA) na Idara ya Bahari na Anga(NOAA)

Wastani wa Joto ulikuwa nyuzi joto 1.51 za kipimo cha Celsius juu ya viwango vya karne ya 20

Soma https://jamii.app/2021JotoNo6