JamiiForums
52.8K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
DKT. MWINYI: KILA NITAKAYEMTEUA ATAWAJIBIKA KUTIMIZA MAJUKUMU YAKE

> Mgombea Urais Zanzibar (CCM) amesema atajenga mawasiliano na wafanyakazi ili kusikiliza changamoto zao na kuzitatua

> Hatakuwa na huruma kwa wabadhirifu na wala rushwa

Soma - https://jamii.app/UwajibikajiMwinyi
#TZ2020
ZEC: KURA YA MAPEMA HAITAHUSISHA ASKARI WOTE

> Tume ya Uchaguzi imesema watakaopiga kura Oktoba 27 ni watu maalum ikiwemo Watumishi wa Tume, Wasimamizi wa Uchaguzi na Askari ambao watahusika katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28

Soma https://jamii.app/KuraMapemaZNZ

#Uchaguzi2020
NEC: VYAMA VYA SIASA VIMERUHUSIWA KUWEKA WAKALA KILA KITUO OKTOBA 28

> NEC imesema, tayari vyama vyote vinavyoshiriki Uchaguzi vimepata nakala tepe ya orodha ya wapiga kura ili kuwawezesha Mawakala kuhakiki wapiga kura wanaofika kituoni

Soma - https://jamii.app/WakalaUchaguzi
#TZ2020
MAMBO YASIYOTAKIWA KUFANYWA NA WATENDAJI WA SERIKALI WAKATI WA UCHAGUZI

> Mawaziri, RC na DC kuchanganya ziara za kikazi na shughuli za kiuchaguzi

> Kutangaza katika vyombo vya habari au kwa namna yoyote misaada au ahadi ya aina yoyote

> Kutoa ahadi za shughuli za maendeleo ya jamii

> Kutumia madaraka au rasilimali za Serikali kwa shughuli za kampeni za uchaguzi

Soma > https://jamii.app/UchaguziMaadili

#TZ2020
MAREKANI: RAIS TRUMP ATOKA HOSPITALI, AWATAKA WATU WASIOGOPE #COVID19

> Rais Donald Trump amesema anajisikia vizuri na amewataka watu wasiruhusu #CoronaVirus itawale maisha yao

> Pia, Rais huyo amesema atarejea kufanya kampeni hivi karibuni

Soma https://jamii.app/TrumpCovidUS
SHAMBULIO LA WESTGATE, KENYA: HUKUMU YA WATUHUMIWA WA UGAIDI KUTOLEWA LEO

> Hukumu hiyo inatarajiwa kutolewa leo baada ya kuahirishwa jana

> Watu 67 walifariki ktk shambulio hilo la Septemba 2013, ambalo kundi la Al-Shabaab lilidai kuhusika

Soma https://jamii.app/WestgateCase
MALAWI: RAIS ATENGUA AHADI YA KUTOA AJIRA MILIONI MOJA

> Rais Chakwera aliyetoa ahadi hiyo ktk Kampeni amesema Serikali inaweza kuajiri watu 200,000

> Amesema, Serikali pekee haiwezi kutengeneza ajira na inahitaji msaada kutoka Sekta Binafsi

Soma https://jamii.app/RaisMalawiAjira
WANAFUNZI ZAIDI YA MILIONI 1 KUANZA MITIHANI YA KUMALIZA DARASA LA 7 KESHO

> Katibu Mtendaji wa NECTA amesema Watahiniwa 1,024,007 nchi nzima wanatarajiwa kufanya mitihani

> Mitihani itafanyika kwa siku mbili kuanzia Oktoba 07 hadi 08, 2020

Soma - https://jamii.app/MitihaniDrs7
JKCI YATOA TAHADHARI YA ONGEZEKO LA WENYE MATATIZO YA MOYO

> Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete imesema wagonjwa wanaofika Kliniki kwa siku ni 200 - 400

> Wengi wao wana shida ya Mishipa ya Damu kuziba, ambapo ikiziba husababisha kifua kuuma

Soma https://jamii.app/WagonjwaMoyo
ZANZIBAR: JESHI LAWATAKA VIONGOZI WA VYAMA KUACHA KUTOA VITISHO

> CP Mohamed Haji Hassan amesema Jeshi linaona baadhi ya matamshi kuwa ni maandalizi ya uvunjifu wa amani

> Jeshi litachukua hatua kali kuhakikisha Amani inalindwa

Soma - https://jamii.app/PolisiAmaniZNZ

#Uchaguzi2020
ZITTO KABWE APATA AJALI YA GARI KIGOMA

> Kiongozi huyo wa Chama cha ACT-Wazalendo amepata ajali wakati akitokea Kalya kuelekea Lukoma kwaajili ya kampeni

> Alikuwa na watu watano kwenye gari na wote wapo salama licha ya kupata majeraha

Soma - https://jamii.app/ZittoAjali
TFF YATAMBULISHA JEZI MPYA ZITAKAZOTUMIWA NA TAIFA STARS

> Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetambulisha jezi mpya ikiwemo jezi ya nyumbani, ya ugenini na jezi namba 3

> Oktoba 11, 2020 Tanzania itacheza mchezo wa kirafiki na Burundi

Soma https://jamii.app/JeziTaifaStars
AFISA HABARI WA ACT-WAZALENDO ATUHUMIWA KUSAMBAZA MAUDHUI YA NGONO TWITTER

> Dotto Rangimoto amefikishwa Mahakama ya Kisutu akidaiwa kutenda kosa hilo kwa jina la James Michael

> Amepata dhamana (Mdhamini 1 ambaye ni Mkazi wa Dar) na Bondi ya Tsh. Milioni 5

Soma https://jamii.app/DottoKizimbani
MAJALIWA: TANZANIA INAHITAJI KIONGOZI ANAYEWEZA KUPAMBANA NA MAFISADI

> Amesema Kiongozi anatakiwa kusimamia Serikali na kuhakikisha aliowateua wanatekeleza majukumu

> Amewataka wananchi wasichague viongozi kwa ushabiki ili wasije kujilaumu

Soma https://jamii.app/MajaliwaKiongoziTZ
#TZ2020
KENYA: WANAFUNZI WA DARASA LA 4, 8 NA KIDATO CHA 4 KUREJEA SHULE JUMATATU IJAYO

> Shule zimetakiwa kuendelea kufuata kanuni za kudhibiti maambukizi ya #COVID19 kama kuvaa barakoa, kupima joto la Wanafunzi na Walimu pamoja na kunawa mikono

Soma https://jamii.app/SchoolResumeKE
RAIS WA #MALAWI KUFANYA ZIARA NCHINI #TANZANIA

> Rais Dkt. Lazarus Chakwera anatarajiwa kufanya ziara ya kitaifa kuanzia Oktoba 7 - 9, 2020

> Yeye na Rais Magufuli wataweka jiwe la msingi ktk Kituo cha Mabasi ya Mkoani cha Mbezi Mwisho, Dar

Soma https://jamii.app/ZiaraRaisMalawi
RAIA WA KIGENI KUDHIBITIWA KUSHIRIKI KTK UCHAGUZI

> Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) imezielekeza Kamati za Ulinzi na Usalama zilizopo mipakani kuwadhibiti raia wa kigeni kushiriki ktk Uchaguzi Mkuu, kwa kuwa kitendo hicho ni kinyume na Sheria

Soma https://jamii.app/NECWageniUchaguzi
#TZ2020
IMF YAIDHINISHA MSAADA WA DHARURA KWA NCHI 28 IKIWEMO TANZANIA

> Msaada wa Shirika la Fedha unalenga kuzisaidia nchi kupunguza madeni na kukabiliana na athari za #COVID19

> Hii ni awamu ya pili ya msaada huo, awamu ya kwanza ilihusisha nchi 25

Soma https://jamii.app/IMFAidTZ
JamiiForums: TUTATOWEKA HEWANI KWA DAKIKA KADHAA NA KUREJEA

> Mtandao wetu wa JamiiForums.com utatoweka hewani kwa dakika kadhaa ili kurekebisha masuala kadhaa na kuboresha upatikanaji wa huduma

> Zoezi hili linatarajiwa kutumia takribani dakika 30. Tunashukuru kwa uelewa na uvumilivu wako
JamiiForums: TUMEREJEA HEWANI BAADA YA MABORESHO YA DAKIKA 15

> Mtandao wetu wa JamiiForums umerejea hewani baada ya kutokuwa hewani kwa dakika 15 za maboresho ya upatikanaji wa huduma

> Zoezi hili limekamilika salama. Tunashukuru kwa uvumilivu wako muda wote ambao hatukuwa hewani