JamiiForums
βœ”
52.5K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
NEC YAKABIDHI NAKALA YA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KWA VYAMA VYA SIASA

> Vyama vimekabidhiwa nakala tepe ya daftari la wapiga kura na orodha ya vituo vya kupigia kura

> Pia, Tume imevikabidhi Karatasi ya mfano ya kupigia kura

Soma https://jamii.app/NECWapigaKura
#Uchaguzi2020
DAR: MVUA YA OKTOBA 13 YAPELEKEA VIFO VYA WATU 8

> Miili 5 imeokotwa Mto Msimbazi, 2 imeokotwa maeneo ya Buguruni na mmoja Mto Mvule uliopo Ukonga

> Wawili kati ya waliofariki dunia ni watoto ambao walipoteza maisha wakiokoana Mto Msimbazi

Soma - https://jamii.app/MvuaMaafaDar
WIZARA YA AFYA YATOA TAHADHARI YA MAGONJWA YA MLIPUKO KUTOKANA NA MAFURIKO

> Wananchi wanaaswa kuchemsha Maji ya kunywa au kutibu kwa dawa kabla ya kuyatumia na kuongeza usimamizi wa usafi ktk maeneo ya mikusanyiko kama Shuleni, Vyuo, Masoko

Soma https://jamii.app/MafurikoMagonjwa
TANZANIA MSHINDI WA TATU TUZO ZA BIASHARA DUNIANI

> Tanzania imepata Tuzo za Taasisi zinazosimamia Biashara Duniani (WTPO 2020) ktk kipengele cha matumizi bora ya ushirikiano ktk huduma ya kliniki ya biashara inayosimamiwa na TanTrade

Soma https://jamii.app/TzYa3Biashara
#JFBiashara
SHEIKH JONGO: VIONGOZI WA DINI MSIPIGIE CHAPUO VYAMA VYA SIASA MNAPOHUBIRI

> Afisa wa Ofisi ya Mufti Zanzibar, Sheikh Thabiti Jongo
amewashauri kutoonesha mahaba ya vyama misikitini ili kutowagawa waumini

> Amewataka wahubiri amani

Soma https://jamii.app/DiniSiasaPemba
#Uchaguzi2020
NJOMBE: MBARONI KWA KUUA NA KUMWAGA UBONGO WA BABU YAKE

> Imani Mbilinyi (25) anatuhumiwa kumuua Elia Mbilinyi (90)

> Baada ya tukio hilo, mtuhumiwa alimuuliza Mwenyekiti kama angeweza kumlinda. Mwenyekiti akawaita Mgambo na kutaarifu Polisi

Soma https://jamii.app/MauajiBabuNjombe
UHOLANZI YARUHUSU KIFO CHA MAPEMA KWA WATOTO WENYE MAGONJWA YASIYOPONA

> Serikali ya #Uholanzi imeidhinisha mpango wa kuruhusu kifo cha mapema kwa watoto wenye mwaka 1 mpaka miaka 12

> Lengo ni kuzuia watoto kuteseka kwa maumivu wanayopitia

Soma https://jamii.app/EuthanasiaHoland
MAALIM SEIF AFUNGIWA KUFANYA KAMPENI KWA SIKU 5

> Kamati ya Maadili ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) imemfungia Mgombea Urais wa ACT-Wazalendo kuanzia kesho hadi Oktoba 20 kwa kuwashawishi watu wapige kura Oktoba 27 badala ya Oktoba 28

Soma - https://jamii.app/MaalimSeifAfungiwa5
#TZ2020
JAJI MSTAAFU: WASAIDIZI WA SHERIA MJIEPUSHE NA USHABIKI WA KISIASA

> Jaji Mkuu Mstaafu wa Tanzania, Mohamed Chande Othman amewataka Wasaidizi wa Sheria wa Majaji kutumia taaluma na kuzingatia weledi katika uendeshaji wa mashauri ya Uchaguzi

Soma https://jamii.app/SheriaWelediUchaguzi
#TZ2020
MDAU: CHUKI NI CHANZO CHA MACHAFUKO, NI MUHIMU KUIEPUKA

> Mdau wa Jamiiforums.com anasema chuki hutokana na hasira inayochochewa na fitina au taarifa mbaya

> Chuki huaribu familia hadi mataifa, ameshauri kujifunza ili kuiepuka

Soma - https://jamii.app/KuepukaChuki
#JFMaarifa
MOROGORO: WATATU MBARONI KWA TUHUMA ZA MAUAJI

> Rajabu Ramadhani, Athumani Ramadhani na Daniel William wanashikiliwa kwa mauaji ya Bernadetha Kibwana na Zabibu Maulidi

> Bernadetha ameuawa kwa shoka na Zabibu alipigwa na mchi kichwani

Soma - https://jamii.app/TuhumaMauaji
#JFLeo
BAKWATA: VIONGOZI WA DINI WASIFANYE KAMPENI KWENYE NYUMBA ZA IBADA

> Baraza za Ulamaa BAKWATA Taifa limewasihi viongozi wa dini kubaki kuwa wasuluhishi na wapatanishi

> Limewataka waislamu kuiombea nchi ili Uchaguzi Mkuu upite salama

Soma https://jamii.app/BAKWATAUchaguzi
#Uchaguzi2020
WIZARA YA AFYA: WAUGUZI WAZOEFU MUWASIMAMIE WATARAJALI

> Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi na Ukunga, Ziada Sellah amesema watarajali (interns) wasifanye kazi wenyewe

> Amesema, si sahihi wakiachwa peke yao kuwahudumia wagonjwa hospitalini

Soma - https://jamii.app/WauguziWatarajali
#JFLeo
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
NEC YATAKA VYAMA VYA SIASA KUZINGATIA MAADILI YA UCHAGUZI
-
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imevitaka Vyama vya Siasa na Wagombea kuendelea kufuata Maadili ya Uchaguzi na kunadi Sera kwa kufuata utaratibu wa ratiba ambayo imepangwa
-
Pia, Vyama vya Siasa vimetakiwa kukwepa maneno ya uchochezi, kukwepa kuhamasisha watu kufanya vurugu, badala yake vihamasishe watu kwa amani kwenda kupiga kura
-
NEC imesisitiza kwamba Sheria za nchi zipo na zinapaswa kuendelea kufuatwa

#JFLeo #JamiiForums #Uchaguzi2020 #TZ2020
ASKOFU SHOO: VIONGOZI WA DINI KUEGEMEA CHAMA KIMOJA CHA SIASA KUNAWAGAWA WANANCHI

> Kiongozi wa Kanisa la KKKT amesema, "Maandiko yanaelekeza namna ya kusimama na kama kuna mahali pa kukemea kutokana na ukiukwaji wowote, fanya bila ubaguzi”

Soma - https://jamii.app/ViongoziDiniSiasa
#TZ2020
SAMIA SULUHU: HATA UKIPIGIA KURA KWINGINE, CCM ITAUNDA SERIKALI

> Amesema kupigia kura Chama kingine ni sawa na kuweka sukari Ziwa Victoria

> Amewaambia wananchi wakifanya hivyo, hawatakuwa sehemu ya maendeleo yatakayoletwa na CCM

Soma - https://jamii.app/SamiaChunya
#Uchaguzi2020
TUNDU LISSU: NITAONGOZA NCHI KWA KUFUATA KATIBA MPYA ITAKAYOPATIKANA

> Mgombea Urais kupitia CHADEMA amesema, Nchi inahitaji #KatibaMpya ili kurudisha Mamlaka kwa Wananchi kujichagulia Viongozi kwenye maeneo yao na kuwawajibisha wanapokosea

Soma https://jamii.app/LissuSimiyu
#TZ2020
SHINYANGA: VIJANA 2 MBARONI KWA KUMBAKA MTOTO WA MIAKA 6

> Jeshi la Polisi linawashikilia vijana 2 wenye umri chini ya miaka 18 kwa tuhuma za kumbaka mtoto kwa zamu baada ya kumlaghai kuwa watamnunulia pipi pamoja na kumpatia hela

Soma - https://jamii.app/VijanaKubakaMtoto
SERIKALI YAHIMIZA WAANDISHI KUSHIRIKI MASHINDANO YA SADC KWA WAANDISHI WA HABARI 2021

> Mashindano hayo yanahusisha washiriki kutoka nchi zote wanachama wa SADC

> Yatakuwa katika makundi manne ambayo ni Picha, Uchapishaji, Runinga na Radio

Soma - https://jamii.app/MashindanoSADC