JamiiForums
52.9K subscribers
34.3K photos
2.43K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
ISRAEL YAFANYA KIKAO CHA DHARURA BAADA YA SHAMBULIZI TEL AVIV

> Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu jana usiku aliitisha majadiliano ya dharura ya kijeshi na makamanda wa Jeshi baada ya shambulizi la maroketi dhidi ya Tel Aviv kutoka Gaza

> Habari mpya zinasema leo alfajiri ndege za kivita za Israel nazo zimefanya mashambulizi ya kujibu

Soma - https://jamii.app/TelAvivAttack
#JFInternational
POLISI AMUUA MKEWE KWA MADAI YA KUZAA NJE YA NDOA

> KENYA: Patrick Nyapara amemuua mkewe, Christine Maonga (28) kwa kumpiga risasi mara tatu kichwani kwa madai kuwa mkewe alipata ujazito nje ya ndoa na kumsingizia kuwa yeye ndiye baba wa mtoto huyo baada ya kujifungua

> Afisa huyo alitoweka baada ya kutenda kitendo hicho

Soma - https://jamii.app/MumeAuaMkeRisasi
#JFInternational
MSUMBIJI HATARINI KUKUMBWA NA KIMBUNGA HATARI

> Watu wanaoishi katika Mji mkuu wa Msumbiji, Maputo wameonywa juu ya kutokea kwa hali mbaya zaidi kutokana na Kimbunga kikali kitakachosababishwa na tufani iliyopewa jina la Idai

> Mpaka sasa Tufani hiyo imeshasababisha vifo vya watu 66 na safari nyingi za ndege zimesitishwa

Soma - https://jamii.app/HatariKimbungaMaputo
#JFInternational
WALAJI WA DONA BILA KUOSHA HATARINI KUPATA SARATANI YA INI

> Ni kutokana na kuwa ni kiasi kikubwa cha sumukuvu ambayo hupatikana kwenye mazao ya nafaka hasa mahindi na karanga, hivyo walaji wa ugali wa dona wapo hatarini zaidi ikiwa hatua za uandaaji wa chakula hicho hautazingatiwa

> Ni lazima mahindi yaoshwe kwa umakini na usahihi kwani wengi huyahifadhi kwa kutumia dawa

Soma - https://jamii.app/OshaDonaSaratani
#JFLeo
MICHEZO: DROO LIGI YA MABINGWA ULAYA

> Shirikisho la Soka Ulaya (UEFA) limetangaza timu zitakazochuana kwenye hatua ya robo fainali
UPDATE: Baada ya UEFA kutangaza michezo ya hatua ya robo fainali ya Klabu Bingwa Ulaya, hivi ndivyo safari ya kuchukua Ubingwa itakavyokuwa

Je, unadhani nani ataibuka kidedea?

#JFSports | #JFMichezo
MICHEZO: DROO YA ROBO FAINALI LIGI YA EUROPA
-
Shirikisho la Soka Ulaya (UEFA) limetangaza timu zitakazochuana kwenye hatua ya robo fainali katika Ligi ya EUROPA
MWILI WA MWANAFUNZI WAKUTWA KWENYE ENEO LA KICHAKA

> Mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari ya Yungwe Mkoani Geita, Alex Pastory amekutwa ameuawa kichakani na sababu za kifo bado hazijajulikana

> Alipotea tangu Machi 1

Soma - https://jamii.app/MwiliMwanafunziKichakani
#JFLeo
GARI LAGONGA TRENI NA KUSABABISHA KIFO CHA MTU MMOJA

> Mtu mmoja amefariki na wanafunzi 19 kati ya 30 wamejeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kwenda kucheza mpira kuligonga Treni eneo la Gofu jijini Tanga

> Kamanda wa Polisi Mkoani Tanga, SACP Edward Bukombe amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo

Soma - https://jamii.app/AjaliTreniGari
#JFLeo
INADAIWA MWANAMKE AKIFANYA HAYA NDOA YAKE HUVUNJIKA

> Ndani ya JamiiForums unaendelea mjadala unaotaja mambo ambayo mwanamke akifanya husababisha ndoa kuvunjika

> Mwanamke kuchelewa kuamka kabla ya mume, kushindwa kumuhudumia mumewe kimwili (tendo la ndoa) kwasababu za kutojisikia au kisingizio cha kuumwa

> Kutomsikiliza mume pindi anapozungumza na kuwaambia marafiki adhaifu wa mume wako

Maoni yako ni yapi?
Soma - https://jamii.app/KeNdoaKuvunjika
#JFMahusiano
JE, MAFANIKIO HULETWA NA BAHATI AU JUHUDI

> Hoja hii imechambuliwa na wanaJamiiForums katika dhana kuu tatu ambazo ni mafanikio ni zao la bahati, mafanikio hutokana na juhudi na dhana ya 3 ikiwa ni juhudi na bahati huleta mafanikio

Soma > https://jamii.app/DhanaZaMafanikio

#JFMaisha
JESHI LA POLISI LAKIRI KUMBAMBIKIA KESI MFANYABIASHARA TABORA

> Jeshi la Polisi nchini, limekiri kuwa taarifa za awali walizopata kutoka Mkoani Tabora zimeonesha kwamba askari wake walimbambikia kesi mfanyabiashara, Mussa Sadiki

> Alibambikiziwa kesi ya kuvunja na kuiba na alikaa kituoni kwa wiki 1 na alipopelekwa Mahakamani, alisomewa shtaka la mauaji

Soma - https://jamii.app/PolisiKubambikaKesi
#JFLeo
MWENDOKASI KUWEKEWA DALADALA ILI KUPUNGUZA ADHA YA USAFIRI

> Waziri wa Nchi ofisi ya Rais TAMISEMI, Selemani Jafo ameagiza kuongezwa kwa mabasi 10 ya kawaida ktk Usafiri wa Mwendokasi jijini Dar es Salaam ili kupunguza changamoto ya usafiri

Soma - https://jamii.app/DaladalaNjiaUDART
#JFLeo
RAIS MSTAAFU ANAWEZA KUFUNGULIWA MASHTAKA NA OFISI YA DPP

> Haya yameelezwa na Jaji Mkuu Mstaafu, Barnabas Samatta katika Mjadala wa Uwajibikaji uliandaliwa na Taasisi ya Wajibu Institute katika Chuo cha Sheria Tanzania(Law School of Tanzania) Jijini Dar es Salaam

> Jaji Samatta amefafanua kuwa Rais mstaafu ana kinga lakini ina mipaka. Kinga haihusu mambo aliyofanya akiwa Rais bali yale aliyofanya kama Rais

#JFLeo
MTUHUMIWA WA MAUAJI YA NEW ZEALAND AFIKISHWA MAHAKAMANI

> Mshukiwa wa shambulio lililotokea jana jijini Christchurch, na kuua watu 49, Brenton Terrant (28) tayari amefikishwa Mahakamani

> Wengine wawili bado wanahojiwa na Polisi

Soma - https://jamii.app/MosqueShootingSuspect
#JFInternational
WALEMAVU WA MIGUU KUPEWA VIUNGO VYA BANDIA BURE

> Walemavu wa viungo vya miguu 600 wanatarajiwa kufanyiwa uchunguzi na kupatiwa miguu bandia katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI)

> Uchunguzi kwa wagonjwa utafanyika mwezi Aprili na wale watakaotakiwa kutumia viungo hivyo watapewa mwezi Mei

Soma - https://jamii.app/MiguuBandiaBure
#JFLeo
WAZAZI NA JAMII WATAJWA KUWA CHACHU YA ONGEZEKO LA RUSHWA

> Watajwa kupokea fedha nyingi toka kwa watoto wao bila maelezo na kuwa kichocheo cha kuendelea kwa ulaji rushwa miongoni mwa watumishi wa umma

> Pia tabia ya kumuona kijana wao asiyetajirika haraka kama mjinga na asiyejituma imekuwa ikiwafanya watumishi kujikita katika vitendo vya rushwa

Soma - https://jamii.app/WazaziJamiiRushwa
PROF. LIPUMBA ATANGAZA MAKATIBU WAKUU WA CUF TAIFA

> Amemtangaza ndugu Khalifa Suleiman Khalifa kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho

> Pia amtangaza Magdalena Sakaya Naibu Katibu Mkuu kwa upande wa Tanzania Bara

Soma => https://jamii.app/MakatibuCUFTaifa

#JFLeo