JamiiForums
52.7K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
DAWASA YATOA TAHADHARI YA UPUNGUFU WA MAJI MKOA WA DAR

> Kutakuwa na upungufu wa huduma ya maji leo hadi kesho ktk Mji wa Bagamoyo, Vijiji vya Zinga, Kerege, Mapinga, Bunju, Boko, Kawe, Kinondoni, Ilala, Temeke na Tabata

> Pia, Tegeta, Kunduchi, Salasala, Jangwani, Mbezi Beach, Mlalakuwa, Mwenge, Mikocheni, Msasani, Sinza, Kijitonyama, Oysterbay, Magomeni, Upanga, Kariakoo, City Centre, Ilala, Ubungo Maziwa, Kigogo, Mburahati na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili

Soma - https://jamii.app/TahadhariUpungufuMaji
ZAMBIA YAHALALISHA BANGI KWA AJILI YA BIASHARA

- Imehalalisha uzalishaji wa Bangi na uuzaji wa mmea huo nje ya nchi kwa matumizi ya Dawa ili kukuza Uchumi

- Haijawekwa wazi kama matumizi ya zao hilo kwa tiba yamehalalishwa ndani ya Zambia

Soma https://jamii.app/ZambiaYaruhusuBangi
MALEZI YA WATOTO NI TAALUMA SIO KITU CHA ASILI

> Kama zilivyo Taaluma nyingine, malezi ya watoto pia ni Taaluma hivyo ili mtu aimudu vizuri ni lazima ajifunze kwa njia rasmi au isiyo rasmi. Ni ngumu kujua namna nzuri ya kuisimamia afya ya mtoto bila kujua misingi na kanuni za afya ya mtoto

> Jifunze malezi kutoka kwa wazazi/walezi waliotangulia. Njia hii ni moja kati ya njia zinazotumiwa na watu wengi duniani lakini madhara yake ni endapo maarifa aliyonayo aliyetangulia sio sahihi basi yana hatari ya kuendelea kurithishwa

Fahamu zaidi - https://jamii.app/ElimuMaleziWatoto
#JFMalezi
APPLE, GOOGLE, TESLA NA MICROSOFT ZAFUNGULIWA MASHTAKA KWA KUTUMIKISHA WATOTO MIGODINI

> Kesi hiyo imefunguliwa na familia 14 za DRC wakiyashutumu makampuni hayo kuwaruhusu watoto wadogo kuchimba madini aina ya Kobalti yanayotumiwa katika bidhaa zao

> DRC inazalisha 60% ya Kobalti Duniani na hutumiwa kutengenezea betri aina ya 'Lithium-ion' zinazotumika kuwasha Magari ya Umeme, Kompyuta Mpakato (Laptop) na Simu Janja

Soma - https://jamii.app/AppleGoogleMicrosoftLawsuit
DAR: CHADEMA YATAKIWA KUTOA BENDERA ZAKE BARABARANI NDANI YA SAA 2

- Mkurugenzi wa Ubungo, Beatrice Dominic ameitaka CHADEMA kuondoa bendera zake karibu na ukumbi wa Mlimani City

- Katika ukumbi huo CHADEMA inafanya Mikutano yake mbalimbali

Zaidi, soma https://jamii.app/BenderaCDM-Ubungo
KILIMANJARO STARS YATOLEWA KWENYE MICHUANO YA CECAFA

- Uganda imeitoa Tanzania Bara #KilimanjaroStars kwa kuifunga goli 1-0 katika mchezo wa Nusu Fainali

- Kilimanjaro Stars itachuana na Kenya kuwania Mshindi wa tatu huku Uganda ikichuana na Eritrea kwenye fainali
DAR: WANNE MBARONI KWA KUKUTWA NA MTAMBO WA KUTENGENEZA FEDHA BANDIA

- Watu hao wamekamatwa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Benki Kuu ya Tanzania

- Wamekutwa na Noti Bandia za Nchi mbalimbali zenye thamani ya zaidi ya Tsh. Milioni 578

Zaidi, zoma https://jamii.app/MbaroniNotiBandia
MWENDELEZO: Polisi wamefika eneo la Ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar unapofanyika Mkutano wa CHADEMA na kuagiza bendera za chama hicho zilizowekwa kushushwa

- Awali, Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo, Beatrice Dominic alikiandikia barua chama hicho kikuu cha Upinzani Nchini kutaka kishushe bendera hizo

Zaidi, soma https://jamii.app/BenderaCDM-Ubungo
MOSHI: WATU 15 WAJERUHIWA BAADA YA BASI KUGONGA MAGARI MENGINE 7

- Wamejeruhiwa na kupelekwa Hospitali ya Mawenzi baada ya basi la Kampuni ya Harambee kudaiwa kupata hitilafu katika mvumo wake wa breki na kuparamia magari hayo 7 katikati ya Mji

Zaidi, soma https://jamii.app/AjaliMoshi15Wajeruhiwa
ZIMBABWE: MKE WA MAKAMU WA RAIS ASHTAKIWA KWA KUTAKA KUMUUA MUMEWE

- Mary Mubaiwa, anadaiwa kujaribu kumuua Jenerali Constantino Chiwenga kwa kuchomoa mrija wa maji (drip) wakati Chiwenga alipokuwa akitibiwa Afrika Kusini miezi 6 iliyopita

Zaidi, soma https://jamii.app/MkeMakamuRais-ZMB
SUDAN KUSINI: KIIR NA MACHAR WAKUBALIANA KUUNDA SERIKALI YA UMOJA FEBRUARI 2020

> Rais Salva Kiir na Kiongozi wa Waasi, Riek Machar wamekubaliana kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa kufikia Februari 2020

> Rais Salva Kiir amesisitiza kwamba swali la idadi ya majimbo, ambalo limekuwa likizua mtafaruku mkubwa katika mazungumzo, bado halijapatiwa ufumbuzi

Soma - https://jamii.app/JointGovKiirMachar
RAIS MAGUFULI KUFANYA UFUNGUZI WA JENGO LA MAHAKAMA WILAYA YA CHATO

> Rais John Magufuli leo anatarajiwa kufungua jengo la Mahakama ya Wilaya ya Chato, Mkoani Geita na pia kuweka Jiwe la Msingi kwa ajili ya Jengo la Zimamoto na Msikiti wa Wilaya ya Chato
SERIKALI YAUTAKA UONGOZI WA UDSM KUWACHUKULIA HATUA VIONGOZI WA WANAFUNZI

> Ni viongozi wa Serikali ya Wanafunzi Chuo cha Dar, walioipa Serikali saa 72 kulipa mikopo ya wanafunzi vinginevyo wataandamana

> Waziri wa Elimu asema tamko lilitolewa kinyume cha utaratibu wa kutoa malalamiko na ni utovu wa nidhamu wa kiwango cha juu

Soma - https://jamii.app/DARUSOKuadhibiwaSerikali
UCHUNGUZI DHIDI YA TRUMP: ALALAMIKA KUNYIMWA HAKI YA KUWASILISHA USHAHIDI

> Rais Donald Trump ameandika barua kwa Spika Nancy Pelosi, akimtuhumu kutangaza vita ya wazi dhidi ya Demokrasia ya Marekani

> Trump anakabiliwa na kura ya uchunguzi itakayopigwa leo

Soma - https://jamii.app/TrumpSlamsIllegalCoup
UTAFITI: WANAWAKE WEUSI HATARINI KUPATA SARATANI YA MATITI KUTOKANA NA DAWA ZA NYWELE

> Wanawake wanaotumia bidhaa hizo maarufu kama 'Relaxer' huongeza nafasi zao za kupata Saratani ya Matiti kwa hadi 60%

> Kulingana na utafiti huo, kuna tofauti za hatari kulingana na rangi ya muhusika ambapo wanawake weusi wanakabiliwa na hatari kubwa (45%) kupata Saratani

Soma - https://jamii.app/RelaxersBreastCancer
MADAI YA MIKOPO: RAIS WA WANAFUNZI UDSM ASIMAMISHWA MASOMO KWA MUDA USIOJULIKANA

> Aliyesimamishwa ni Rais wa Serikali ya Wanafunzi (DARUSO), Hamis Musa Hamis

> Waziri wa Elimu alikipa Chuo hicho saa 24 kuwachukulia hatua wanafunzi waliotoa tamko kinyume cha utaratibu
Baadhi ya maneno ya Rais Magufuli wakati akizindua Jengo la Ofisi ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Jengo la Mahakama ya Wilaya, Wilayani Chato katika Mkoa wa Geita