JamiiForums
52.7K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
LIBYA: KAMBI YA WAHAMIAJI YASHAMBULIWA, ZAIDI YA 40 WAFARIKI

> Wahamiaji zaidi ya 40 wameuawa katika shambulio la angani dhidi ya kambi yao katika moja ya vitongoji vya mji wa Tripoli na watu wengine 70 wamejeruhiwa katika shambulio hilo

> Inaripotiwa idadi ya waliofariki inaweza kuongezeka kutokana watu wengi kufunikwa na kifusi

Soma - https://jamii.app/MigrantsCampAttack
#JFLeo
MARA: MWAMUZI AFARIKI UWANJANI MECHI IKIENDELEA

> Gugumiya Werema(30) amepoteza maisha ghafla wakati akichezesha mpira kati ya Nyakitono FC na Nyanungu FC Wilaya ya Serengeti

> Tukio hilo lilitokea jana muda mfupi baada ya mwamuzi huyo kupokea simu na ghafla kuishiwa nguvu na kuanguka

#JFMichezo
MITANDAO YA WHATSAPP, INSTAGRAM NA FACEBOOK YASUMBUA BAADHI YA MAENEO

> Watumiaji wa mitandao hiyo duniani wametoa malalamiko hasa kupitia mtandao wa Twitter kuhusu kupata shida katika kutuma ujumbe wa maandishi, kutuma na kupokea picha

> Hali inaonekana kuwa mbaya zaidi katika maeneo ya Ulaya, Brazil na Kaskazini mwa Marekani

Soma - https://jamii.app/WhatsupFBIGDown
#JFLeo
NIGERIA: LORI LA MAFUTA LALIPUKA, WATU 35 WAPOTEZA MAISHA

> Watu 35 wamefariki na wengine 101 kujeruhiwa baada ya lori ya mafuta ya Petroli kulipuka katika kijiji cha Ahumbe

> Janga hilo lilitokea jana baada ya lori hilo kupoteza uelekeo na kuanguka na kisha kugongwa na basi aina ya Toyota na kusababisha milipuko 2

Soma - https://jamii.app/AjaliMlipukoLori
RAIS KENYATTA KUFANYA ZIARA YA SIKU 2 NCHINI, ATAWASILI CHATO IJUMAA HII

> Rais wa Kenya anatarajiwa kufanya ziara binafsi nchini kwa mwaliko wa Rais Magufuli

> Atawasili katika Uwanja wa Ndege wa Chato Mkoani Geita Ijumaa wiki hii

Zaidi, soma => https://jamii.app/KenyattaChato
UNASHAURIWA KUZINGATIA HAYA KATIKA KUCHAJI SIMU ILI KUTUNZA UBORA WA BETRI

> Usiache simu yako iishe chaji hadi 0% ndipo uichaji. Weka utaratibu wa kuchaji simu yako ikiwa kati ya asilimia 5 – 50%

> Kuacha simu yako kwenye umeme muda mrefu hasa pale ambapo imeshajaa huharibu ubora wa betri la simu yako hasa kuacha simu ikichaji usiku kucha

> Kama umenunua simu kwa bei ya juu, ni bora pia uhakikishe unatumia chaja zenye kiwango cha juu cha ubora

Soma - https://jamii.app/ChajiSimuBetri
#JFTeknolojia
KENYA: MTANZANIA AHUKUMIWA JELA MAISHA KWA KUHUSIKA NA UGAIDI

> Mahakama ya Kenya imemhukumu Rashid Mberesero na wenzake 2 baada ya kuwakuta na hatia ya kutekeleza shambulio la kigaidi mwaka 2015 katika Chuo Kikuu cha Garissa, Kenya na kusababisha vifo vya wanafunzi 148

> Walitekeleza shambulio hilo wakishirikiana na kundi la Al Shabaab

Soma - https://jamii.app/MtzJelaUgaidiGarisa
BEIJING, CHINA: UWANJA MKUBWA ZAIDI WA NDEGE KUFUNGULIWA

> Uwanja huo wenye mita za mraba milioni 1.4 unatarajiwa kuwa na uwezo wa kuhudumia wasafiri milioni 45 kwa mwaka ifikapo mwaka 2021 na kuhudumia watu milioni 75 ifikapo 2025

Zaidi, soma > https://jamii.app/BeijingDaxing
UN: SHAMBULIO LA WAHAMIAJI LIBYA LAWEZA KUWA NI UHALIFU WA KIVITA

> Afisa wa Umoja wa Mataifa amesema, shambulio lililofanywa dhidi ya kituo cha wahamiaji na kuua zaidi ya watu 44 linaweza kuwa ni uhalifu wa kivita

> Wengi wa waliouawa wanaaminiwa kuwa ni watu wa asili ya Kiafrika kutoka eneo la jangwa la Sahara ambao wamekuwa wakijaribu kuingia Ulaya kupitia Libya

Soma - https://jamii.app/UhalifuKivitaLibya
#JFLeo
TAKWIMU KIWANGO CHA UMASIKINI: MKOA WA RUKWA WAONGOZA

> Ofisi ya Taifa ya Takwimu imesema mikoa inayoongoza kwa wananchi wake kuwa masikini Tanzania bara kwa mwaka 2017/2018 ni mkoa wa Rukwa kwa 45%, Simiyu 39.2%, Geita 37.5%, Lindi 36% na Kigoma 34.5%

> Umasikini wa mahitaji ya msingi umepungua kutoka 28.2% mwaka 2011/12 hadi 26.4% mwaka 2017/18

Soma - https://jamii.app/HaliUmasikiniTz
#JFLeo
ENGLAND: FRANK LAMPARD KOCHA MPYA WA CHELSEA FC

> Frank Lampard ambaye ni miongoni mwa Wachezaji waliowahi kuichezea Klabu hiyo kwa mafanikio makubwa ametangazwa rasmi kuwa kocha mpya baada ya tetesi za muda mrefu

Zaidi, soma => https://jamii.app/Lampard-ChelseaFC

#JFLeo #JFSports
VIONGOZI 3 WATUHUMIWA KUTAFUNA FEDHA ZA MAUZO YA DHAHABU

> M/kiti, Katibu na Meneja wa kikundi cha wachimbaji dhahabu cha Winima Group kilichopo katika mgodi wa Kitunda Wilayani Sikonge wako hatiani kukamatwa kwa tuhuma za kutafuna Tsh milioni 342 za mauzo ya kilo 1.549 za dhahabu

> Walikwenda kufanya mauzo ya dhahabu ikiwa ni mali ya wanakikundi lakini hawakukabidhi fedha za mauzo

Soma - https://jamii.app/HujumaMauzoDhahabu
KISUTU, DAR: WEMA SEPETU AACHIWA NA KUKAMATWA TENA

> Msanii huyo wa filamu amezua kizaazaa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu alipokuwa akigoma kukamatwa tena na Askari wa Jeshi la Polisi

> Wema aliachiwa huru baada ya shahidi wa Jamhuri kutofika Mahakamani

Soma > https://jamii.app/WemaAkamtwaTena
KAMPUNI YA ACACIA YATAKA MAZUNGUMZO NA SERIKALI YA TANZANIA

> Acacia inatafuta suluhu ya mgogoro wa kodi uliopo baina yake na Tanzania

> Tanzania ilizuia shehena ya Makinikia hadi hapo Acacia itakapolipa deni la kodi la kiasi cha TSh. Trilioni 436

Soma > https://jamii.app/Acacia-Tanzania
NIGERIA: MWANAUME AFARIKI BAADA YA KUFANYA MAPENZI KWA MIZUNGUKO 7

> Mwanaume huyo aliyefahamika kwa jina moja tu la Davy amefariki wakati akiwa kwenye mashindano ya kufanya mapenzi na Mwanamke aitwaye Loveth

> Inaelezwa kuwa Davy aliimudu vyema mizunguko ya awali kabla ya kuzidiwa na kufariki akiwa kwenye mzunguko wa 7

Kusoma kisa hiki, fungus => https://jamii.app/AfarikiAkifanyaMapenzi
MUME AWACHOMA MOTO KWA PETROLI MAMA NA MTOTO

> Mkazi wa kijiji cha Mlazo, Wilaya ya Chamwino, Mkami Mbarahi(19) na mwanaye wenye umri wa miezi mitatu wamelazwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma baada ya kujeruhiwa kwa moto na mumewe, kwenye maeneo mbalimbali ya mwili

> Tukio hilo lilitokea Juni 28 baada ya mume kumkuta mkewe akipika kwa kutumia kuni

Soma - https://jamii.app/MeAchomaKeMtoto
TANZIA: MAMA MKUU WA SHIRIKA LA KIFUNGILO PAMOJA NA DEREVA WAFARIKI KATIKA AJALI

> Waliofariki ni Sister Octavia pamoja na dereva wake Aminiel

> Ajali hiyo imetokea katika maeneo ya Wilaya ya Same, Kilimanjaro

Zaidi, soma => https://jamii.app/TanziaSisterKifungilo
FARU MWEUSI AFARIKI WAKATI AKISAFIRISHWA KUTOKA UINGEREZA KUJA TANZANIA

> Faru huyo alikuwa akisafirishwa kwa ushirikiano wa Grumeti na Serikali ya Tanzania kama sehemu ya mkakati wa kuongeza idadi ya Faru Weusi kwenye Hifadhi ya Serengeti

Soma > https://jamii.app/FaruUKTanzaia
HISTORIA: FAHAMU KUHUSU ASILI YA KABILA LA WAKURYA

> Wakurya ni kabila la watu wanaoishi katika Wilaya ya Rorya, Tarime na Serengeti Kaskazini mwa Tanzania, na katika Wilaya za Magharibi na Mashariki mwa Mkoa wa Nyanza katika sehemu ya Kenya

> Shuguli zao kubwa ni Kilimo na Ufugaji, huku Wakurya wa Kenya wakiegemea sana kwenye kilimo na Tanzania wakiegemea sana kwenye ufugaji

> Wakurya hawapendi kutawaliwa wala kuonewa hivyo walikuwa na saiga lika ya vijana kwa ajili ya ulinzi na usalama hivyo utumwa haukuwaathiri sana

Fahamu zaidi - https://jamii.app/HistoriaKabilaWakurya
#JFHistoria
CHATO: RAIS MAGUFULI KUZINDUA HIFADHI YA BURIGI JULAI 9, 2019

> Hifadhi ya Taifa ya Burigi iliyopo Chato, Geita itazindulia siku ya Jumanne baada ya kupandishwa hadhi hivi karibuni

> Hifadhi hii ilikuwa ikijulikana kama Pori la Akiba la Burigi.

Soma > https://jamii.app/HifadhiBurigi