JamiiForums
βœ”
52.8K subscribers
34.4K photos
2.44K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
KUELEKEA MIAKA 60 YA UHURU: RAIS SAMIA AHUTUBIA TAIFA

- Rais Samia Suluhu Hassan anahutubia Taifa kuelekea maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanganyika (Tanzania Bara)

- Tanganyika ilipata Uhuru kutoka kwa Uingereza mnamo Desemba 09, 1961

Fuatilia: https://jamii.app/SamiaHotuba-Dec21
Rais Samia Suluhu Hassan katika kipindi cha miaka 60, Tanzania imefanikiwa kujenga Uchumi hadi kufikia Nchi ya Uchumi wa Kati wa Chini mapema kuliko ilivyokadiriwa kwenye Malengo ya Dira ya Taifa

Asema, "Wastani wa Pato kwa Mtu kwa mwaka 1961 lilikuwa Tsh. 776 na kwa mwaka jana 2020 ni Tsh. 2,653,790"

Soma - https://jamii.app/SamiaHotuba-Dec21
Rais Samia Suluhu Hassan amesema Tanzania imepiga hatua kubwa kwenye Miundombinu ya Umeme, akieleza kuwa kabla ya Uhuru Nchi ilikuwa na uwezo wa kuzalisha Megawati 17.5 za Umeme lakini sasa ni Megawati 1,909

Amesema, "Lengo letu ni kuendelea kuongeza uzalishaji wa umeme ili kuendana na malengo ya kugeuza Tanzania kuwa Nchi ya Viwanda"

Soma - https://jamii.app/SamiaHotuba-Dec21

#Miaka60YaUhuru
AFYA: Rais Samia Suluhu Hassan amesema mwaka 1961 kulikuwa na Hospitali 113, Vituo vya Afya 22 na Zahanati 1,188. Hivi sasa Nchi ina jumla ya Zahanati 7,163, Vituo vya Afya 929 na Hospitali 369

Asema, "Tunaendelea kuboresha sekta hii kwa kuhakikisha tunaajiri Madaktari wengi zaidi ili tuweze kufikia viwango vya WHO"

Soma - https://jamii.app/SamiaHotuba-Dec21

#Miaka60YaUhuru
RAIS SAMIA: TUNA MFUMO BORA WA KUWEKA VIONGOZI MADARAKANI

Amesema sote ni mashahidi Tanzania imekuwa na Mfumo bora wa kuweka Viongozi madarakani unaoheshimiwa na imara kupitia Chaguzi zinazofanyika kila baada ya miaka mitano

Ameeleza, "Wananchi wamekuwa wakitekeleza Haki yao ya msingi ya kikatiba ya kuchagua viongozi wanaowataka"

Soma - https://jamii.app/SamiaHotuba-Dec21

#Miaka60YaUhuru
Katika siku za karibuni mitandao ya kijamii na Mifumo ya Kidijitali imekuwa maeneo muhimu kwa Jamii ya Tanzania kutumia #UhuruWaKujieleza na kupigania haki zao nyingine

Tukifurahia Miaka 60 ya Uhuru wa #Tanganyika ni kwa kiwango gani tumeweza kuitumia mifumo ya Digitali katika kusimamia Haki za Binadamu, Demokrasia na Utawala Bora?

Ungana nasi katika Mjadala huu utakaofanyika kupitia Clubhouse Desemba 9, 2021

#JamiiForums #DigitalSpaces #Democracy
MAADHIMISHO YA MIAKA 60 YA UHURU WA TANGANYIKA

Tanganyika ilipata Uhuru wake kutoka kwa Waingereza Desemba 09, 1961. Harakati za Uhuru ziliongozwa na Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere

Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara imetajwa kuchangia kuleta mafanikio mbalimbali yakiwemo; Kujenga Umoja wa Kitaifa, Kuimarisha Uchumi, kuboresha Huduma za Kijamii na kuimarisha Demokrasia na Utawala wa Sheria

Unazungumziaje miaka 60 ya Uhuru wa Tanganyika?

#Miaka60YaUhuru #Tanzania60
Katika siku za karibuni mitandao ya kijamii na Mifumo ya Kidijitali imekuwa maeneo muhimu kwa Jamii ya Tanzania kutumia #UhuruWaKujieleza na kupigania haki zao nyingine

Tukifurahia Miaka 60 ya Uhuru wa #Tanganyika ni kwa kiwango gani tumeweza kuitumia mifumo ya Digitali katika kusimamia Haki za Binadamu, Demokrasia na Utawala Bora?

Ungana nasi katika Mjadala huu utakaofanyika kupitia Clubhouse Desemba 9, 2021

#JamiiForums #DigitalSpaces #Democracy
Matukio Katika Picha: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwaongoza Viongozi wa Kitaifa na Kimataifa pamoja na Wananchi katika Maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yanayofanyika katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam

#Miaka60YaUhuru
MIAKA 60 YA UHURU WA TANGANYIKA

Desemba 9, 1961 mambo makubwa mawili yalifanyika kama sehemu ya maadhimisho ya Uhuru wa #Tanganyika; Kushusha Bendera ya Mkoloni na kupandisha ya Taifa huru pamoja na Mwenge wa Uhuru kwenye kilele cha Mlima #Kilimanjaro

Tukio la kupandisha Bendera lilifanyika katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, Uwanja uliojengwa mahsusi kwa ajili ya sherehe za uhuru na umuhimu wake ulikuwa kuonesha kuondoka kwa Mkoloni

#Miaka60YaUhuru #JamiiForums #Tanzania60
Katika siku za karibuni mitandao ya kijamii na Mifumo ya Kidijitali imekuwa maeneo muhimu kwa Jamii ya Tanzania kutumia #UhuruWaKujieleza na kupigania haki zao nyingine

Tukifurahia Miaka 60 ya Uhuru wa #Tanganyika ni kwa kiwango gani tumeweza kuitumia mifumo ya Digitali katika kusimamia Haki za Binadamu, Demokrasia na Utawala Bora?

Ungana nasi katika Mjadala huu utakaofanyika kupitia Clubhouse Desemba 9, 2021

#JamiiForums #DigitalSpaces #Democracy
Tukifurahia Miaka 60 ya Uhuru wa #Tanganyika ni kwa kiwango gani tumeweza kuitumia mifumo ya Digitali katika kusimamia Haki za Binadamu, Demokrasia na Utawala Bora?

Ungana nasi katika Mjadala huu kuanzia saa 12 kamili kupitia Clubhouse

Link - https://www.clubhouse.com/join/jamiiforums/apMXkmgH/xerKXO6Y
KARIBU TUJADILI, TUELIMISHANE NA KUTOA HOJA ZETU

- JamiiForums inaendesha mjadala unaoendelea sasa kupitia Clubhouse kuhusu β€œMiaka 60 ya Uhuru na Mchango wa Digitali”

- Ungana nasi, tujadili, tuwasiliane na kuelimishana kuhusu mada hiyo kwa kupitia ; https://www.clubhouse.com/room/PA0oo9ge

#JamiiForums
Yanayojiri katika Mjadala wa "Miaka 60 Ya Uhuru: Mchango wa Digitali katika Uhuru wa Kujieleza, Demokrasia na Utawala Bora" kupitia Clubhouse

Ungana Nasi - https://www.clubhouse.com/room/PA0oo9ge