Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
KATAVI: Wakulima wa zao la tumbaku kutoka Chama Cha Msingi Cha Ushirika Cha Wakulima wa Tumbaku Mpanda Kati, Manispaa ya Mpanda wamelalamika kutolipwa fedha zao licha ya Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe kutoa maagizo kuwa kabla ya Sikukuu ya Nanenane Wakulima wote wawe wamelipwa.
Wakulima hao wamefika Ofisi ya Chama hicho kufikisha malalamiko yao ambapo pia wamesema kuna nyongeza ya makato ya fedha ya 3% kinyume na utaratibu wa vikao.
Akijibu madai hayo Meneja wa Chama hicho, Zaituni Tembo amekiri Wakulima hao kutolipwa na kufafanua kuwa makato wanayosema ni makubaliano ya Bima ya Mkopo kutoka Benki ya NMB ambayo waliafikiana katika vikao vya Wakulima tofauti na benki waliyokuwa wakifanya nayo kazi awali.
Zaidi soma https://jamii.app/MpandaKati
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFMatukio #JFEconomy #Accountability
Wakulima hao wamefika Ofisi ya Chama hicho kufikisha malalamiko yao ambapo pia wamesema kuna nyongeza ya makato ya fedha ya 3% kinyume na utaratibu wa vikao.
Akijibu madai hayo Meneja wa Chama hicho, Zaituni Tembo amekiri Wakulima hao kutolipwa na kufafanua kuwa makato wanayosema ni makubaliano ya Bima ya Mkopo kutoka Benki ya NMB ambayo waliafikiana katika vikao vya Wakulima tofauti na benki waliyokuwa wakifanya nayo kazi awali.
Zaidi soma https://jamii.app/MpandaKati
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFMatukio #JFEconomy #Accountability
Mdau ametoa wito kwa Mkurugenzi wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (#PSSSF) kufuatilia utendaji wa baadhi ya Watendaji wake wa Tawi la Dodoma akidai anapigwa 'danadana' nyingi bila majibu ya msingi tangu alipoanza kufuatilia madai ya malipo yake ya kupoteza ajira tangu Mwaka 2024.
Anadai awali aliwasilisha malalamiko kupitia JamiiForums.com akasaidiwa na Ofisi ya PSSSF Kinondoni lakini alipotakiwa kwenda Makao Makuu Dodoma huko ndipo shida ilipo, akidai huduma zinaenda polepole na kila hatua inahitaji wahusika wapigiwe simu ndiyo watimize majukumu yao.
Zaidi soma https://jamii.app/UmunguWatu
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFMdau2025 #ServiceDelivery #JFHuduma #Accountability
Anadai awali aliwasilisha malalamiko kupitia JamiiForums.com akasaidiwa na Ofisi ya PSSSF Kinondoni lakini alipotakiwa kwenda Makao Makuu Dodoma huko ndipo shida ilipo, akidai huduma zinaenda polepole na kila hatua inahitaji wahusika wapigiwe simu ndiyo watimize majukumu yao.
Zaidi soma https://jamii.app/UmunguWatu
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFMdau2025 #ServiceDelivery #JFHuduma #Accountability
❤1
Mdau ndani ya JamiiForums.com ametoa wito kwa Waziri wa TAMISEMI kuingilia kati madai ya uwepo wa 'uchakachuaji' wa Fedha za Kujikimu kwa Watumishi wa Ajira Mpya Kada mbalimbali, akidai kuna changamoto ya utoaji wa malipo hayo na hata wanapoulizia hawapati majibu mazuri kutoka kwa Wasimamizi.
Soma https://jamii.app/FedhaKujikimuKuzungushwa
#JamiiForums #JamiiAfrica #Uwajibikaji #Accountability #JFMdau2025
Soma https://jamii.app/FedhaKujikimuKuzungushwa
#JamiiForums #JamiiAfrica #Uwajibikaji #Accountability #JFMdau2025
❤1
DODOMA: Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umeeleza kwa kutumia mfumo wao wa #TEHAMA kwa sasa Watu wanaweza kuhudumiwa na tawi lao lolote nchi nzima bila kulazimika kwenda Makao Makuu.
Hayo yameelezwa baada ya Mdau wa JamiiForums.com kudai huduma za baadhi ya Watumishi wa Makao Makuu ya #PSSSF si nzuri, akitoa mfano kuwa alihudumiwa vizuri katika Tawi la Kinondoni lakini alipofika Tawi la Dodoma mambo yakabadilika, hivyo akatoa wito kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko kufuatilia suala hilo.
Akijibu hoja ya Mdau, Meneja - Uhusiano na Elimu kwa Wanachama wa PSSSF, Omega Ngole amesema “Tumepokea taarifa hii, tunashukuru, kwa kuwa hatuna mawasiliano ya Mdau huyo, tunapitia kumbukumbu zetu ili kumpatia huduma kwa haraka kama anavyotarajia. Dhamira ya Mfuko wa PSSSF ni kujenga Kesho Bora na si vinginevyo.”
Zaidi soma https://jamii.app/PSSSFUfafanuzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFMdau2025 #DigitalRights #Accountability #JFHuduma
Hayo yameelezwa baada ya Mdau wa JamiiForums.com kudai huduma za baadhi ya Watumishi wa Makao Makuu ya #PSSSF si nzuri, akitoa mfano kuwa alihudumiwa vizuri katika Tawi la Kinondoni lakini alipofika Tawi la Dodoma mambo yakabadilika, hivyo akatoa wito kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko kufuatilia suala hilo.
Akijibu hoja ya Mdau, Meneja - Uhusiano na Elimu kwa Wanachama wa PSSSF, Omega Ngole amesema “Tumepokea taarifa hii, tunashukuru, kwa kuwa hatuna mawasiliano ya Mdau huyo, tunapitia kumbukumbu zetu ili kumpatia huduma kwa haraka kama anavyotarajia. Dhamira ya Mfuko wa PSSSF ni kujenga Kesho Bora na si vinginevyo.”
Zaidi soma https://jamii.app/PSSSFUfafanuzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFMdau2025 #DigitalRights #Accountability #JFHuduma
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
KATAVI: Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika, Onesmo Buswelu ameutaka uongozi wa Chama cha Msingi cha Ushirika cha Wakulima wa Tumbaku Mpanda Kati kuhakikisha wanawalipa Wakulima waliocheleweshewa malipo yao Agosti 13, 2025.
Hatua hiyo imefikiwa baada ya JamiiForums.com kuripoti malalamiko ya Wakulima hao mnamo Agosti 11, 2025 ambao walidai licha ya maelekezo ya Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe kutoa maagizo kuwa walipwe kabla ya Sikukuu ya Nanenane 2025 lakini haikuwa hivyo.
Awali Agosti 11, 2025, alipoulizwa kuhusu malipo hayo, Meneja wa Chama cha Msingi cha Ushirika cha Wakulima wa Tumbaku Mpanda Kati, Zaituni Tembo alisema “Kimsingi hatujalipa, tulifunga masoko tangu Julai 11, 2025 sababu Kampuni ambayo tunafanya nazo biashara haikutulipa.”
Soma https://jamii.app/WakulimaKulipwa
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFMatukio #JFEconomy #Accountability
Hatua hiyo imefikiwa baada ya JamiiForums.com kuripoti malalamiko ya Wakulima hao mnamo Agosti 11, 2025 ambao walidai licha ya maelekezo ya Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe kutoa maagizo kuwa walipwe kabla ya Sikukuu ya Nanenane 2025 lakini haikuwa hivyo.
Awali Agosti 11, 2025, alipoulizwa kuhusu malipo hayo, Meneja wa Chama cha Msingi cha Ushirika cha Wakulima wa Tumbaku Mpanda Kati, Zaituni Tembo alisema “Kimsingi hatujalipa, tulifunga masoko tangu Julai 11, 2025 sababu Kampuni ambayo tunafanya nazo biashara haikutulipa.”
Soma https://jamii.app/WakulimaKulipwa
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFMatukio #JFEconomy #Accountability
MAREKANI: Mtanzania Subiro Osmund Mwapinga amekamatwa nchini Ghana, Aprili 8, 2025 baada ya Idara ya Kudhibiti Dawa za Kulevya ya Marekani (DEA) kutoa taarifa kwa Vyombo vya Ulinzi na Usalama nchini humo kuwa anahusika katika mpango wa kusambaza silaha kwa moja ya magenge ya biashara ya Dawa za Kulevya.
Alikamatwa na baadaye kukabidhiwa Marekani mnamo Julai 25, 2025 ambapo Subiro ni miongoni mwa watuhumiwa wanne wa kigeni ambao walikuwa na mpango wa kusambaza silaha zenye thamani ya Tsh. Bilioni 150 (Dola Milioni 58).
Watuhumiwa wengine ni kutoka Kenya na Bulgara, iwapo watapatikana na hatia wanaweza kuhukumiwa adhabu ya kifungo cha Miaka 10 au kifungo cha Maisha.
Soma zaidi https://jamii.app/MtanzaniaSilahaGenge
#JamiiForums #JamiiAfrica #Uwajibikaji #Accountability #JFMatukio
Alikamatwa na baadaye kukabidhiwa Marekani mnamo Julai 25, 2025 ambapo Subiro ni miongoni mwa watuhumiwa wanne wa kigeni ambao walikuwa na mpango wa kusambaza silaha zenye thamani ya Tsh. Bilioni 150 (Dola Milioni 58).
Watuhumiwa wengine ni kutoka Kenya na Bulgara, iwapo watapatikana na hatia wanaweza kuhukumiwa adhabu ya kifungo cha Miaka 10 au kifungo cha Maisha.
Soma zaidi https://jamii.app/MtanzaniaSilahaGenge
#JamiiForums #JamiiAfrica #Uwajibikaji #Accountability #JFMatukio
❤1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
JF Kumbukizi: Aliyekuwa Mbunge wa Kawe kupitia #CCM, Askofu Josephat Gwajima, aliwahi kusema kuwa mafanikio ya mtu hupimwa wakati hayupo.
Alisisitiza kuwa mafanikio ya kweli ni yale yanayoendelea kuishi hata baada ya waanzilishi kutokuwepo, alichokiacha kinatakiwa kuongea bila muhusika kuzungumza.
Soma zaidi https://jamii.app/WanasiasaZilizobamba
#JamiiAfrica #JamiiForums #Governance #Accountability #Uwajibikaji #UtawalaBora #Siasa #JFKumbukizi
Alisisitiza kuwa mafanikio ya kweli ni yale yanayoendelea kuishi hata baada ya waanzilishi kutokuwepo, alichokiacha kinatakiwa kuongea bila muhusika kuzungumza.
Soma zaidi https://jamii.app/WanasiasaZilizobamba
#JamiiAfrica #JamiiForums #Governance #Accountability #Uwajibikaji #UtawalaBora #Siasa #JFKumbukizi
❤4👍1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
ZANZIBAR: Akizungumza katika Mkutano Mkuu wa tisa wa Chama cha Walimu Zanzibar (ZATU), Wilaya ya Mjini Unguja Agosti 13, 2025, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Lela Mohammed Mussa amesema kumfundisha Mtoto ndani ya chumba hakumpi nafasi Mwanafunzi kujifunza kwani Watoto wanahitaji eneo la kutosha ili kujifunza.
Waziri Lela amesema hayo yanafanyika kutokana na baadhi ya Wazazi kuendelea kuwapeleka Watoto wao katika maeneo hayo ambayo hayakidhi vigezo vya kuwafundisha Watoto hasa ngazi ya awali, hivyo Serikali imepiga marufuku shule ambazo zipo ndani ya nyumba (skuli nyumba) na kuwataka wamiliki kujenga majengo yanayokidhi utoaji wa huduma kwa Wanafunzi wao.
Ikumbukwe, Mwaka 2023, Ripoti ya Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ilionesha vitendo vya ukatili wa kijinsia vimeripotiwa kuongezeka #Zanzibar kutoka matukio 1,222 Mwaka 2021 hadi 1,360 Mwaka 2022, ambapo kati ya hayo matukio 1,173 yalijumuisha Watoto.
Soma zaidi https://jamii.app/SkuliNgumbaMarufuku
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFElimu #Uwajibikaji #Accountability #Governance
Waziri Lela amesema hayo yanafanyika kutokana na baadhi ya Wazazi kuendelea kuwapeleka Watoto wao katika maeneo hayo ambayo hayakidhi vigezo vya kuwafundisha Watoto hasa ngazi ya awali, hivyo Serikali imepiga marufuku shule ambazo zipo ndani ya nyumba (skuli nyumba) na kuwataka wamiliki kujenga majengo yanayokidhi utoaji wa huduma kwa Wanafunzi wao.
Ikumbukwe, Mwaka 2023, Ripoti ya Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ilionesha vitendo vya ukatili wa kijinsia vimeripotiwa kuongezeka #Zanzibar kutoka matukio 1,222 Mwaka 2021 hadi 1,360 Mwaka 2022, ambapo kati ya hayo matukio 1,173 yalijumuisha Watoto.
Soma zaidi https://jamii.app/SkuliNgumbaMarufuku
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFElimu #Uwajibikaji #Accountability #Governance
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
GEITA: Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (#TAKUKURU) imewakamata Wajumbe wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Kata ya Nyankumbu walioonekana katika picha mjongeo wakigawana rushwa Agosti 2, 2025 katika mchakato wa uchaguzi ndani ya #CCM.
TAKUKURU imeeleza kuwa baada ya tukio hilo kusambaa, ofisi ya mkoa ilichukua hatua ya haraka kwa kuwatambua na kuwakamata wajumbe waliokuwa wakionekana kwenye picha hizo na kwamba Inadaiwa kuwa vitendo hivyo vilifanyika mara baada ya zoezi la kuwanadi wagombea Ubunge kukamilika.
Aidha, Mkuu wa TAKUKURU Mkoa, James Ruge amesema kutokana na matukio hayo na mengine, ofisi imeanzisha uchunguzi unaoelekea kukamilika, ikiwa ni hatua ya kukusanya ushahidi ili kuthibitisha tuhuma za rushwa dhidi ya wahusika.
Zaidi soma https://jamii.app/WajumbeUWTTuhumaRushwa
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #UchaguziMkuu2025 #KataaRushwa
TAKUKURU imeeleza kuwa baada ya tukio hilo kusambaa, ofisi ya mkoa ilichukua hatua ya haraka kwa kuwatambua na kuwakamata wajumbe waliokuwa wakionekana kwenye picha hizo na kwamba Inadaiwa kuwa vitendo hivyo vilifanyika mara baada ya zoezi la kuwanadi wagombea Ubunge kukamilika.
Aidha, Mkuu wa TAKUKURU Mkoa, James Ruge amesema kutokana na matukio hayo na mengine, ofisi imeanzisha uchunguzi unaoelekea kukamilika, ikiwa ni hatua ya kukusanya ushahidi ili kuthibitisha tuhuma za rushwa dhidi ya wahusika.
Zaidi soma https://jamii.app/WajumbeUWTTuhumaRushwa
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #UchaguziMkuu2025 #KataaRushwa
❤2
GEITA: Jeshi la Polisi linawashikilia Askari wanne wa Jeshi la Uhifadhi (JESHI USU) kwa tuhuma za mauaji ya Eziboni Fikiri (20), Mkulima, Mkazi wa Kijiji cha Msonga, Wilaya ya Bukombe ambaye walimkuta akikata mti eneo la Pori la Hifadhi ya Kigosi, Wilaya ya Bukombe, Agosti 13, 2025.
Taarifa ya Polisi imesema Mwili umehifadhiwa Hospitali ya Wilaya kwa ajili ya uchunguzi huku Watuhumiwa wakihojiwa na kwamba uchunguzi utakapokamilika watafikishwa Mahakamani.
Ikumbukwe hatua hiyo imechukuliwa ikiwa ni saa chache tangu Mdau wa JamiiForums.com awasilishe andiko akitoa wito kwa Jeshi la Polisi na TFS kufuatilia tukio hilo akidai kuna ukimya na hatua hazijachukuliwa.
Soma https://jamii.app/Askari4MauajiGeita
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji
Taarifa ya Polisi imesema Mwili umehifadhiwa Hospitali ya Wilaya kwa ajili ya uchunguzi huku Watuhumiwa wakihojiwa na kwamba uchunguzi utakapokamilika watafikishwa Mahakamani.
Ikumbukwe hatua hiyo imechukuliwa ikiwa ni saa chache tangu Mdau wa JamiiForums.com awasilishe andiko akitoa wito kwa Jeshi la Polisi na TFS kufuatilia tukio hilo akidai kuna ukimya na hatua hazijachukuliwa.
Soma https://jamii.app/Askari4MauajiGeita
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji
🤬1