JamiiForums
52.4K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
RAIA WA KIGENI MBARONI KWA KUSAFIRISHA DHAHABU BILA KIBALI

> Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia raia wawili wa Uingereza na mmoja wa Ireland kwa kosa la kusafirisha dhahabu gramu 1,044.95 bila kuwa na kibali kutoka Wilaya ya Chunya kuelekea Jijini Dar es salaam

Soma - https://jamii.app/UsafiriDhahabuWageni
MAREKANI: WANASAYANSI WAFANIKIWA KUONDOA VVU KWA PANYA

> Watafiti nchini Marekani wamesema wamefanikiwa kuondoa Virusi Vya Ukimwi kutoka kwenye vinasaba (DNA) vya panya 9 kati ya 23

> Kutokana na mafanikio hayo endapo mamlaka za chakula na dawa zitathibitisha tiba hiyo kwa binadamu inaweza kuanza kutumika mapema mwaka ujao

Soma - https://jamii.app/TibaVVUPanya
MICHEZO: Timu ya Taifa ya #Nigeria yafanikiwa kusonga mbele katika hatua ya robo fainali baada ya kuinyuka timu ya Taifa ya #Cameroon kwa mabao 3 kwa 2

#AFCON2019 #JFLeo
Mchezo wa #AFCON2019 kati ya #Misri na #SouthAfrika maarufu kama #Bafanabafana umekwenda mapumziko kwa timu hizo kutoka suluhu ya bao 0 kwa 0

> Je, unaweza kubashiri timu gani itaibuka na ushindi katika kipindi cha pili?
#AFCON2019: Timu ya Taifa ya #SouthAfrica maarufu ‘#Bafanabafana’ imefanikiwa kuingia hatua ya robo fainali baada ya kuifunga timu ya Taifa ya #Egypt goli 1-0

- Katika hatua ya robo fainali, South Africa itakutana na #Nigeria iliyofanikiwa kuitoa #Cameroon

#JFLeo #EGYRSA
#CopaAmerica2019: #Argentina imeibuka mshindi wa tatu katika michuano hiyo baada ya kuifunga #Chile goli 2-1

> Katika mchezo huo, Lionel Messi wa Argentina na Gary Medel wa Chile walipewa kadi nyekundu

> Mchezo wa Fainali utafanyika kesho kati ya #Brazil na #Peru mida ya saa 5 za usiku kwa saa za Afrika Mashariki
MSAIDIZI WA MEMBE, ALLAN KILUVYA ANADAIWA KUTEKWA NA WATU ‘WASIOJULIKANA’

> Taarifa kwa kina zinafuata...
MSUMBIJI: IS IMEKIRI KUHUSIKA KWENYE SHAMBULIO LILILOUA WATU 7

- Shambulio hilo lilitokea siku ya Jumatano kwenye kijiji cha Lidjungo huko Nangade

- Hii ni mara ya pili kwa kikundi hicho kukiri kuhusika kwenye mashambulio Nchini humo

Soma https://jamii.app/ISAttackInMoz
#JFLeo
RAIS MAGUFULI AMZAWADIA TAUSI RAIS KENYATTA

- Amemzawadia Tausi wanne kama kumbukumbu ya Uhusiano, Urafiki na Ujirani mwema baina ya Nchi hizo mbili

- Rais Kenyatta alifika wilayani Chato Julai 5, kwaajili ya ziara binafsi ya siku 2

Soma https://jamii.app/KenyattaApewaTausi
#JFLeo
WAZIRI LUGOLA ARUHUSU MABASI YA ABIRIA KUSAFIRI SAA 24

- Amewataka makamanda wa Polisi kutozuia mabasi kwa kisingizio cha kuhofia majambazi

- Amesisitiza mabasi yanayotoka Kanda ya Ziwa kutozuiwa Morogoro na yanayotoka Dar kutozuiwa Shinyanga

Soma https://jamii.app/MabasiKusafiriSaa24
#JFLeo
Mchezo wa #AFCON2019 kati ya #Madagascar na #DR Congo umekwenda mapumziko kwa timu hizo kutoka suluhu ya bao 1 kwa 1

> Je, unaweza kubashiri timu gani itaibuka na ushindi katika kipindi cha pili?
FIFAWWC: Timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya Wanawake ya USA imefanikiwa kutetea ubingwa wake kwenye mchuano ya Kombe la dunia kwa kuifunga Netherland goli 2-0

- Marekani inachukua Kombe hilo mara ya 4 sasa na kuwa timu iliyochukua Kombe hilo mara nyingi zaidi
IRAN KUVUNJA MKATABA WA NYUKLIA

- Imesema itaanza kuvunja mkataba huo na kupunguza uzingatiaji wake baada ya kila siku 60

- Itafanya hivyo iwapo mataifa yaliyosaini mkataba huo hayatachukua hatua za kuilinda dhidi ya vikwazo vya Trump

Soma https://jamii.app/IranKurutubishaUranium
INDIA: WATU 29 WAFARIKI NA ZAIDI YA 20 KUJERUHIWA KATIKA AJALI YA BASI

- Ajali hiyo imetokea leo asubuhi ambapo basi hilo limepinduka karibu na mji wa Agra, Kaskazini mwa India

- Inadaiwa dereva wa basi hilo la ghorofa moja alikuwa amesinzia

Soma https://jamii.app/BusCrashKills29-India
DKT. BASHIRU: JIMBO LA HAI SI NGOME YA CHADEMA

- Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally amesema hayo jana wakati akieleza sababu ya ziara yake Mkoani Kilimanjaro

- Amesema katika ziara yake ameanzia Hai kimkakati na mahesabu yametumika kuamua

Soma https://jamii.app/BashiruJimboMbowe
MCHEZAJI WA AJAX, MATTHIJS DE LIGT KUJIUNGA NA JUVENTUS

- Meneja wake, Mino Raiola amethibitisha kuwa beki huyo raia wa Uholanzi amefikia makubaliano binafsi na klabu ya Juventus

- Inaaminika kuwa De Ligt amekubali malipo ya Paundi 230,000(Tsh. 661,958,247) kwa wiki