JamiiForums
52.6K subscribers
34.4K photos
2.46K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
RUKWA: WANAFUNZI KUPIGA KURA ZA SIRI KUWAFICHUA WALIMU WENYE MAHUSIANO YA KIMAPENZI NA WANAFUNZI

> Mkuu wa Mkoa wa Rukwa amesema, kumekuwa na ongezeko la Walimu wa kiume katika Shule za Msingi na Sekondari kujihusisha katika mapenzi na wanafunzi na kuwasababishia ujauzito

> Takwimu kwa kipindi cha 2017 hadi 2019 ni mimba 722 zimeripotiwa kati ya hizo, 171 walikuwa Shule za Msingi na 551 walikuwa Sekondari

Soma - https://jamii.app/KuraWanafunziWakware
DANGOTE AONGOZA KWA UTAJIRI AFRIKA, MO DEWJI ASHIKA NAFASI YA 16

> Ripoti ya Forbes 2020 imemtaja Dangote kuwa tajiri namba moja
Afrika

> Utajiri wa Mo washuka kwa Trilioni 3.69. Ameshuka nafasi mbili ikilinganishwa na Ripoti ya 2019

Soma - https://jamii.app/ForbesUtajiriAfrika
HOJA: VIFAA VYA KIELETRONIKI VIMEWAPOTEZEA WATOTO UWEZO WA KUANDIKA VIZURI

> Mdau kutoka JamiiForums.com anasema, matumizi ya Kopyuta, Simujanja, 'Tablets' na vifaa kama hivyo yamepunguza uwezo wa vijana na watoto kuwa na mwandiko mzuri au hata kujua kuandika kwa mkono

> Anashauri Mtoto wako akifika miaka 2, mnunulie mkasi wa plastiki, akiweza kushika mkasi na kuutumia hatopata shida kushika kalamu

> Akifika miaka 3.5 - 4 anza kumpa maneno ya kurudia kuandika akianza na jina lake na mahali anapoishi

Tembelea - https://jamii.app/GadgetsEffectsChildren
#JFMalezi
FAHAMU KUHUSU TIBA YA KUWEKEWA BETRI KWENYE MOYO

> Betri ya Moyo ambayo kitabibu huitwa ‘Pacemaker’ ni kifaa kilichobuniwa ili kumsaidia mtu ambaye Moyo wake unashindwa kuzalisha nguvu ya kusukuma damu kwenda sehemu mbalimbali za mwili

> Inaelezwa kuwa, binadamu wa kwanza kunufaika nacho, aliwekewa kifaa hicho mwaka 1960 na tangu kuanzishwa kwa huduma hii, watu zaidi ya milioni 3 duniani huwekewa kifaa hicho kila mwaka

> Miongoni mwa watu maarufu waliopandikizwa mashine hiyo ni Kocha aliyewahi kuifundisha Manchester United ya Uingereza, Sir Alex Ferguson aliyewekewa kifaa hicho mwaka 2003

Fahamu zaidi - https://jamii.app/KnowledgePacemaker
#JFAfya
USAJILI WA LAINI ZA SIMU: WADAU WAHOJI MAMBO KADHAA

- Mdau wa JamiiForums anahoji uko wapi umakini wa zoezi hilo ikiwa kuna vijana wanaopita mtaani wakisajili laini wanaoweza kutumiwa vibaya

- Kwa kuwa Mtu anaweza kusajili laini 5 za mtandao mmoja anahoji itakuwaje Mtu akisajili laini tofauti na kumpa ndugu yake?

Zaidi, tembelea https://jamii.app/MaoniUsajiliLaini
ESWATINI: KESI YA KWANZA YA UBAKAJI NDANI YA NDOA

> Nhlanhla Dlamini ni wa kwanza kushtakiwa kwa ubakaji kwa kufanya tendo la ndoa na mkewe bila ya idhini yake

> Ni kwa kutumia Sheria ya Makosa ya Kijinsia na Vurugu za Nyumbani ya mwaka 2018

Soma https://jamii.app/KesiNdoaUbakaji
ULINZI WA KIDIGITALI: Jamii Forums inatoa Elimu ya Mtandaoni kuhusu Ulinzi na Usalama wa Vifaa na Mifumo ya Kidigitali kutokana uwepo wa matukio ya kila siku yanayohusisha mashambulizi na kuingiliwa kwa Vifaa vya Kidigitali na Mifumo yake

> Hii ni kutokana na Maendeleo ya Teknolojia kubadili namna ya uendeshaji wa mambo katika jamii, matumizi ya Vifaa vya Kidigitali na Mtandao wa Intaneti yameongezeka kwa kasi

> Hata hivyo, ziko hatari kadha wa kadha zinazowanyemelea watumiaji wa Mifumo ya Kidigitali

> Baadhi ya hatari hizo ni pamoja na shambulizi la Nywila, shambulizi la Barua Pepe, shambulizi la 'DDoS', shambulizi la Virusi, Udukuzi, Wizi wa Fedha n.k
ULINZI WA KIDIGITALI: Ulinzi huu unahusisha elimu ya kulinda vifaa(simu, kompyuta n.k), mifumo na utambulisho wa Mtu dhidi ya kuingiliwa na Mtu asiyehitajika

Elimu ya Ulinzi wa Kidigitali husaidia sana kutunza faragha ya mtumiaji

> Swali la kujiuliza: Je, unazijua njia unazoweza kuzitumia kujilinda dhidi ya Mashambulizi ya Kimtandao?

> Baadhi ya njia hizo ni kuweka nywila(Password) kwenye vifaa vyako, hakikisha vifaa vyako vyako pamoja na Mifumo yake na Programu Tumishi (Application) ziko katika sasa 'Updated'

> Nyingine ni kuhakikisha unatumia Programu zilizothibishwa kuwa ni salama, hakikisha unatumia 'Anti-Virus' iliyoidhinishwa, epuka kufungua Kiunganishi (Link) usichokitambua

> Fanya 'Setting' za Kiusalama kwenye Barua Pepe, Simu na Kompyuta yako
ULINZI WA KIDIGITALI: JIFUNZE KUHUSU NYWILA (PASSWORD)

> Nywila ni mfano wa Ufunguo wa Kidigitali unaotumika kufungua milango ya akaunti na taarifa zilizohifadhiwa katika Mifumo na Programu za Kidigitali

> Nywila hupaswa kuwa Siri ya Mmliki au Wamiliki kwasababu nywila ni ulinzi namba 1 wa taarifa na faragha za Mtumiaji wa Vifaa na Mifumo ya Kidigitali

> Nywila ina umuhimu mkubwa lakini inapaswa kutengenezwa vizuri ili isiwe rahisi Kudhaniwa, Kuhisiwa na Kukisiwa

> Nywila Bora huundwa kwa kutumia, Herufi Kubwa na Ndogo, Namba, na Alama na ni lazima Iwe Ndefu (herufi 16) na ya Kipekee
ULINZI WA KIDIGITALI: JIFUNZE KUHUSU NYWILA (PASSWORD)

Ili kuilinda Password yako isiweze kudukuliwa unapaswa kuzingatia mambo yafuatayo;

> Usitumie Nywila (Password) moja kwenye kurasa zako zote za Mitandao ya Kijamii. Hakikisha kila mtandao unatumia Password yake

> Hakikisha Nywila yako ina jumla ya herufi/alama zisizopungua 16 au na zaidi (Mfano: M1m1$%678abc@£+#)

> Usitumie jina la ndugu, Mtoto au Mzazi wako au mfugo wako(mfano Mbwa, Paka etc), mwaka wa kuzaliwa au namba ya simu kama nywila yako. Ni rahisi Mtu kuhisi na kukufanyia udukuzi

> Usitumie maneno ya kwenye Kamusi kama nywila yako. Na usiruhusu kivinjari chako (Web browsers -Chrome, Opera, Firefox, Brave n.k) kuhifadhi nywila yako
MTU AKIOMBA RUSHWA YA NGONO ANAKUWA AMETENDA DHAMBI NGAPI?

> Anakuwa amezini, amesema uongo, ameiba, amesaliti, amepoka #HakiYaMtu

> Anakuwa amevunja #SheriaZaNchi na kumuonea mnyonge

#KemeaRushwa
ULINZI WA KIDIGITALI: JIFUNZE KUHUSU NYWILA (PASSWORD)

> Nywila dhaifu unahusisha Jina la Mmiliki wa Akaunti, mfano: henrik19. Unatumia herufi zilizo mtiririko kama vile ABCDEFG au QWERTY ambazo ziko kwenye 'Keyboard' ya Kompyuta

> Inahusisha tarehe, mwezi na mwaka wa kuzaliwa, au namba nyingine kama za kitambulisho, mtihani, bima ya afya au pasipoti

> Usihifadhi nywila yako kwa kuandika kwenye karatasi, hii itamrahisishia mdukuzi endapo ataipata karatasi hiyo

> Mambo mengine ya kuzingatia, ni kubadili nywila yako kila baada ya miezi 3
MAKONDA: ASIYE NA NAMBA WALA KITAMBULISHO CHA TAIFA AMEENDEKEZA UMBEA

- RC Paul Makonda amedai Wananchi wa Mkoa wa Dar ambao hadi jana hawakuwa na Namba wala Kitambulisho cha Taifa waliendekeza zaidi umbea kuliko kufuatilia mambo ya msingi

Zaidi, soma https://jamii.app/MakondaKitambulishoUmbea
SHERIA YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA NA. 11 MWAKA 2007

- Kifungu kinaeleza, Mtu ambaye kwa udanganyifu atajifanya Afisa wa TAKUKURU au ana Ofisi na kufanya chochote kuhusiana na Kazi za Afisa huyo atakuwa ametenda Kosa

- Atawajibika kwa kupigwa faini isiyozidi Tsh. Milioni 2 au kifungo kisichozidi mwaka mwaka au vyote

#KemeaRushwa
OLE SABAYA AAGIZA KUKAMATWA WAMILIKI WA MABASI KWA KUHUJUMU MIUNDOMBINU YA RELI

> Wanadaiwa kuunda makundi ya Watu na kuharibu reli ya Dar-Moshi ili kuathiri usafiri huo

> Waliotakiwa kuripoti Polisi ni Clemence Mbowe na Rodrick Uronu

Zaidi, soma https://jamii.app/SabayaUhujumuReli
WAZIRI MKUU AZUIA SUKARI KUAGIZWA KUTOKA NJE YA NCHI

- Kassim Majaliwa amezuia hadi sukari inayozalishwa na Kiwanda cha Zanzibar kilichopo Mahonda iishe

- Amesema, haiwezekani kiwanda hicho kinachozalisha tani 6,000 kwa mwaka kikakosa wateja

Zaidi, soma https://jamii.app/SukariKutojaNjeMarufuku
KENYA: WATANO WASHIKILIWA NA POLISI KWA TUHUMA ZA KUTAKA KUFANYA SHAMBULIO LA KIGAIDI

> Ni wanawake wawili na wanaume watatu, Raia wa Marekani, Kenya na Somalia

> Walitaka kushambulia Klabu moja iliyopo Barabara ya Kiambu

Zaidi, soma - https://jamii.app/UgaidiPolisiNairobi
SERIKALI KUTUMIA BUSARA KATIKA UFUNGAJI WA LAINI ZISIZOSAJILIWA

- Itawasaidia walioshindwa kusajili kwa kukosa Kitambulisho cha Taifa au Namba licha ya kuanza mchakato

- Imesema, wale wenye vitambulisho na hawajasajili, laini zao zitafungwa

Zaidi, soma https://jamii.app/SerikaliHekimaKufungaLaini
TANGA: POLISI WAZUIA MSAFARA WA PROF. LIPUMBA

- Msafara wa Mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba umezuliwa na Polisi Wilayani Mkinga

- Polisi hao wamedai hawana Taarifa za Msafara wa Lipumba aliyeenda Mkoani humo kwa Ziara ya Kikazi

Zaidi, soma https://jamii.app/TangaZiaraLipumba
YEMEN: WANAJESHI 83 WAUAWA NA 148 KUJERUHIWA

> Mashambulizi hayo yanafuatia miezi kadhaa ya utulivu kiasi

> Yemen inakabiliwa na vita kati ya Waasi wa Kihouthi wanaoungwa mkono na Iran, na Majeshi ya Serikali

Zaidi, soma https://jamii.app/YemenWanajeshi