JamiiForums
52.7K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
MICHEZO: Klabu ya Yanga imepinga adhabu iliyopewa na Kamati ambayo iliwafungia wachezaji wake 3 na kutoa onyo kwa kocha Luc Eymael
-
Imesema, haikubaliani na adhabu hizo kwani kuna mambo mengi ya kisheria hayakufuatwa mpaka kuamua kutoa hukumu hiyo ambayo awali walipeleka malalamiko yao kwa Wasimamizi wa Ligi lakini hawakupewa majibu
-
Yanga wameamua kuandika barua TFF, CAF, FIFA, TAKUKURU na Mamlaka nyingine husika kulalamika juu ya hilo
-
Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi (TPLB), alitangaza kuwafungia mechi 3 na faini ya Tsh. 500,000 wachezaji 3 baada ya kugoma kutoka uwanjani katika pambano dhidi ya Mbeya City
KENYA HATARINI KUKUMBWA NA BAA LA NJAA KUTOKANA NA WINGI WA NZIGE

> Nzige hao wamesharipotiwa kufika katika kaunti 13 kufikia mwishoni mwa wiki iliyopita na wanaendelea kuenea maeneo mengi nchini humo

> Serikali imekiri hali hiyo itasababisha ugumu wa hali ya maisha kwa mwaka 2020 kutokana na athari mbaya kwa Kilimo na Uchumi

Soma - https://jamii.app/NjaaUvamiziNzigeKE
LUGOLA: NITAVUA NGUO KAMA ITATHIBITIKA NILINUNUA SARE HEWA ZA POLISI

> Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), amemtaka Lugola ambaye alikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, kutoa maelezo kuhusu sakata la ufisadi katika ununuzi wa sare za Jeshi la Polisi nchini

> Lugola alimtuhumu Mussa Assad (Aliyekuwa CAG) kupotosha ukweli juu ya ununuzi wa sare hizo

Soma https://jamii.app/UfisadiKangiPAC
JE, NI SAHIHI MAGARI YA ABIRIA KUJAZA MAFUTA ZIKIWA NA ABIRIA NDANI?

> Mdau ndani ya JamiiForums.com anasema, imekuwa kawaida siku zote kuona Daladala na hata Mabasi ya Mikoani yakijaza mafuta huku yakiwa yamepakia abiria ndani ya gari

> Anahoji kuhusu usalama wa maisha ya abiria kwani moto unaweza kutokea. Je, hatuna sheria za kumlinda abiria katika hili?

Kwa mjadala zaidi - https://jamii.app/DaladalaMafutaAbiria
ARUSHA: JESHI LA POLISI LAUA WATU WATANO WANAODHANIWA KUWA MAJAMBAZI SUGU

> Wamekutwa na Shotgun Pump Action 32265, Chinese Pistol, Bastola bandia, risasi 11, simu 2 na pikipiki 3

> Mkuu wa Mkoa aahidi kuwazawadia waliofanikisha zoezi hilo

Soma https://jamii.app/WatanoWauawa
BUNGE LAJADILI SHERIA YA DHAMANA KWA KESI ZA UHUJUMU UCHUMI

> Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani amesema, kwa kuwa kesi za Uhujumu Uchumi hazina dhamana, ipo haja kwa Bunge kutunga Sheria ya marekebisho na kubadilisha pale ambapo itaona panafaa

> Mbunge Sabrina Sungura alihoji sababu ya vijana wengi wakiwemo kina Tito magoti kukutwa na kesi za Uhujumu Uchumi na kukaa mahabusu muda mrefu

Soma - https://jamii.app/DhamanaUhujumuUchumi
WATOTO MILIONI 6.3 WANATARAJIWA KUFARIKI KWA KICHOMI

> Kichomi husababishwa na Bakteria, Virusi au Kuvu hufanya watoto kushindwa kupumua, mapafu yao huwa yamejaa usaa na maji

> Kichomi kilisababisha vifo laki nane mwaka 2019

Soma https://jamii.app/UNICEFKichomi
NIGERIA: UGONJWA WA LASSA UMEUA WATU 41

> Watu 258 wamethibitishwa kuwa na Homa hiyo, wakiwemo wafanyakazi wa Kupambana na Homa hiyo

> Taasisi ya Kudhibiti Magonjwa ya Kuambukiza nchini Nigeria, imeanzisha vituo vya dharura vya tiba

Soma https://jamii.app/LassaNigeria
MAONI YAKO NI YAPI KUHUSU MKE KUMSALIMIA MUMEWE 'SHIKAMOO'?

> Kwa desturi, mazungumzo karibia yote huanza kwa salamu. Aina ya salamu hutegemea wakati gani mmekutana na mna mahusiano gani

> "Shikamoo" ni moja kati ya salamu na wengi husema asili yake ni ya kitumwa na ina maana ya 'nipo chini ya miguu yako'. Je, unadhani salamu hii inafaa kutumiwa na wanandoa au wapenzi?

Tembelea - https://jamii.app/SalamuShikamooMeKe
#JFMahusiano
ULINZI WA KIDIGITALI: NJIA IPI SALAMA ZAIDI YA KUFUNGA 'SCREEN' YA SIMU YAKO?

Moja ya njia inayotumiwa sana ili kuzuia simu yako (smartphone) kutochakata mambo kinyume na matakwa ya mmiliki au kuzuia mtu asiyehusika kuitumia ni kufunga 'screen' ya simu

Ziko njia nyingi za kufunga screen ya simu. Soma maelezo yafuatayo kisha chagua inayokufaa

> SLIDE TO UNLOCK: Hii ni njia rahisi na isiyoshauriwa, kuweka hii ni sawa na kufunga mlango kisha unaweka jiwe dogo ili usifunguliwe. Kamwe usitumie njia hii!

> PIN CODE LOCK: Hizi ni namba sita zinazotumika kufunga screen ya simu yako. Ni njia kongwe zaidi ya ulinzi wa simu ambapo miliki anapaswa kuweka namba 6 zilizopangiliwa bila ya kufuatana na anapaswa kuzikumbuka wakati wote

> PATTERN LOCK: Hii si njia kongwe ya ulinzi wa simu, imetokana na Maendeleo ya Teknolojia. Njia hii imekuwa ikikosolewa sana na wataalam wa #UlinziWaKidigitali. Inaelezwa kuwa ni rahisi kwa mdukuzi kukariri mchoro ama 'pattern'.

> FINGER PRINT LOCK: Njia hii inahusisha matumizi ya alama za vidole vya mmiliki wa simu. Kila anapotaka kuitumia simu yake basi lazima aguse kwa kidole alichosajili ili simu ifunguke. Njia hii ni bora ingawa ina changamoto kadhaa. Mdukuzi anaweza kujaribu vidole vya mhusika awapo usingizini au akiwa kwenye hali ya kulewa

> FACE ID LOCK: Utambulisho wa sura unatumika kufungua screen ya simu. Teknolojia hii kwa kiasi kikubwa ilianza kutumiwa na Kampuni ya Apple. Hii si maarufu na hakuna ushahidi wa wazi kuhusu udukuzi unaoweza kufanywa dhidi ya 'Face ID'

> EYE LOCK: Kila mwanadamu ana jicho la tofauti na mwengine. Utofauti huu ni nyenzo inayotumika katika ulinzi wa simu. Matumizi yake si makubwa ingawa inatajwa kuwa na usalama wa juu

> PASSWORD LOCK: Hii ni njia rahisi na maarufu zaidi. Ni salama na inashauriwa zaidi ingawa mmiliki anapaswa kufuata vigezo vyote vya utengenezaji wa nywila
INDIA: MTANZANIA AKAMATWA NA DAWA ZA KULEVYA

> Ejike Celestine amemkamatwa na vidonge 600 vya #DawazaKulevya, zenye uzito wa gm 250

> Dawa zilizokamatwa zina thamani ya zaidi ya Tsh. milioni 64.3

> Pia, Ejike amekutwa na 'Visa' bandia

Soma https://jamii.app/DawaKulevyaIndia
MWENDELEZO: Shirika la Afya Duniani (WHO) limevitangaza Virusi vipya vya #Corona kuwa Janga la Dharura kutokana na ugonjwa huo kusambaa mataifa mengine kwa kasi huku kukiwa na Mfumo Duni wa Afya
-
Watu takriban 213 wameshafariki kutokana na virusi hivyo nchini China na kumekuwa na visa 98 katika mataifa mengine 18 ingawa hakuna vifo vilivyobainika
DODOMA: LUGOLA AFIKA TAKUKURU KUHOJIWA

- Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amewasili Makao Makuu ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU)

- Anakabiliwa na kashfa ya kuingia mkataba wa kifisadi wa Vifaa vya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini
SERIKALI YAWATAKA WATANZANIA WANAOSOMA CHINA KUTORUDI HUKO

> Serikali imewataka wanafunzi wanaosoma China ambao wako likizo nchini Tanzania, kutorudi China hadi pale zitakapopatikana taarifa za kidiplomasia kuhusiana na ugonjwa wa Corona

> Itakaporidhika na hali inayoendelea China itatoa tamko kwa Watanzania hao kurudi kuendelea na masomo

Soma - https://jamii.app/CoronaWatzMasomoChina
MPANDA: MTOTO WA MWAKA MMOJA NA NDUGUZE WANNE WATELEKEZWA NA BABA YAO

> Mama yao, aliondoka muda mrefu

> Afisa Ustawi wa Jamii alisema, tabia hiyo inakua kwa kasi mwaka 2019 pekee matukio zaidi ya 170 yaliripotiwa Mkoani humo

Soma https://jamii.app/WatotoWatelekezwa
ULINZI WA KIDIGITALI: ZINGATIA YAFUATAYO ILI KUWA SALAMA UNAPOTUMIA SMART TV

> Maendeleo ya Teknolojia yameleta mabadiliko ya Runinga. Kwasasa kuna wimbi kubwa la watu kutoka katika TV za Analogia na kuhamia kwenye Runinga ambazo ni za Kidigitali

> Jamii Forums inakukumbusha kuhusu umuhimu wa kuhakikisha unaendana na Maendeleo ya Teknolojia ukiwa salama wewe na familia yako

Kwa elimu zaidi, soma > https://jamii.app/UlinziSmartTv
BUNGENI: ZITTO ATAKIWA KUFAFANUA KUHUSU BARUA YA KUZUIA MKOPO WA ELIMU

- Spika Ndugai amesema, wanamsubiri Zitto Kabwe awaeleze kwanini aliandika barua hiyo kwa Benki ya Dunia

- Amesema, hilo limewagusa na kuwakera wengi wasiojua limekujaje

Soma https://jamii.app/ZittoAsubiriwaBungeni
JEFF BEZOS APATA TSH. TRILIONI 29.9 NDANI YA DAKIKA 15

> Mkurugenzi Mtendaji wa Amazon amekuwa tajiri mkubwa Duniani baada ya kumpita Bill Gates

> Amepata utajiri zaidi, baada ya hisa za Amazon kupanda na kufikia $2100 sawa na Tsh. 4,840,000

Soma https://jamii.app/AmazonMkurugenzi
NJIA ZINAZOWEZA KUKUSAIDIA KUITAWALA HASIRA (ANGER) YAKO

> Kama upo mazingira fulani na ukaudhiwa na hasira kali ikakushika, ondoka kwa dakika chache eneo hilo ili ubongo upate nafasi ya kutafakari upya

> Fikiria kabla ya kuzungumza: Ukiwa na hasira, ni rahisi kuzungumza maneno makali ambayo yanaweza yakashusha utu wako au wa yule unayemwambia

> Usilimbikize matukio: Kusamehe matukio yaliyopita na kuyasahau ni njia inayopunguza uzito wa tukio jipya. Ukisamehe utakuwa umejisaidia mwenyewe na waliokukosea

Fahamu zaidi - https://jamii.app/NjiaKudhibitiHasira
WAZIRI WA FEDHA ADAIWA KULISABABISHIA TAIFA HASARA YA TSH. MIL 80 KILA SIKU

> Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (CHADEMA) amedai, Waziri Philip Mpango ameshindwa kuruhusu Shirika la Nyumba (NHC), kumalizia miradi yake 4 ya ujenzi wa nyumba na Serikali imelazimika kuwalipa wakandarasi 4 kila mmoja Tsh. milioni 20 kwa siku

Soma - https://jamii.app/DktMpangoHasaraMil80