JamiiForums
βœ”
52.8K subscribers
34.4K photos
2.44K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
MABAHARIA WANAWAKE WAHIMIZA WASICHANA KUSOMA MASOMO YA SAYANSI

> Ni siku ya leo katika kusherekea Siku ya Mabaharia Duniani

> Kampeni ya kuhamasisha itafanyika katika Kanda za Bahari ya Hindi, Ziwa Victoria, Ziwa Tanganyika na Ziwa Nyasa

Soma - https://jamii.app/MabahariaKike
MICHEZO: SAMATTA AWASILI UTURUKI, MAZUNGUMZO NA FENERBAHCE YANAENDELEA

> Mbwana Samatta amesema mazungumzo na Klabu hiyo yanaendelea na hawajasaini hadi sasa

> Januari mwaka huu, Mtanzania huyo alijiunga na Aston Villa akitokea Genk

Soma - https://jamii.app/SamattaUsajiliUturuki

#JFMichezo
#COVID19 KENYA: MAAFISA WA SERIKALI WAHUSISHWA KWENYE KASHFA YA UFISADI

> Serikali ilipokea msaada wa takriban Dola Bil. 2 ili kupambana na mlipuko huo

> Wachunguzi wanatarajia kupendekeza Maafisa na Wafanyabiashara takriban 15 kushtakiwa

Soma https://jamii.app/CovidCorruptionKE
AIDAN EYAKUZE ACHAGULIWA KUWA MWENYEKITI MWENZA WA ASASI ZA KIRAIA KATIKA OGP

> Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza amechaguliwa kuwa Mwenyekiti Mweza wa Asasi za Kiraia katika Open Government Partnership (OGP)

> Muhula wake kwa kushirikiana na Serikali ya Italia utaanza mwaka 2021. Hii ni mara ya pili kwa Tanzania na Twaweza kutoa Mwenyekiti Mwenza

Soma - https://jamii.app/AidanCo-ChairOGP
#CORONAVIRUS-UK: VISA ZAIDI YA 6,600 VYAREKODIWA NDANI YA SAA 24

> Visa vipya 6,634 vimerekodiwa, idadi ambayo ni kubwa zaidi kuripotiwa tangu kuanza kwa mlipuko

> Mapema wiki hii Waziri Mkuu alitangaza masharti mapya ili kudhibiti maambukizi

Soma https://jamii.app/COVID19Updates
KISUTU, DAR: KESI ZA TUNDU LISSU KUSIKILIZWA BAADA YA UCHAGUZI

> Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Augustina Mmbando amekubali ombi lililowasilishwa na Wakili wa utetezi na kuahirisha kesi hizo hadi Novemba 6 ambapo zitasikilizwa mfululizo

Soma https://jamii.app/LissuKesiNov6
MALI: RAIS WA MPITO KUAPISHWA LEO

> Bah Ndaw (70) ataongoza Serikali ya Mpito kwa miezi 18. Kanali Assimi Goita atakuwa Makamu wa Rais

> Ndaw alikuwa Waziri wa Ulinzi katika utawala wa Rais aliyepinduliwa na Jeshi, Ibrahim Boubacar Keita

Soma - https://jamii.app/RaisMaliKiapo
PROF. LIPUMBA: UCHAGUZI USIWE CHANZO CHA UVUNJIFU WA AMANI

> Mgombea Urais kupitia CUF amesema, Tanzania imekuwa Kisiwa cha Amani kwa kipindi kirefu hivyo watanzania wanao wajibu wa kuhakikisha amani hiyo inadumu hasa kipindi hiki

Soma - https://jamii.app/LipumbaAmaniTZ
#Uchaguzi2020
MUHAS YATAJWA KAMA CHUO NO.1 TANZANIA

> Ni kwa mujibu wa University Ranking by Academic Performance (URAP)

> Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili kinashika nafasi ya 1,551 duniani, huku UDSM ikiwa ya 2,047 na SUA 2,206

Soma https://jamii.app/URAPRankings
MAJALIWA: KITI CHA URAIS SIO MCHEZO, KINAHITAJI MTU MAKINI

> Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM amesema, β€œUongozi wa nchi siyo jambo la mchezo, linataka kiongozi makini, anayetetea rasilimali na anayetetea wanyonge dhidi ya rushwa na ufisadi"

Soma https://jamii.app/KitiUraisMajaliwa
#Uchaguzi2020
RASMI: SAMATTA AJIUNGA NA FENERBAHCE YA UTURUKI

> Mbwana Samatta amejiunga na Fenerbahce kwa mkopo wa mwaka mmoja huku Fenerbahce wakieleza kuwa baada ya muda huo wamekubaliana kumpatia Samatta mkataba wa miaka minne

Soma - https://jamii.app/SamattaUsajili
#JFMichezo
POLEPOLE: TUME YA UCHAGUZI IMEWAPENDELEA UPINZANI

> Msemaji wa CCM, Humphrey Polepole amesema, Tume ya Uchaguzi ya Taifa (NEC) ingefuata Sheria bila kutumia Hekima wagombea wasingerudishwa kwenye Uchaguzi Mkuu

Soma https://jamii.app/PolepoleNEC
#Uchaguzi2020
MANYARA: TAKUKURU YAAGIZA KUONDOLEWA KWA MILANGO 83 YA KITUO CHA AFYA KWA KUKOSA UBORA

> Milango hiyo inayodaiwa kuwa ni mipya ktk kituo cha Hirbada imeonekana kupasuka huku mingine ikiwa imepinda na kuvunjika kabla ya kituo kuanza kutumika

Soma - https://jamii.app/MilangoUbora
FAHAMU SABABU ZA MAMA KUJIFUNGUA MTOTO NJITI

- Umri mdogo wa Mama unaweza kupelekea ajifungue kabla ya miezi tisa kutimia kwasababu maumbile yao yanakuwa hayapo tayari kubeba mtoto

- Magonjwa au maambukizi aliyonayo Mama yanaweza kuathiri ujauzito na kusababisha ajifungue mapema

Soma - https://jamii.app/WatotoNjiti
#JFAfya
LISSU: TUTASHINDA UCHAGUZI HUU, OLE WAO WALIOENGUA WAGOMBEA WETU

> Amesema, Serikali ya CHADEMA haitakaa na mtu ambaye hajachaguliwa na Wananchi

> Amesema, Uchaguzi utarudiwa kwa Majimbo na Kata zote ambazo wagombea wao wameenguliwa

Soma - https://jamii.app/KampeniMisungwi
#Uchaguzi2020
MBEYA: MWALIMU MKUU MBARONI KWA RUSHWA YA NGONO

> Adelhard Mjingo (44) anashikiliwa kwa kuomba rushwa ya ngono kwa Mwanafunzi (14)

> Aliahidi kumsaidia Mtihani wa Darasa la 7 huku akitishia kuwa, akikataa atahakikisha hafaulu

Soma - https://jamii.app/RushwaMwl-MBY

#KemeaRushwa
SHIBUDA: VYAMA VIJENGE HOJA, UONGO WA SIASA HUZAA DHULUMA

> Mwenyekiti huyo wa Baraza la Vyama vya Siasa amesema mfumo wa vyama vingi ni kichocheo cha maendeleo sio mafarakano

> Amewataka wagombea kuepuka kupandikiza chuki ktk taifa

Soma https://jamii.app/ShibudaVyamaHoja

#Uchaguzi2020
MAADILI YA UCHAGUZI: KUKOSOANA KWA WAGOMBEA/VYAMA KUJIKITE KATIKA SERA

> Hairuhusiwi kubeba sanamu/kinyago kinachoonesha kudhalilisha, kebehi au kufedhehesha chama kingine cha siasa, kiongozi wake au Serikali katika mkutano wa kisiasa

Soma - https://jamii.app/MaadiliUchaguzi
#Uchaguzi2020
WFP: WAKIMBIZI WENGI WA #MSUMBIJI WANAKIMBILIA #TANZANIA KUTOKANA NA MAPIGANO

> Makadirio ya Shirika la Chakula Duniani ni kuwa, idadi ya wakimbizi hao ni takriban 1000 ambapo inasemekana baadhi hutumia boti huku wengine wakiogolea Mto Ruvuma

Soma - https://jamii.app/WakimbiziMsumbiji
AMBER RUTY, MUMEWE NA JAMES DELICIOUS WAHUKUMIWA MIAKA 5 JELA

> Wamehukumiwa kifungo hicho au kulipa faini (Amber Rutty milioni. 3, Mume wa Amber milioni. 3 na James milioni. 5)

> Wameshindwa kulipa faini na hivyo kupelekwa gerezani

Soma - https://jamii.app/HukumuAmberRuty