JamiiForums
52.6K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
FIFAWWC: Timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya Wanawake ya USA imefanikiwa kutetea ubingwa wake kwenye mchuano ya Kombe la dunia kwa kuifunga Netherland goli 2-0

- Marekani inachukua Kombe hilo mara ya 4 sasa na kuwa timu iliyochukua Kombe hilo mara nyingi zaidi
IRAN KUVUNJA MKATABA WA NYUKLIA

- Imesema itaanza kuvunja mkataba huo na kupunguza uzingatiaji wake baada ya kila siku 60

- Itafanya hivyo iwapo mataifa yaliyosaini mkataba huo hayatachukua hatua za kuilinda dhidi ya vikwazo vya Trump

Soma https://jamii.app/IranKurutubishaUranium
INDIA: WATU 29 WAFARIKI NA ZAIDI YA 20 KUJERUHIWA KATIKA AJALI YA BASI

- Ajali hiyo imetokea leo asubuhi ambapo basi hilo limepinduka karibu na mji wa Agra, Kaskazini mwa India

- Inadaiwa dereva wa basi hilo la ghorofa moja alikuwa amesinzia

Soma https://jamii.app/BusCrashKills29-India
DKT. BASHIRU: JIMBO LA HAI SI NGOME YA CHADEMA

- Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally amesema hayo jana wakati akieleza sababu ya ziara yake Mkoani Kilimanjaro

- Amesema katika ziara yake ameanzia Hai kimkakati na mahesabu yametumika kuamua

Soma https://jamii.app/BashiruJimboMbowe
MCHEZAJI WA AJAX, MATTHIJS DE LIGT KUJIUNGA NA JUVENTUS

- Meneja wake, Mino Raiola amethibitisha kuwa beki huyo raia wa Uholanzi amefikia makubaliano binafsi na klabu ya Juventus

- Inaaminika kuwa De Ligt amekubali malipo ya Paundi 230,000(Tsh. 661,958,247) kwa wiki
SINGIDA: WATU 7 WAKIWEMO WAFANYAKAZI 5 WA AZAM TV WAFARIKI AJALINI

- Wafanyakazi wengine watatu wamejeruhiwa katika ajali hiyo iliyotokea wakati wakielekea Chato mkoani Geita

- Ni baada ya gari walilokuwa wakisafiria kugongana na Lori

Zaidi, soma https://jamii.app/WafanyakaziAzamWafarikiAjalini
SHAMIMU NA MUMEWE WARUDISHWA RUMANDE, MAHAKAMA BADO INASUBIRI RIPOTI YA MKEMIA MKUU

- Jamhuri imesema inasubiri majibu ya ripoti hiyo ili iwasilishe kama kielelezo Mahakamani hapo

- Kesi imeahirishwa hadi Julai 22, 2019 kwa ajili ya kutajwa

Zaidi, soma https://jamii.app/ShamimuMumeweWasotaRumande
LIGI KUU BARA 2019/20 KUANZA AGOSTI 23. SIMBA NA YANGA KUKUTANA JANUARI 04, 2020

- Pazia la ligi hiyo litafunguliwa kwa mchezo mmoja kati ya Simba SC na JKT Tanzania

- Bodi ya Ligi nchini imesema Msimu huu imezingatia ratiba za Kimataifa

Zaidi, soma https://jamii.app/LigiKuuBara2019-20
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Kocha wa Timu ya Taifa “Taifa Stars”, Emmanuel Amunike wafikia makubaliano ya pamoja kusitisha mkataba baina yao

> TFF imesema itatangaza Kocha wa muda atakayekiongoza Kikosi cha Timu ya Taifa kwa mechi za CHAN
THE HAGUE: ALIYEKUWA KIONGOZI WA WAASI CONGO, BOSCO NTAGANDA ATIWA HATIANI

- Ni kwa uhalifu dhidi ya ubinadamu na uhalifu wa kivita wa mwaka 2002 na 2003 katika eneo la Ituri

- Ntaganda(45) maarufu ''Terminator'' anakabiliwa na kifungo cha maisha

Ziadi, soma https://jamii.app/BoscoNtagandaAtiwaHatianiICC
MAHUSIANO: Mtoa mada ndani ya JamiiForums anawashauri Wanaume kwamba “unapotaka kuoa hakikisha unaoa Mwanamke ambaye unamzidi Elimu, Kipato na Mali kwa wakati huo”

- Anasema kuwa kuoa Mwanamke aliyekuzidi vitu hivyo utateseka kwenye ndoa na maisha yako yatakuwa mafupi kwani utakufa kwa msongo wa mawazo

Je, una maoni gani kuhusu suala hili?

Kutoa maoni, Tembelea > https://jamii.app/MwanamkeVsKipato
FAMILIA YA ALLAN KILUVYA, ANAYEDAIWA KUTEKWA YAJITOKEZA KUOMBA MSAADA

- Imeomba msaada kwa Rais Magufuli, Serikali na Watanzania kusaidia kumpata ndugu yao

- Imedai gari lililomteka ni Land Cruiser lenye namba T 810 BQS, rangi ya kijivu

Zaidi, soma https://jamii.app/FamiliaAllanYaombaMsaadaKumtafuta
AFCON2019: Timu ya Taifa ya Ivory Coast imefanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya timu ya Taifa ya Mali katika mchezo wa hatua ya mtoano

- Ivory Coast imefuzu kucheza hatua ya robo fainali ya michuano na sasa itapambana na Algeria iliyoitoa Guinea
MFUMUKO WA BEI WAONGEZEKA KWA ASILIMIA 0.2 NDANI YA MWEZI

- Umeongezeka hadi asilimia 3.7 kwa mwezi Juni kutoka asilimia 3.5 kwa mwezi Mei, 2019

- Hali hiyo inamaanisha kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwezi Juni imeongezeka

Zaidi, soma https://jamii.app/MfumukoBeiWaongezeka-Juni2019
HANDENI, TANGA: MBARONI KWA KUMCHINJA MKEWE

- Juma Hemedi(45) mkazi wa Kwamaraho, anashikiliwa na polisi kwa kumuua mkewe Amina Hussein(38)

- Kamanda Bukombe amethibitisha kutokea kwa mauaji hayo na amesema polisi inaendelea na uchunguzi

Soma https://jamii.app/AmchinjaMkewe
MIILI YA WAFANYAKAZI WATANO WA AZAM MEDIA GROUP YAAGWA

- Miili ya Wafanyakazi hao waliofariki jana inaagwa leo katika ofisi za Azam Media zilizopo Tabata jijini Dar

- Viongozi kadhaa wamehudhuria akiwemo Waziri wa Habari, Harrison Mwakyembe

Zaidi, soma https://jamii.app/WafanyakaziAzamWaagwa
Amesema hayo wakati wa Uzinduzi wa Hifadhi ya Burigi-Chato unaofanyika Wilayani Chato Mkoani Geita ambapo Rais Magufuli ni mgeni rasmi
KATIBU MKUU CCM AMUONYA WAZIRI WA VIWANDA

- Dkt. Bashiru Ally amesema Waziri Innocent Bashungwa atatumbuliwa ikiwa atashindwa kutizima azma ya Serikali ya kufufua viwanda

- Amehoji “Barabara zinajengwa unaziona, SGR unaiona, kwa nini hatuoni viwanda vinafufuliwa?”

Zaidi, soma https://jamii.app/BashiruAmuonyaWaziriViwanda
IRAN: TUTAJIBU HATUA YA UINGEREZA KUKAMATA MELI YETU

- Imesema Uingereza kukamata meli yao ya mafuta iitwayo Grace 1, nje ya eneo la Gibraltar hakutapita bila majibu

- Ilikamatwa Alhamisi ikishutumiwa kuvunja vikwazo kwa kupeleka mafuta Syria

Zaidi, soma https://jamii.app/IranKisasiUK
RAIS MAGUFULI AZINDUA HIFADHI YA BURIGI-CHATO, AMPONGEZA FARU RAJABU

- Amempongeza Faru huyo kwa kuzalisha Watoto 40 na hivyo kuongeza idadi ya Faru

- Aidha, amesema “Nadhani wajina wangu John(baba wa Faru Rajabu) alikuwa hajitumi vizuri”

Zaidi, soma https://jamii.app/MagufuliAmpongezaFaruRajabu