JamiiForums
52.8K subscribers
34.4K photos
2.44K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Radi imewajeruhi wanafunzi 39 wa Darasa la Nne katika Shule ya Msingi Ihumilo iliyopo Wilayani Geita, wakati wakiwa Darasani

> Mkuu wa Mkoa wa Geita, Robert Gabriel amethibitisha kutokea kwa tukio hilo

Soma > https://jamii.app/WanafunziWajeruhiwaNaRadi
CHALAMILA ATAKA KUWACHAPA VIBOKO WASIOOA AU KUOLEWA

- RC wa Mbeya, Albert Chalamila amesema atakuja na mpango wa kuwacharaza bakora Wanawake na Wanaume mkoani kwake ambao hawajaoa au kuolewa na kisha wakatafute wapenzi wa kufunga nao ndoa

Zaidi, soma https://jamii.app/BakoraWasiooaWasioolewa-MBY
AFGHANISTAN: MLIPUKO WATOKEA MSIKITINI. TAKRIBANI WATU 31 WAUAWA

- Wengine 55 wamejeruhiwa leo, ikiwa ni siku moja baada ya Umoja wa Mataifa kusema vurugu nchini humo zimefikia kiwango kisichokubalika

Zaidi, soma https://jamii.app/31KilledAfghanistan
ALI MUFURUKI AJIUZULU UENYEKITI BODI YA WAKURUGENZI VODACOM

> Ametangaza kujiuzulu wadhifa huo kuanzia Desemba 1, 2019 na pia ametangaza kujiuzulu nafasi za Mkurugenzi huru na kamati ya uteuzi wa kampuni hiyo

> Imeelezwa kuwa amechukua uamuzi huo ili kupata muda zaidi wa kuendelea na biashara zake

Soma https://jamii.app/MufurukiResignsVoda
UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA: DAR YAVUKA LENGO UANDIKISHAJI WAPIGA KURA

Mikoa iliyoongoza ni Dar 108%, Pwani 96%, Mwanza 95%, Tanga 90% na Singida 90%

Jumla ya wapiga kura 19,681,259 wamejiandikisha nchi nzima ikiwa ni 86% ya lengo (22,916,412)

Soma https://jamii.app/UandikishajiSrklMitaa
CHAN: TAIFA STARS YAPINDUA MEZA SUDAN

> Taifa Stars imefuzu kucheza michuano ya CHAN 2020 nchini Cameroon baada ya kushinda 2-1 dhidi ya Sudan na kufuzu kwa faida ya goli la ugenini

> Magoli ya Tanzania kwenye mchezo wa leo yamefungwa na Nyoni 49’ na Nchimbi 78’
ANAYEDAIWA KUMBAKA ALIYEKUWA AKIMUUGUZA MAMAYE, ASIMAMISHWA KAZI

- Leseni ya Uuguzi ya Damian Mgaya (41), aliyemchoma sindano ya usingizi na kisha kumbaka kwa saa nne msichana mwenye umri wa miaka 16, imesimamishwa kwa miezi mitatu

Zaidi, soma https://jamii.app/MuuguziAbakaAsimamishwaKazi
RUVUMA: KAKA AKAMATWA KWA TUHUMA ZA KUMUUA MDOGO WAKE

> Mohamed Luambano(70) anashikiliwa kwa tuhuma za kumuua kwa kumkata na kitu chenye ncha kali kichwani na kiganjani Abeid Luambano(65)

> Ni kutokana na madai kwamba siku za hivi karibuni kumekuwapo na kutoelewana kati ya ndugu hao

Soma - https://jamii.app/KakaMauajiNdugu
WAZIRI MKUU: VIWANDA 4,000 VIMEJENGWA NDANI YA AWAMU YA 5

> Amesema tangu Serikali ya Awamu ya 5 iingie madarakani, viwanda vipya zaidi ya 4,000 vimejengwa na kufanya sekta hiyo kuchangia Pato la Taifa kwa 8.05% na kutoa ajira 306,180 mwaka 2018

> Aidha, Sekta ilichangia 18.1% ya mauzo yote ya nje, ikilinganishwa na 15% mwaka 2017

Soma - https://jamii.app/UjenziViwandaAwamu5
WAZIRI MAHIGA: KOMPYUTA ZILIZOIBWA SI ZA OFISI YA DPP

> Waziri wa Katiba na Sheria, Balozi Augustine Mahiga amesema Kompyuta zilizoibwa ni za Ofisi ya Mashtaka ya Mkoa wa Dar na sio Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) nchini Tanzania, Biswalo Mganga
RUKWA: MUME AHUKUMIWA KWENDA JELA KWA UBAKAJI, MKE AJINYONGA KWA UCHUNGU

> Shija Lutoja(23) amejinyonga huku akiacha ujumbe kuwa amefikia uamuzi huo kutokana na uchungu mkubwa alioupata baada ya mumewe kuhukumiwa kifungo cha miaka 30 kwa kosa la ubakaji

> Sababu nyingine ya kujinyonga ni baada ya kupimwa na kubainika kuwa na maambukizi ya VVU

Soma - https://jamii.app/MeUbakajiKeAjinyonga
MUSEVENI: BOBI WINE NI ADUI WA MAENDELEO UGANDA

- Rais wa Uganda, Yoweri Museveni amesema anamshughulikia Robert Kyagulanyi (Bobi Wine) kama adui

- Amemlaumu Bobi Wine akisema alikwenda Marekani na kuwaambia watu wasiende kuwekeza Uganda

Zaidi, soma https://jamii.app/Museveni-BobiWineAduiUG
MWANZA: MAFURIKO YACHIMBUA MAKABURI

- Mafuriko yaliyotokana na mvua kubwa iliyonyesha kwa zaidi ya saa moja jana, yamefukua zaidi ya makaburi 20 ya Waislam eneo la Mswahili katika Kata ya Mkuyuni

Zaidi, soma https://jamii.app/MafurikoYachimbuaMakaburi-MWZ
LIGI KUU ENGLAND: EVERTON YAPATA USHINDI WA 3 KATIKA LIGI

- Klabu ya Everton imefanikiwa kupata ushindi wa goli 2-0 dhidi ya Klabu ya West Ham katika mchezo wa Ligi Kuu, mzunguko wa 9

- Michezo mingine inayofuata kwenye Ligi hiyo siku ya leo ni kama ionekanavyo kwenye picha
WHO: MAAMBUKIZI YA EBOLA DRC YAPUNGUA, HALI BADO SIO SALAMA

> Takwimu zinaonesha idadi ya wagonjwa sasa ni 3,228 na kati ya hao 3,114 wamethibitishwa kuugua na 114 wanashukiwa kuwa na maambukizi

> Changamoto kubwa ni ukosefu wa fedha, kwani kati ya dola zaidi ya milioni 66.6 zinazohitajika kukabiliana na ugonjwa huo, ni dola milioni 4.5 zilizoahidiwa

Soma - https://jamii.app/WHOMaambukiziEbola
IKULU: RAIS MAGUFULI AFANYA TEUZI MBALIMBALI

- Miongoni mwao, Mathias Kabunduguru ameteuliwa kuwa Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania

- Pia, amemteua Hashim Abdallah Komba kuwa Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea akichukua nafasi ya Rukia Muwango

Zaidi, soma https://jamii.app/MagufuliTeuziMbalimbali
VIONGOZI 99 WA AMCOS MBARONI KWA KUWADHULUMU WAKULIMA

- Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) inawashikilia viongozi 99 wa Vyama 31 vya Msingi vya Ushirika (AMCOS) wanaodaiwa kuwadhulumu Wakulima wa ufuta Tsh. Bilioni 1.2

Zaidi, soma https://jamii.app/Viongozi99AMCOSMbaroni
LIGI KUU ENGLAND: CHELSEA YASHINDA, TOTTENHAM YABANWA

- Michezo kadhaa za Ligi Kuu za mzunguko wa 9 zimemaliza huku klabu ya Tottenham ikiwa nyumbani ikitoka sare ya goli 1-1 na klabu ya Watford

- Klabu ya Chelsea ikiwa nyumbani imepata ushindi mwembamba wa goli 1-0 dhidi ya Newcastle United huku Leicester City nayo ikipata ushindi wa goli 2-1 dhidi ya Burnley
UINGEREZA: WABUNGE WAPIGA KURA KUCHELEWESHA MPANGO WA BREXIT

> Wabunge wamepiga kura 322 dhidi ya 306 za kuchelewesha mpango wa Waziri Mkuu, Boris Johnson wa kujiondoa Umoja wa Ulaya

> Wametaka muda zaidi kusoma na kuyaelewa vizuri yaliyomo ndani ya mpango huo kabla ya tarehe ya mwisho, Oktoba 31

Soma - https://jamii.app/UKMPsDelayBrexit
LEBANON: WANANCHI WAANDAMANA KUIPINGA SERIKALI

- Maelfu ya Waandamanaji wameingia katika mitaa ya Lebanon jana, ikiwa ni siku ya tatu ya maandamano ya kuipinga Serikali, wakiwalenga vingozi wao juu ya kuporomosha Uchumi

Zaidi, soma https://jamii.app/MaandamanoLebanon