JamiiForums
βœ”
52.5K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
UKRAINE: Waandishi wa Habari 12 wamefariki na 10 kujeruhiwa Nchini humo tangu kuzuka kwa Vita mwezi mmoja uliopita

Hadi sasa karibu Wawakilishi wa Vyombo vya Habari 56 wameshambuliwa ikiwa ni pamoja na Vyombo 15 vya kigeni

Soma - https://jamii.app/MediaDeathUkr
#RussiaUkraineWar
KENYA: Rais Uhuru Kenyatta amesema Naibu wa Rais, William Ruto alikuwa akimuhujumu na kusimamia mipango ya kumfanyia hujuma ili ashitakiwe

> Kenyatta amesisitiza Raila Odinga ndiye mtu sahihi kwa Nafasi ya Urais ktk uchaguzi wa mwaka huu

Soma - https://jamii.app/Kenyatta
UFARANSA: Wanafunzi Mjini Paris, wameandamana wakipinga Ujenzi wa Bomba la Mafuta la #Tanzania na #Uganda wakisema ni uharibifu wa mazingira

> Omar Elmawi ambaye ni Raia wa Kenya ameonekana kuwa kinara wa kampeni hiyo ya #StopEACOP

Soma https://jamii.app/BombaLaMafuta
BIDEN ATOA KAULI KALI KWA PUTIN, IKULU YAINGILIA KUPOZA MAKALI

Rais wa Marekani, Joe #Biden amesema Rais Putin hatakiwi kuendelea kuwepo Madarakani

Ikulu ya Marekani imefafanua kuwa Biden hakumaanisha kushawishi mabadiliko Urusi

Soma - https://jamii.app/PutinBiden

#JamiiForums
UNYANYASAJI WAFANYAKAZI PEPSI: UCHUNGUZI WAANZA

Serikali imekiri kutambua taarifa za madai ya unyanyasi na madhila kwa wafanyakazi wa Kiwanda cha #Pepsi (SBC LTD) Jijini Dar

Ukaguzi na uchunguzi unaendelea kiwandani hapo

Soma - https://jamii.app/UtuKazini
#JamiiForums #HumanRights
#KENYA: WASIOJULIKANA WAZIDI KUUA, IDADI YAFIKA 29

Miili miwili iliyopatikana ikielea Mto Yala imefikisha idadi ya Maiti za Watu 29 wanaodaiwa kuuawa tangu Oktoba 2021

Mwili mmoja umetobolewa Macho huku mwingine ukiwa umefungwa mfuko Kichwani

Soma - https://jamii.app/KenyaMauaji
#Iraq imejenga ukuta kwenye mpaka wake na #Syria ili kuzuia wanajihadi wa kundi la Islamic State kuingia

Ukuta umejengwa Ninawi, eneo la #Sinjar na una urefu Kilometa 12 na Mita 3.5 kwenda juu. Ujenzi ulianza 2018 na haitambuliki lini utakamilika

Soma - https://jamii.app/UkutaIS
πŸ‘1
TANZIA: PROF. NGOWI AFARIKI DUNIA

Prof. Honest Ngowi ambaye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu Mzumbe akiwa na Dereva wake wamefariki kwa ajali ya gari iliyotokea maeneo ya Mlandizi, Pwani wakiwa njiani kuelekea Morogoro

> Ajali imetokea Machi 28, 2022 asubuhi

Soma https://jamii.app/ProfNgowi
πŸ‘1
EL SALVADOR YATANGAZA HALI YA HATARI KUTOKANA NA MAUAJI YA MAGENGE

Vurugu za magenge zimeongezeka sana ambapo Watu 62 wameuawa Machi 26 pekee

Tangazo hilo linadhibiti Mikusanyiko huru, Uhuru wa Mawasiliano na linaruhusu ukamataji bila waranti

Soma - https://jamii.app/ElSavadorUnrest
GEITA: Watoto watatu wa Darasa la Tatu (Wa familia moja) wamebakwa na kulawitiwa na Mfanyabiashara (Mwanafamilia) mwenye uwezo kifedha kwny familia yao

> Walimu walimgundua mmoja wa Watoto hao baada ya kwenda shule akiwa na maumivu makali

Soma https://jamii.app/WatotoWabakwa
Ili kuweza kutuma Maombi ya nafasi hizi tembelea - https://jamii.app/NafasiAjira

#JamiiForums
BURKINA FASO: Spika wa Zamani, Alassane Bala SakandΓ© amekamatwa na baadaye kuachiwa baada ya kuwaambia Waandishi wa Habari kwamba Rais aliyeondolewa Madarakani, Roch KaborΓ© hayuko kwenye kifungo cha Nyumbani bali yuko kizuizini

Soma - https://jamii.app/SakandeArrested
#JamiiForums
MBEYA: Kamanda wa Polisi, Ulrich Matei amesema β€œWatu waache kuzua taarifa zinazosasababisha taharuki. Ajali ya Machi 27, 2022 iliyotokana na Scania kufeli breki imesababisha vifo vya watu wawili tu ambao ni Jeremiah Mwasega na Suza Mbwiga.”

Soma - https://jamii.app/MbeyaAjali
TANGA: MBARONI KWA TUHUMA ZA MAUAJI BAADA YA KUFUMANIA

Mohamed B. Lukindo (43) anatuhumiwa kumuua Athumani Dolly usiku wa kuamkia Machi 28, 2022 Mtaa wa Vunja Bei, Handeni

> Inadaiwa, Mtuhumiwa alimkuta Athuman akiwa na mkewe nyumbani kwake usiku

Soma https://jamii.app/TangaMauaji
NSONGWI, MBEYA: Jeshi la Polisi linamshikilia Fidelis Komba (42), ambaye ni Mganga wa Tiba Asili kwa tuhuma za kumiliki noti bandia zenye thamani ya Tsh. 3,340,000

> Mutuhumiwa alikamatwa akiwa na noti 219 za Tsh. 10,000 na noti 230 za Tsh. 5,000

Soma - https://jamii.app/Mganga
#UKRAINE: Waziri wa Uchumi, Yulia Svyrydenko amesema vita inavyoendelea imegharimu Nchi yao Dola bilioni 564.9 (sawa na Tsh. trilioni 1,310)

> Inaelezwa kuwa, Kilomita 8,000 za barabara na mita za mraba milioni 10 za makazi zimeharibiwa

Soma https://jamii.app/WarCosts
MOROGORO: Jeshi la Polisi linamshikilia Abdilah Yassin (Mpigadebe) ktk Kituo Kikuu cha Mabasi cha Msamvu kwa kumuua kwa kumchoma kisu Tazani Mndeme (Mpigadebe) wakati wakigombea abiria

> Tukio hilo limetokea leo Machi 28, 2022, saa 12 asubuhi

Soma - https://jamii.app/MpigaDebe
#URUSI: Serikali inaandaa Amri ya Rais itakayowazuia Raia kutoka Marekani na Washirika wake ikiwemo Uingereza kuingia nchini humo

> Hatua hiyo ni kulipa kisasi dhidi ya vitendo visivyo vya kirafiki vya mataifa kadhaa ya kigeni kwa Nchi hiyo

Soma https://jamii.app/UrusiRaia
MAREKANI: Rais Joe Biden amesema hataomba radhi kwa kauli yake ya hivi karibuni kuwa Rais Vladimir Putin wa #Urusi hawezi kusalia madarakani

> Asema kauli yake ilikuwa kuonesha hasira ya kimaadili na siyo wito wa kuondoa utawala wa Urusi

Soma https://jamii.app/PutinVsBiden
TANGA: Watu sita wamefariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya gari aina ya Fuso (T 239 AFB) kuacha njia na kutumbukia kwenye korongo katika eneo la Barabara ya Soni/Mombo, Wilayani Lushoto

> Ajali hiyo imetokea Machi 29, 2022

Soma - https://jamii.app/FusoAjali
#JamiiForums