JamiiForums
55.4K subscribers
33.4K photos
2.03K videos
30.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Serikali imependekeza kutoza Ushuru wa bidhaa kwa kiwango cha Tsh. 50 kwa kilo ya 'crisps' zinazozalishwa Nchini, na Tsh. 100 kwa kilo ya 'crisps' zinazoingizwa kutoka nje ya Nchi

Akisoma Bajeti Kuu, Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba, amesema Lengo la hatua hii ni kupunguza athari za Kiafya ikiwemo ongezeko la uzito (Obesity) zinazotokana na matumizi ya bidhaa hizo na kuongeza Mapato ya Serikali. Hatua hii inatarajia kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha Tsh. Milioni 6,475;

Soma https://jamii.app/BajetuKuu2025

#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #BajetiKuu2025 #Governance #Uwajibikaji #Transparency
Serikali imependekeza kupunguza kiwango cha Ushuru wa Bidhaa kwenye Vinywaji vya kuongeza nguvu (Energy drinks) vinavyozalishwa ndani ya Nchi kutoka Tsh. 561 kwa kila Lita hadi Tsh. 134.2 kwa kila lita

Waziri wa fedha, Mwigulu Nchemba amesema Lengo la hatua hii ni kuweka unafuu kwa Wazalishaji wa ndani, kuongeza Ushindani na kuchochea Uwekezaji Nchini. Hatua hii inatarajia kupunguza mapato ya Serikali kwa kiasi cha Tsh. Milioni 170.2

Soma https://jamii.app/BajetuKuu2025

#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #BajetiKuu2025 #Governance #Uwajibikaji #Transparency
Serikali imependekeza kutoza ushuru wa bidhaa kwa kiwango 5% kwa Soseji na bidhaa zingine zinazofanana na hizo zinazozalishwa Nchini, na 10% kwa zile zinazoingizwa kutoka nje ya Nchi

Waziri Mwigulu Nchemba, amesema lengo ni kuongeza mapato ya Serikali, kuvutia Uwekezaji Nchini na kulinda Wazalishaji wa ndani. Hatua hii inatarajia kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha Tsh. Milioni 2,413.9

Pia imependekeza kutoza ushuru wa bidhaa kwa kiwango cha 10% kwenye sabuni zinazoingizwa kutoka nje ya Nchi, Lengo likiwa kulinda Wazalishaji wa ndani na kuongeza Ajira, hatua hii inatarajia kuongeza mapato ya Serikali kwa Tsh. Milioni 143,395.8

Soma https://jamii.app/BajetuKuu2025

#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #BajetiKuu2025 #Governance #Uwajibikaji #Transparency
Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amependekeza kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Kodi ya Mapato, Kutoza kodi ya zuio kwa kiwango cha 10% kwenye malipo ya Kamisheni inayotokana na matangazo ya Michezo ya kubahatisha

Amesema Kodi hii itakuwa ni kodi ya mwisho (final), lengo la hatua hii ni kuendana na Kanuni za usawa za utozaji kodi na kupanua wigo wa kodi, na hatua hii inatarajia kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha Tsh. Milioni 6,787.2

Soma https://jamii.app/BajetuKuu2025

#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #BajetiKuu2025 #Governance #Uwajibikaji #Transparency
Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amependekeza kutoza ushuru wa bidhaa kwa kiwango cha 30% kwenye vifaa vya Sigara za Kielektroniki na vimiminika vya Sigara za Kielektroniki, ili kupunguza athari zinazotokana na matumizi ya bidhaa hizo na kuongeza wigo wa Kodi

Amesema hatua hiyo inatarajia kuongeza Mapato ya Serikali kwa kiasi cha Tsh. Milioni 3,322.2

Soma https://jamii.app/BajetuKuu2025

#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #BajetiKuu2025 #Governance #Uwajibikaji #Transparency
Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amependekeza kupunguza ada ya usajili wa pikipiki za biashara kutoka Tsh. 340,000 hadi Tsh. 170,000 kwa miaka mitatu, huku akisema ada hiyo husika italipwa wakati wa usajili wa awali pekee

Vile vile amependekeza kupunguza ada ya leseni ya uendeshaji wa pikipiki, bajaji na guta kutoka Tsh. 70,000 hadi Tsh. 30,000

Soma https://jamii.app/BajetuKuu2025

#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #BajetiKuu2025 #Governance #Uwajibikaji #Transparency
Kukosea siyo tu jambo la kawaida, bali pia ni muhimu sana kwa ukuaji na kujifunza.

Tunajifunza kutokana na makosa yetu, tunaboresha ujuzi wetu na tunakuwa watu wenye Hekima zaidi.

Makosa yanatuonesha pale tulipofanya vibaya na kutupa fursa ya kurekebisha na kusonga mbele.

#JamiiAfrica #JamiiForums #Maisha #GoodMorning #AmkaNaJF
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
#DIPLOMASIA: #Israel imefanya mashambulizi Nchini #Iran katika Mji wa #Tehran ikiwa ni sehemu ya Oparesheni kwa kile ambacho Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu amesema walilenga kudhoofisha Miundombinu ya Nyuklia ya Iran na Viwanda vya Makombora ya masafa marefu

Pamoja na hivyo, Israel imetangaza hali ya hatari, ikisema inatarajia mashambulizi ya kulipiza kisasi kutoka kwa Iran, wakati ambapo Iran imesema mashambulizi hayo yameathiri Makazi ya raia na kuua Watu kadhaa wakiwemo Watoto

Wakati huohuo, Rais wa Marekani, #DonaldTrump amekiambia Kituo cha #FoxNews kuwa alikuwa na taarifa kuhusu mashambulizi hayo kabla lakini Nchi yake haikuhusika kwa namna yoyote

Soma https://jamii.app/IsraelAgainstIran

#Diplomacy #Governance #HumanRights #JamiiForums #JamiiAfrica
UTEUZI: Rais Samia amemteua Jaji wa Mahakama ya Rufani, George Mcheche Masaju kuwa Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, akichukua nafasi ya Prof. Ibrahim Hamis Juma ambaye amestaafu

Taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi, Dkt. Moses Kusiluka, imeeleza uapisho wa Jaji Mkuu utafanyika Juni 15, 2025 Ikulu, Chamwino - Dodoma, Saa 4.00 Asubuhi

Soma https://jamii.app/UteuziGeorgeMcheche

#Uteuzi #JamiiForums #Governance
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema mifumo ya Hali ya Hewa haioneshi uwepo wa mvua hivi karibuni hapa nchini badala yake kutakuwa na ukavu na ubaridi ambapo Wananchi wametakiwa kuchukua tahadhari za kujilinda na baridi

Meneja wa Utabiri wa TMA, Dkt. Mafuru Kantamla amesema mvua zilizonyesha hivi karibuni Ukanda wa Pwani zimetokana na ongezeko la Joto katika Bahari ya Hindi hususan katika Mwambao wa Pwani lakini hazitakuwa na mwendelezo kwa kuwa joto la Bahari limeanza kupungua kwa kasi

Soma https://jamii.app/HaliYaHewaJuni

Video Credits: Torch Media

#ClimateChange #JamiiForums #JamiiAfrica