JamiiForums
52.5K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
RAIS MAGUFULI: MAKONDA RUDISHA FEDHA ZA TASAF KAMA ULIZITUMIA

- RC Makonda amesema alinufaika na TASAF mwaka 2012 alipopewa nauli na Rais Mstaafu Mkapa kwenda Dodoma kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa UVCCM

- Rais Magufuli amesema anafikiri Makonda alitumia fedha zilizotumika kwa Kaya 22,034 ambazo kwenye uchunguzi zilibainika si masikini

Zaidi, soma https://jamii.app/MakondaVsMagufuli-TASAF
RWANDA: MSANII KIZITO MIHIGO AKUTWA KAFA AKIDAIWA AMEJINYONGA KITUO CHA POLISI

> Kizito Mihigo (38) alikamatwa na Polisi siku tatu zilizopita kwa madai kuwa alikuwa kwenye harakati za kujiunga na kundi linalopinga Serikali

> Aliwahi kuhukumiwa kifungo cha miaka 10 kwa mashtaka ya kutaka kumuua Rais Paul Kagame

Zaidi, soma https://jamii.app/KizitoMihigoDead
NJIA ZA KUFANYA NYUMBANI KWAKO KUWA ENEO LA ELIMU KWA MTOTO WAKO

> Ishi kwa mfano unaotaka kuuona kwa mtoto. Wazazi wawe wamoja katika kulea

> Jifunze miongozo ya malezi kwa kujielimisha kupitia vitabu, majarida na makala

Soma https://jamii.app/ElimuNyumbani
UINGEREZA: TAHADHARI YA HALI MBAYA YA HEWA NA MAFURIKO YATOLEWA

> Mamlaka zimetoa tahadhari kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha

> Serikali imesema imewekeza mabilioni ya pesa katika miundombinu ili kukabiliana na mafuriko hayo

Zaidi, soma https://jamii.app/StormDennis-UK
KILIMO CHA PILIPILI ZA MWENDOKASI ‘HABANERO’

> Andaa kitalu mbinuko, tumia samadi. Siku 2 baada ya mbegu kuota mwagilia maji ya kutosha, pulizia dawa

> Baada ya Siku 30-35 hamishia miche shambani. Panda kwa sm 30-60 kutoka mmea na mmea na sm 70-100 mstari. Mavuno ni baada ya siku 90

Soma zaidi jamii.app/PilipiliMwendokasi
CAMEROON: WATU 22 WAUAWA KATIKA SHAMBULIO LA KIJIJI

> Umoja wa Mataifa (UN) umesema watu 22 wakiwemo Watoto wamefariki katika shambulio lililofanywa katika Kijiji cha Ntumbo

> Haijafahamika bado waliofanya shambulio hilo lakini katika eneo hilo kumekuwa na mapigano kati ya Waasi na Serikali

Soma - https://jamii.app/CameroonMassacre
LUKUVI AKABIDHI EKARI 715 KAMA ALIVYOAGIZWA NA RAIS MAGUFULI

> Rais Magufuli tarehe 11 Februari, 2020 alimwagiza Waziri wa Ardhi, William Lukuvi kuhamisha umiliki wa ekari hizo kutoka katika Wizara yake kwenda kwa Manispaa ya Kigamboni

Zaidi, soma https://jamii.app/ArdhiLukuvi
GUARDIOLA NA STERLING KUBAKI MAN. CITY

- Inadaiwa Kocha Pep Guardiola (49) na Mchezaji Raheem Sterling (25) hawataondoka hata kama klabu hiyo isiposhinda rufaa yake

- Man. City imefungiwa kwa misimu 2 kushiriki michuano ya UEFA kwa kuvunja Kanuni za ‘Financial Fair Play’
ARUSHA: POLISI WAANZA KUTEKELEZA MAAGIZO YA RC GAMBO

> Jeshi la Polisi limeanza kuyafanyia kazi maelekezo ya kuwakamata wanaosambaza video za ubovu wa barabara kwenye hifadhi ya Ngorongoro

> Polisi imemtaka Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema kutoingilia suala hilo

Zaidi, soma https://jamii.app/AgizoKutekelezwa
MALALAMIKO: MAMLAKA KUKAZANIA UKATAJI WA BIMA NA KUSHINDWA KUTETEA WATEJA ITOKEAPO AJALI

- Mdau wa JamiiForums amehoji, kwanini mamlaka imshurutishe mtu akate Bima ya chombo cha moto, lakini haiwashurutishi mawakala wa Bima kulipa wateja wao wanapopata matatizo?

- Ameuliza, “Kwanini Sheria isingeweka wazi kwamba Mteja wa Bima alipwe ndani ya siku kadhaa baada ya ajali kuthibitishwa na Polisi na endapo akichelewa pesa iwe inaongezeka na baada ya siku 15 kama atakuwa hajalipa mtoa huduma akamatwe kwa nguvu?”

Kujadili, tembelea https://jamii.app/BimaMagari
TATIZO LA KUSHINDWA KURUDIA TENDO NA MADHARA YA DAWA ZINAZOTUMIKA

> ‘Refractory period’ ni kipindi ambacho haiwezekani kwa mwanaume kurudia tendo baada ya mshindo

> Hudumu kwa dakika chache mpaka siku chache. Matumizi ya Dawa huweza kusababishia utegemezi

Zaidi, soma https://jamii.app/RefractoryPeriod
DAR: SOKO LA TEGETA NYUKI LATEKETEA KWA MOTO

> Maduka, Vibanda na Magenge ya Wafanyabiashara ndani ya soko hilo lililopo Tegeta Jijini Dar yametekea kwa moto usiku wa tarehe 17 Februari, 2020

> Inadaiwa kuwa chanzo cha moto huo uliosababisha hasara kubwa ni hitilafu ya umeme

Zaidi, soma > https://jamii.app/MotoSokoTegetaNyuki
UPDATE: Watu waliofariki kwa #coronavirus wamefikia 1,873 huku Watu zaidi ya 73,325 wakiambukizwa virusi hivyo

- Vifo vitano vimetokea Taiwan, Ufaransa, Hong Kong, Ufilipino na Japan

- Watu 12,552 wamepata ahueni dhidi ya maambukizi hayo na kuruhusiwa kutoka hospitalini
MOSHI, KILIMANJARO: MEYA MBOYA (CHADEMA) ATAKIWA KURIPOTI POLISI

> Yadaiwa huenda Meya Raymond Mboya akafikishwa Mahakamani leo akidaiwa kuhujumu uchumi kwa kufanya biashara ya madini bila kulipa mrabaha (Royalties)
CHATO: AHUKUMIWA MIAKA 30 KWA KUBAKA MWANAFUNZI WA DARASA LA 6

> Medi Maliatabu alikamatwa Oktoba 2019 na alikiri kufanya mapenzi na mtoto huyo

> Kufanya ngono na mtoto ni kosa la jinai kinyume na kifungu cha sheria namba 130(1) na 2(e)

Soma https://jamii.app/JelaKwaKubaka
LINDI: MWANAJESHI ADAIWA KUMUUA MWENZAKE KWA KUMPIGA RISASI 19

> Askari Pascal Lipita (28) anatuhumiwa kumuua, Askari Baserisa Ulaya kwa kile kinachodaiwa kuwa ni wivu wa mapenzi

> Tukio lilitokea Februari 10, 2020 ktk kambi ya Nang’ondo

Zaidi, soma https://jamii.app/AskariAuaAskari
NYARAKA ZINAZOONESHA CHINA ILIVYOWAFUNGA WAUIGHUR ZAVUJA

- Zinaonesha China inavyotumia teknolojia ya juu kuwafuatilia, kuwatambua na kuwakamata

- Zimeelezea hatma ya watu 311 waliopelekwa kambini kwa kufuga ndevu, kufunga au kuomba pasipoti

Zaidi, soma https://jamii.app/NyarakaWauighurChina
UTEUZI: Rais Magufuli amemteua Dkt. Benson Otieno Ndiege kuwa Mrajis wa Vyama vya Ushirika Tanzania na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika (TCDC)

> Wengine walioteuliwa ni Mulande Charles Msolwa na Nyakunga Collins Bernedict

Zaidi, soma - https://jamii.app/RaisUteuziTCDC
NIGER: WATU 20 WAFARIKI BAADA YA KUKANYAGANA WAKATI WAKIPOKEA MSAADA

> Wanawake 15 na Watoto 5 wamepoteza maisha huku watu wengine 10 wakijeruhiwa

> Maelfu ya watu walijitokeza kupata msaada, jambo lililopelekea vurugu na kukanyangana

Zaidi, soma https://jamii.app/DeadlyStampede-Niger
KISUTU, DAR: MBUNGE ZITTO KABWE AKUTWA NA KESI YA KUJIBU

- Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemkuta na kesi ya kujibu Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT- Wazalendo), Zitto Kabwe

- Ni katika kesi ya Uchochezi inayomkabili ambapo Mahakama imesema ana mashtaka matatu ya uchochezi

Zaidi, soma https://jamii.app/ZittoKesiKujibuUchochezi