JamiiForums
52.4K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: WEZI SUGU 30 WAKAMATWA NA POLISI

> Jeshi la Polisi mkoa wa kipolisi Kinondoni limekamata wezi hao wakiwa na mali mbalimbali

> Watu wote waliopotelewa/kuibiwa na vitu wametakiwa kufika kituoni na risiti kubaini vitu hivyo kama ni vyao

Soma https://jamii.app/Wizi30Polisi

#JFLeo
PROF. LIPUMBA: TUTAJENGA UCHUMI WENYE USHINDANI KITAIFA NA KIMATAIFA

> Amesema, ukuaji wa uchumi unahitaji uongozi imara, utawala makini na mipango

> CUF itaweka misingi itakayohakikisha uchumi unakua kwa 8%–10% kila mwaka kwa miaka 10 ijayo

Soma https://jamii.app/LipumbaLindi
#TZ2020
AAFP: TUTAKUSANYA ILANI ZA VYAMA VYOTE NA KUUNDA SERIKALI YENYE SERA JUMUISHI

> Mgombea Urais, Seif Maalim Seif amesema dhana ya Chama kitakachoshinda kuchukua kila kitu ni kama ulaghai kwani Watanzania wamegawanyika katika nadharia tofauti

Soma https://jamii.app/SeifMaalimAAFP
#TZ2020
UMOJA WA ULAYA WAZUNGUMZA KUHUSU UCHAGUZI WA TANZANIA

> Umoja wa Ulaya (EU) umesisitiza Vyama vyote kuwajibika ktk kuweka mazingira ya Uwazi na Uchaguzi wa amani

> EU wanategemea hatua hii itajenga ushirikiano mkubwa kati yao na #Tanzania

Soma https://jamii.app/EUUchaguziTZ
#TZ2020
ADC: TUNALENGA KUMPA MTANZANIA MAISHA MAZURI

> Mgombea Urais, Queen Sendiga amesema Wakulima wategemee neema ndani ya Uongozi wa ADC

> Ameahidi kuboresha miundombinu akisema barabara zitatengenezwa kwa kiwango cha kupita nyakati zote

Soma - https://jamii.app/ADCBabati
#Uchaguzi2020
WAANGALIZI WA NDANI WA UCHAGUZI WALALAMIKIA UKOSEFU WA FEDHA

> Mkurugenzi wa Uchaguzi amewashauri Waangalizi kuwa na fedha badala ya kutegemea Wafadhili

> Asema, Serikali haijategemea Wafadhili ktk Uchaguzi huu unaogharimu Tsh. Bilioni 331

Soma https://jamii.app/WatazamajiHela
#TZ2020
SEIF MAALIM: WANANCHI WASISHAWISHIKE NA IDADI YA WATU KATIKA KAMPENI

> Amewataka wananchi kumpigia kura Mgombea mwenye nia ya dhati ya kutatua changamoto zao

> Amesema, Vyama vinavyopiga sana kelele havina ufumbuzi wa matatizo ya wananchi

Soma - https://jamii.app/SeifMaalimAAFP
#TZ2020
UPDATES: MAWAKALA WA CHADEMA WALIOFARIKI KWA AJALI WAFIKIA 6

> Mawakala 9 walipata ajali wakienda kuapishwa baada ya utaratibu kubadilika

> 3 walifariki palepale, 3 wamefariki wakitibiwa, 1 ameruhusiwa na 2 wanaendelea na matibabu

Soma - https://jamii.app/Ajali6Mawakala
#Uchaguzi2020
MWANZA: POLISI WACHUNGUZA KIFO CHA KATIBU KATA WA CCM ALIYEFARIKI BAADA YA KULA MAKANDE

> Deogratias Medard(42) alifariki muda mfupi baada ya kula Makande na Chai akiwa kwenye Kampeni za Mgombea Ubunge Sengerema (CCM), Hamis Tabasamu

Soma - https://jamii.app/KatibuCCMKata
#Uchaguzi2020
UPDP: ADHABU YA KUNYANYASA NA KUDHALILISHA WANAWAKE NI MIAKA 25 JELA

> Mgombea Urais, Twalib Kadege amesema Serikali yake itatoa adhabu hiyo bila huruma

> Chama hicho kimetoa kipaumbele na kuwasimamisha Wagombea Wanawake wengi

Soma - https://jamii.app/UPDPWanawake
#Uchaguzi2020
NEC YAONYA WAANGALIZI WA NDANI NA NJE KUINGILIA UCHAGUZI

> Mjumbe wa NEC, Balozi Omar Mapuri amewataka wazingatie Sheria, #Katiba na miongozo ya kufanya wajibu wao, na kuhakikisha hawaingilii mwenendo wa Uchaguzi au kusababisha vurugu

Soma - https://jamii.app/NECWaangalizi
#Uchaguzi2020
KADEGE: NITAANZISHA WIZARA YA MIKOPO NA KUWAPA HALI NZURI KIMAISHA

> Mgombea Urais kupitia UPDP amesema, ataanzisha Wizara ya Mikopo itakayowakopesha fedha Vijana na Wanawake

> Ataongeza kima cha chini cha Mshahara kufikia TSH. 400,000

Soma - https://jamii.app/KadegeUPDP
#TZ2020
DKT. MAGUFULI: SIKUMFUKUZA GAMBO UKUU WA MKOA

> Amesema hakumfukuza aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo kwenye nafasi hiyo

> Ameeleza, kama angemfukuza asingelipitisha jina la Gambo ili awe Mgombea wa ubunge Jimbo la Arusha Mjini

Soma https://jamii.app/ArushaMjiniJPM
#TZ2020
SAFARI ZA BOTI NA MELI KUSITISHWA SIKU YA UCHAGUZI

> Mamlaka ya Usafiri wa Baharini #Zanzibar(ZMA) imetangaza kusitisha safari zote za Boti na Meli za abiria na mizigo Jumatano ijayo, Oktoba 28, 2020 ili kutoa fursa kwa Wananchi kupiga kura

Soma https://jamii.app/SafariOktoba28
#TZ2020
KADEGE: UPDP ITATOA RUZUKU ZA UCHAGUZI HATA VYAMA VISIVYO NA WABUNGE

> Mgombea Urais wa Chama hicho amesema Ruzuku ya Uchaguzi ni keki ya Taifa, kila Chama lazima kipate

> Wasio na Wabunge watapata ruzuku ili waweze kuzunguka kuomba kura

Soma - https://jamii.app/UPDPRuzukuUchaguzi
#TZ2020
MBOWE: KUNA MAMILIONI YA WAPIGA KURA HEWA NA MAELFU YA VITUO BANDIA

> Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amedai kuna uvurugwaji mkubwa wa Daftari la Wapiga kura

> Ameitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutoa maelezo na suluhisho haraka

Soma https://jamii.app/MboweUchaguzi
#Uchaguzi2020
#NIGERIA: MITIHANI YA SHULE ZA SEKONDARI YAHAIRISHWA KUTOKANA NA GHASIA

> Pia, Baraza la Taifa la Mitihani(NECO) limefikia uamuzi huo baada ya baadhi ya Majimbo kuweka amri ya kutotoka nje

> Waandamanaji wanaendelea kupinga ukatili wa Polisi

Soma https://jamii.app/EndSARSNigeria
DPP: YEYOTE ATAKAYEVURUGA AMANI ATASHUGULIKIWA

> Mkurugenzi wa Mashtaka, Biswalo Mganga amesema jukumu la amani ni la kila Mwananchi

> Taratibu na Sheria zinatakiwa kufuatwa ili kupata Haki, amani na usalama, na Taifa liweze kupata maendeleo

Soma https://jamii.app/DPPAmaniTZ
IVORY COAST: UPINZANI WAKATAA MABADILIKO YA TUME YA UCHAGUZI

> Vyama vya Upinzani vimesema vitaendelea kuasi dhidi ya utekelezaji wa #Sheria ya kumruhusu Rais Alassane kugombea kwa awamu ya 3

> Wamezitaka Taasisi za Kimataifa kuingilia kati

Soma https://jamii.app/ProtestsInIvoryCoast
KAMATI YA AMANI YAOMBA MFUNGO WA SIKU TATU KUOMBEA UCHAGUZI WA AMANI

> Pia, imewataka wazazi na walezi kuwaasa vijana kujiepusha kushawishiwa na wanaoitakia mabaya Tanzania

> Wamesisitiza kuviacha Vyombo ya Uchaguzi vifanye kazi yake

Soma https://jamii.app/KuombeaUchaguzi
#TZ2020