JamiiForums
52.8K subscribers
34.4K photos
2.44K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
RAIS HUSSEIN MWINYI: Tunaanza Ziara rasmi ndani ya mwezi huu katika maeneo yote ambayo fedha za #UVIKO19 zimefika

Ningependa niwaambie wanaohusika wote wahakikishe wana maelezo mazuri. Na kazi hizo ziwe zina ubora unaoendana na fedha zilizotolewa

#KemeaRushwa #AfricaAgainstCorruption
👍4
Akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mapambano dhidi ya Rushwa Afrika, Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi amesema ipo haja ya kuongeza kasi na umahiri katika kupambana na Rushwa na Uhujumu Uchumi

Amesisitiza, jitihada za Taasisi za Kupambana na Rushwa pekee (TAKUKURU na ZAECA) haziwezi kuleta ushindi katika mapambano hayo, na Wadau wote wanapaswa kuhusika

#KemeaRushwa #AfricaAgainstCorruption
🔥1
DAR: MSTAAFU WA JESHI ATUHUMIWA KUUA KWA RISASI

Jonas Ziganyige (71) anatuhumiwa kusababisha kifo cha Patient Romwadi kwa kumpiga na risasi kutokana na mgogoro wa mipaka

> Baada ya tukio Mtuhumiwa alikimbia, amekamatwa akiwa Kibaha-Pwani

Soma https://jamii.app/TuhumaZaMauaji

#JFMatukio
👍4👏1
KIMARA, DAR: Polisi inamshikilia Selemani Haruna 'Kwata' (24) kwa mauaji ya Editha Charles (22) aliyekuwa akifanya Kazi za Ndani

> Mtuhumiwa alifika ktk nyumba anayofanya kazi Editha na kumshambulia na kitu chenye ncha kali, kisha kuiba Tsh. 1,800,000

Soma https://jamii.app/DarMauaji

#JFMatukio
😢14👍5👎1🔥1🤯1
ACP AHMED MAKARANI: Siku za karibuni kumekuwa na changamoto ya Waendesha Mashtaka kufanya kazi ya kupeleleza Washtakiwa wa Rushwa na Uhujumu Uchumi

> Asema hiyo ni kazi ya Wapelelezi yaani Polisi na Watu wa #DawaZaKulevya na si ya TAKUKURU

Soma https://jamii.app/KemeaRushwa

#KemeaRushwa
🤔6👍4
KAGERA: AJALI YAUA NANE, WATANO NI FAMILIA MOJA

Ni baada ya Lori kugongana na Toyota Succeed katika ya Barabara Lusahunga - Nyakahura, Wilayani Biharamulo leo Julai 12, 2022

> Ndugu wa Familia moja waliofariki ni Mama na Watoto wake wanne

Soma https://jamii.app/AjaliYauaNane

#JFMatukio
😢18👍2🤔2👎1
#SRILANKA: KAKA WA RAIS AZUIWA KUTOKA NJE YA NCHI

Basil Rajapaksa ambaye Mwezi Aprili ajiuzulu Uwaziri wa Fedha amezuiwa na Maafisa wa Uhamiaji kuondoka nje ya Sri Lanka

Familia ya Rajapaksa imeshikilia Siasa za Taifa hilo kwa muda mrefu, na wananchi wengi wanailaumu kwa matatizo yanayoikumba Nchi hiyo kwa sasa

Soma - https://jamii.app/BasilZuioSL

#Accountability
👍5
SERIKALI: WATOTO 3,333 WAREJESHWA SHULE

Watoto hao walishindwa kuendelea na masomo kwa sababu mbalimbali ikiwemo Ujauzito

> 900 kati yao wamerejea Mfumo wa Elimu wa Kawaida huku wengine wakijiunga na Mfumo wa Elimu Mbadala wanaosoma kwa miaka miwili

Soma https://jamii.app/WarejeaShuleni

#HakiMtoto #JFElimu
👍19👎5
SRI LANKA: RAIS GOTABAYA RAJAPAKSA AKIMBIA NCHI

Ikiwa ni saa chache kabla ya kutakiwa kujiuzulu rasmi, Rais Rajapaksa ameondoka kwa ndege ya kijeshi ikidaiwa ameshawasili Mji Mkuu wa Maldives, Male

Inaelezwa, Rais Rajapaksa alitaka kutoka #SriLanka kabla ya kujiuzulu ili asikamatwe

Soma - https://jamii.app/RaisAtokaSL

#Democracy
👍13
SIMIYU: Watu wanne wamepoteza maisha baada ya magari waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso eneo la Nyaumata-Bariadi Julai 12, 2022

> Kamanda wa Polisi-Simiyu amesema chanzo cha ajali ni mwendo kasi na Madereva wanashikiliwa na Polisi

Soma https://jamii.app/AjaliBariadi

#JFMatukio
😢9👍3👎1
KAIMOSI, KENYA: ATUHUMIWA KUMUUA BINAMU KATIKA UGOMVI WA KUCHAJI SIMU

Inadaiwa alimuua kwa kumchoma mshale kifuani wakati kila mmoja alipokuwa akitaka kuwa wa kwanza kuanza kuchaji simu

Mtuhumiwa alikimbia baada ya tukio na anatafutwa na Polisi

Soma > https://jamii.app/AmuuaBinamuKE

#JFMatukio
😢14👍11👎1
Fuatilia Mkutano na Waandishi wa Habari kuhusu Uzinduzi wa Awamu ya Pili ya Shindano la Stories Of Change Mwaka 2022 litakaloanza Julai 15

Bonyeza > https://fb.watch/eecsLXntHU/

#StoriesOfChange #SOC2022
👍5
AWAMU YA PILI YA SHINDANO LA "STORIES OF CHANGE" YAZINDULIWA

Shindano linakusudia kuongeza maudhui bora Mtandaoni na kuhamasisha ushiriki wa raia

Andiko linatakiwa kuchochea mabadiliko kwenye nyanja mbalimbali zikiwemo za Elimu, Uchumi, Kilimo, Utawala, Afya, Sayansi na Teknolojia

Kwa taarifa zaidi - https://jamii.app/Shindano2

#StoriesOfChange #SOC2022
👍11
STORIES OF CHANGE: Maandiko yawasilishwe kuanzia Julai 15 hadi Septemba 14, 2022 kwenye Jukwaa la “JF Stories Of Change"

Mtanzania yeyote mwenye umri wa miaka 18 na zaidi anaweza kushiriki

Maelezo zaidi > https://jamii.app/Shindano2

#StoriesOfChange #SOC2022
👍11
UPDATE: Waziri Mkuu wa Sri Lanka, Ranil Wickremesinghe ambaye anakaimu nafasi ya Urais kwa sasa baada ya Rais Gotabaya Rajapaksa kukimbia, ametangaza Hali ya Hatari

Inaripotiwa kuwa, Ofisi yake imezingirwa na mamia ya Waandamanaji

Soma - https://jamii.app/SOESriLanka

#Democracy
👍12🔥2
UGONJWA USIOFAHAMIKA LINDI: Wizara ya Afya imesema kufikia Julai 12, 2022 kulikuwa na Wagonjwa 13, na 3 kati yao wamefariki dunia

Sampuli za awali zimeonesha Majibu Hasi kwa Magonjwa ya Ebola, Marburg na UVIKO-19, vipimo zaidi vinasubiriwa

Wenye dalili za Homa, Kuvuja Damu puani, kuumwa kichwa na mwili kuchoka wanaendelea kutafutwa

Soma - https://jamii.app/UgonjwaLindiWA

#JFAfya
🤔9👍7
RWANDA: AFISA WA ZAMANI WA SERIKALI AHUKUMIWA MIAKA 20 JELA KWA MAUAJI YA HALAIKI

Laurent Bucyibaruta aliyekuwa Gavana wa Gikongoro Kusini amekutwa na hatia ya mauaji ya mwaka 1994, akidaiwa kutumia ushawishi wa nafasi yake kuhimiza maelfu ya Watutsi kukimbilia Shule ya Ufundi ya Murambi kwa hifadhi ambapo waliuawa

Soma - https://jamii.app/RwandaGenocide
👍8🤔1
MALI: Takriban Wanajeshi 50 wa Ivory Coast wanashikiliwa ikidaiwa ni Mamluki waliowasili Nchini humo kwa mgongo wa Umoja wa Mataifa (UN)

> UN imesema Wanajeshi hao waliingia Mali kwa kazi maalum ktk Mradi wa Sahelian Aviation Services

Soma https://jamii.app/WanajeshiWazuiwaMali

#Governance
👍6😁1
KENYA: Baraza la Habari limetoa wito kwa Polisi kuchunguza kwa haraka mashambulizi dhidi ya Wanahabari siku chache baada ya kushambuliwa kwa Mwanahabari Ian Byron

> Anadaiwa kushambuliwa kufuatia kuandika habari kumhusu Mbunge, Junet Mohamed

Soma https://jamii.app/PressFreedom

#PressFreedom
👍8
TERAT, ARUSHA: Watu watatu wa familia moja wamefariki Dunia papo hapo kwa kugongwa na gari wakati wakitoka hospitalini wakiwa wamepanda pikipiki

> Waliofariki ni Ebenezer Mollel (1), Neema Mollel (27) na Agustino Mollel (24)

Soma https://jamii.app/AjaliArushaJulai

#JFMatukio
😢12👍1👎1