JamiiForums
52.8K subscribers
34.4K photos
2.44K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
INDIA: HEWA CHAFU YAPELEKEA MAHAKAMA KUAMURU OFISI ZIFUNGWE

Mahakama ya Juu imeelekeza Mamlaka kufunga Ofisi New Delhi na Miji ya karibu

Hii itaruhusu Mamilioni kufanyia kazi nyumbani wakati Maafisa wakitafuta mbinu za kupunguza hewa chafu

Soma - https://jamii.app/PollutionIndia
#SOMALIA: WANAJESHI WA UGANDA WAHUKUMIWA KWA KUUA RAIA

Wanajeshi 5 wa #Uganda wanaofanya Kazi na Vikosi vya AU Nchini Somalia wamekutwa na hatia ya kuwaua raia 7

Wawili wamehukumiwa kifo, watatu kifungo cha miaka 39 kila mmoja

Soma - https://jamii.app/JeshiUgandaKifo

#HumanRights #JFLeo
MDAU: MASOMO YA BIASHARA YAENDANE NA MAZINGIRA YA KITANZANIA

Mshiriki wa Shindano la Stories Of Change anasema bado tunafundishwa jinsi ya kutunza na kuhesabu Fedha lakini Dunia ya leo imebadilika

Anasema Serikali inakubali Teknolojia inazidi kukua lakini bado imeshindwa kufumua Mfumo uliopo ili kuendana na Soko la Ajira

Soma Makala yake - https://jamii.app/MasomoBiashara

#StoriesOfChange
SERIKALI YA MAREKANI KUTOA TSH. BILIONI 437 KWA SEKTA YA AFYA

Waziri Dorothy Gwajima amesema, "Serikali ya Marekani inatarajia kutoa fedha hizo kwa kipindi cha miaka 5 kuanzia mwaka kesho na zitatumika kuboresha utoaji Huduma za Afya"

Soma - https://jamii.app/MarekaniAfyaTZ
WAZIRI LUKUVI: MARUFUKU MADALALI KULAZIMISHA KULIPWA POSHO YA MWEZI 1

Asema "Baadhi ya Madalali wanapangisha nyumba halafu wanachukua kwa Wapangaji Kodi ya mwezi. Ni wizi wa mchana kabisa. Wewe umeajiriwa na mwenye nyumba, yeye lazima akulipe wewe"

Soma https://jamii.app/DalaliPosho1
MISRI: Marufuku ya Wafanyakazi wa Sekta ya Umma kuingia Ofisini ikiwa hawajachanjwa na kupimwa #COVID19 imeanza kutekelezwa

Zaidi ya watu Milioni 14 Nchini humo wamepata Dozi 2. Serikali inalenga kuchanja 40% ya Raia kufikia mwisho wa mwaka

Soma - https://jamii.app/MarufukuMisri

#UVIKO3 #JFLeo
Wizara ya Mambo ya Ndani imesema itazifutia leseni Jumuiya na Taasisi ambazo zitashindwa kuwasilisha Vyeti, Katiba na Kanuni za Uendeshaji kwa Msajili ndani ya Siku 15

Mikoa ya Mbeya na Songwe yatajwa vinara wa Jumuiya nyingi ambazo hazijasajiliwa

Soma - https://jamii.app/JumuiyaMsajili15
DRC: Mahakama ya Katiba imesema haina uwezo wa kumhukumu aliyekuwa Waziri Mkuu, Seneta Augustin Matata Ponyo anayeshutumiwa kwa Ubadhirifu wa Fedha za ujenzi wa Bustani ya Kilimo

Serikali imetakiwa kutafuta Mahakama itakayopewa Mamlaka ya kuhukumu

Soma - https://jamii.app/PonyoFailedCase
Ripoti ya Uwajibikaji ya WAJIBU 2019/20 imeeleza kuwa, upungufu wa Watumishi unaathiri Utendaji wa Mamlaka ya Serikali za Mitaa na kusababisha utoaji duni wa Huduma za Msingi kama Elimu, Afya na Maji salama

Kutowasilisha makato ya kisheria ya mishahara ya Watumishi katika Taasisi husika huwasababishia usumbufu usio wa lazima unapofika wakati wa kustaafu

Soma - https://jamii.app/MikopoMishahara

#JFUwajibikaji
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
UGANDA: Milipuko miwili imeripotiwa katika Mji Mkuu wa Nchi hiyo, Kampala. Kuna taarifa za kuwepo majeruhi

Inaripotiwa, Maafisa wa Usalama wameamuru kila mtu kuondolewa Bungeni baada ya mlipuko mojawapo kuripotiwa karibu na eneo la Bunge

Soma - https://jamii.app/UGExplosions
#SUDAN: Idadi ya waliouawa tangu Jeshi kuchukua Madaraka imefikia Watu 23 huku Raia wakiendelea kuandamana kuupinga Utawala wa Kijeshi

Zaidi ya majeruhi 200 wamerekodiwa hadi sasa, wakiwemo 10 waliojeruhiwa kwa risasi za Moto

Soma - https://jamii.app/DeathTollsSudan

#HumanRights #JFLeo
DAR: Kesi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na wenzake 3 imeahirishwa hadi Novemba 17, 2021

Jaji Joachim Tiganga ameshindwa kutoa uamuzi juu ya pingamizi lililowasilishwa na upande wa Utetezi kutokana na wingi wa Hoja

Soma - https://jamii.app/MboweKesiJaji
VIASHIRIA VYA RUSHWA, UDANGANYIFU NA UBADHIRIFU

Taasisi ya WAJIBU imeainisha kiasi ambacho hakikukusanywa au kimetumika na Serikali pasipo kupata tija kimeongezeka kutoka Tsh. bilioni 232.52 Mwaka 2018/19 hadi Tsh. bilioni 1,770.84 Mwaka 2019/20

Mamlaka za Serikali za Mitaa ndizo zimekuwa na ongezeko kubwa zaidi kutoka Tsh. bilioni 103.93 Mwaka 2018/19 hadi Tsh. bilioni 863.85 Mwaka 2019/20 ambapo kasoro nyingi zilionekana eneo la ununuzi wa Umma na usimamizi wa mikataba

Soma - https://jamii.app/UbadhirifuRushwa
#JFUwajibikaji
UPDATE: Polisi Nchini Uganda wamesema Milipuko iliyotokea #Kampala ilitekelezwa na watu 3 waliojitoa mhanga, na walifariki papo hapo

Raia 3 wamefariki dunia na 33 wamejeruhiwa, ikielezwa idadi ya Vifo inaweza kuwa kubwa kuliko inayoripotiwa

Soma - https://jamii.app/KampalaExplosions
KUCHANJA CHANJO YA COVID-19 HUCHUKUA MUDA MFUPI

Wataalamu wa #Afya wanashauri kuwa ni vema kila mmoja kutafuta muda katika ratiba yake ili kupata Chanjo ya #COVID19

Mara nyingi mchakato huo si marefu na hukamilika ndani ya dakika 20

Soma - https://jamii.app/ChanjoMuda

#UVIKO3
DONDOO ZA KIUSALAMA UNAPOTUMIA MITANDAO YA KIJAMII

1. Rekebisha faragha ya akaunti yako: (Personalize your privacy settings). Pangilia kwa kuchagua nani awe na uwezo wa kuangalia taarifa zako

2. Kabla ya kuweka (post) kitu chochote jiulize endapo kuna ulazima wa kuweka maudhui hayo na Watu watachukuliaje. Maudhui kuhusu masuala yako binafsi yanaweza kuwa mwanya kwa wahalifu

Soma - https://jamii.app/SafetySME

#DigitalSafety
HOJA: KUMCHAPA MTOTO HUMSAIDIA KUBADILIKA?

Kupitia Shindano la #StoriesOfChange, Mdau wa JF anahoji, je tulishachukua muda kujiuliza viboko Watoto wetu vinawasaidia?

Anasema imekuwa kawaida Mtoto kuchapwa anapokosea kidogo tu, lakini athari zake ni kubwa kulinganisha na faida

Nini maoni yako kuhusu hoja hii?

Soma - https://jamii.app/HojaViboko

#Malezi
Taarifa binafsi ni taarifa yoyote inayokutambulisha, iwe inahusiana na Maisha yako binafsi, Kitaaluma, au ya umma (Mfano: Majina, Namba za Simu, Anwani n.k)

Ni mara ngapi umeshakutana na taarifa za Watu wengine katika Mazingira ambayo hukupaswa kukutana nazo? Kama ni mara nyingi, basi huenda hata taarifa zako zinazagaa bila wewe kujua

Ungana nasi katika Mjadala wa Haki ya faragha na ulinzi wa taarifa binafsi kupitia Clubhouse ya JamiiForums Novemba 18, 2021

#JamiiForums #dataprivacy
DKT. ELISHA OSATI: CHANJO ZA COVID-19 HAZISABABISHI DAMU KUGANDA

Tafiti zilizofanyika zimebaini Watu waliokumbwa na shida hiyo walikuwa na matatizo mengine kiafya

Huweza kusababishwa na Shinikizo la Damu, unene kupita kiasi au Kisukari

Soma - https://jamii.app/ChanjoMaswaliMajibu

#UVIKO3
Shirika la Afya Duniani (WHO) limeyataka Mataifa kuchukua hatua zaidi kudhibiti uraibu wa Tumbaku inayokadiriwa kuua zaidi ya Watu Milioni 8 kila mwaka

Ripoti imebainisha Watu Bilioni 1.3 Ulimwenguni walikuwa wanatumia Tumbaku mwaka 2020

Soma - https://jamii.app/TumbakuWHO

#JFLeo
👍1