JamiiForums
52.5K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
RIPOTI: MAKADIRIO YA UKUAJI WA UCHUMI WA DUNIA NI 2.5% MWAKA 2020

> Benki ya Dunia imesema, ukuaji wa Uchumi wa Dunia kwa 2020 unakadiriwa kufikia 2.5% ikilinganishwa na asilimia 2.4 ya 2019

> Ukuaji ktk masoko yanayoibuka na nchi zinazoendelea unatarajiwa kufikia 4.1% kutoka 3.5% ya mwaka 2019

Soma - https://jamii.app/WorldEconomicGrowth
👍1
YANGA YATANGAZA KOCHA MPYA KUTOKA UBELGIJI

- Imemtangaza Luc Eymael atakayekuja kukinoa kikosi hicho kilicho chini ya Kocha wa Muda, Charles Mkwasa

- Luc amewahi kufundisha timu za As Vita, AFC Leopard, Rayon Sports, Al Nasr, Al-Merrikh, Polokwane na Black Leopard
BAADHI YA MAMBO YA KUYAJUMUISHA KATIKA MALENGO YAKO YA KUMLEA MTOTO

> Tenga muda wa faragha na watoto wako. Iwapo unao watoto zaidi ya mmoja, fanya kila uwezalo kupata muda na kila mmoja ili akueleze mipango aliyonayo na wewe umshauri

> Azimia kutomlinganisha mtoto wako na watoto wa wengine. Watoto huzaliwa na vipaji na karama tofauti hivyo usishawishike kutaka mtoto wako afanane na wa majirani

> Mfundishe mwanao stadi moja mwaka huu. Zipo stadi kadhaa muhimu katika maisha ikiwamo kupika, kufua, kutunza bustani, usimamizi wa fedha na kadhalika

Tembelea - https://jamii.app/MalengoKuleaMtoto
DRC: 6000 WAFARIKI KWA UGONJWA WA SURUA

- Hali hiyo imefanya kuwa, kati ya majanga makubwa ya milipuko mabaya zaidi ya magonjwa yanayoambukiza kutokea Duniani

- Kwa Tanzania hali iko tofauti kwa kuwa watoto hupatiwa chanjo ya surua wakiwa na umri mdogo

Zaidi, soma https://jamii.app/PolioDeathRateDRC
USIANZISHE BIASHARA YA MTAJI MKUBWA KWASABABU TU UNA FEDHA NYINGI

> Mdau katika Jukwaa la Biashara ndani ya JamiiForums.com anasema, kuna Kanuni Tatu za Msingi ambazo anaziamini zinafaa katika uwekezaji

> Anashauri kuwekeza kiasi ambacho uko tayari kupoteza iwapo hasara itatokea, wekeza kwa watu na sio vitu na wekeza katika kile unachokipenda na kukiamini na sio vutio la faida kubwa

> Anasema, kanuni hizi ni muhimu sana kwani unapozifuata kuna uwezekano mkubwa sana wa kufanikiwa katika biashara

Tembelea - https://jamii.app/BiasharaKubwaVsMtajiMkubwa
MURANG'A, KENYA: AWAUA WANAYE BAADA YA KUGOMBANA NA MUMEWE

- Esther Wambui (25), amewaua Watoto wake wawili wa Kike hapo jana huko Kimwiriini katika Kijiji cha Gatanga

- Aliwanywesha sumu watoto hao kabla na yeye kujaribu kujiua kwa simu hiyo

Zaidi, soma https://jamii.app/WomanPoisonsDaughters
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Kumetokea vurugu katika Kikao cha Baraza la Madiwani wa Jiji hilo, kwenye kikao maalum cha kujadili na kuamua hatma ya Meya wa Jiji la Dar, Isaya Mwita

- Chanzo cha vurugu ni kusainiwa kwa mahudhurio na Mjumbe ambaye hayupo ndani ya ukumbi wa mkutano

Zaidi, soma https://jamii.app/VuruguBarazaMadiwaniDar
MAREKANI YAZUIA MALI ZA MAKAMU WA KWANZA WA RAIS WA SUDAN KUSINI

> Wizara ya Fedha imezuia mali za Taban Deng Gai (69) nchini Marekani na imepiga marufuku Raia wake kushirikiana na Taban

> Anatuhumiwa kwa ukiukaji wa Haki za Binadamu na kuhusika na kifo cha Wakili Samuel Dong Luak na Mpinzani Aggrey Idry

Zaidi, soma - https://jamii.app/USBlacklistsTabanDeng
MATOKEO YA KIDATO CHA NNE KWA MWAKA 2019 YATANGAZWA

- Katibu Mkuu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), Dkt. Charles Msonde, ametangaza matokeo hayo leo

- Pia, matokeo ya Upimaji ya Kidato cha Pili na matokeo ya Maarifa (QT) yatangazwa

Zaidi, soma https://jamii.app/MatokeoKidato42019
MABASI YANAYOSAFIRISHA VIFURUSHI BILA LESENI YA TCRA YAPEWA ONYO

> Naibu Waziri Nditiye ataka mabasi kufuata taratibu zilizowekwa na Mamlaka

> Ametoa wito kwa Shirika la Posta kuboresha huduma zao ili mizigo isafirishwe na Shirika hilo

Zaidi, soma - https://jamii.app/UkaguziBasiVifurushi
MKAKATI WA TAIFA DHIDI YA RUSHWA NA MPANGO WA UTEKELEZAJI(2017-2022)

> Umelenga kuimarisha na kuwezesha umma kushiriki katika kudai Haki & Uwajibikaji wa Serikali

> Mazingira wezeshi yatawekwa kuhakikisha ushiriki kamilifu wa Wananchi ktk Mapambano dhidi ya Rushwa

#KemeaRushwa
POLISI: TANZANIA IPO SALAMA DHIDI YA VITENDO VYA UGAIDI

> Polisi imewataka Raia wa Kigeni na watalii kuendelea na shughuli zao kama kawaida

> Wamesema kuwa ulinzi unaendelea kuimarishwa nchini kote

Zaidi, soma https://jamii.app/PolisiUsalamaTZUgaidi
ALIYESAFIRI KWA NJIA HARAMU MWILI WAKE WAKUTWA KWENYE GURUDUMU LA NDEGE

> Mwili ulipatikana asubuhi ya Jumatano, Januari 8, karibu na Mji wa Paris, ikitokea Abidjan

> Wengi wanaamini kwamba kijana huyo alikufa kutokana na kukosa hewa au baridi

Zaidi, aoma https://jamii.app/MwiliTairiNdege-UFR
IRAN: NDEGE ILIYOUA WATU 176 ILIKUWA IKIUNGUA KABLA YA KUDONDOKA

- Wachunguzi wamedai wafanyakazi hawakufanya mawasiliano ya redio kuomba msaada

- Pia, sanduku zote mbili ambazo zina data na mawasiliano ya kutoka kwenye ndege zimepatikana

Zaidi, soma https://jamii.app/UchunguziNdegeUkraine-IRN
MHAMIAJI AJIKATA KOO BAADA YA KUKATALIWA KUINGIA MAREKANI

> Raia huyo kutoka Mexico amejiua mita kadhaa kutoka Daraja la Kimataifa la Pharr – Reynosa, Texas

> Maafisa wa eneo hilo wamesema, mtu huyo bado hajatambulika hadi sasa

Zaidi, soma https://jamii.app/MhamiajiAjikataKoo-MXC
MAREKANI YASEMA IKO TAYARI KUFANYA MAZUNGUMZO NA IRAN

> Iko tayari kujadiliana bila masharti baada ya uhasama uliozuka baina yao

> Katika barua yake kwa Umoja wa Mataifa ilijitetea kuwa, ilimuua Qasem Soleimani kama hatua ya kujilinda

Zaidi, soma https://jamii.app/MarekaniMazungumzoIran
NETFLIX KUIFUTA FILAMU INAYOONYESHA YESU KAMA SHOGA

- Uamuzi ulifikiwa ktk kujibu ombi la Shirika la Katoliki lililosema filamu hiyo imeumiza heshima yao

- Uamuzi huo wa Mahakama ni halali hadi Mahakama nyingine itoe amri nyingine tofauti na hiyo

Zaidi, soma https://jamii.app/NetflixFilamuYesu
TETESI: YOUNG AKATAA MKATABA. MAN UTD YAJIONDOA KUMUWANIA ERIKSEN

- Nahodha wa Manchester United, Ashley Young anadaiwa kukataa mkataba wa kuendelea kuitumikia timu hiyo huku akihusishwa kuhamia Inter Milan

- Pia, Man. Utd inadaiwa kufutilia mbali mpango wake wa kutaka kumsajili Kiungo wa Tottenham, Christian Eriksen huku mchezaji huyo naye akihusishwa na Inter Milan
ARUSHA: MWALIMU MBARONI KWA KUMUOMBA MWANAFUNZI RUSHWA YA NGONO

- Ni William Mollel anayefundisha Kidato cha 5 na 6 shule ya Sekondari Embarway

- Inadawia, alikuwa akimnyanyasa Mwanafunzi huyo na kumuambia ili awe na amani, washiriki ngono

Zaidi, soma https://jamii.app/MwalimuEmbarwayMbaroni
TANZIA: Mwandishi Nguli wa Kazi za Fasihi ya Kiswahili Prof. Euphrase Kezilahabi amefariki leo baada ya kuugua kwa muda mrefu

> Atakumbukwa kwa kazi zake kama Rosa Mistika, Uwanja wa Fujo, Kaptula la Marx, Nagona na Mzingile na jinsi alivyotetea Mashairi ya Kisasa

Soma - https://jamii.app/RIPProfKezilahabi
#JFLeo