JamiiForums
βœ”
55.4K subscribers
33.4K photos
2.03K videos
30.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
MATOKEO KIDATO CHA 4: WANAFUNZI WAONESHA UMWAMBA KWENYE KISWAHILI NA KEMIA

Katika wanafunzi waliofaulu mtihani wa kidato cha nne 2021, waliofaulu Kiswahili ni 95.58% na Kemia 92.02%

> Hisabati imeendelea kuwaburuza, waliofaulu Hisabati ni 19.24%

Soma https://jamii.app/CSEE2021

#JFElimu
WASICHANA WANG’ARA KUMI BORA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2021

Nafasi ya Kwanza hadi ya Saba zimeshilikiliwa na Wasichana, ya Nane na Tisa zimeshikiliwa na Wavulana

Nafasi ya Kumi pia imefungwa na Msichana

Soma - https://jamii.app/CSEE2021

#JFElimu
UN: WATU TAKRIBAN 108 WAMEUAWA TANGU JANUARI MOSI 2022 NCHINI #ETHIOPIA

Raia hao wameuawa ktk mashambulizi ya anga kwenye Jimbo la #Tigray

Mashambulizi yalifanyika dhidi ya Basi dogo, Uwanja wa Ndege na kambi ya Watu wasio na makazi

Soma - https://jamii.app/DeathTigrayJAN

#HumanRights
SHULE MOJA YA SERIKALI YAINGIA KUMI BORA

Mzumbe Sekondari iliyopo Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro imekuwa Shule pekee ya Serikali iliyoingia kumi bora

Imeshika nafasi ya kumi huku nafasi tisa za awali zikishikwa na Shule binafsi

Soma - https://jamii.app/CSEE2021

#JFElimu
UTAFITI: 2021 UMESHIKA NAFASI YA 6 KWA MIAKA YENYE JOTO ZAIDI

Ni kwa Takwimu za Shirika la Utafiti wa Anga za Mbali (NASA) na Idara ya Bahari na Anga(NOAA)

Wastani wa Joto ulikuwa nyuzi joto 1.51 za kipimo cha Celsius juu ya viwango vya karne ya 20

Soma https://jamii.app/2021JotoNo6
DAR: SOKO LA KARUME LATEKETEA KWA MOTO

Soko la Karume lililopo Wilayani Ilala Dar es Salaam limeteketea kwa moto ambao chanzo chake bado hakijafahamika

> Taarifa zaidi kukujia

Soma - https://jamii.app/KarumeMoto

#JFMatukio
Polisi Nchini #Haiti imesema Seneta wa zamani, John Joel Joseph ambaye ni mshukiwa mkuu ktk mauaji ya aliyekuwa Rais wa Nchi hiyo ametiwa mbaroni Nchini #Jamaica

Rais Moise alivamiwa Nyumbani kwake Julai 7, 2020 na kuuawa kwa kupigwa risasi

Soma - https://jamii.app/JosephHaitiArr

#Accountability
TANGA: TRENI YA ABIRIA YAPATA AJALI, MTOTO AFARIKI

Treni iliyokuwa inatoka Arusha kuelekea Dar ikiwa na abiria 700 imepata ajali alfajiri ya leo, Januari 16 Wilayani Pangani

Mabehewa 5 yamepinduka, 4 yameacha njia na kusababisha majeruhi 5

Soma - https://jamii.app/AjaliTRC

#JFMatukio
AUSTRALIA: Mahakama ya Shirikisho la #Australia imeikataa rufaa iliyoletwa na Bingwa wa Tennis Duniani, Novak Djokovic akipinga kufutwa kwa 'visa' yake na kufukuzwa kwa kutochoma Chanjo

Michuano ya #Tennis ya Australian Open inaanza leo, Januri 17 ambapo alikuwa amenuia kutafuta taji la 21 la Grand Slam

Soma - https://jamii.app/DjokovicNoRufaa

#JFSports
RIPOTI: MATAJIRI WATAJIRIKA ZAIDI WAKATI WA COVID-19

Shirika la Oxfam lasema utajiri wa Mabilionea 10 wakubwa zaidi umeongezeka maradufu wakati wa #CoronaVirus

Mapato ya chini ya Mataifa masikini zaidi yalichangia vifo vya watu 21,000 kila siku

Soma - https://jamii.app/OxfamReport

#JFMatukio
MDAU: WANASIASA WANAWACHUKULIAJE WANANCHI WA KAWAIDA?

Anasema kwa Mfano katika Kampeni za Uchaguzi, Mwanasiasa huweza kuwaambia Wananchi jambo fulani litakamilika muda mfupi tu baada ya kumchagua, lakini inaweza kupita hata miaka 10 hakuna kinachofanyika

Anashauri wananchi kujitahidi kadri ya uwezo wao kung'amua Mwanasiasa anayefaa na asiyefaa kupitia vitendo vyao na si maneno. Pia, Wanasiasa wanapaswa kujua zama zimebadilika, sasa sio kama zamani

Soma - https://jamii.app/SOCSiasa

#StoriesOfChange #JFSiasa #Uwajibikaji
MDAU: MAMBO YA KUZINGATIA KABLA HUJAANZA KUFUGA KUKU KIBIASHARA

1. Uwepo wako (Availability): Anasema kabla ya kuanza ufugaji wa Kuku Kibiashara hakikisha unapata nafasi ya kushiriki kwa karibu katika mradi wako

2. Kujitoa (Commitment): Unatakiwa kujitoa kweli kwa kuweka imani kuwa hawa Kuku ndio ajira yangu, watanisaidia kuendesha familia yangu

Zaidi, soma - https://jamii.app/KukuBiashara

#JFMdau
DAR: Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma amesema hakuna mtu yeyote anatakiwa kumwingilia au kumpigia simu Hakimu ambaye suala au kesi fulani ipo mbele yake

Ameeleza hayo katika Hafla ya kuapishwa Mahakimu Wakazi na kuwataka waepuke kuzungumzia masuala ya Mahakama kwenye makundi ya WhatsApp

Soma - https://jamii.app/UapishoMahakimu

#JFSheria
DAR: Polisi wametumia mabomu ya machozi kuwatawanya Wafanyabiashara wa soko la Karume (Mchikichini) wakishinikiza kuruhusiwa kuendelea na biashara ktk soko hilo lililoungua

Walitumia mawe na magogo kufunga Barabara ktk makutano ya Uhuru na Kawawa, Ilala Boma

Soma - https://jamii.app/MachingaMabomu

#JFMatukio
SUDAN: Madaktari Nchini humo wameandama kupinga mashambulizi dhidi ya Hospitali na Vikosi vya Usalama

Aidha, Mamlaka imekifuta kibali cha kituo cha Habari cha Al Jazeera Mubasher cha #Qatar pamoja na vibali vya Waandishi wake wawili

Soma - https://jamii.app/BanAlJazeeraSudan

#PressFreedom
MDAU: USIKIMBILIE UJASIRIAMALI KISA UMECHOKA BARUA ZA ONYO ZA MWAJIRI WAKO

Anasema Ujasiriamali ni kazi ngumu ambayo kila kitu kinategemea jitihada na Akili zako mwenyewe. Kwa Mwajiri una uhakika wa Mshahara lakini kujiajiri inategemea kiasi gani ulijitoa

Anasema kama kazi ya Mwajiri unaona ni mzigo, basi kinachokusumbua ni uvivu. Ujasiriamali unahitaji Nguvu na Nidhamu ya kiwango cha juu kuliko ulivyokuwa kwa Mwajiri wako.

Mjadala, soma - https://jamii.app/AjiraVsUjasiriamali

#Ujasiriamali #JFMdau
MICHEZO: Tiketi za Michezo ya Olimpiki ya Msimu wa Baridi 'Winter Olympics' iliyopangwa kuanza Februari 4, 2022 huko Beijing zitatolewa kwa makundi kadhaa ya watu na hazitauzwa kwa Umma

China inapambana kudhibiti maambukizi ya #Omicron

Soma - https://jamii.app/BeijingWO

#JFSports
#AFCON2021: CAMEROON, BURKINA FASO ZAFUZU HATUA YA MTOANO

Mwenyeji wa michuano, #TeamCameroon ameingia hatua ya mtoano baada ya kutoka sare ya goli 1-1 na #TeamCapeVerde

Aidha, #TeamBurkinaFaso imetinga hatua hiyo baada ya kutoka sare ya goli 1-1 na #TeamEthiopia

#JFSports
LIBYA: Umoja wa Mataifa (UN) umependekeza Uchaguzi wa Rais ulioshindwa kufanyika Desemba 2021 kufanyika Juni 2022

Mshauri Maalum wa UN kuhusu Masuala ya Libya, Stephanie Williams asema Raia wanataka kuchagua Serikali ya Kidemokrasia

Soma - https://jamii.app/UNUchaguziLibya

#Democracy