JamiiForums
52.7K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
TEXAS, MAREKANI: HUKUMU YA KWANZA YA KIFO KWA MWAKA 2020 YATEKELEZWA

- John Gardner ameuawa kwa kuchomwa Sindano ya Sumu hapo jana baada kukutwa na Hatia ya kumuua mkewe

- Pia, alikuwa na historia ya muda mrefu ya dhuluma dhidi ya wake zake

Soma https://jamii.app/HukumuKifoMauajiMke
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
UPDATE: Wabunge wa Baraza la Wawakilishi wamepitisha Azimio la kumshtaki Rais Trump kwa kupiga kura 228 dhidi ya 193

> Spika Nancy Pelosi amesaini uamuzi huo sambamba na Timu ya Wabunge wa Democratic ambao wataendesha mashtaka ya kesi hiyo itakayoanza Januari 21

#JFLeo
MVUA DAR: BARABARA YA JANGWANI YAFUNGWA

> Mvua yasababisha Barabara ya Morogoro eneo la Jangwani kufungwa baada ya maji kujaa

> Mamlaka ya Hali ya Hewa, imesema Mvua inatarajiwa kunyesha tena kesho Januari 17, 2020

Soma https://jamii.app/MadharaMvuaDar
LUKUVI AANIKA DHULUMA ZA MAOFISA MIKOPO BENKI

> Asema, baadhi yao hushirikiana na Madalali Matapeli kuwaibia Wananchi kwa kuuza nyumba zao kwa mnada bila kufuata taratibu

> Serikali yawataka wanaondesha Mtandao huo kuacha mara moja

Soma https://jamii.app/DhulumaOfisaBenki

#JFLeo
MBEYA: WATUMISHI 4 WA HOSPITALI WAKAMATWA KUTOKANA NA UTENDAJI MBOVU

> Naibu Waziri wa Afya ameagiza kuwekwa ndani na kutolewa katika nafasi zao Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Tukuyu na Afisa Ugavi

> Pia, amegiza kukamatwa na kuwekwa ndani kwa Mfamasia na Afisa Manunuzi wa Hospitali hiyo kutokana na usimamizi mbovu wa Stoo ya Dawa

Soma - https://jamii.app/DaktariMbaroniHudumaMbovu
MKAKATI WA TAIFA DHIDI YA RUSHWA NA MPANGO WA UTEKELEZAJI (AWAMU YA 3: 2017-2022)

- Vitendo vya Rushwa vinatafsiriwa kuwa ni kutoa, kupokea au kushawishi moja kwa moja au kitu chochote cha thamani kinachotolewa ili kupindisha utaratibu katika Utoaji wa Maamuzi

#KemeaRushwa
WAZIRI KAMWELWE: MUDA WA KUSAJILI LAINI ZA SIMU HAUTAONGEZWA

> Serikali haitaongeza muda baada ya siku 20 alizoongeza Rais Magufuli kumalizika

> Wananchi wameshauriwa kuwa makini katika siku zilizosalia kwani Wizi wa Kimtandao umeongezeka

Soma - https://jamii.app/MudaUsajiliLaini-TZ
MISRI, ETHIOPIA NA SUDAN ZAINGIA MAKUBALIANO KUHUSU MATUMIZI YA MTO NILE

> Nchi hizo zimefikia Makubaliano ya Awali ya kujaza maji kwenye Bwawa la Grand Renaissance

> Makubaliano ya mwisho yatafanyika Washington, Januari 28-29 mwaka huu

Soma - https://jamii.app/MakubalianoMtoNile
UPINZANI NAMIBIA WAGOMA KUTUMIA KISWAHILI KAMA LUGHA YA HIYARI KWA SHULE ZA SERIKALI

> Wasema kuna mambo ya muhimu ya kushinikiza kwa wakati huu kuhusu Mfumo wa Elimu

> Wizara ya Elimu ilisema itafanya Kiswahili Lugha ya Hiari 2021

Soma zaidi https://jamii.app/KswahiliNamibia
TANZANIA vs KENYA vs UGANDA: UCHAGUZI WA RAIS

- Katiba ya Tanzania inasema Mshindi wa Urais ni yule atakayepata Kura Nyingi kuliko Mgombea mwingine

- Katiba za Kenya na Uganda zinasema Mshindi wa Urais ni yule atakayekuwa amepata Zaidi ya Nusu ya Kura zote

Zaidi, soma https://jamii.app/Katiba-TZvsUGvsKE

#Katiba
MWANAFUNZI AGOMA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA, ADAI HANA AKILI

> Amesema mbele ya Mkuu wa Wilaya kuwa, yupo tayari kufungwa na sio kusoma

> Aomba ajifunze kushona Cherehani kwani anatamani kuwa Mwanamitindo

Soma - https://jamii.app/MwanafunziAkataaMasomo
JENGA TABIA YA KUAGA KILA UNAPOTOKA KWA KUTOA TAARIFA SAHIHI

> Ni taarifa kama Jina la unakokwenda, Mtu na Anuani ya mtu unayekutana naye na Muda utakaokuwa haupo

> Hii itarahisisha upatikanaji wako pindi utakapopatwa na matatizo

Soma https://jamii.app/TabiaKuagaUnapotoka
#JFLeo
DALILI ZA MLIPUKO WA NZIGE MKOA WA KILIMANJARO

> Mdau kutoka JamiiForums anadai kuwa, kuna kila dalili ya Nzige Tanzania

> Ni vema Serikali ikachukua tahadhari kabla ya tatizo kuwa kubwa zaidi

Some zaidi https://jamii.app/NzigeKilimanjaroTz
KIJANA AUNDA EMOJI KUUTANGAZA UZURI WA AFRIKA

> O'Plerou Denis Grebet (22), aliona Vyombo vya Habari vinazungumza upande mbaya wa Afrika (Umaskini na Njaa)

> Sanaa yake inaonesha kuwa Afrika ina vitu vya kustaajabisha Dunia

Soma Zaidi https://jamii.app/MwanafunziEmojisAfrika
KAGERA: AMUUA MWANAYE KWA KUMCHOMA MOTO MAKALIONI NA USONI

> Juma Daniel anatuhumiwa kumchoma moto mwanaye, na kumjeruhi sehemu za haja kubwa kwa kifaa cha ncha kali

> Ni baada ya mtoto huyo kujisaidia haja kubwa kitandani wakiwa wamelala

Soma - https://jamii.app/BabaAmuunguzaMwanaye-KGR
RASMI: MBWANA SAMATTA AKUBALI KUJIUNGA NA KLABU YA ASTON VILLA

> Mshambuliaji huyo raia wa Tanzania siku ya kesho atasafiri hadi nchini England kwa ajili ya kufanyiwa vipimo vya afya

> Imeelezwa kuwa Aston Villa imekubali kulipa kiasi cha Paundi Milioni 9 sawa na zaidi ya Shilingi za Kitanzania Bilioni 27 kwa ajili ya uhamisho wa Samatta

#JFSports
MATUMIZI YA INTANETI: VODACOM YAONGOZA KUWA NA GHARAMA KUBWA

> Kwa mujibu wa taarifa ya TCRA ya robo mwaka iliyoishia Septemba 2019 Vodacom hutoza Tsh. 205 kwa Megabyte (MB)

> Zantel hutoza Tsh. 93 kwa MB, huku wateja wa Airtel na Tigo wakilipa kiwango sawa ambapo gharama ya MB moja ni Tsh. 29

> Gharama zote hizi ni bila kodi na zinatozwa endapo mteja hajajiunga kifurushi

Soma - https://jamii.app/GharamaIntanetiTz
TANZANIA vs KENYA vs UGANDA: MSAMAHA WA RAIS

#KatibaTanzania, Ibara-45 (1), Rais anaweza kumsamehe kwa masharti au la, mtu aliyepatikana na hatia Mahakamani kwa kosa lolote

- #KatibaKenya, Ibara-172 (1): Kutakuwa na Msamaha utakaotekelezwa kwa Ombi la Rais kwa mtu yeyote kulingana na Ushauri wa Kamati ya Ushauri

- #KatibaUganda, Ibara-121: Kwa ushauri wa Kamati, Rais anaweza kumsamehe aliye hatiani kwa masharti au la, Kusamehe sehemu au adhabu yote, Kurahisisha adhabu kali aliyopewa

Zaidi, soma https://jamii.app/Katiba-TZvsUGvsKE
KESI YA KUMUONDOA TRUMP MADARAKANI: MASENETA 100 WAAPISHWA

> Maseneta 100 wameapishwa jana kama Baraza la Mahakama litakaloshughulikia kesi inayomkabili Rais Donald Trump ya matumizi mabaya ya madaraka na kuingilia Bunge

> Kesi hiyo itaanza kusikilizwa Januari 21

Soma - https://jamii.app/Senates100ImpeachmentTrump
MTWARA: WAKULIMA WA KOROSHO WALIPWA TSH. BILIONI 68

> Wakulima wameanza kulipwa fedha zao ambapo awali malipo hayo yalikuwa yamechelewa

> Vyama 41 kati ya 87 vya Wilaya ya Nanyumbu na Masasi vimefunga msimu kwa sababu korosho zimekwisha

Soma https://jamii.app/WakulimaKoroshoMasasi