JamiiForums
52.7K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
MBUNGE AOMBA MUONGOZO JUU YA MADAI YA TAIFA STARS KUKATWA POSHO

> Mbunge wa Mbozi, Paschal Haonga(CHADEMA) amedai kuna tetesi kwamba wachezaji hao walitakiwa kupewa posho ya Dola 300 kwa siku lakini Serikali imewapa Dola 70

> Inadaiwa kuna mgomo wa kimyakimya katika timu hiyo na kuna siku wachezaji waligoma kufanya mazoezi

Soma - https://jamii.app/PoshoStarsAFCON
#JFMichezo
UBUNGO: ABIRIA AFARIKI NDANI YA BASI KABLA YA SAFARI KUANZA
-
Mwanaidi Said (83), aliyekuwa anasafiri kutoka Dar Es Salaaam kwenda Tabora, alifariki jana alfajiri na alikuwa akisumbuliwa na saratani

> Alikuwa anakwenda mkoani Tabora baada ya kumaliza matibabu yake hapa Dar

Soma - https://jamii.app/AbiriaAfarikiBasi
SAUDI ARABIA: UWANJA WA NDEGE WASHAMBULIWA, MMOJA AFARIKI

> Waasi wa Houthi wa nchini Yemen wameushambulia uwanja wa ndege wa Abha ulioko Kusini Magharibi mwa Saudi Arabia leo, Juni 24 na kusababisha kifo cha mtu mmoja huku wengine saba wakijeruhiwa

> Hata hivyo, mpaka sasa Serikali haijatoa tamko kuhusiana na shambulio hilo

Soma - https://jamii.app/ShambulioUwanjaNdege
TANZANIA YAPATIWA TSH. BILIONI 60 ZA MSAADA NA CHINA

- Imepatiwa fedha hizo bila masharti yoyote na itaamua matumizi yake katika miradi ya maendeleo

- Baadhi ya maeneo ya kipaumbele ni ujenzi wa mabwawa ya umeme ya Ruhudji na Rumakali

Zaidi, soma https://jamii.app/ChinaTanzania-Bilioni60
NDUGAI: LISHE DUNI IMECHANGIA TAIFA STARS KUFUNGWA

> Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema miongoni mwa sababu iliyochangia timu ya Taifa kupoteza mchezo wa kwanza jana kwenye michuano ya AFCON dhidi ya Senegal ni lishe duni ya wachezaji wetu

> Amesema viongozi wengi wa soka na michezo mingine hapa nchini siyo watu sahihi wa kuongoza

Soma - https://jamii.app/NdugaiMpiraStars
#JFMichezo
AFCON2019: Timu ya Taifa ya Ivory Coast imefanikiwa kupata ushindi wa goli 1-0 dhidi ya timu ya Taifa ya South Afrika katika mchezo wa pili wa Kundi D

- Kwa matokeo hayo Ivory Coast inaongoza katika Kundi D lakini ikiwa na alama 3 sawa na Morocco iliyo nafasi ya pili
BAADHI YA MAMBO YANAYODAIWA KUWEPO KWENYE SAIKOLOJIA YA MAPENZI

> Ni ngumu kubaki na hasira kwa mtu unayempenda kwa dhati kwasababu hasira zinazoishi hadi kufikia siku tatu zinadhibitisha kuwa hakuna mapenzi ya dhati baina ya wapenzi hao

> Mapenzi huwa yanaacha kumbukumbu ambayo ni ngumu kwa mtu mwingine kuifuta, vilevile huacha maumivu ambayo ni ngumu kwa mwingine kuyatibu

Una maoni gani kuhusu madai haya?

Tembelea zaidi - https://jamii.app/SaikolojiaMapenzi
#JFMahusiano
IRAN: SHAMBULIO LA KIMTANDAO LA MAREKANI HALIKUFANIKIWA

- Imesema mashambulio hayo yaliyofanywa dhidi ya mifumo yake ya kufyetulia makombora hayakufanikiwa

- Imesema mwaka 2018 imezuia mashambulizi Milioni 33 kama hayo na kuyaita ni ugaidi

Zaidi, soma https://jamii.app/IranShambulioMtandao-US
AFCON2019: Timu ya Tunisia imetoka sare ya goli 1-1 na timu ya Angola katika mchezo wa kwanza wa Kundi E katika dimba la Suez nchini Misri

- Mchezo unaofuata majira ya saa 5:00 usiku, saa za Afrika Mashariki ni katika ya Mali na Mauritania ambazo zote zipo Kundi E
TRUMP AMUWEKEA KIONGOZI WA DINI WA IRAN VIKWAZO

- Ameiwekea Iran vikwazo vipya vikali ikiwemo Ofisi ya Kiongozi Mkuu wa dini, Ali Khamenei

- Iran imesema Marekani haipendi diplomasia na kuushutumu utawala wa Trump kwa kuwa na kiu ya vita

Zaidi, soma https://jamii.app/VikwazoKiongoziDini-Iran
TABORA: MKUU WA MKOA AMSIMAMISHA KAZI MENEJA WA TRA, IGUNGA

- Aggrey Mwanri amemsimamisha kazi, John Mgeni ili kupisha uchunguzi wa tuhuma za rushwa zinazomkabili

- Inadaiwa alidai Mfanyabiashara mmoja rushwa ya Tsh. Milioni 2

Zaidi, soma https://jamii.app/MenejaTRAIgunga
UGANDA YAPINGA MAHAKAMA YA EAC KUAMUA KUHUSU UKOMO WA MIAKA YA URAIS

> Serikali ya Uganda imesema Mahakama ya Afrika Mashariki iliyoko Arusha, haina mamlaka ya kusikiliza kesi kuhusu kipengele cha umri wa Rais

> Kesi hiyo ilipelekwa na wanaharakati wakitaka ibatilishe uamuzi wa Mahakama ya Katiba iliyokubaliana na Bunge kuondolewa kwa ukomo wa umri wa mtu kuwania urais mwezi Aprili 2019

Soma - https://jamii.app/UGVsEACCourt
#JFInternational
HARRY MAGUIRE AGOMBANIWA NA MANCHESTER UNITED NA MANCHESTER CITY

- Inadaiwa beki huyo wa Leicester City yupo tayari kujiunga na Man. City na 'kuitosa' Man. Utd

- Inadaiwa United ipo tayari kulipa ada ya Tsh. 234,597,076,000 lakini yeye anataka kujiunga na Man. City
IRINGA: WATUMISHI 2 WA TARURA MKOANI SONGWE WAFARIKI AJALINI

- Wengine 3 wamejeruhi katika ajali hiyo iliyotokea maeneo ya Izazi katika barabara kuu ya Iringa-Dodoma

- Gari lao limegongana na lori lililohama upande baada ya kumshinda dereva

Zaidi, soma https://jamii.app/AjaliTARURASongwe-IRN
RAIS MAGUFULI ASISITIZA MATUMIZI YA GESI KWA WANANCHI

> Ametoa wito hasa wananchi wa Dar ambao kwa siku wanatumia magunia 40 elfu ya mkaa sawa na asilimia 90 ya mkaa wote nchini kuanza kubadilika na kutumia gesi

> Hayo ameyasema leo wakati akizindua Ghala na Mitambo ya Gesi ya LPG ya Taifa Gas Tanzania Limited katika eneo la Vijibweni Kigamboni

Soma - https://jamii.app/RaisGesiVsMkaa
RAIS MAGUFULI AIKINGIA KIFUA TAIFA STARS

- Amesema kufungwa goli 2 na timu inayoongoza Afrika ambayo Wachezaji wake wote wanacheza nje si mwanzo mbaya

- Amemruhusu RC Makonda kwenda Misri na kuwaambia Stars wasikate tamaa na wajitume zaidi

Zaidi, soma https://jamii.app/MagufuliStarsMakonda
KENYA: WAFANYABIASHARA RAIA WA KIGENI WAPEWA SAA 24 KUONDOKA

> Wafanyabiashara kutoka mataifa mengine wanaofanya biashara katika jimbo la Starehe wamepewa saa 24 kuondoka la sivyo watapigwa

> Taharadhi hiyo imetolewa na Mbunge wa jimbo la Starehe, Charles Njagua maarufu kwa jina la kisanii Jaguar

Soma - https://jamii.app/FukuzoWageniKE
BALOZI WA KENYA, TANZANIA: MANENO YA MBUNGE WA KENYA SI MSIMAMO WA SERIKALI YA KENYA

- Amesema ule ni mtazamo wake na Serikali yake itachukua hatua

- Waziri Mkuu, Majaliwa amewataka Watanzania kuwa watulivu kwani Kenya na Tanzania ni marafiki

Zaidi, soma https://jamii.app/KenyaYamrukaJaguar
BUNGENI, DODOMA: Bunge la Tanzania limepitisha mapendekezo ya makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2019/2020 ya Tsh trilioni 33.1

> Wabunge waliopiga kura ni 380; 83 walisema hapana na 297 walipiga kura za ndio

Soma - https://jamii.app/PitishoBajetiSerikali
#JFLeo
NDUGAI: TUNA VIONGOZI WA SERIKALI WANAODIRIKI KUMDANGANYA RAIS HADHARANI

- Amesema “Kiongozi wa Serikali unapoongea mbele ya Rais, ongea ukweli Mwenyezi Mungu anaoujua“

- Akaongeza “Bahati mbaya kijana wetu huyu hajitambui, hajielewi”

Zaidi, soma https://jamii.app/NdugaiKijanaSerikaliHajitambui