JamiiForums
56.4K subscribers
32.7K photos
1.81K videos
29.9K links
Official JamiiForums Telegram Channel | Be Informed, Engaged & Entertained
Download Telegram
KIGOMA: MGANGA ATUHUMIWA KUMUUA MTEJA ALIYETAKA KUZIKA FEDHA ZA BIASHARA

Dereva wa Pikipiki na Mganga wa Kienyeji wanatuhumiwa kumuua na kisha kumfukia Mwanamke aliyekuwa ameenda kuzindika Fedha za Biashara kiasi cha Tsh. Milioni 9

Soma - https://jamii.app/MtejaKifoZindiko
#HumanRights
MAREKANI: ASKARI 3 WANAOTUHUMIWA KUMUUA GEORGE FLOYD WAKUTWA NA HATIA

Maafisa hao wa zamani wa #Minneapolis walishtakiwa kwa kumnyima Floyd Haki yake ya matibabu wakati Afisa Derek Chauvin alipomkandamiza kwa goti shingoni mnamo Mei 25, 2020

Soma - https://jamii.app/FloydCaseGuilt
#UKRAINE YATAKA MAZUNGUMZO NA URUSI

Rais Volodymyr Zelensky ametaka mazungumzo na Rais Vladimir Putin ili kunusuru Raia wasio na hatia

China imesema Urusi ipo tayari kwa mazungumzo baada ya Rais Putin kuongea na Rais Xi Jinping

Soma https://jamii.app/Mazungumzo

#RussiaUkraineConflict
#KENYA: MWANAFUNZI AFUNGWA KWA VIFO VYA MOTO SHULENI

Msichana (18) amehukumiwa kifungo cha Miaka 5 jela kwa kuua bila kukusudia kufuatia kuwasha Moto katika Bweni la Shule na kuua wenzake tisa

Alitenda kosa hilo 2017 ktk Shule ya Wasichana ya Moi

Soma - https://jamii.app/JelaMotoShule
AFYA: 43% YA CHUMVI NCHINI HAICHANGANYWI NA MADINI JOTO

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Prof. Abel Makubi amesema 43% ya chumvi ni hatari kwa Afya kwa kuwa hazichanganywi na madini joto

Athari zake ni Magonjwa kama Goita na kujifungua Watoto Njiti

Soma - https://jamii.app/ChumviHatari
TONY RASHID AMKALISHA BONGANI MAHLANGU

Bondia wa #Tanzania, Tony Rashid arejesha ubingwa wa ABU-Super Bantam Weight baada ya kumpiga kwa point bondia wa Afrika Kusini, Bongani Mahlangu(Profesa) kwenye pambano la Marudio

Soma https://jamii.app/TonyRashid
#JFSports
#UKRAINE: MBUNGE ASEMA WANAWAKE WATAPIGANIA NCHI

Kira Rudik amechapisha picha akiwa ameshika bunduki na kusema anajifunza kuitumia ili kutetea ardhi yake dhidi ya Urusi

Amesema Wanawake watatetea Nchi yao kama Wanaume

Soma - https://jamii.app/WanawakeUkraine

#RussiaUkraineConflict
RAIS WA UKRAINE AVAA GWANDA NA KUINGIA VITANI

Rais Volodymyr Zelensky ameingia "Uwanja wa Vita" kutetea Nchi yake

Awali, kulikuwa na tetesi Rais huyo amekimbia Nchi. Alijitokeza na kuomba Wananchi wapuuzie taarifa hizo

Soma - https://jamii.app/GwandaUkraine

#RussiaUkraineConflict
MAREKANI: RAIS BIDEN ATEUA MWANAMKE MWEUSI KUWA JAJI WA MAHAKAMA YA JUU

Ketanji Jackson anakuwa Mwanamke wa kwanza Mweusi kwenye Mahakama ya juu kabisa ambayo awali ilitangaza hastahili kupata Uraia wa Marekani kutokana na rangi ya Ngozi yake

Soma https://jamii.app/KentanjiSupreme
#JFLeo
RELI, DARAJA VYASOMBWA NA MAJI. ABIRIA WAKWAMA MOROGORO

Mvua zinazoendelea kunyesha Mkoani Morogoro zimesababisha uharibifu wa Miundombinu ya Reli ya kati na Barabara ambapo Daraja la Kidete limekatika na kupelekea Treni kusimamisha safari zake

Soma - https://jamii.app/AbiriaKilosa
URUSI: Mtandao wa #Facebook unaomilikiwa na Kampuni ya Meta umezuiwa Nchini Urusi kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kupishana ktk Masharti ya vitu vya kuweka Mitandaoni wakati huu wa vita na #Ukraine

Soma - https://jamii.app/FBBanRussia

#DigitalRights #RussiaUkraineConflict #PressFreedom
RAIS SAMIA AKUTANA NA MTAWALA WA DUBAI

Rais Samia amezungumza na Makamu wa Rais ambaye ni Waziri Mkuu wa UAE na Mtawala wa Dubai, Sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum

> Ni baada ya kuhutubia katika Maonesho ya Dubai Expo 2020 Mjini Dubai

Soma https://jamii.app/RaisSamiaDubai

#JFLeo
POLAND KUKATAA KUCHEZA NA URUSI MECHI YA KUFUZU KOMBE LA DUNIA

- Poland imesema itakataa kucheza mchezo huo wa Machi 25, 2022 baada ya Urusi kuivamia Ukraine

- Pia itakuwa mwenyeji wa michezo yote ambayo Ukraine ilitakiwa kuwa mwenyeji ila itashindwa kutokana na vita

#JFSports
SERIKALI YATOA TAHADHARI YA MLIPUKO WA POLIO

Serikali kupitia Wizara ya Afya imesisitiza Wazazi kuhakikisha Watoto wanapatiwa dozi kamili ya chanjo #Polio

> Hatua hii imekuja baada ya Malawi kuripoti kisa cha kwanza baada ya muda mrefu

Soma https://jamii.app/MlipukoPolio
#JFAfya
PWANI: MELI YA MAFUTA YAUNGUA

Meli ndogo iliyokuwa na Mafuta imeungua ikiwa kwenye maegesho ya Bandari ya Nyamisati. Meli hiyo ilikuwa na safari ya kuelekea Kisiwa cha Mafia kupeleka mafuta hayo

Soma - https://jamii.app/MeliNdogo

#JamiiForums #JFLeo
UKRAINE: MASHAMBULIZI YAPELEKEA MAELFU KUKIMBILIA NCHI JIRANI

Zaidi ya Raia 150,000 wa #Ukraine wamevuka Mipaka kuingia Mataifa jirani katika upande wa Magharibi kutafuta usalama, wakati Urusi ikishambulia Mji Mkuu wa Nchi hiyo pamoja na Miji mingine kwa mashambulizi ya angani

Soma - https://jamii.app/UkraineUsalama

#RussiaUkraineConflict
SWEDEN YAUNGANA NA POLAND KUKATAA KUCHEZA NA URUSI

- Sweden imeungana na Poland kukataa kucheza na Urusi katika mchezo wa kufuzu kucheza Kombe la Dunia nchini Qatar

- Mshindi wa mchezo kati ya Poland na Urusi angekutana na Mshindi kati ya Sweden na Jamhuri ya Czech

#JFSports
BILIONEA ABRAMOVICH AJIWEKA KANDO CHELSEA LAKINI BADO NI MMILIKI

Mmiliki wa Chelsea FC ametangaza kujiweka kando na majukumu ya Uongozi ndani ya Klabu hiyo na kukabidhi kwa Bodi ya Wadhamini ambapo yeye ataendelea kubaki katika nafasi ya umiliki

Soma - https://jamii.app/ChelseaUnrest
SERIKALI KUSAIDIA WATANZANIA WALIO UKRAINE KURUDI NCHINI

Serikali inawasaidia Watanzania takriban 300 waliopo #Ukraine kuingia Poland na Romania ambapo kuna utulivu ili waweze kurejea Nchini

Hadi sasa, hakuna madhara yaliyoripotiwa kwa Watanzania

Soma - https://jamii.app/WatanzaniaUkraine
UKRAINE: WAFUNGWA WENYE UZOEFU WA KIJESHI KUACHWA HURU

Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali asema wataachwa huru ili wasaidie kuipigania Nchi yao

Aidha, Wanawake wamesema watapambana kwa kuchangia damu ili kunusuru majeruhi

Soma - https://jamii.app/MilitaryExperience

#RussiaUkraineConflict