JamiiForums
βœ”
52.7K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
LISSU: KILA MTU ANA HAKI YA KULINDWA FARAGHA YAKE

> Amesema, #Katiba ya Tanzania inatamka wazi kuwa kila mtu ana haki ya kulindwa faragha yake

> Amesema, Maisha ya chumbani na mkeo au yeyote yule ni marufuku kwa Serikali kuchungulia

Soma https://jamii.app/PoliticalCoalition
#Uchaguzi2020
SHIRIKA LA NDEGE LA QATAR AIRWAYS LAINGIA MAKUBALIANO NA AIR TANZANIA

> Abiria wataweza kusafiri kwa urahisi kati ya Afrika na Doha kwa kuunganisha na Asia, Pasifiki, Amerika, Ulaya na Mashariki ya Kati

Soma > https://jamii.app/AirTzVsQatarAir

#AirTanzania #QatarAirways #JFLeo
KESI YA MTUHUMIWA WA MAUAJI YA KIMBARI RWANDA KUSIKILIZWA TANZANIA

> Mahakama ya Rufaa nchini Ufaransa imekubali Felicein Kabuga kushtakiwa Tanzania

> Kabuga alikamatwa baada ya kujificha kwa miaka 26. Anatuhumiwa kufadhili mauaji ya 1994

Soma https://jamii.app/KabugaKushtakiwa
#JFLeo
PROF. LUHANGA ATEULIWA KUWA MWENYEKITI WA BARAZA LA CHUO KIKUU MZUMBE

> Rais Magufuli amemteua Prof. Matthew Luhanga kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Mzumbe kwa Kipindi cha Pili

> Uteuzi huo unaanza Septemba 30, 2020

Soma https://jamii.app/LuhangaMwenyekiti
#JFLeo
LISSU: DUNIA HAIHITAJI TANZANIA ILA TANZANIA INAIHITAJI DUNIA

> Amesema bidhaa kama Dhahabu, Korosho na Chai zinaweza kupatikana ktk nchi nyingine hivyo, Serikali yake (CHADEMA) itahakikisha inashirikiana vyema na Mataifa mengine

Soma https://jamii.app/PoliticalCoalition

#TZ2020
SIKU YA WAZEE DUNIANI: DUNIA NA JAMII TUWAJIBIKE KUWATUNZA WAZEE

> Oktoba 1 kila mwaka, ni Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani inayotumiwa kutambua Ustawi wa Wazee

> Tanzania imefanikiwa kupunguza mauaji na kuboresha Huduma na Vituo vya Wazee

Soma https://jamii.app/SikuYaWazee
MTU WA KWANZA KUTIBIWA UKIMWI, AFARIKI KWA SARATANI

> Raia wa Marekani, Timothy Ray Brown (54), alipata UKIMWI 1995, alipandikizwa Uboho (Bone Marrow) wa mtu aliyekuwa na kinga ya VVU

> Njia iliyotumika kumtibu ni ghali sana lakini ilileta tumaini Duniani

Soma https://jamii.app/UKIMWISaratani
ZANZIBAR: MAALIM SEIF AAHIDI MUUNGANO WA SERIKALI 3

> Akiwa Pemba, amewataka wananchi kumpa kura na kumuwezesha kuleta mabadiliko

> Pia, amesema akipewa ridhaa, atazungumza na Serikali ya Muungano kuhusu muundo wa Jeshi la Polisi

Soma - https://jamii.app/MaalimKampeniZNZ

#Uchaguzi2020
DKT. MAGUFULI: SERIKALI IKO PAMOJA NA WAZEE

> Ktk kuadhimisha Siku ya Wazee(Oktoba 1) amesema, Serikali imehakikisha Wazee wanatibiwa bure kwenye hospitali za Serikali

> Changamoto chache zilizobaki watazishughulikia miaka 5 inayokuja

Soma https://jamii.app/MagufuliMbalizi
#Uchaguzi2020
DAR: SERIKALI YAZINDUA CHUO CHA MAFUNZO YA ELIMU YA MICHEZO NA UKOCHA

> Chuo hicho cha Maendeleo ya Michezo kinatoa Stashahada ya Utawala na Uongozi ktk #Michezo na Stashahada ya Ukocha nchini kwa kuzingatia Mitaala iliyopitishwa Kimataifa

Soma https://jamii.app/ChuoMichezo
UCHAGUZI MAREKANI: MIKE POMPEO AKATALIWA KUONANA NA PAPA FRANCIS

> Wanadiplomasia wa juu wa Vatican wamesema uamuzi huo umefikiwa kwasababu Kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki aliweka wazi kuwa Wanasiasa hawatapokelewa kipindi cha Uchaguzi

Soma - https://jamii.app/PompeoVatican
VYAMA VINAVYOTAKA KUUNGANA OKTOBA 03 VYATAKIWA KUACHA MPANGO HUO

> Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa amevitaka kutofanya hivyo kwasababu ni ukiukwaji wa Sheria

> Amesema, Ofisi yake imeshaviandikia barua vyama hivyo

Soma - https://jamii.app/MsajiliVyamaOkt3
#Uchaguzi2020
DKT. MAGUFULI AAHIDI TSH. MILIONI 5 YA KUJENGEA MADARASA YA SHULE YA MSINGI ULANGA

> Ameahidi hela hiyo baada ya mwanafunzi aliyekuwa kwenye mkutano kutaja madarasa kuwa changamoto

> Amesema hakutoa palepale kuepuka rushwa ya Uchaguzi

Soma https://jamii.app/MagufuliTshMil5
#Uchaguzi2020
πŸ‘1
MAGANJA: TANZANIA INGEONGOZWA VIZURI TANGU UHURU BASI INGEKUWA UJERUMANI YA AFRIKA

> Mgombea Urais wa JMT kupitia NCCR, Yeremia Maganja amesema chanzo cha haya ni utekelezaji wa Azimio la Arusha ambao haukuzingatia mazingira ya watu wake

Soma - https://jamii.app/MgombeaNCCR
#Uchaguzi2020
GUINEA: VIKOSI VYA USALAMA VYALAUMIWA KUUA WATU 50 KATIKA MAANDAMANO

> Ripoti zinataja watu 50 kuuawa, 200 kujeruhiwa na 70 kuzuiliwa kinyume cha Sheria mwaka 2019

> Ni katika maandamano ya kupinga Rais Alpha CondΓ© kuongeza Muhula wa Tatu

Soma https://jamii.app/Maandamano50Guinea
RAIS MAGUFULI AFUTA TOZO YA TSH. 50,000 KWA WAJAWAZITO WANAOCHELEWA KLINIKI

> Amesema kumekuwa na malalamiko dhidi ya kampeni ya Mama Kamandoo ya kuwatoza wajawazito wanaochelewa kujiandikisha kliniki Tsh. 50,000

> Amewataka Viongozi wa Serikali na Wizara ya Afya kusimamia utekelezaji wa agizo hilo kuhusu tozo

Angalia https://youtu.be/4OQ-dYNWxOI
#Uchaguzi2020
#COVID19: AFRIKA KUSINI YAFUNGUA MIPAKA KWA NCHI ZA AFRIKA

> Wasafiri kutoka nchi zenye idadi kubwa ya visa na vifo kuliko Afrika Kusini hawataruhusiwa kuingia kwa ajili ya utalii

> Nchi hiyo ina visa 674,339, vifo 16,734 na 608,112 wamepona

Soma https://jamii.app/SAOpensBorders
JESHI LA POLISI LAWATAKA WANANCHI KUTII SHERIA

> Wakati huu wa Uchaguzi, Jeshi limetoa rai kwa wananchi kuepuka matusi, kujichukulia Sheria mkononi na kutotoa taarifa za uongo ambazo zinalenga kuleta chuki miongoni mwa Watanzania

Soma - https://jamii.app/SheriaPolisiUchaguzi
#Uchaguzi2020
LISSU: CHADEMA YA LEO SIO ILE YA 2015, TUTAWEKA MAWAKALA KILA MAHALI

> Amesema hivi sasa wana uongozi na matawi kwenye takriban kila Kijiji

> Amesema hawatokubali Mawakala wao wasiapishwe, watatumia mbinu zote kuhakikisha wanaapishwa

Soma https://jamii.app/CHADEMAPress
#Uchaguzi2020
DPP AIDHINISHA MASHTAKA YA KUUAWA KWA KADA WA CCM IRINGA

> DPP Biswalo Mganga ameidhinisha mashtaka dhidi watuhumiwa 4 (3 ni Makada wa CHADEMA) ambao wamekiri kumteka na kumuua Emmanuel Mlelwa, aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM Vyuo Vikuu Iringa

Soma https://jamii.app/DPPMauajiMlelwa