JamiiForums
52.8K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
MAN. CITY YACHEZEA KIPIGO KIZITO MBELE YA LEICESTER

> Manchester City ikiwa nyumbani katika uwanja wa Etihad imejikuta ikiambulia kipigo cha goli 5-2 kutoka kwa Leicester City katika mchezo wa Ligi Kuu ya England

> Leicester City inaongoza Ligi kwa tofauti ya magoli ikiwa na alama 9 huku Manchester City ikiwa katika nafasi ya 13 na alama 3
-
#JamiiForums #JFMichezo #Michezo #Sports #JFSports
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
MKURUGENZI WA UCHAGUZI NEC: WATANZANIA WANATAKA BARABARA, HAWATAKI BLAH! BLAH!

> Dkt. Charles Mahera amesema, watanzania wanataka Afya iliyoimarika, miradi ya umeme na viongozi watakaolinda madini na sio watakaopeleka madini kwa wageni nje

Soma https://jamii.app/MkurugeziWaUchaguzi
#JFSiasa
LISSU: SIWEZI KUACHA KAMPENI KUITIKIA MAMBO YA MTANDAONI

> Tundu Lissu amesema hajapokea malalamiko wala wito wa kufika Tume ya Taifa ya Uchaguzi

> Jana (Septemba 27), Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Dkt. Charles Mahera alisema wamemuandikia barua Lissu

Soma https://jamii.app/NECLissuMaadili
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MGOMBEA URAIS WA ADC AAHIDI KUFUTA TOZO NA KODI ZISIZO NA MASHIKO

> Septemba 27, Queen Sendiga alitembelea Soko la Stereo Temeke na kuwaahidi wafanyabiashara kufuta tozo na kodi

> Pia, alifanya Mkutano Mbagala katika Viwanja vya Kurasini Mpya

Soma https://jamii.app/QueenSendiga
#TZ2020
ACT-WAZALENDO: WATAKAOIBA KURA WATAADHIBIWA NA MUNGU

> Mwenyekiti wa Ngome ya Wazee ya ACT-Wazalendo, Yassin Mohammed amesema maombi ya aliyedhulumiwa hukubaliwa haraka

> Pia, amewataka wananchi wachague Chama kinachojali maslahi ya wananchi

Soma https://jamii.app/ACTKuraKampeni
#JFLeo
TIK TOK YAFUTA MAMIA YA VIDEO BAADA YA KUPOKEA MAOMBI 296 KUTOKA SERIKALI YA URUSI

> Baada ya kupokea maombi hayo wameondoa maudhui 711

> Aidha, video 104,543,719 zimeondolewa kwenye mtandao huo kutoka maeneo mbalimbali duniani

Soma > https://jamii.app/TikTokUrusi

#TikTok
AFRIKA KUSINI: WAZIRI AKATWA MSHAHARA MIEZI MITATU KWA KUCHANGANYA CHAMA NA SERIKALI

> Nosiviwe Mapisa-Nqakula alikuwa ktk ziara rasmi ya kitaifa nchini #Zimbabwe Septemba 9 na aliwabeba abiria wengine wanachama wa ANC kwa hisani.

Soma https://jamii.app/WaziriAfrikaKusini
#JFLeo
TARIME: POLISI WAKANUSHA KUSHAMBULIA MSAFARA WA LISSU

- Kamanda wa Polisi, ACP Mkonda amesema wamewapiga mabomu ya machozi waliokuwa wanawarushia mawe Polisi

- Msafara wa Lissu upo njiani kuelekea Serengeti ukiongozwa na Polisi

Soma https://youtu.be/TWn9fTZN5hg
#Uchaguzi2020
BILIONEA AGAWA MALI ZOTE ILI AISHI MAISHA YA KAWAIDA

> Charles Feeney alianzisha Atlantic Philanthropies Foundation na ametoa Dola bilioni 8 sawa na Tsh. trilioni 18.56

> Hivi sasa anaishi kwenye nyumba ya vyumba viwili na Mkewe huko San Francisco

Soma https://jamii.app/BilioneaHelaHai
#JFLeo
LISSU: NITABADILI KATIBA ILI WABUNGE WAWE NA MAAMUZI JUU YA FEDHA ZA SERIKALI

> Tundu Lissu amesema kwa Katiba ya sasa mamlaka juu ya maamuzi ya fedha yapo kwa Rais

> Amesema hali hiyo inawafanya Wabunge wawe omba omba kwa Rais

Soma https://jamii.app/LissuKatibaMpya
#Uchaguzi2020
WAZIRI WA ARDHI ZANZIBAR ATOA WITO KWA WANAWAKE KUWALINDA WATOTO DHIDI YA #COVID19

> Salama Aboud Talib ni miongoni mwa watu waliopata virusi hivyo na kulazwa

> Amesema ni muhimu kuchukua tahadhari ili kuhakikisha gonjwa hilo halitorejea tena

Soma https://jamii.app/ZnzCOVID19Women
#JFLeo
MDAU: SERIKALI FUNGENI SHULE ZA MSINGI ZA BWENI. NI UZEMBE WA MALEZI

> Anasema hakuna sababu ya kumpeleka Mtoto wa Shule ya Msingi shule bweni

> Umri wa miaka 6 hadi 13 ni umri wa kujifunza na kupata tabia pamoja na ulinzi maalumu kutoka kwa Wazazi. Vyote hivi hatavipata shuleni

Soma > https://jamii.app/WatotoShuleBweni
DAR: BINTI WA MIAKA 25 AKAMATWA NA GRAMU 448.12 ZA HEROINE

> Maria Edson Mtambo amekamatwa akiwa maeneo ya Tegeta Kwa Ndevu

> Alizificha ndani ya vifurushi viwili vya vitabu akijiandaa kuvisafirisha kwenda India kwa mpenzi wake

Soma > https://jamii.app/BintiHeroinDar

#JFLeo #Heroine
UTEUZI: RAIS MAGUFULI AMEMTEUA DKT. MJINGO KUWA MKURUGENZI MKUU TAWIRI

> Kabla ya Uteuzi huu, alikuwa Mkuu wa Kitengo cha Tiba za Wanyamapori na Huduma za Maabara wa TAWIRI

> Anachukua nafasi ya Dkt. Mduma ambaye amestaafu

Soma > https://jamii.app/UteuziTAWIRI

#JamiiForums #JFLeo
RUKWA: WAPIGA KURA WADAIWA KUUZA KADI ZAO

> Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Sumbawanga Mjini amesema baadhi ya wananchi wanauza kadi za kupigia kura kisirisiri

> Amewatahadharisha kuhusu kitendo hicho ambacho ni Kinyume cha Sheria

Soma https://jamii.app/RukwaVitambulisho
#TZ2020
UN: AFRIKA INAPOTEZA TSH. TRILIONI 206.521 KWA MWAKA KWA UHUJUMU UCHUMI

> Fedha zinazopotea ni zaidi ya fedha za misaada zinazopokelewa Afrika

> Nusu ya fedha hizo ni mapato ya bidhaa zinazouzwa nje kama Dhahabu, Almasi na Madini ya Platinum

Soma https://jamii.app/AfrikaFedhaUhujumu
#JFLeo
TANZIA: SAID MABERA WA MSONDO NGOMA AFARIKI DUNIA, ATAZIKWA LEO SAA 10 ALASIRI

> Gwiji huyo wa kupiga Gitaa la Solo amefariki dunia usiku wa kuamkia leo baada ya kuugua kwa muda wa zaidi ya miezi 2

> Alijiunga na Msondo Ngoma mwaka 1973

Soma https://jamii.app/RIPMabela
#RIPMabera
NJOMBE: MAKADA 3 WA CHADEMA WASHIKILIWA KWA TUHUMA ZA MAUAJI

> Makada hao ni Tadei Mwanyika, George Sanga, Optatus Mkwera wakishirikiana na Goodluck Mfuse (Dalali wa Magari) ambao wanatuhumiwa kumuua Emmanuel Mlelwa (UVCCM) Iringa

Soma https://jamii.app/CHADEMAMauajiUVCCM
#JFLeo
MDAU: UKIAMUA KUJIAJIRI NI LAZIMA UWE NA NIDHAMU YA KAZI ZAIDI YA ULIVYOKUWA UMEAJIRIWA

> Anasema, kuna watu wanadhani kuajiriwa ni utumwa na kutokana na uzembe wanaona ni bora wawe na biashara ili waweze kuamka saa 5 asubuhi

> Kama bosi utatakiwa kuwa mfano wa kutunza muda, mazingira na kuonesha vile ambavyo unahitaji wafanyakazi wako wawe. Hii inahitajika nidhamu zaidi kuliko ile ya mtu aliyeajiriwa

Soma https://jamii.app/NidhamuKujiajiri
#JFBiashara
FAHAMU CHANGAMOTO ZINAZOMKABILI MTOTO NJITI

> Mtoto Njiti anaweza kuwa na changamoto ya kupumua hivyo punde tu baada ya kuzaliwa, anatakiwa kupatiwa huduma ya upumuaji

> Hawezi kuhimili baridi hivyo lazima ahifadhiwe kwenye chumba chenye joto la kutosha

> Wana hatari kubwa ya kupata maambukizi kwasababu kinga yao ya mwili haijakomaa

Soma - https://jamii.app/WatotoNjiti

#JFAfya