JamiiForums
52.4K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
KENYA: WAFANYABIASHARA WAKIMBILIA ETHIOPIA SABABU YA GHARAMA ZA UMEME

> Bei za umeme za Ethiopia zipo chini kwa zaidi ya 80% ukilinganisha na Kenya

> Kampuni kadhaa zimeshahama huku nyingine zikiwa zimefunga shughuli kutokana na bei za umeme

Soma https://jamii.app/UmemeKenya
DAR: POLISI WAPIGA MARUFUKU DISKO TOTO KWENYE SIKUKUU YA EID

Kamanda Lazaro Mambosasa amepiga marufuku disko toto katika kumbi za starehe na kuwataka Wananchi kusherehekea Eid El Fitri kwa amani na utulivu ikiwemo kutovunja #Sheria

Soma - https://jamii.app/BanDiskoToto
MWANZA: DC AAGIZA KUONDOLEWA KWA MWALIMU ANAYEDHALILISHA WANAFUNZI

DC wa Magu ameagiza Mwalimu Martin Mambosasa wa Shule ya Msingi Ilungu anayetuhumiwa kuwafanyia michezo michafu Wanafunzi hata 2 ktk kitanda kimoja kuondolewa Wilayani humo

Soma - https://jamii.app/MwlNgonoWanfz
PETRA DIAMONDS KULIPA FIDIA YA TSH. BILIONI 14.02 KWA KUKIUKA HAKI ZA BINADAMU TANZANIA

Kampuni imethibitisha walinzi waliwapiga na kuwatesa wachimbaji wadogo walioingia Mgodi wa Mwadui na kusababisha vifo 7

> Wamekubali kuwalipa fidia wahanga

Soma https://jamii.app/MgodiWalipaFidia
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Tausi wana uwezo wa kuruka/kupaa lakini sio kwa umbali mrefu. Mara nyingi hupaa kutoka Ardhini hadi juu ya Mti au dari kutokana na Uzito wa Mabawa yake

Ni mara chache sana kumkuta Tausi akiwa amepaa juu zaidi kama Tai au aina nyingine ya Ndege

#JFLeo
MATUMIZI MABAYA YA FEDHA NI ADUI WA MAFANIKIO

Kutokuwa na mpangilio wa matumizi ya Pesa ni changamoto inayowakumba wengi ambapo Mtu hutamani kununua kila anachokiona mbele yake

Kukopa pesa ovyo hupelekea madeni yanayowaelemea Watu. Baadhi ya Watu wanakopa bila kuangalia faida au hasara za Mkopo na kujikuta wakilipa Madeni kwa miaka mingi

Soma - https://jamii.app/MatumiziFedha
#Uchumi
NJOMBE: DC AAGIZA KITUO CHA AFYA KUACHA KUWATOZA FEDHA WATOTO CHINI YA MIAKA MITANO

Kituo cha Afya Makambako huwatoza Watoto Tsh. 4000 ili kumuona Daktari ambapo ni kinyume na Sera ya Afya ya 2007

> Mkuu wa Wilaya ameagiza kusitishwa kwa tabia hiyo

Soma https://jamii.app/WatotoKulipa
ZIMBABWE: MKE WA MUGABE AITWA MAHAKAMANI KWA KUMZIKA MUMEWE KINYUME NA MILA

Waraka wa Chifu Zvimba umemtaka Grace Mugabe kuufukua mwili ili uzikwe tena kulingana na utamaduni wa Watu wa Zvimba

Pia, alipe faini ya Ng’ombe na Mbuzi kwa kukiuka Mila

Soma - https://jamii.app/GraceMugabeCourt
ISRAEL vs PALESTINA: Mpaka sasa Vifo vya Wapalestina vimefikia 83 huku Watu 480 wakijeruhiwa kutokana na Mapigano yanayoendelea

- Mapigano hayo kati ya Israel na kundi la Wanamgambo wa #Hamas yamesababisha uharibifu mkubwa huko Gaza

#GazaUnderAttack #IsraelPalestineConflict
FAINALI YA UEFA KATI YA MAN. CITY NA CHELSEA KUCHEZWA URENO

Mchezo wa Fainali ya kuwania Kombe la Klabu Bingwa Ulaya kati ya #ManchesterCity na #Chelsea umehamishiwa Ureno kutokana na UEFA na Serikali ya Uingereza kutofikia muafaka wa mchezo huo kuchezwa Wembley

UEFA ililazimika kutafuta uwanja mbadala kutokana na mlipuko wa Ugonjwa wa #COVID19 katika nchi ya Uturuki uliosababisha Uingereza kuiweka nchi hiyo katika nchi hatari za kutembelea

#JamiiForums #UCL #JFSports
MAMBO YA KUZINGATIA IKIWA UNAFIKIRIA KUANZA KUJENGA NYUMBA YAKO

1. Fedha: Kabla ya kuanza ujenzi hakikisha una chanzo kizuri cha mapato ambacho kitakurahisishia shughuli ya ujenzi. Pia, ni vyema kuwa makini na matumizi ya fedha katika kila hatua ya ujenzi

2. Mchoro/Ramani: Ikiwa tayari una Kiwanja basi jitahidi kutafuta Msanifu Majengo (Architect) atakayekupa ushauri wa kitaalamu kulingana na kile unachokitaka

Soma - https://jamii.app/NyumbaUjenzi
#Ujenzi
MDAU: JITAHIDI USIWE SABABU YA NDOA YA RAFIKI YAKO KUVUNJIKA

> Anafafanua, kuvunjika kwa ndoa huweza kuwa na madhara makubwa kwa watoto na wewe kama rafiki usiwe sababu ya hilo

> Anasema rafiki unapaswa kuwa mshauri mzuri ili ndoa iweze kudumu

Soma https://jamii.app/UrafikiNdoa
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amemsimamisha kazi Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya ili kupisha uchunguzi wa tuhuma mbalimbali zinazomkabili kuanzia leo, Mei 13, 2021

- Aidha, Rais Samia amefanya teuzi za Viongozi mbalimbali ambao uteuzi wao unaanza leo

#JFLeo
TUNAWATAKIA SIKUKUU NJEMA YA EID-AL-FITR

> Bodi, Menejimenti na Wafanyakazi wote wa JamiiForums wanawatakia Waislamu na watu wote kwa ujumla Sikukuu njema ya #EidAlFitr

> Asante kwa kuendelea kuwa pamoja nasi; tunawatakia mapumziko mema!

#EidMubarak #Eid #EidUlFitr
CDC-USA: WALIOMALIZA KUPATA CHANJO WANAWEZA KUTOVAA BARAKOA

Kwa waliomaliza kupatiwa chanjo ya #COVID19 wanaweza kuendelea na shughuli walizosimamisha kwa sababu ya Corona

> Hawatakuwa na haja ya kuvaa barakoa wala kuweka umbali kati ya mtu na mtu

Soma https://jamii.app/BarakoaCDC
KENYA: MAHAKAMA YA JUU YAZUIA MAPENDEKEZO YA KUBADILISHA KATIBA

Mahakama imesema mpango wa BBI ni hatua binafsi ya Rais Kenyatta ambaye hana Mamlaka ya Kisheria kuanzisha mchakato wa mabadiliko yoyote ya #Katiba

Mpango huo unapendekeza mgawanyo wa Madaraka baina ya Makabila hasimu ili kuzuia ghasia zinazotokea kila baada ya Uchaguzi

Soma - https://jamii.app/CourtBBIKE
TAFITI: #COVID19 INAWEZA KUPELEKEA UHANITHI

Watafiti wameandika ktk Jarida la Afya ya Wanaume kuwa Corona huathiri mishipa ya Damu hivyo huweza kupelekea uhanithi

> Wameona haja ya Wanaume kuangaliwa zaidi katika Chanjo ili kuepuka tatizo hilo

Soma https://jamii.app/UhanithCorona